Mag3,
As a politician I believe Mrema is a man who's time has come and gone. Tanzania tunahitaji uongozi unao "inspire" si kupikapika majungu tu. We have so much to learn from the Obama phenomenon.
Umemaliza, asante sana kwa ukweli.
Mag3,
As a politician I believe Mrema is a man who's time has come and gone. Tanzania tunahitaji uongozi unao "inspire" si kupikapika majungu tu. We have so much to learn from the Obama phenomenon.
Haya mambo ya Mrema niliyaeleza toka mwaka jana, watu humu wanakinishambulia sana!
PM
Hii inaitwa 'Controlled Democracy'Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema ameitisha kikao cha ghafla cha NEC ya chama hicho na kumtimua kwenye chama hasimu wake na mshindani wake katika nafasi ya uenyekiti ya chama hicho, Benedict Mutungirehi. Awali kikao hicho cha Halmashauri kuu kilipangwa kufanyika tarehe 18 Aprili siku moja kabla ya mkutano mkuu wa chama hicho, lakini Mrema akameitisha jana na leo kikao cha dharura na kuwalipia wajumbe gharama zote yeye mwenyewe kwa fedha za mfukoni. Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe 60 bila kuwa na ajenda nyingine yoyote Mrema alitumia fursa hiyo pia kutangaza maandalizi ya mkutano mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Aprili katika ukumbi ambao mpaka sasa ni siri. Mrema aliwatangazia wajumbe kuwa msajili wa vyama vya siasa amekubali kwamba chama hicho kinaweza kupunguza wajumbe wa mkutano huo kutoka 1407 wanaopaswa kufkisha akidi kwa mujibu wa katiba ya chama hicho mpaka wajumbe 163 ambayo ilipunguzwa kwa azimio la kikao cha Halmashauri kuu ya chama hicho.
...........ndiyohiyo
Huyu Mzee arudi kwao Moshi akagombee ubunge huu uongozi awaachie vijana
Jamani mimi nikifikiri zaidi ya hapo naona hizi ndizo siasa za nchi yetu, hivi kiujumla kunatofauti gani alichofanya Mrema na kauli za wana CCCM "2010 ni Kikwete tu!, Mwacheni JK amalizie miaka yake 10!, Ataempinga Kikwete 2010 kukiona!" na matakataka mengi tu!?
Hamna tofauti, hakuna demokrasia ya kweli kwenye vyama vyetu, na hii ndiyo inatuletea 'watawala wabovu' nchini kwetu.