TRA valuation system ya magari haiko fair

TRA valuation system ya magari haiko fair

Kuna wakati unakuwa mbishi hadi unakeraView attachment 390654View attachment 390655 Hiyo ya 17mil vitz ni ya 2016, hiyo nyingine ni ya 2005. Nimeshindwa kupiga full pics.

Yani hiyo ya 2016 ni 17.mil wakati ya 2005 ni 4.mil. usiwe mbishi kila mara.
Kuna wakati unakuwa mbishi hadi unakeraView attachment 390654View attachment 390655 Hiyo ya 17mil vitz ni ya 2016, hiyo nyingine ni ya 2005. Nimeshindwa kupiga full pics.

Yani hiyo ya 2016 ni 17.mil wakati ya 2005 ni 4.mil. usiwe mbishi kila mara.


Huyu jamaa mkuu hadi anashangaza,yaani anatetea vitu vilivyo wazi kabisa,sijui ana maslahi gani na kuumizwa kupitia kodi kwa watanzania
 
Mkuu, malalamiko yako ni kweli kabisa. Hayo yametukumbuka wengi. Ni jambo lisiloeleweka kwa mwerevu yeyote. Tunabaki vinywa wazi na kuwashangaa "wasomi" watungasera. Kwa mtindo huu lazima bandari ibaki tupu na uchumi kudorora kwa kasi.
 
Naona mkuu umesahau kodi ya Reli ya kwrnda Rwanda tunalipia sie Watanganyika mzee. Mie mwenzio naugulia maumivu tu. Niliwrka bandiko langu week iliyopita na chombo kinaelea sasa hivi kuna bongo. Pole sana mkuu.
 
Wewe hata gari huna halafu unabishana na wanaume. Pumbaf.
Achana nae huyo hajuwi analo liongelea. Anazani kila gari lazima mtumiaji afikishe kilometa laki moja. Mm nina gari ipo TZ ya 2006 nimetumia nje ya bongo na nimeileta bongo mpaka sasa ina 54000 na nilinunua ikiwa mpya.
 
Ndiyo hivyo umeibiwa Volvo iliyotembea km 30 000 haiwezi kuuzwa bei hiyo, na ndiyo maana umepigwa uchakavu, dola 4000 ni gari iliyotembea zaidi ya km 100 000 !
Iyo Gari watakuwa waliichezea odometer, ionekane imetembea kilometers chache. TRA office wakichukua documents za Gari wakiingiza katika system inaonyesha kwamba kilometers sahihi iliyotembea. Wauzaji wengi wa magari hudanganya hata kwamba Gari imetengenezwa mwaka fulani, lakini ukipata ile kadi yake baada ya kununua inaonyesha tofauti
 
Lkn pia linachafua mazingira, na ndiyo maana kodi ni kubwa ili ununue gari mpya ambayo haichafui mazingira sana, hiyo ndiyo sababu na Dunia nzima hufanya hivi kwa namna moja au nyingine!
mkuu hata ukinunua gari mpya bado kodi ni juu sana. kwa ufupi kodi zetu unapoagiza gari sio rafiki hata kidogo. ni kama vile tunakomoana. huo ndo ukweli.
 
Kwanza niaze kwa kusema kuwa sina nia ya KULETA UCHOCHEZI! Maana siku hizi kila jambo linalosemwa au kuandikwa ambalo linalenga kutofautiana au kukosoa mfumo mpya wa uongozi wa nchi yetu basi linatafsiriwa kama uchochezi. Siku hizi hatuna budi kufunga midomo yetu na kumuacha Rais wetu afanye kazi yake.

Nirudi kwenye hoja iliyonileta. Sasa mimi nina malalamiko na TRA valuation system ya magari. Nimemwagizia mama yangu gari kutoa Japan. Gari yenyewe ni Volvo V50. Ni ya mwaka 2009 na ina mileage ya 30k. CIF ya gari hii ni $4,455 (approx. Tshs 9,701,000). Sasa sijui kwa kigezo gani kilichotumika, TRA’s assessment ime-value gari kwa $10,884 (approx. Tshs 23,727,120). Sasa kulingana na valuation ya TRA, nimechajiwa ushuru wa Tshs. 15,477,959. Hebu jaribu ku-imagine gari ununue kwa milioni 9, halafu TRA wakuchaji ushuru wa milioni 15! How fair is that? Gari ya mwaka 2009, ambayo sio chakavu, inawezaje kuchajiwa kodi 15m??? Halafu cha kusikitisha zaidi ni kwamba hakuna room ya ku-negotiate.

