Wote wanaotaka kugombea toka CCM kama ni akima Mwandosya na wengineo wote waruhusiwe kuchukua form na kuwe na mjadala kati yao na atakayeonekana anafaaa kuliko mwingine basi apitishwe. Hili la kutoa jina kwamba fulani anafaa mimi siliafiki maana nakumbuka Mwalimu (RIP) alisema Mkapa ndiye aliyemuona anafaa kuwa Rais 1995 yalitokea baada ya hapo wote tunayajua.
Vigezo gani mlivyotumia kufikia conclusion kwamba ndani ya CCM hakuna mbadala wa Kikwete? Hata wanaotaka kugombea hawajapewa nafasi ya kufanya hivyo, tayari nyie mmeshaona kwamba hakuna mwingine ila Kikwete!!! Je mmeenda kwa Sheikh Yahya au kwa Toboa tobo kuweza kufikia conclusion yenu!?
Kikwete kashindwa kupambana na mafisadi ndiyo maana wahusika wote wa ufisadi akina Chenge, Rostam, Idissa Rashid na wengine wengi bado wanapeta uraiani. Huoni Rais ambaye anashindwa kutetea sheria za nchi na kuweka maslahi ya nchi mbele kwamba hafai kuiongoza nchi hiyo maana sheria za nchi zinazidi kukiukwa kila kukicha bila athari yoyote kwa wale wanaokiuka sheria hizo? Wakati umefika wa kutafuta mtu atakayeisafisha CCM na Tanzania kwa ujumla
Kwako wewe ufisadi si kila kitu katika maendeleo lakini inapotokea watu wanaifisadi nchi karibu shilingi Trilioni ($1 billion approximately)moja katika kipindi kifupi na kama ukaguzi wa EPA ungefanywa kuanzia 1995 mpaka 2006 badala ya 2005/2006 basi si ajabu pesa iliyoibwa ingefika hata shilingi Trilioni 2 ($2 billion approximately) , hili ni tatizo kubwa sana kwa nchi yoyote ile inayotaka kupata maendeleo kwa wananchi wake wote, kama wewe unaliona hili ni dogo hiyo ni juu yako. Inapotokea Rais anashindwa kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha wageni badala ya wananchi wake pamoja na kuwa aliahidi kulishughulikia tatizo hilo hii ni dalili nyingine ya kiongozi dhaifu ambaye hastahili tena kurudi madarakani. Je ni akina nani hao uliowasema hapo juu walioshindwa na Kikwete!? Na wameshindwa katika mambo gani!? Na hiyo tathmini iliyomuonyesha Kikwete kawashinda hao ilifanyika lini na wapi!?[/B]
Narudia tena, ndani ya CCM kuna wengi ambao wanaona wana uwezo wa kuiongoza Tanzania vizuri zaidi ukilinganisha na Kikwete. Katiba ya CCM na ya nchi pia zinawaruhusu kugombea nafasi hiyo bila vitisho wala mizengwe toka kwa Malecela, Chiligati, Msekwa au Wazee wa CCM. Hakuna haja ya mimi kutamka kwamba fulani ndiye anayefaa kuwa Rais 2010. Wote wanaotaka kugombea ndani ya CCM waachwe wafanye hivyo na kama baada ya taratibu zote ndani ya CCM kufuatwa na bado ikaonekana Kikwete ndiye anayefaa kuwa mgombea wa CCM basi hapo taratibu za CCM zitakuwa zimefuatwa bila upendeleo wala vitisho dhidi ya wagombea wengine, lakini huu udikteta wa "watakaompinga Kikwete watakiona" na "Wasitumie ufisadi kutaka umaarufu wa kisiasa' Kamwe hilo mimi silikubali. Mambo ya kulinda viongozi dhaifu na mafisadi ni lazima tuyapige vita kwa nguvu zetu zote maana hawa ndiyo tatizo kubwa la nchi yetu kutokuwa na maendeleo ya kuridhisha pamoja na misaada na mikopo chungu nzima tunayopata toka nchi mbali mbali za wafadhili na mashirika ya kimataifa pamoja na rasilimali nyingi tulizojaaliwa na Mungu.