The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Ndiyo maana nikasema Mrema anatakiwa agombee sehemu neutral kama Dr au Arusha hata Mbatia pia kwa sababu siasa zao ni za juu ya majimbo.Huko wangemuacha Suzan Lyimo na mgombea wa CCM. Wakigombea Dar au Arusha wanaongeza chance za kuwa na viti vingi zaidi Bungeni na pia majimbo ya Dar hayana watu kutoka upinzani.So very powerful politicians ndiyo wanahitajika frm opposition.

Apo umenena Ben.Tatizo wana social capital waliyokuwa nayo miaka ya 90 especially kwa Dar? Mrema akigombea Temeke watamkubali tena?
 
Ndiyo maana nikasema Mrema anatakiwa agombee sehemu neutral kama Dr au Arusha hata Mbatia pia kwa sababu siasa zao ni za juu ya majimbo.Huko wangemuacha Suzan Lyimo na mgombea wa CCM. Wakigombea Dar au Arusha wanaongeza chance za kuwa na viti vingi zaidi Bungeni na pia majimbo ya Dar hayana watu kutoka upinzani.So very powerful politicians ndiyo wanahitajika frm opposition.

Umenena vyema Ben, Hawa kina Mbowe, Mrema, Lipumba ni watu wanao takiwa kuchukua majimbo yote ya mjini kwani watu wana uelewa na wakiwaelimisha kwamba wanataka kwenda liamusha bunge kuacha kuwa rubber stamp ya kupitisha ma buzwagi watapata!, Labda kama sheria zina wabana wasigombee huko, Mrema arudi kwake Temeke!
 
Kila la heri mzee wa Kiraracha. Ila nina wasiwasi kama atapata ubunge Vunjo. Kweli tunapenda bunge lichangamke kwa upinzani ila tukitaka kupata hivyo viti ni lazima tuwe makini na cadidates wapinzani wanapitisha kwa ajili ya kupigiwa kura na wananchi. Sijui nyie mnaotoka Vunjo mnasemaje, maamuzi yapo mikononi mwenu.
 
Ata mimi nampa Mrema Kura yangu.. tunaitaji watu kama yeye bungeni. Mr Mrema akiongezeka itakuwa a blessing news to Tanzania.. Huyu ni mtu mmoja ambaye aogopi CCM wala Mafisadi. Watanzania si mnajua Historia ya huu mzee? hata kama CCM wataiba kula 2010 za uraisi kuwepo kwa wabunge wakali kali itakuwa chimbuko la mabadiliko na haki wasa kwa wote ata sisi masikini

Just imagine for a second Michango bungeni kutoka kwa dr slaa, kobwe na Mrema..

Mungu ibariki Tanzania
 
Hawa ndugu zetu walishaambiwa na Nyerere na wengineo, siku nyingi kuwa wajikusanye huko bungeni wakaona wanaowaambia hivyo wanawachukia. Kila mmoja akangang'ania uraisi wakithani CCM watauachia kiurahisi.

Angalau sasa wamefunguka macho, lakini nafikiri ni baada ya kuona umaarufu wa Zitto na Dr. Slaa umepanda mara-dufu ndani na nje ya bunge. Hata hivyo good lucky guys.
 
Wazo zuri ili kuongeza nguvu Bungeni. Lipumba na Mbowe nao wakagombee ubunge majimboni kwao maana wote sio watu wa kushinda uraisi.

Sidhani kama Lipumba anahitaji kugombea Ubunge kwa stage aliofikia si wa kugombea ubunge ,yeye ni mtu mkubwa sana ukilinganisha na wanaogombea ubunge.Ila kama anataka ubunge tutampeleka Pemba akagombee.
 
Ila naona Mrema ameshazeeka sii yule wa 1995!

Si bora awaachie vijana?

Vijana hawapo?
 
Kuna uzuri gani katika hili? Mrema, Suzan na Mbatia wagombee alongside mgombea wa CCM! Si kuipa ushidni CCM bila jasho jingi! Inachotakiwa waelewane kabla kuwa wanamwachia mmoja wao na hakuna kuhujumiana

That's so right, wakigombea wote kura zitagawanyika hivyo CCM itashinda kirahisi simple mathematics
 
Naamini watu wa Vunjo kwa sasa sio wakati muafaka kwa Jimbo lao kuwa sehemu ya wastaafu , kwani wako vijana wengi huko wenye uwezo wa kuwawakilisha , ila Mrema anapaswa kuwa mshauri na sio kutaka kungangania mpaka afie Jimboni kama Kinyata .

