MWENYEKITI wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augostine Mrema amekituhumu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai kuwa kinahusika na vurugu zinazotokea katika chama chake.
Mrema aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kurejesha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho.
Alidai kuwa Chadema kimekuwa kikiwatumia wagombea wenzake wa nafasi ya uenyekiti na wapambe wao na kwa kusambaza taarifa chafu dhidi yake kwasababu wamesikia kuwa anataka kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo.
Hata Makamba anavyosema nyinyi vyama vinne ni sawasawa na mapaka yaliyofungwa mikia ni kweli kabisa,alisema Mrema.
Mwenyekiti huyo jana aliwaonyesha waandishi wa habari kadi za Chadema ambazo anadai kuwa zilipelekwa kwa wanachama wake ngazi ya vitongoji na vijiji ili wakihame chama cha TLP.
Sasa huu ni upinzani gani ninazo kadi za Chadema zaidi ya 150 ambazo zilipelekwa kwa wanachama wangu na kadi hizi wala hazijaandikwa chochote,alisisitiza Mrema.
Alisema pia Katibu Mkuu wa chama hicho katika mkoa wa Kilimanjaro aliitwa na wagombea hao ili awape namba yake ya akaunti wamuingizie hela endapo atafanikisha kuwachagua.
Alisema kuwa mkutano mkuu wa chama hicho utafanyika kama ulivyopangwa Aprili 19 na kwamba wajumbe 763 ndio watakaohudhuria badala ya 1,704 kwasababu chama hicho hakina hela za kutosha.
Alisema kwasasa chama hicho kinapata ruzuku ya Sh 2.4 milioni kila mwezi na kwamba kuwaita wajumbe wote 1,407 kwa siku tatu gharama yake ni Sh 250 milioni fedha ambazo hawana.
Akizungumzia wagombea wenzake wa nafasi ya uenyekiti Benedict Mutungirei na Joram Kinanda, Mrema alisema wao hawawanyanyasi bali kinachotokea ni uhuni kwani wagombea hao hawakuwahi kuomba kutumia ofisi ya chama hicho kuzungumza na waandishi wa habari.
Siombi radhi na nitamsaidia Rais Kikwete kupambana na rushwa kwa kumshughulikia Kinanda kwasababu amekuwa mla rushwa mkubwa,alisema Mrema.
Alisema pia mkutano mkuu wa chama hicho ndio utaamua kama yeye agombee urais mwakani au agombee ubunge.
Hali ilikuwa shwari katika makao makuu ya chama hicho wakati Mrema alipokuwa akirejesha fomu na kuzungumza na waandishi wa habari tofauti na siku nyingine, ambapo kulitokea vurugu wakati wagombea wengine walipokuwa wakirejesha fomu.
my take;
Lyatonga hayuko kwenye siasa kwa ajili ya kutimiza majukumu ya wananchi bali yeye yuko kwa ajili ya masilahi anayoyajua yeye, ndio maana hayuko tayari kuondoka na kuacha chama mikononi mwa vijana ambao wamejitokeza ili kumsaidia katika kukiendesha chama na kukijenga.
Mrema aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kurejesha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho.
Alidai kuwa Chadema kimekuwa kikiwatumia wagombea wenzake wa nafasi ya uenyekiti na wapambe wao na kwa kusambaza taarifa chafu dhidi yake kwasababu wamesikia kuwa anataka kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo.
Hata Makamba anavyosema nyinyi vyama vinne ni sawasawa na mapaka yaliyofungwa mikia ni kweli kabisa,alisema Mrema.
Mwenyekiti huyo jana aliwaonyesha waandishi wa habari kadi za Chadema ambazo anadai kuwa zilipelekwa kwa wanachama wake ngazi ya vitongoji na vijiji ili wakihame chama cha TLP.
Sasa huu ni upinzani gani ninazo kadi za Chadema zaidi ya 150 ambazo zilipelekwa kwa wanachama wangu na kadi hizi wala hazijaandikwa chochote,alisisitiza Mrema.
Alisema pia Katibu Mkuu wa chama hicho katika mkoa wa Kilimanjaro aliitwa na wagombea hao ili awape namba yake ya akaunti wamuingizie hela endapo atafanikisha kuwachagua.
Alisema kuwa mkutano mkuu wa chama hicho utafanyika kama ulivyopangwa Aprili 19 na kwamba wajumbe 763 ndio watakaohudhuria badala ya 1,704 kwasababu chama hicho hakina hela za kutosha.
Alisema kwasasa chama hicho kinapata ruzuku ya Sh 2.4 milioni kila mwezi na kwamba kuwaita wajumbe wote 1,407 kwa siku tatu gharama yake ni Sh 250 milioni fedha ambazo hawana.
Akizungumzia wagombea wenzake wa nafasi ya uenyekiti Benedict Mutungirei na Joram Kinanda, Mrema alisema wao hawawanyanyasi bali kinachotokea ni uhuni kwani wagombea hao hawakuwahi kuomba kutumia ofisi ya chama hicho kuzungumza na waandishi wa habari.
Siombi radhi na nitamsaidia Rais Kikwete kupambana na rushwa kwa kumshughulikia Kinanda kwasababu amekuwa mla rushwa mkubwa,alisema Mrema.
Alisema pia mkutano mkuu wa chama hicho ndio utaamua kama yeye agombee urais mwakani au agombee ubunge.
Hali ilikuwa shwari katika makao makuu ya chama hicho wakati Mrema alipokuwa akirejesha fomu na kuzungumza na waandishi wa habari tofauti na siku nyingine, ambapo kulitokea vurugu wakati wagombea wengine walipokuwa wakirejesha fomu.
my take;
Lyatonga hayuko kwenye siasa kwa ajili ya kutimiza majukumu ya wananchi bali yeye yuko kwa ajili ya masilahi anayoyajua yeye, ndio maana hayuko tayari kuondoka na kuacha chama mikononi mwa vijana ambao wamejitokeza ili kumsaidia katika kukiendesha chama na kukijenga.