Ni vigumu Mrema kuacha siasa kwani yeye ni pandikizi la chama tawala,Mie nawaeleza leo CCM ikipigwa mwereka mtaona kama Mrema atangangania tena siasa.
Payroll ya Mrema bado iko serikalini panga pangua Mzee huyu anataka ale pensheni yake kiulaini.Ni mpinzani gani kila mara anazua mitafaruku ndani ya upinzani pamoja na kuhakikisha kuwa Muungano wa upinzani haufanikiwi kwa jinsi yoyote ile.Ni hukumu gani kati ya kesi zote alizonazo Mrema mahakamani aliwahi kushindwa?Hivi watanzania hatuelewi nini katika hili la Augostine Lyatonga Mrema?
Leo anarudi jimboni kwake akawachanganye wananchi wamchague.Hakika kuna somo twapaswa kujifunza kuliko kudhani kuwa huyu Bwana ajipumzikie!!!
Kama kuna kazi kubwa aliyowahi kuifanya katika historia ya chama chake ni pale alipohakikisha kuwa Bwana Benjamen William Mkapa anaingia Ikulu akisaidiana na Marehemu Mwalimu Nyerere.Mkapa alikuwa hafaahamiki vizuri kwa wananchi pia uwezo wake haukujulikana kuwa angeweza kuingoza nchi hii .Mwalimu ndiye alijua siri hiyo.Mrema alitumika kama chombo cha kuhakikisha Mkapa anaingia Ikulu.JAMBO LILOWEZEKANA!
Sasa Mrema katulia tuli baada ya kuona Kikwete anakubalika kiurahisi hasa wakati wa kampeni.Leo hii Mrema anajitokeza kutaka kurudi actively kwenye sias a baada ya kuona mwelekeo wa CCM unaenda mrama.Anataka tena kututosa tumchague JK ili CCM iendelee kupeta tena.MREMA ACHA MAMBO HAYA!!!!
Kimatire hapo umenigusa.
Ndugu yangu huyu jamaa alipelekwa upinzani kwa makusudi mazima.
Alitakiwa aibue vipaji na wale wote ambao ni wapinzani wa kweli.
Kati ya aliowaibua ni akina Masumbuko Lamwai na baadhi ya maafisa wa polisi na marehemu Kombe akiwemo. Kombe akiwa usalama wa taifa kama alivyo Lyatonga alikuwa akivujisha siri na kuwafanya wapinzani wapate updated issues toka serikalini, walimfanya nini? Wote tunajua,,,,, kamwe huwezi kumlinganisha Kombe na White Sambuo, Hilo haliingii akilini.
Masumbuko, kijana msomi wa pale chuo kikuu akajitosa kwenye ukombozi wa nchi hii bila kujijua kuwa anajiangamiza. Alikuwa na potential ya upinzani wa kweli. Akawachemsha kweli,,, ni nani asiyejua yaliyompata. Aliachishwa kazi pale mlimani, akajichimbia kwenye uwakili,,,, wakamfutia leseni akakimbilia Zanzibar,,, wakamwambia kuwa nako ni Tanzania,,, akarudi Kimara kufuga. Baadhi ya wazee wakamshauri arudi CCM na alipofanya hivyo mambo yakamnyookea,,,, nani anabisha.
Hali kadhalika yule bwana Nyaucho, kijana wa usalama wa Taifa hili baada ya kuubomoa upinzani yuko wapi? Anakula kuku baada ya kuteuliwa na CCM kuwa mbunge wa Africa Mashariki,,,,, Uongo?
Tunakula nao humuhumu ndugu zangu,,,,,
Mrema keshasema hana mpango wa kugombea Uraisi wa Tanzania anarudi kugombea ubunge huko Kiraracha kwake,,,, kuna akina Aloyce Kimaro huko wanagusa mambo ya wazee ni lazima waondoke!
Mrema ni msanii mzuri sana anaweza kuwafanya ndugu zangu Wachaga wakacheza mbasa (ngoma ya kichagga)na kumchagua tena kuwa mbunge wao.
Tusubiri anakuja na episode gani tena.
Aika Mangi