Mrema , kama sio mroho wa madaraka anapaswa kuwashauri vijana waingie front .
 
Wapinzania muwe makini mnaweza kuchezewa mkajikuta mnaitengenezea CCM njia kwa kupingana wenyewe,ni muhimu mkubaliane katika kugombea,wenyeviti wa vyama wagombee ubunge urais wawaachie wengine kama Dr.Slaa na Hamad Rashid.Kuhusu Mrema yeye abaki mshauri kwani ameshachoka hataweza mikiki ya ubunge.
 
Excellency, it is good for him and other leaders to go back to their provinces to build their voting base to their provinces and to join effort into the house of parliament so that some bills in favour to them are jointly passed, this will assist them in 2015.
 
Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema amesema amesoma alama za nyakati na kuona kwamba ipo haja ya kuachana na siasa za kugombea urais na badala yake ameamua kuwania ubunge katika Jimbo `lake` la Vunjo katika Uchaguzi Mkuu mwakani.

Hata hivyo, alisema uamuzi huo ambao ameuchukua baada ya kuombwa na kusumbuliwa kila mara, lazima upitishwe na vikao vya TLP.

Mbali na Mrema, kuna kila dalili kwamba viongozi wa Wakuu wa Vyama vya upinzani nchini, wameamua kukacha kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu ujao kama ilivyozoeleka, na badala yake wamepanga kugombea ubunge.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi na baadaye kuhojiana na viongozi hao, umeonyesha kwamba safari hii wapinzani wamepania kuwekeza nguvu zao katika ubunge.

Lengo la kufanya hivyo ni kutaka kupata viti vingi bungeni ili kuongeza upinzani katika chombo hicho cha kutunga sheria na mhimili muhimu.

Mrema, ambaye mwaka 1995, alishauriwa na Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere awanie ubunge badala ya urais, sasa amesema amekubali wito huo.

Mrema ambaye amegombea urais mara tatu bila mafanikio, alisema hatua hiyo inazingatia zaidi matakwa ya Watanzania na wanachama wa TLP. Alifafanua kwamba amekuwa mtumishi wa umma miaka yote hivyo kila wakati analenga kufanya jambo ambalo litakuwa na faida kwa watu wengine na si kwake binafsi.

Hata hivyo, alisema japokuwa suala hilo (la kuachana na kugombea urais) ameliridhia, lakini lazima liamuliwe na mkutano Mkuu wa TLP unaotarajia kufanyika mapema Aprili, mwaka huu.

Mrema alisema suala la kugombea ubunge hakuwa nalo ila ameombwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo 2000- 2005 Meja Jesse Makundi.

Alipoulizwa kama anaweza kushinda ubunge Jimbo la Vunjo, alisema mgombea wa TLP mwaka 2005, alipata zaidi ya kura 26,000, Chadema 8,000 na NCCR- Mageuzi kura 6,000.

Alisema kura hizo zikijumlishwa zinapita zile za mgombea wa CCM aliyeshinda kwa kura 30,000.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, Mrema aligombea kupitia NCCR-Mageuzi na kushika nafasi ya pili kwa kupata kura milioni 1.8 nyuma ya Benjamin Mkapa wa CCM.

Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000, Mrema aligombea kupitia TLP na kushika nafasi ya tatu kwa kupata kura 600,000 nyuma ya Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyeshika nafasi ya pili na Mkapa aliyeshika nafasi ya kwanza.

Chati ya Mrema iliporomoka katika uchaguzi wa mwaka 2005 baada ya kushika nafasi ya nne kwa kupata kura 80,000 nyuma ya Freeman Mbowe wa Chadema, aliyeshika nafasi ya tatu, Profesa Lipumba aliyeshika nafasi ya pili na Rais Jakaya Kikwete aliyeongoza.

Alisifu hekima za Meja Makundi na kusisitiza kwamba bila TLP kusimama `Buldoza` kuna hatari jimbo hilo likaendelea kushikiliwa na CCM na `washirika wake`.

