TRA valuation system ya magari haiko fair

Hiyo ni gari KUU KUU na hapo unadanganya/umedanganywa haiwezekani gari ya miaka zaidi ya 8 iwe imetembea km 30 000 tu!
Huo ni uongo mweupe hizo km inazimaliza kwa mwaka mmoja tu na isitoshe kama ni kweli imetembea km 30 000 haiwezi ikauzwa
Dola 4 500 hilo haliwezekani, hivyo TRA wetu wako sawa kabisa kwa maana wewe ni muongo/ umedanganywa!
Ushuru unatozwa kwa kilometers?
 
Kwanza niaze kwa kusema kuwa sina nia ya KULETA UCHOCHEZI! Maana siku hizi kila jambo linalosemwa au kuandikwa ambalo linalenga kutofautiana au kukosoa mfumo mpya wa uongozi wa nchi yetu basi linatafsiriwa kama uchochezi. Siku hizi hatuna budi kufunga midomo yetu na kumuacha Rais wetu afanye kazi yake.

Nirudi kwenye hoja iliyonileta. Sasa mimi nina malalamiko na TRA valuation system ya magari. Nimemwagizia mama yangu gari kutoa Japan. Gari yenyewe ni Volvo V50. Ni ya mwaka 2009 na ina mileage ya 30k. CIF ya gari hii ni $4,455 (approx. Tshs 9,701,000). Sasa sijui kwa kigezo gani kilichotumika, TRA’s assessment ime-value gari kwa $10,884 (approx. Tshs 23,727,120). Sasa kulingana na valuation ya TRA, nimechajiwa ushuru wa Tshs. 15,477,959. Hebu jaribu ku-imagine gari ununue kwa milioni 9, halafu TRA wakuchaji ushuru wa milioni 15! How fair is that? Gari ya mwaka 2009, ambayo sio chakavu, inawezaje kuchajiwa kodi 15m??? Halafu cha kusikitisha zaidi ni kwamba hakuna room ya ku-negotiate.

Sasa basi, hivi ndivyo TRA walivyonipiga na ushuru wa kukatishana tamaa. Kulingana na invoice value ya gari (milioni 9), ushuru wake ni milioni 6. Hii ina maana, kama TRA wangetumia gharama nilizonunulia gari $4,455, basi ningechajiwa ushuru wa milioni 6 tu. Lakini kwa kuwa wamehamua ku-value gari, basi wameongeza nyongeza nyingine ya ushuru wa milioni 9. Hii ina maana kuwa, ile nyongeza ya valuation kutoka invoice value mpaka base value (milioni 23 – milioni 9 = milioni 14) ndiyo wameichaji ushuru wa milioni 9. So ushuru wa invoice value (milioni 6) + ushuru wa nyongeza iliyotokana na valuation (milioni 9) = ushuru wa milioni 15. Sijui niite huu ni uhuni au nini? Nakosa la kusema!

Kwa TRA kukomoa hivyo wanajaribu kutuma ujumbe gani? Tusiagize magari/vitu kutoka nje au ndo mambo ya ‘kumfanya kila Mtanzania haishi kama shetani”? Kwa style hii, kweli bandari yetu haitaacha kukauka?

Haya ni malalamiko yangu.
Mkuu naunga mkono hoja. Mi nilidhani nchi kama Japan ama china ndo zingekua na ushuru mkubwa ili discourage kuingiza magari toka nje coz wao wanatengeneza. Napata shida kuelewa kwanini nchi yetu inafanya hivyo, labda mwenye uelewa zaidi wa suala atujuze KWA NINI?
 
Ndiyo hivyo umeibiwa Volvo iliyotembea km 30 000 haiwezi kuuzwa bei hiyo, na ndiyo maana umepigwa uchakavu, dola 4000 ni gari iliyotembea zaidi ya km 100 000 !
Tembelea website ya tra utajua vizuri ,gari inaangaliwa cc ,mwaka na wala hawaangalii kilometers
 
Juzi nimechoka nina million tisa naambiwa huwezi nunua ist kwa bei iyo anzia million 15
 
Ndiyo hivyo umeibiwa Volvo iliyotembea km 30 000 haiwezi kuuzwa bei hiyo, na ndiyo maana umepigwa uchakavu, dola 4000 ni gari iliyotembea zaidi ya km 100 000 !

