Kinachouma wengi hapa (pamoja na mimi) ni
1. kushindwa kwa kiongozi uliepo madarakani kuleta maendeleo yoyote ambayo aliahidi kwenye uchaguzi uliopita,
2. kushindwa kutekelezwa kwa ilani ya CCM (chama ambacho hata mimi ni mwanachama),
3. kushindwa kutekelezwa kwa sheria sawia kwa watu wote nchini (wezi wadogo kufungwa hata bila kuwepo ushahidi wa kutosha, na wezi wakubwa kutochukuliwa hatua zozote hata kama ushahidi upo),4. kuanza kwa kampeni zenye nia ya kukemea wanaCCM kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Urais (kikatiba) ndani ya chama chao,
5. kuanza kwa kampeni kabla ya wakati (kumpigia chapuo kiongozi aliepo madarakani).
Siamini kuwa kuna mtu mwenye mamlaka ya kukataa mtu yeyote asiteue mtu ampendae. Kinachosumbua ni kuanza mapema uteuzi usio rasmi wenye nia ya kulazimisha (ku-influence) viongozi wengine wote kuunga mkono azimio lisilo la kikatiba, lenye nia ya kudhoofisha haki ya mtu kuchaguliwa. Viongozi wanaotakiwa kuwa na subira hadi wakati muafaka wa kuchagua/kuteua/kupendekeza wameanza mapema mno na hasa kwa kuwafanya wengine wasitumie haki yao kwa ukamilifu. Viongozi wengine wote wanalazimika sasa kuonyesha msimamo wao katika utetezi wa mgombea Urais (watake, wasitake). Madhara yake ni wao kushiriki kwenye kile wasichokiamini.
Kila mtu anaweza kuwa na chaguo lake la mTanzania anaemuona kuwa anafaa kuwa Rais wa nchi. Ila mapenzi yoyote kwa mtu huyo, hayana maana kama mtu huyo hana nia ya kuomba kuwa Rais kwa kufuata taratibu zilizopo (ambazo zimeanza kukiukwa makusudi). Mimi naweza kusema kuwa, ninaamini kuwa naweza kufanya vizuri zaidi ya yaliyofanywa na Rais wetu kwa miaka mitano (5 years). Ninaamini kuwa ninaweza:
1. kutetea na kuilinda sheria ya nchi kwa kuhakikisha kuwa inatumika ipasavyo kwa wote bila kujali tabaka la mhusika
2. Ninaamini kuwa ninaweza kulinda rasilimali za nchi hii zisitumike kufaidisha watu binafsi na kuliacha Taifa likiangamia katika umasikini
3. Ninaamini kuwa nchi ina watu wenye uwezo, nia, na matamanio ya kuwa na hali bora na wako tayari kushirikiana na serikali kufikia malengo yoyote yanayokubalika. Nina uwezo wa kuwashirikisha kufanya hivyo
4. Ninaamini kuwa ninaweza kudumisha/kuendeleza/kuhakikisha uhuru, amani na utulivu unakuwa wa kweli nchini
5. Ninaamini kuwa kila tatizo lina ufumbuzi wake, na ufumbuzi wake ni nia ya kulitatua tatizo hilo kwa vitendo bila subira.
6. Ninaamini kwa dhati kuwa KATIBA ya nchi hii inatakiwa iundwe upya ili kuweka usawa wa kweli kwa kila mtanzania, kuweka mipaka ya utendaji wa mihimili mikuu ya nchi, kuweka demokrasia zaidi, na kuhakikisha utawala bora.
Huu ni uongo mkubwa na aibu kwa Taifa hili. Haiwezekani kufikiria kuwa nchi hii ni masikini wa upeo/uwezo/ujuzi na akili kiasi cha kutokuwa na watu wenye uwezo wa kufanya mambo makubwa kwa Taifa hili zaidi ya JK. Ni kauli inayosikitisha sana.
Ninaamini kuwa ndani ya CCM kuna watu wengi sana ambao wana uwezo wa kufanya mambo mazuri zaidi ya wote uliowataja hapo juu. Watu hao ambao wamedidimizwa wasionekane au hawana nafasi ya kufanya mambo hayo (either kwa kujali amani, utulivu, na hekima) wanafanya hao unaowataja hapo juu waanze sasa kukemea nia ya yeyote kuomba kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania kupitia chama chake.