Habari za ndani kutoka kwa vyama hivyo zinasema hatua hiyo ya viongozi wa upinzani, (ya kugombea urais kila mara) ambayo ilikuwa ikilalamikiwa mno, inalenga kujiimarisha ili kuweza kuchukua nchi mwaka 2015.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam juzi, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe, alisema suala la chama hicho kusimamisha au kutosimamisha mgombea urais, litategemea maamuzi ya wanachama ambayo yatazingatia maoni ya Watanzania walio wengi.

Alisema Chadema hakipo kwa ajili ya maslahi ya mtu au kikundi kimoja, bali kwa ajili ya Watanzania wote, hivyo mikakati yake ya kisiasa na uamuzi, lazima ufuate matwaka ya wananchi.

Alipoulizwa kama suala la kuacha kuwania urais na kugombea ubunge Jimbo la Hai kama inavyosema lina maslahi kwa Taifa, Mbowe alikubali.

Japokuwa hakuwa tayari kukanusha au kukubali, Mbowe alisema yupo tayari kugombea nafasi yoyote atakayoteuliwa na chama hata kama ni ubunge.

Kuna habari kwamba Mbowe amejipanga kuwania ubunge katika Jimbo la Hai, ambalo alipata kuliwakilisha mwaka 2000 hadi 2005, alipogombea urais na kushindwa.

Kwa upande wa NCCR-Mageuzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho, Faustine Sungura alisema kwa utamaduni wa kwao, si lazima Mwenyekiti wao James Mbatia awanie urais.

Ili kuondoa msuguano kati yake na Mrema, Mbatia ambaye pia ni mzaliwa wa Vunjo, inasemekana anapanga kugombea ubunge Jimbo la Kawe, jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, japokuwa Mbatia hakupatikana kuzungumzia suala hilo, Sungura alisema ni haki ya kiongozi huyo kugombea mahali anapotaka.

Naye Mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba hakupatikana kuzungumzia jambo hilo baada ya wasaidizi wake kueleza kwamba alikuwa anashughulikia kusafirisha wajumbe waliokuja jijini kuhudhuria Mkutano Mkuu wa chama hicho uliomalizika juzi.

SOURCE: Nipashe
 
Mwaka 1995 Baba wa Taifa alaimshauri Mrema akagombee Ubunge badala ya Urais akakataa. Machungu sasa anajuta. Pengine nyota yake ingeng'ara zaidi akiwa Bungeni.

Vivyo hivyo, mimi kama Mtoto wa Taifa, namshauri ahachane na siasa (astaafu mambo ya siasa) mwaka 2010. Simshauri hata akagombee ubunge kama kweli amesoma alama za nyakati. Otherwise he his not srious.
 
MWENYEKITI wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Agustino Mrema amesema baadhi ya wagombea ambao wamedai kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho hawana historia yoyote ya chama hicho hivyo kushinda nafasi hiyo ni ndoto.

Mrema aliyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa Nifahamishe ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Alisema amekuwa akisikia kupitia vyombo vya habari kuwa wapo watu ambao wametangaza nia ya kugombea nafasi hiyo ya Uenyekiti lakini ukweli utabakia pale pale kuwa hamna zaidi ya Mrema.

Mwenyekiti huyo wa TLP alisema watu kujitokeza kugombea nafasi yoyote ni haki yao ya msingi na ndiyo demokrasi ya kweli lakini wagombea hao watakuwa wasindikizaji.

Mrema alisema pamoja na kuwa suala la wao kugombea nafasi ni haki yao ya msingi wajumbe wa mkutano huo ndio wataweza kutoa maamuzi juu ya nani anafaa kuwaongoza hivyo anawaachia wao waamue.

Alisema katika uchaguzi huo ambao unatarajiwa kufanyika Aprili 19 jijini Dar es Salaam anaamini kuwa wajumbe wa chama hicho watakuwa makini ili kukiendelezea chama na sio kukiweka rehani.

"Ni kesho kutwa Aprili 19 jibu litapatikana na hao wote ambao wanadai kuwa wana uwezo wa kushindana na mimi wataona matokeo," alisema.

Source: Nifahamishe.com
 
"Alisema amekuwa akisikia kupitia vyombo vya habari kuwa wapo watu ambao wametangaza nia ya kugombea nafasi hiyo ya Uenyekiti lakini ukweli utabakia pale pale kuwa hamna zaidi ya Mrema.[/B]"

Sultani Augustino Lyatonga Mrema, atafute ajira nyingine yakumpa kula yake maana huku kwenye siasa kesha choka.
 
