Nafikiri siyo kweli anayosema ndg yangu Mrema mbona ulikiacha NCCR-MageuziMwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema amekiri, kwamba Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kina utaratibu mzuri wa kuandaa wagombea wake katika nyadhifa za juu ukiwamo urais. Mrema alisema hayo jana kwenye mahojiano katika kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) .
Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, suala la mtafaruku ndani ya TLP, si la yeye kungangania madaraka, bali inapokuwa chama hakijaandaa mgombea madhubuti atakayeweza kuwa mtetezi mkubwa wa chama hicho, ndipo suala hilo linapojitokeza.
Watu wanaandaliwa, kama watu wa CCM, unawasikia kuwa mwaka 2010 ni Kikwete tu, wana utaratibu wanaandaa, hawaendi kiholela ili mradi tu umechukua fomu sijui nani na wanajua kazi aliyofanya Kikwete na wameridhika, alisema Mrema na kuongeza: Wao wanafikiri kwamba si kazi ya kubughudhi tena kwa sasa wanatamka hivyo na kwa jambo hilo huwezi kusema hiyo si demokrasia ama huo ni udikteka, alisema Mrema.
Alishangazwa kuona wakati CCM ikijipanga vizuri namna ya kuachiana madaraka, vyama vya Upinzani hususan chama chake, jambo hilo ni tofauti kiasi cha kufikia kuwapo mtafaruku mkubwa wa kuwania madaraka. Hata hivyo alisema, hanganganii madaraka ya kuwa mwenyekiti wa chama hicho, bali hakuna mwanachama madhubuti kwa sasa aliyeandaliwa kukiongoza vyema chama hicho. Akiandaliwa mtu sawa nimewaambia Halmashauri Kuu ya Chama, kwamba singanganii uenyekiti watu wanaandaliwa kushika nyadhifa hizi, alisema Mrema na kuongeza:
Mnataka Mrema aondoke haondoki mtu mpaka chama hiki kijengwe na nijue nitamwachia nani, siwezi kukiacha chama changu barabarani, haiwezekani. Akizungumzia nia yake ya kugombea ubunge mwakani Moshi Vijijini kwa tiketi ya TLP, alisema atafanya hivyo kutokana na kuombwa na wananchi wa jimbo hilo. Hivi sasa Moshi Vijijini inawakilishwa na Dk. Cyril Chami wa CCM ambaye pia ni Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.
.......ndiyohiyo
hata TLP unaweza kuacha/stepdown uwaachie wengine waongoze kisha nyie wazee wa siku nyingi muwe washauri wa vijana/damu mpya.