Sawa Barbosa nimekuelewa.

Ok nimeibiwa. Sasa kwanini Serikali inaniadhibu zaidi?

Kwani kwa TRA kuongeza thamani ya gari ni kunaashiria kuwa gari ni chakavu au lina thamani kubwa? Nimeuziwa gari kwa $4,455 na TRA wamelithaminisha $10,880. Kitu kinachothaminishwa zaidi ya bei/uhalisia kinamaanisha hicho kitu kina hadhi kubwa au ni chakavu? Labda unipe ufafanuzi hapa ili nijifunze.
 
Hiyo ni gari KUU KUU na hapo unadanganya/umedanganywa haiwezekani gari ya miaka zaidi ya 8 iwe imetembea km 30 000 tu!
Huo ni uongo mweupe hizo km inazimaliza kwa mwaka mmoja tu na isitoshe kama ni kweli imetembea km 30 000 haiwezi ikauzwa
Dola 4 500 hilo haliwezekani, hivyo TRA wetu wako sawa kabisa kwa maana wewe ni muongo/ umedanganywa!
Kwani TRA wana base kwenye km au mwaka? Ila vyovyote iwavyo kodi yetu bado naona ni kubwa mno kwa upande wa magari. Mi nadhan wengi tunachukulia gari kama chombo cha starehe (luxury good) lakini kumbe inamrahisishia mtu kuongeza kipato binafsi ambacho huenda sanjari na kuongeza pato la nchi
 
Pole jamaa yangu. Ushauri ungepitia website ya TRA wanaonyesha bei ya gari kulingana mwaka wa kutengenezwa na siyo bei uliyonunulia. Wanatumia retail selling price ambayo hiyo V50 ni kati ya dola 60,000 mpaka 67,000. Hapo ndiyo kukokotoa kunaanzia hapo na dhamani ya gari yako haitumiki uliyonunulia na itakuwa retail selling price kutoka kwenye list ya TRA na hapo unajikuta unalipa VAT peke yake karibu dola 8000. Kama alivyoshauri jamaa hapo before kuagiza angalia online calculator ya TRA

Ahsante DN kwa ufafanuzi.

Lakini sasa kwanini TRA wameniadhibu, kwa kitu ambacho sikuwa na control nacho? Mimi nimeliona gari na nikalipenda. Nikauliza bei nikapewa na nikaikubali. Sasa kwanini TRA wamehamua kuniadhibu zaidi kwa kunipiga ushuru ambao hauna uhalisia kwa bei niliyolipa? Ni kwamba hawaamini kuwa nimelipa hiyo bei ama? Kama ni hivyo, kwanini wasingenipa nafasi ya kuwasilisha documents ambazo zinaweza kuthibitisha/kutothibitisha kuwa nimelipa kiasi ninachosema nimelipa?
 
Kwanza niaze kwa kusema kuwa sina nia ya KULETA UCHOCHEZI! Maana siku hizi kila jambo linalosemwa au kuandikwa ambalo linalenga kutofautiana au kukosoa mfumo mpya wa uongozi wa nchi yetu basi linatafsiriwa kama uchochezi. Siku hizi hatuna budi kufunga midomo yetu na kumuacha Rais wetu afanye kazi yake.

Nirudi kwenye hoja iliyonileta. Sasa mimi nina malalamiko na TRA valuation system ya magari. Nimemwagizia mama yangu gari kutoa Japan. Gari yenyewe ni Volvo V50. Ni ya mwaka 2009 na ina mileage ya 30k. CIF ya gari hii ni $4,455 (approx. Tshs 9,701,000). Sasa sijui kwa kigezo gani kilichotumika, TRA’s assessment ime-value gari kwa $10,884 (approx. Tshs 23,727,120). Sasa kulingana na valuation ya TRA, nimechajiwa ushuru wa Tshs. 15,477,959. Hebu jaribu ku-imagine gari ununue kwa milioni 9, halafu TRA wakuchaji ushuru wa milioni 15! How fair is that? Gari ya mwaka 2009, ambayo sio chakavu, inawezaje kuchajiwa kodi 15m??? Halafu cha kusikitisha zaidi ni kwamba hakuna room ya ku-negotiate.