Last edited:
Mzee Mrema apumzike sasa, keshachoka kwenye siasa!!
 
Ni vigumu Mrema kuacha siasa kwani yeye ni pandikizi la chama tawala,Mie nawaeleza leo CCM ikipigwa mwereka mtaona kama Mrema atangangania tena siasa.
Payroll ya Mrema bado iko serikalini panga pangua Mzee huyu anataka ale pensheni yake kiulaini.Ni mpinzani gani kila mara anazua mitafaruku ndani ya upinzani pamoja na kuhakikisha kuwa Muungano wa upinzani haufanikiwi kwa jinsi yoyote ile.Ni hukumu gani kati ya kesi zote alizonazo Mrema mahakamani aliwahi kushindwa?Hivi watanzania hatuelewi nini katika hili la Augostine Lyatonga Mrema?
Leo anarudi jimboni kwake akawachanganye wananchi wamchague.Hakika kuna somo twapaswa kujifunza kuliko kudhani kuwa huyu Bwana ajipumzikie!!!
Kama kuna kazi kubwa aliyowahi kuifanya katika historia ya chama chake ni pale alipohakikisha kuwa Bwana Benjamen William Mkapa anaingia Ikulu akisaidiana na Marehemu Mwalimu Nyerere.Mkapa alikuwa hafaahamiki vizuri kwa wananchi pia uwezo wake haukujulikana kuwa angeweza kuingoza nchi hii .Mwalimu ndiye alijua siri hiyo.Mrema alitumika kama chombo cha kuhakikisha Mkapa anaingia Ikulu.JAMBO LILOWEZEKANA!
Sasa Mrema katulia tuli baada ya kuona Kikwete anakubalika kiurahisi hasa wakati wa kampeni.Leo hii Mrema anajitokeza kutaka kurudi actively kwenye sias a baada ya kuona mwelekeo wa CCM unaenda mrama.Anataka tena kututosa tumchague JK ili CCM iendelee kupeta tena.MREMA ACHA MAMBO HAYA!!!!
 
Ni vigumu Mrema kuacha siasa kwani yeye ni pandikizi la chama tawala,Mie nawaeleza leo CCM ikipigwa mwereka mtaona kama Mrema atangangania tena siasa.
Payroll ya Mrema bado iko serikalini panga pangua Mzee huyu anataka ale pensheni yake kiulaini.Ni mpinzani gani kila mara anazua mitafaruku ndani ya upinzani pamoja na kuhakikisha kuwa Muungano wa upinzani haufanikiwi kwa jinsi yoyote ile.Ni hukumu gani kati ya kesi zote alizonazo Mrema mahakamani aliwahi kushindwa?Hivi watanzania hatuelewi nini katika hili la Augostine Lyatonga Mrema?
Leo anarudi jimboni kwake akawachanganye wananchi wamchague.Hakika kuna somo twapaswa kujifunza kuliko kudhani kuwa huyu Bwana ajipumzikie!!!
Kama kuna kazi kubwa aliyowahi kuifanya katika historia ya chama chake ni pale alipohakikisha kuwa Bwana Benjamen William Mkapa anaingia Ikulu akisaidiana na Marehemu Mwalimu Nyerere.Mkapa alikuwa hafaahamiki vizuri kwa wananchi pia uwezo wake haukujulikana kuwa angeweza kuingoza nchi hii .Mwalimu ndiye alijua siri hiyo.Mrema alitumika kama chombo cha kuhakikisha Mkapa anaingia Ikulu.JAMBO LILOWEZEKANA!
Sasa Mrema katulia tuli baada ya kuona Kikwete anakubalika kiurahisi hasa wakati wa kampeni.Leo hii Mrema anajitokeza kutaka kurudi actively kwenye sias a baada ya kuona mwelekeo wa CCM unaenda mrama.Anataka tena kututosa tumchague JK ili CCM iendelee kupeta tena.MREMA ACHA MAMBO HAYA!!!!

It is very possible Kimatire. Ukijaribu kufuatilia trend nzima ya huyu mzee, utatambua kuna doubt kuwa kwake upinzani. Kimsingi hana mawazo mapya, for the past 15 years ame-prove kuwa mchonganishi tu. Lets get rid of him kwa kumnyima huo uenyekiti na ubunge moshi tuone ana akili gani zaidi za kimapinduzi.
 
Back
Top Bottom