Sasa basi, hivi ndivyo TRA walivyonipiga na ushuru wa kukatishana tamaa. Kulingana na invoice value ya gari (milioni 9), ushuru wake ni milioni 6. Hii ina maana, kama TRA wangetumia gharama nilizonunulia gari $4,455, basi ningechajiwa ushuru wa milioni 6 tu. Lakini kwa kuwa wamehamua ku-value gari, basi wameongeza nyongeza nyingine ya ushuru wa milioni 9. Hii ina maana kuwa, ile nyongeza ya valuation kutoka invoice value mpaka base value (milioni 23 – milioni 9 = milioni 14) ndiyo wameichaji ushuru wa milioni 9. So ushuru wa invoice value (milioni 6) + ushuru wa nyongeza iliyotokana na valuation (milioni 9) = ushuru wa milioni 15. Sijui niite huu ni uhuni au nini? Nakosa la kusema!

Kwa TRA kukomoa hivyo wanajaribu kutuma ujumbe gani? Tusiagize magari/vitu kutoka nje au ndo mambo ya ‘kumfanya kila Mtanzania haishi kama shetani”? Kwa style hii, kweli bandari yetu haitaacha kukauka?

Haya ni malalamiko yangu.
Mkuu calculator yao hakuna sehemu inapokwambia ujaze bei uliyonunulia gari. Hivyo basi moja kwa moja ni kwamba kodi yao haitokani na cif/bei uliyouziwa gari.
Unachojaza ni aina ya mafta, model ya gari, mwaka na cc za gari.
Halafu anayesema gari mpya kodi ndogo anadanganya jaribu kuchukua gari mfano allion ya mwaka 2002 na ya mwaka 2008 utakuta ya mwaka 2008 ina kodi zaidi.
 
Mkuu calculator yao hakuna sehemu inapokwambia ujaze bei uliyonunulia gari. Hivyo basi moja kwa moja ni kwamba kodi yao haitokani na cif/bei uliyouziwa gari.
Unachojaza ni aina ya mafta, model ya gari, mwaka na cc za gari.
Halafu anayesema gari mpya kodi ndogo anadanganya jaribu kuchukua gari mfano allion ya mwaka 2002 na ya mwaka 2008 utakuta ya mwaka 2008 ina kodi zaidi.


Tumia asilimia kwenye kukokotoa kwako kwa mfano kodi ya gari ya 2002 ni asilimia ngapi ya thamani ya gari ukilinganisha na ya 2008 hapo ndiyo utajua lkn siyo kwa kuangalia tarakimu tu, jaribu kupiga hesabu kwa asilimia!
 
Wala sihitaji kwa maana najali mazingira yetu zaidi, hivyo TRA yetu wako sawa kabisa ukitaka nunua gari mpya ambayo ina teknolojia inayozuia uchafuzi wa mazingira!
Watanzania tunaumia sana kwa kodi hizi za kukomoana. Ile ahadi ya rais wa wananchi masikini hapa inatenda kinyume chake.

Watakaomudu kutembelea magari binafsi ni matajiri tu. Siye masikini tutaishia kuomba lift
 
Tumia asilimia kwenye kukokotoa kwako kwa mfano kodi ya gari ya 2002 ni asilimia ngapi ya thamani ya gari ukilinganisha na ya 2008 hapo ndiyo utajua lkn siyo kwa kuangalia tarakimu tu, jaribu kupiga hesabu kwa asilimia!
Kwa Mtz wa kawaida anayehitaji usafiri kwa bei rahisi kwa magari anayoona yanafanana mfano passo ya 2003 na ya 2009 kimtazamo sioni tofauti yake hajalo asilimia anajali figure so atachukua ya 2003 coz anaona he/will pay less
 
Pole Sana mkuu, hili Ni tatizo la kutegemea kodi Tu kwa kila kitu wakati resources zipo kibao.
TRA wamekuwa ndo wauzaji wenyewe kwa maana Wao ndo hupanga bei, invoice inaonesha labda $500 Wao wana uplift to $800 unabaki unajiuliza Ina maana Wao wanajua thamani ya kitu husika kuliko muuzaji? Hii Ni ajabu Sana Na Ni tatizo la Kutokuwa creative.