Sasa basi, hivi ndivyo TRA walivyonipiga na ushuru wa kukatishana tamaa. Kulingana na invoice value ya gari (milioni 9), ushuru wake ni milioni 6. Hii ina maana, kama TRA wangetumia gharama nilizonunulia gari $4,455, basi ningechajiwa ushuru wa milioni 6 tu. Lakini kwa kuwa wamehamua ku-value gari, basi wameongeza nyongeza nyingine ya ushuru wa milioni 9. Hii ina maana kuwa, ile nyongeza ya valuation kutoka invoice value mpaka base value (milioni 23 – milioni 9 = milioni 14) ndiyo wameichaji ushuru wa milioni 9. So ushuru wa invoice value (milioni 6) + ushuru wa nyongeza iliyotokana na valuation (milioni 9) = ushuru wa milioni 15. Sijui niite huu ni uhuni au nini? Nakosa la kusema!

Kwa TRA kukomoa hivyo wanajaribu kutuma ujumbe gani? Tusiagize magari/vitu kutoka nje au ndo mambo ya ‘kumfanya kila Mtanzania haishi kama shetani”? Kwa style hii, kweli bandari yetu haitaacha kukauka?

Haya ni malalamiko yangu.
Mkuu Quemu, yawezekana kuna kitu flani ulikuwa haukijui! Angalia CIF price yako uliyonunulia gari na Custom Value CIF iliyopo kwenye kikokotozi cha TRA.
Kama custom value CIF ni ndogo kuliko CIF uliyolipia gari lako basi utachajiwa hela kubwa na TRA kuliko inayoonekana kwenye calculator yao (hapo sijui wanafanyaje mpaka hela inakuwa kubwa) , ila kama CIF yako ni ndogo ama inalingana na custom value CIF basi utalipia exactly kama iliyopo kwenye TRA calculator.

Mimi niliagiza gari kidogo niingie kwenye matatizo haya bahati nzuri kabla sijalipia pesa Japan nikawa nimeingia JF nikakuta uzi unaongelea kuhusu hili, ikabidi nibadili maamuzi na ku-negotiate na seller na bahati nzuri tukashushana mpaka CIF price nikawa chini ya custom value CIF ya TRA (difference ilikuwa 200USD). B/L zilipokuja TRA wakafanya analysis na kodi ilikuja ile ile niliyotarajia ambayo haipo juu kihivyo, CIF price inatofautiana kwa 1.5mil na kodi niliyotakiwa kulipa!!
 
Yoyote atakaye agiza Gari CIF $2500 ajiandae kulipia 6M Kodi ya ushuru. Saivi kuna kuchangia Kodi ya Ujenz wa Reli.
 
hili jambo la TRA kuwa kamua wananchi wanapotaka kujikomboa kwa kujipatia kau safiri hata mimi nawaomba Serikali kupitia waziri wa Fedha walipitie upya maana ni kero sana Jamani.

Yaani ushuru ni mkubwa kuliko hata bei ya kununulia gari lenyewe!!!!!!!

Chonde chode serikali yetu Embu tunaomba mtusaidie wananchi wenu Ushuru huu umekuwa mzigo mzito sana.
 
Kwani TRA wana base kwenye km au mwaka? Ila vyovyote iwavyo kodi yetu bado naona ni kubwa mno kwa upande wa magari. Mi nadhan wengi tunachukulia gari kama chombo cha starehe (luxury good) lakini kumbe inamrahisishia mtu kuongeza kipato binafsi ambacho huenda sanjari na kuongeza pato la nchi


Lkn pia linachafua mazingira, na ndiyo maana kodi ni kubwa ili ununue gari mpya ambayo haichafui mazingira sana, hiyo ndiyo sababu na Dunia nzima hufanya hivi kwa namna moja au nyingine!
 
