TRA: Pikipiki (Bodaboda) kuanza kulipa Kodi ya Tsh. 65,000/- kwa mwaka

Hiyo hela ni kubwa sana hasa kwa bodaboda!
Kuna watu wanafunga mwaka hawana hata akiba ya 10000 na wamefanya kazi mwaka mzima.
Kuna sehemu tuliambiwa tulipe 3000 kwa mwezi huku uswahilini na bado watu hawapati hiyo hela, ambapo ni wastani wa shilingi 100 kwa siku.
Kuitoa 3000 kwa pamoja bila sababu zinazoeleweka ni ngumu sana kwa watu wa uchumi fulani.
Akiba hawezi pata ila on daily basis anapata.

Wamama wanalipa ushuru wa 200 Kila siku masokoni
 
Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Naungana nawe ila pia ela ya kodi kusikia inapgwa na wapigaji wapo tu si uzalendo
 
Twendeni tu, kila mtu yatamkuta, itafika hatua mtu mwenyewe anatoka nyumbani kwenda kupinga unyonyaji.

HAtupingi kulipa kodi, maisha yaemdane na kodi zetu, tunalipa kodi kisha pesa zinaingia kwa mafisadi, wanakula bata, gari za milioni 400.

Wanatunyonya mnoo, itafika hatua wao wanaenda chooni wanakunya kinyesi, sisi ni povu tu.😂
 
Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Kuna siku moja nilikuwa naongea na jamaa mmoja Mtanzania anakaa Finland siku nyingi sana, kuhusu kodi.

Akawa anasema, Watanzania si kweli kwamba hawapendi kulipa kodi. Watanzania hawapendi kulipa kodi ambazo hawaoni zinachofanya katika maisha yao. Yani kodi wanalipa, halafu zile huduma za kijamii zinazotakiwa kufanywa na hizo kodi hawazioni.

Akasema, Watanzania hawahawa wakienda kukaa nchi kama Finland, wanatozwa kodi kubwa kuliko Tanzania, lakini hawalalamiki.

Kwa nini? Kwa sababu kazi nzuri zipo, mishahara mizuri ipo, na hata kukiwa na kodi kubwa sana, wanaona kabisa kodi zetu zinafanya kazi gani, kuanzia shule nzuri, hospitali nzuri, zenye madawa na huduma tele, madaktari wazuri na wengi, mifuko ya jamii kuhudunia watu wasio na kazi ipo vizuri, wazee wakistaafu wanahudumiwa vizuri, nyumba nzuri, huduma kama zimamoto na ufagizi wa mitaa nzuri, barabara nzuri, takataka zinakusanywa vizuri, maji unapata vizuri, mtu unaona wachukue tu hiyo kodi, maana kazi ya kodi unaiona.

Sasa Tanzania mnaenda kuwaminya mpaka mapumbu kwa kodi hao bodaboda ambao hata kula kwao kwa tabu, halafu kodi zote mnaenda kununua ma VX na kujenga ma Ikulu kedekede, huku hospitali hazina dawa, takataka hamzoi, miji michafu, maji ya shida mpaka mjini, mnategemea vipi watu wafurahie kutozwa kodi?
 
Bodaboda mmesikia hii? Sasa rasmi mtaanza kulipa Kodi. Hapa Serikali mmechemka na mnawaonea Bodaboda, maana kupata 20,000 kwa siku ni kazi kubwa.

----
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa katika mabadiliko ya Sheria za kodi mwaka 2023, serikali imeweka kodi ya mapato kwa wasafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki zenye magurudumu mawili (Bodaboda) ambapo watatakiwa kulipa kiasi cha Sh. 65,000 kwa Mwaka.

Hayo yamesemwa jana na Afisa mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hamad Mterry, wakati akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu.

Mterry amesema kuwa hiyo ni moja ya sheria ya kodi ambayo ni mpya na imewagusa Bodaboda, ambapo watatakiwa kuichagia serikali kiasi cha Sh. 65,000 kwa mwaka, kuanzia mwaka huu wa fedha ambao tayari umeanza tangu Julai Mosi, 2023.

Afisa Mawasiliano na elimu kwa umma kutoka (TRA) Mkoa wa Simiyu, Benjamin John amesema kuwa Bodaboda anaweza kulipa kodi hiyo kwa awamu nne ndani ya mwaka, ambapo kila awamu atatakiwa kulipa Sh. 16,250.

Hata hivyo wafanyabiashara za kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki (Bodaboda) wanaona kodi hiyo inakwenda kuongeza ugumu wa maisha kwao, kutokana na kipato chao cha kila siku kuwa kidogo sana.

“ Ukizingatia kwa sasa kupata Sh. 10,000 kwa siku ni ngumu sana, lakini mafuta yamepanda bei, tunalipa LATRA, tunalipa Bima, bado familia inakutegemea, leo tumeletewa TRA, ukweli kodi hii inakwenda kutuumiza sana,” amesema Ntoni Deus.

My Take
Siungi mkono,Kwa nini pombe na Sigara zisiongezewe Kodi? Rais Samia umegombanishwa na Watu huku.
Na kodi zilizowekwa kwenye mafuta inahesabika wapi, huu sio ubunifuti kwa kutafuta mapato
 
Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
shida sio kulipa Kodi, shida ni matumizi ya hizo Kodi. kuchangia mafisadi kunakera sana hata kama ni mia mbili.

Yesu ni Bwana na Mwokozi
 
Ni sawa kwani serikali kuna wakati waliwa brand kwamba wao (bodaboda)ni ma-Afisa usafirishaji.
Ni sawa walipe kodi kwa maana hata wenzao ma-Afisa ubashiri wanalipa kodi ya asilimia 18 kwa kila mkeka.
Pili, Hawa bodaboda wamekua wakijinasibu kwamba wana maisha mazuri kuliko watumishi wa umma hasa walimu.
Ni hatua stahiki wakilipa kodi.
 
Back
Top Bottom