Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 46
😀 😀
Ukisikia umbeya ndio kama hivyo
Na ukisikia ushambenga ndio huu! Uanaume kama...
Asha
😀 😀
Ukisikia umbeya ndio kama hivyo
Mpango Mkakati kamili hauko kwenye website ya chama, huo ni muktasari tu wa maeneo ya juu kwa ajili ya umma wa wanachama. Mpango Mzima ni siri.
Jiunge na CHADEMA utapata hayo kwenye vikao vya ndani.
Haya hebu tupe japo kwa ufupi Strategic Plan ya vyama vingine tulinganishe na CHADEMA.
Halafu mbona waliokupongeza wote ni wanaCCM tu waliojitambulisha humu JF? Inaelekea maoni yako yamewakuna sana wenzako eeehhhhh
Asha ikiwa wewe uliendani ya Chadema..hujapewa..itakuwa mwanachama Mpya?...au kusubiri makapi ya CCM akina Mwita muyachukue!!!..... Hata sisi kwenye mafunzo ya Zanzibar hatukupewa mpango mzima lakini nyaraka tuliyowepewa ilikuwa na SWOT, Objectives, Stakeholders na Targets za CHADEMA za mwaka 2010. Sasa hizi ni silaha za ushindi haziwezi kumwagwa hadharani wewe. Jiunge na CHADEMA utapata hayo kwenye vikao vya ndani.
Asha
Mrema ndio mnafiki zaidi dhidi ya CHADEMA:
a. Aliahidi kwenda Kiteto kuunga mkono CHADEMA, hakwenda aliishia DSM. Chaguzi za CUF zote huenda mwenyewe
b. Tarime, Mrema aliunga mkono NCCR Mageuzi. Kwanini hakuunga mkono CHADEMA iliyokuwa na nguvu zaidi?
c. Huyu ndiye aliyeshiriki kusema Mbowe alimuua Wangwe, na naibu katibu Mkuu wake akaandika barua kwa IGP kuwa Mbowe alifanya sherehe Afrika Kusini. Mrema akamsifu kwa barua hiyo
Kwa ujumla ni hasira zake kwa Mbowe na CHADEMA kwa kuchukua nafasi ambayo yeye na TLP walikuwa nayo katika siasa za Tanzania.
Hivi kwanini vyama vyote vinaishambulia CHADEMA jamani? Ina nini cha pekee, CCM, CUF,TLP, NCCR nk
Asha
FMES,
Mkuu wajishushe mara ngapi?...Chadema tayari wamekwisha bugia sumu ya wale waliotaka kuibomoa... Na trust me, acha watu waseme wanavyotaka lakini ukweli ni kwamba Chadema, CUF na TLP wote hawana tena nguvu iliyojengwa mwanzoni..
huo sasa uwe ndo mwendo wa kukuza demokrasia kwa wapinzani wetu.Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustino Mrema ambaye ameombwa kugombea ubunge Jimbo la Vunjo lililopo mkoani Kilimanjaro mwaka 2010 amekubali kugombea nafasi hiyo ikiwa atatakiwa hivyo na Mkutano Mkuu wa Chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya kumwandikia barua Mrema ya kumtaka kugombea jimbo hilo, aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo kati ya mwaka 2000 na 2005, Jesse Makundi alisema kuwa ameandika barua hiyo Februari 8 mwaka huu na kuikabidhi jana kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Komba ili amkabidhi Mrema.
Alisema lengo la kumwomba kugombea nafasi hiyo, ni kutokana na mgawanyiko wa vyama vya upinzani ambao wameshajipanga kugombea jimbo hilo hali inayoonekana itaifanya CCM kupata ushindi jimboni humo.
Tayari Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ameshatangaza kugombea jimbo hilo na kwa mujibu wa Makundi, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema, Susan Lyimo atagombea jimbo hilo mwaka 2010.
Kwa upande wake, Mrema aliliambia gazeti hili jana kwa njia ya simu akiwa mkoani Kilimanjaro kuwa yupo tayari kugombea nafasi hiyo ikiwa atapitishwa na Mkutano Mkuu wa Chama chake.
"Hilo jambo kubwa inabidi Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu waangalie hali ya siasa nchini na baadaye Mkutano Mkuu utatoa uamuzi kama nigombee au nisigombee nafasi hiyo, mimi nitatekeleza maamuzi ya Mkutano Mkuu" alisema Mrema.
Akitoa sababu za kumtaka Mrema agombee nafasi hiyo, Makundi alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuona katika jimbo hilo anahitajika mtu mwenye nguvu kisiasa ambaye ni tishio kwa CCM na mpambanaji asiyekata tamaa.
Mrema atakuwa Mwenyekiti wa nne kugombea nafasi ya ubunge. Tayari Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameshatangaza kugombea Jimbo la Hai, Mbatia atagombea Vunjo na kwa sasa Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo ni Mbunge wa Bariadi Mashariki.
Source:Habari leo
Ni wazo zuri, wapinzani wakifanikiwa kuongeza wabunge na madiwani ni mwanzo mzuri wa kujitangaza. Na kwa kuwa bunge ndio linalotunga sheria, itakuwa rahisi kwao kupigania yaliyo muhimu kwa demokrasia, kama katiba ambayo itatupeleka kwa tume ya uchaguzi iliyo huru.