Sawa Barbosa nimekuelewa.

Ok nimeibiwa. Sasa kwanini Serikali inaniadhibu zaidi?

Kwani kwa TRA kuongeza thamani ya gari ni kunaashiria kuwa gari ni chakavu au lina thamani kubwa? Nimeuziwa gari kwa $4,455 na TRA wamelithaminisha $10,880. Kitu kinachothaminishwa zaidi ya bei/uhalisia kinamaanisha hicho kitu kina hadhi kubwa au ni chakavu? Labda unipe ufafanuzi hapa ili nijifunze.


Unatakiwa ununue gari mpya ambayo haichafui mazingira yetu hiyo ndiyo sababu!
 
Ndugu pole.Naona ulivyoandika ni kama umekuwa "taken in surprise" na huo mchanganuo wa hizo gharama. Ukiuliza humu katika JF kwa waliowahi kuagiza magari watakuambia kwamba huo ni utaratibu uliopo kwa sasa ambao kama ulivyosema unatoa maswali mengi zaidi ya majibu.Ni vyema next time ukitaka kuagiza gari tumia JF kupata ushauri (Kuuliza si ujinga) hasa katika mambo yanayohusu Kodi za kulipa Tra, website za kupata magari mazuri, jinsi ya kunegotiate nk.
Ahsante
 
Kwanza niaze kwa kusema kuwa sina nia ya KULETA UCHOCHEZI! Maana siku hizi kila jambo linalosemwa au kuandikwa ambalo linalenga kutofautiana au kukosoa mfumo mpya wa uongozi wa nchi yetu basi linatafsiriwa kama uchochezi. Siku hizi hatuna budi kufunga midomo yetu na kumuacha Rais wetu afanye kazi yake.

Nirudi kwenye hoja iliyonileta. Sasa mimi nina malalamiko na TRA valuation system ya magari. Nimemwagizia mama yangu gari kutoa Japan. Gari yenyewe ni Volvo V50. Ni ya mwaka 2009 na ina mileage ya 30k. CIF ya gari hii ni $4,455 (approx. Tshs 9,701,000). Sasa sijui kwa kigezo gani kilichotumika, TRA’s assessment ime-value gari kwa $10,884 (approx. Tshs 23,727,120). Sasa kulingana na valuation ya TRA, nimechajiwa ushuru wa Tshs. 15,477,959. Hebu jaribu ku-imagine gari ununue kwa milioni 9, halafu TRA wakuchaji ushuru wa milioni 15! How fair is that? Gari ya mwaka 2009, ambayo sio chakavu, inawezaje kuchajiwa kodi 15m??? Halafu cha kusikitisha zaidi ni kwamba hakuna room ya ku-negotiate.

Sasa basi, hivi ndivyo TRA walivyonipiga na ushuru wa kukatishana tamaa. Kulingana na invoice value ya gari (milioni 9), ushuru wake ni milioni 6. Hii ina maana, kama TRA wangetumia gharama nilizonunulia gari $4,455, basi ningechajiwa ushuru wa milioni 6 tu. Lakini kwa kuwa wamehamua ku-value gari, basi wameongeza nyongeza nyingine ya ushuru wa milioni 9. Hii ina maana kuwa, ile nyongeza ya valuation kutoka invoice value mpaka base value (milioni 23 – milioni 9 = milioni 14) ndiyo wameichaji ushuru wa milioni 9. So ushuru wa invoice value (milioni 6) + ushuru wa nyongeza iliyotokana na valuation (milioni 9) = ushuru wa milioni 15. Sijui niite huu ni uhuni au nini? Nakosa la kusema!

Kwa TRA kukomoa hivyo wanajaribu kutuma ujumbe gani? Tusiagize magari/vitu kutoka nje au ndo mambo ya ‘kumfanya kila Mtanzania haishi kama shetani”? Kwa style hii, kweli bandari yetu haitaacha kukauka?

Haya ni malalamiko yangu.
hamna namna kodi italipwa tu, Ipande tu maradufu tuwe nchi ya viwanda
 
Back
Top Bottom