TRA: Pikipiki (Bodaboda) kuanza kulipa Kodi ya Tsh. 65,000/- kwa mwaka

Unajua serikali inapo anzisha au kuongeza wigo wa Kodi,inamaana hapa Kuna watu watapata ajira waliosoma Mambo ya kodi, xo nijambo jema,sema daa! Nawaonea huruma boda Boda mtapata tabu Sana alafu wafanya biashara watapumzika kidogooo,maana nyie Boda Boda mtataka kusumbua kulipa xo Kuna ka nguvu katatumika 😄 poleni bhana
 
Bodaboda mmesikia hii? Sasa rasmi mtaanza kulipa Kodi. Hapa Serikali mmechemka na mnawaonea Bodaboda, maana kupata 20,000 kwa siku ni kazi kubwa ila Nchi itajengwa na Watanzania wote.

----
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa katika mabadiliko ya Sheria za kodi mwaka 2023, serikali imeweka kodi ya mapato kwa wasafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki zenye magurudumu mawili (Bodaboda) ambapo watatakiwa kulipa kiasi cha Sh. 65,000 kwa Mwaka.

Hayo yamesemwa jana na Afisa mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hamad Mterry, wakati akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu.

Mterry amesema kuwa hiyo ni moja ya sheria ya kodi ambayo ni mpya na imewagusa Bodaboda, ambapo watatakiwa kuichagia serikali kiasi cha Sh. 65,000 kwa mwaka, kuanzia mwaka huu wa fedha ambao tayari umeanza tangu Julai Mosi, 2023.

Afisa Mawasiliano na elimu kwa umma kutoka (TRA) Mkoa wa Simiyu, Benjamin John amesema kuwa Bodaboda anaweza kulipa kodi hiyo kwa awamu nne ndani ya mwaka, ambapo kila awamu atatakiwa kulipa Sh. 16,250.

Hata hivyo wafanyabiashara za kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki (Bodaboda) wanaona kodi hiyo inakwenda kuongeza ugumu wa maisha kwao, kutokana na kipato chao cha kila siku kuwa kidogo sana.

“ Ukizingatia kwa sasa kupata Sh. 10,000 kwa siku ni ngumu sana, lakini mafuta yamepanda bei, tunalipa LATRA, tunalipa Bima, bado familia inakutegemea, leo tumeletewa TRA, ukweli kodi hii inakwenda kutuumiza sana,” amesema Ntoni Deus.

My Take
Naunga mkono,Pia pombe na Sigara ziongezewe Kodi.View attachment 2714625
Tutarajie ile motor vehicle licence kurudi soon
 
Bodaboda mmesikia hii? Sasa rasmi mtaanza kulipa Kodi. Hapa Serikali mmechemka na mnawaonea Bodaboda, maana kupata 20,000 kwa siku ni kazi kubwa ila Nchi itajengwa na Watanzania wote.
----
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa katika mabadiliko ya Sheria za kodi mwaka 2023, serikali imeweka kodi ya mapato kwa wasafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki zenye magurudumu mawili (Bodaboda) ambapo watatakiwa kulipa kiasi cha Sh. 65,000 kwa Mwaka.
Hayo yamesemwa jana na Afisa mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hamad Mterry, wakati akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu.
Mterry amesema kuwa hiyo ni moja ya sheria ya kodi ambayo ni mpya na imewagusa Bodaboda, ambapo watatakiwa kuichagia serikali kiasi cha Sh. 65,000 kwa mwaka, kuanzia mwaka huu wa fedha ambao tayari umeanza tangu Julai Mosi, 2023.
Afisa Mawasiliano na elimu kwa umma kutoka (TRA) Mkoa wa Simiyu, Benjamin John amesema kuwa Bodaboda anaweza kulipa kodi hiyo kwa awamu nne ndani ya mwaka, ambapo kila awamu atatakiwa kulipa Sh. 16,250.
Hata hivyo wafanyabiashara za kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki (Bodaboda) wanaona kodi hiyo inakwenda kuongeza ugumu wa maisha kwao, kutokana na kipato chao cha kila siku kuwa kidogo sana.
“ Ukizingatia kwa sasa kupata Sh. 10,000 kwa siku ni ngumu sana, lakini mafuta yamepanda bei, tunalipa LATRA, tunalipa Bima, bado familia inakutegemea, leo tumeletewa TRA, ukweli kodi hii inakwenda kutuumiza sana,” amesema Ntoni Deus.
My Take
Naunga mkono,Pia pombe na Sigara ziongezewe Kodi.View attachment 2714625
 
Boda wawe na kadi maalum za kununulua mafuta ili hiyo Kodi ikatwe kwenye mafuta hivyo Liwe jukumu la Sheli kuhakikisha boda wote wamekatwa kwa siku
 
Kuna siku moja nilikuwa naongea na jamaa mmoja Mtanzania anakaa Finland siku nyingi sana, kuhusu kodi.

Akawa anasema, Watanzania si kweli kwamba hawapendi kulipa kodi. Watanzania hawapendi kulipa kodi ambazo hawaoni zinachofanya katika maisha yao. Yani kodi wanalipa, halafu zile huduma za kijamii zinazotakiwa kufanywa na hizo kodi hawazioni.

Akasema, Watanzania hawahawa wakienda kukaa nchi kama Finland, wanatozwa kodi kubwa kuliko Tanzania, lakini hawalalamiki.

Kwa nini? Kwa sababu kazi nzuri zipo, mishahara mizuri ipo, na hata kukiwa na kodi kubwa sana, wanaona kabisa kodi zetu zinafanya kazi gani, kuanzia shule nzuri, hospitali nzuri, zenye madawa na huduma tele, madaktari wazuri na wengi, mifuko ya jamii kuhudunia watu wasio na kazi ipo vizuri, wazee wakistaafu wanahudumiwa vizuri, nyumba nzuri, huduma kama zimamoto na ufagizi wa mitaa nzuri, barabara nzuri, takataka zinakusanywa vizuri, maji unapata vizuri, mtu unaona wachukue tu hiyo kodi, maana kazi ya kodi unaiona.

Sasa Tanzania mnaenda kuwaminya mpaka mapumbu kwa kodi hao bodaboda ambao hata kula kwao kwa tabu, halafu kodi zote mnaenda kununua ma VX na kujenga ma Ikulu kedekede, huku hospitali hazina dawa, takataka hamzoi, miji michafu, maji ya shida mpaka mjini, mnategemea vipi watu wafurahie kutozwa kodi?
Mule mule!.
 
kipindi kile Lema alivyosema boda boda sio kazi rasmi walikuja juu na kudai wanaingiza pesa nyingi kupitia boda boda na wengine wamejenga. kuna mwingine alisema anaingiza hata milioni kadhaa kwa mwezi. Sasa leo 65,000 kwa mwaka ni kubwa? boda boda bhana

Hamna cha lema wala nani kikubwa ni kulipa kodi tena wamehurumiwa wanatakiwa kulipa zaidi ya 365000
Wengine ni hawa bajaji za abiria
Bajaji za mizigo wote hawa wanapata hela bila kukatwa kodi
Usipolipa kodi maendeleo yatatoka wapi ?
 
Back
Top Bottom