Hivi suala lako huwezi kwenda li-challenge Tax appeals tribunal?
 
...e
Kwa Mtz wa kawaida anayehitaji usafiri kwa bei rahisi kwa magari anayoona yanafanana mfano passo ya 2003 na ya 2009 kimtazamo sioni tofauti yake hajalo asilimia anajali figure so atachukua ya 2003 coz anaona he/will pay less
Sijakuelewa
 
..
Hiyo ni gari KUU KUU na hapo unadanganya/umedanganywa haiwezekani gari ya miaka zaidi ya 8 iwe imetembea km 30 000 tu!
Huo ni uongo mweupe hizo km inazimaliza kwa mwaka mmoja tu na isitoshe kama ni kweli imetembea km 30 000 haiwezi ikauzwa
Dola 4 500 hilo haliwezekani, hivyo TRA wetu wako sawa kabisa kwa maana wewe ni muongo/ umedanganywa!
..yaani it is very possible, tena hapo mengi Tu ambayo mileage Ni ndogo Sana Na gari Ni ya muda mrefu, 2009 Ni juzi Tu Na kwa Tz Ni gari mpya kabisa, unless huna mazoea ya hiyo biashara, yaani gari Ina miaka 7 tokea iundwe unashangaa?
 
Pole Sana mkuu, hili Ni tatizo la kutegemea kodi Tu kwa kila kitu wakati resources zipo kibao.
TRA wamekuwa ndo wauzaji wenyewe kwa maana Wao ndo hupanga bei, invoice inaonesha labda $500 Wao wana uplift to $800 unabaki unajiuliza Ina maana Wao wanajua thamani ya kitu husika kuliko muuzaji? Hii Ni ajabu Sana Na Ni tatizo la Kutokuwa creative.

Hivi suala lako huwezi kwenda li-challenge Tax appeals tribunal?
Mkuu kwenye calculator ya tra kumbuka hakuna sehemu unajaza bei uliyonunulia gari which means kodi haiwi calculated toka kwenye bei uliyonunua gari. Inaelekea wao washa set bei zao
 
..
..yaani it is very possible, tena hapo mengi Tu ambayo mileage Ni ndogo Sana Na gari Ni ya muda mrefu, 2009 Ni juzi Tu Na kwa Tz Ni gari mpya kabisa, unless huna mazoea ya hiyo biashara, yaani gari Ina miaka 7 tokea iundwe unashangaa?


Uwezekano upo ingawaje ni mdogo sana kwa gari yenye umri zaidi ya miaka 8 kutembea km 30 000 tu! Na isitoshe Volvo V50 iliyotembea km 30 000 tu kuuzwa dola 4 000 hapo hapana, labda kama umepewa zawadi lkn kwa bei ya sokoni siyo kweli!
 
Mkuu kwenye calculator ya tra kumbuka hakuna sehemu unajaza bei uliyonunulia gari which means kodi haiwi calculated toka kwenye bei uliyonunua gari. Inaelekea wao washa set bei zao
....bado ni tatizo, and it must be challenged na hapa serikali inatapeli wananchi wake yenyewe, kama mtu ananunua kitu 500 kihalali kabisa, wewe unasema ni 700 ilimradi tu kodi iwe kubwa, huo ni utapeli
 
Kwa Mtz wa kawaida anayehitaji usafiri kwa bei rahisi kwa magari anayoona yanafanana mfano passo ya 2003 na ya 2009 kimtazamo sioni tofauti yake hajalo asilimia anajali figure so atachukua ya 2003 coz anaona he/will pay less


Ndiyo maana nasema inategemea kwako kulipa less maana yake nini lkn ukikokotoa kiasilimia utaona mwenye gari mpya analipia asilimia ndogo ukilinganisha na mwenye gari ku kuu!
 
Back
Top Bottom