Tofauti na wachaga, kwanini wakabila mengine hayaendelezi makwao na hawapendi kurudi kwao?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
A. MAENDELEO (Kujenga kwao)

1666445933618.png


Mtu ana mafanikio makubwa huku mjini ana nyumba ya kisasa, gari nzuri, kipato cha uhakika, n.k lakini huko kwao hali ni mbaya, Nyumba imekaa kimasikini mpaka aibu, bati lina kutu,ndani vitanda vimechoka, jikoni sufuria ni za kale, n.k… Huu ni uungwana kweli ? kuna makabila unakuta profesa kasimamisha mjengo kijijini humo ndani lakini ukiangalia hali za mjirani zinatia huruma.

Hakunaga kitu kinaleta baraka kama kusaidia kwenu kwa kupelekea maendeleo, na ndio maana mkoa wakilimanjaro si ajabu ni namba 2 kwa kiwango cha chini cha umasikini,,,, wachaga huwa hawasahau kwao, yani ukifika huko vijijini watu wamejenga,

KURUDI KUSALIMIA NA KUKUTANA

1666446000693.png


Kwenda kusalimia kijijini wengine mwaka mzima unapita hawajarudi ila nauli ipo, hata kwa wale wanaorudi kila moja anaenda kivyake vyake awajumuiki kwa pamoja,,, mwezi huu mjomba, mwezi unaofata, shangazi, mwezi mwengine ba mdogo, mwisho wa mwaka ni kaka, n.k.

wachaga wana utamaduni mzuri, ikifika mwezi wa 12 wachaga wanarudi kwao "KWA PAMOJA", hata waliopo New York, Dubai, London hufanya jitihada kurudi, kukutana ndugu wote ama wengi kwa wakati mmoja kuna umuhimu zaidi kuliko kila mtu akienda kivyake vyake,, Ondoa shaka, si ndugu tu utawakuta bali hata majirani na marafiki
 
Sio kweli punguza ukabila zile za December ni Kik tu watu kibao wanarudi kwao ndo maana watu Wana likizo na wapo wachaga kibao hawarudi haswa waliofeli kimaisha..
 
Kati ya miji michafu hapa Tanzania Moshi inashika nafasi ya kwanza, yaani kamji kako hovyo afadhali hata Njombe wamejitahidi
 
Kina Nshomile mijini wakimiliki gari au nyumba ni fujo mwanzo mwisho kujitamba, vijijini hali ni mbaya

Kagera ndio mkoa wa mwisho kuchangia Pato la Taifa (GDP) na vile vile ni mkoa unaoongoza kwa umasikini, asimilia 31% ya Wakazi wake wanaishi chini ya mstari wa umasikini (hawafikii Matumizi ya TZS 49,320 Kwa Mwezi).


1666444171986.png
 
Sio kweli punguza ukabila zile za December ni Kik tu watu kibao wanarudi kwao ndo maana watu Wana likizo na wapo wachaga kibao hawarudi haswa waliofeli kimaisha..
Ndugu kutoka Mikoa ya nje na nchi za nje wanarudi kwa pamoja kukutana wote vijijini kwao, sidhani kama unajua hata maana ya kiki ..

Wengine hurudi bila mpangilio huwa inakuwa ngumu sana kukutana kwa pamoja, Kwa wachaga ikifika December utawakuta hata marafiki zako na majirani..
 
Ndugu kutoka Mikoa ya nje na nchi za nje wanarudi kwa pamoja kukutana wote vijijini kwao, sidhani kama unajua hata maana ya kiki ..

Wengine hurudi bila mpangilio huwa inauwa ngumu sana kukutana hata na majirani ama marafiki, Kwa wachaga ikifika December utawakuta hata marafiki zako na majirani..
Usiwapangie maana wengine Kuna interval ya likizo ambayo huwezi kupata kwa wakati mmoja kila baada ya miezi nane ...na kingine wale wakristo wanaweza kuomba siku za x-mass kwenda huko ila waislamu haiwezekani ndo maana ile x-mass wanasema ni sherehe ikuwa Bomba huko uchagani kwa sana
 
Back
Top Bottom