Bubu ataka Kusema,
Mkuu una kila haki ya kusema Kikwete hakuleta maendeleo yoyote.. Wala hauko peke yako.. Ni imani ambayo hata huko Marekani unakozungumzia wapo watu kibao walichukia Bush aliporudia kipindi cha Pili, Clinton aliporudia kipindi cha Pili inategemea na mtazamo wa kila mtu ktk ujenzi wa Taifa..
Sasa ajabu unatuletea mfano wa Obama, kama vile baadhi ya wanachama wa Domokratik walimpendekeza Kelly arudie kusimama na McCain..Licha ya yote hayo Obama kama situation ingekuwa sawa na yetu nina hakika watu wangependekeza majina ikiwa ni pamoja na Obama kusimama against Kelly..hawa watu wote kina Obama, Clinton, Joe wangesimama na kupinga mfumo huo wakisema wao watapenda kugombea Urais na sifa zao watazitaja..
Hii inakwenda vyama vyote, Chadema wanaweza kumsimamisha tena Mbowe, CUF wakamsimamisha Lipumba, TLP na Mrema bila upinzani inategemea na vyama hivyo vimejipanga vipi..Siwezi kutumia sababu za Mbowe kushindwa uchaguzi ama kukiendeleza chama wakati sina mfano mzuri kama vile Dr. Slaa, Zitto na wengineo..
Unapinga kitu ukiwa na mtu mwenye uwezo zaidi ktk matakwa yako, hupingi kwa sababu unapinga wakati gari halina dereva zaidi yake ukisema tu kila mtu anaweza kuendesha.. Cheo ni dhamana ya chama na wananchi.. sasa chama kimechagua nani dereva wao wewe hutaki, tupe jina la dereva mwingine.. hutaki unatumia mfano wa Obama ambaye tunajua kwanza ilikuwa lazima demokratik wawe na ushindani ndani ya chama kumpata mgombea tofauti naa wakati Bush auClinton walipopendekezwa kugombea awamu ya pili...
Mkuu wangu mjadala huu ni mfano mzuri sana wa fikra zetu sisi wenyewe, dhahiri inaonyesha wazi jinsi tulivyojipanga nyuma ya CCM hata kama tunapinga uongozi wa chama hicho na madudu yake yote..
Moja ya miiko ya chama hicho ni KUTUPANA.. nikiwa na maana KULINDANA ni moja ya maadili ya chama nje ya maandishi..na Kikwete anafanya kama chama kinavyotaka KUKILINDAchama na KULINDA viongozi wake waliobarikiwa kama tulivyomuomba Mungu ktk wimbo wa Taifa..
Sasa mimi nitapenda sana kujua mtu huyo ambaye yuko tayari kukiuka haya maadili ya chama ya kulindana ambaye yuko tayari kuwafikisha Mafisadi wote mahakamani kama atapewa nafasi ya Urais mwaka 2010..navyofahamu mimi viongozi wote wa CCM wamekubaliana swala la kumfikisha Mkapa, Lowassa, au Rostam mahakamani ni kuliweka taifa ktk hatari ya kudhoofisha usalama wa taifa... sasa wewe nambie nani ambaye anaamini tofauti na wazo hilo kwani kinacvhogomba hapa ni sisi wote kuamini kwamba JK ameshindwa kuwafikisha mahakamani Mafisadi kwa sababu anakilinda chama badala ya maslahi ya Taifa..
Mkuu there is a thin line between LOVE and HATE, unapoona wewe na kuchukia kwamba JK ameshindwa, hafai na kadhalika, wanachama wanaona JK ameweza kukilinda na kuinusuru nchi toka machafuko ya kisiasa..tena kuna baadhi wanamwona amekuwa soft kuwafikisha mahakamani baadhi ya viongozi au kuachia magazeti kuwazungumzia viongozi waliobarikiwa..Kwa mtazamo wao watu kama wewe are Hater!...na Kikwete hakutakiwa kuwasikiliza, wakati wewe unafikiria kufanya hivyo na zaidi ni kutokana na mapenzi ya nchi yako..
Kwa nini nguvu zako usiziweke kwa Wapinzani!.. hata kamaKikwete atasimama against watu kama Mwakyembe au Lau Masha..nadhani muhimu pia utazame uwezekano wa watu hawa kutuongoza vizuri kwa sababu sio swala la katiba ya chama kutazama maslahi ya Taifa isipokuwa chaguo lako ndilo litatazama maslahi ya taifa. Huyo Mwakyembe , Masha na wengine wote wamesimama upande wa Mafisadi,sasa wanapoweka ushindani ndani ya chama itakusaidia nini wewe zaidi ya kuona utaratibu unaopendekeza wewe umefanyika..Utaratibu ambao won't change maisha ya mwananchi..