The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Ninamkumbuka Mrema kama mbunge na waziri mwenye meno; alikuwa na uwezo wa kuuma tofauti na viongozi wetu wengi ambao ni wasanii tu majukwaani.

Afadhali kuongozwa na Mrema kuliko hawa waliopo sasa ambao wanashindwa kushughulikia hata mambo ambayo yako wazi mno.

Namshauri Mrema akagombee ubunge Vunjo, akifanya hivyo mimi nitamchangia hata kama ni laki moja tu, haitamsaidia sana lakini ni ishara ya kushukuru kwa kazi zake kubwa alizofanya huko nyuma kama mbunge na waziri.

Bila Mrema kuingia upinzani kabla ya uchaguzi wa 1995 huenda mpaka leo upinzani ungelikuwa hoi mno. Wale watu ambao Mrema aliwaonjesha harufu ya upinzani ndio hao ambao sasa wengi wako na vyama vingine vya upinzani.

Popote ninapomwona Mrema mimi huwa namvulia kofia. Anaweza kuwa hakusoma kama wengine lakini amefanya kazi kubwa kuliko hao wanasiasa maprofesa na madaktari wa Tanzania.

Uliyosema ni kweli bali naogopa kukuunga mkono. Hivi lucifer hakuwa mkuu wa malaika na akiongoza sifa? Sasa tufuate yapi aliyoyafanya nyuma au anayoyafanya sasa? Kweli aliyoyafanya mrema yanaweza kuwa yalikuwa mazuri ila kwa sasa yeye ni sawa na lucifa tu amehasi watanzania na wanyonge na mazuri yake yamefutika
 
Uliyosema ni kweli bali naogopa kukuunga mkono. Hivi lucifer hakuwa mkuu wa malaika na akiongoza sifa? Sasa tufuate yapi aliyoyafanya nyuma au anayoyafanya sasa? Kweli aliyoyafanya mrema yanaweza kuwa yalikuwa mazuri ila kwa sasa yeye ni sawa na lucifa tu amehasi watanzania na wanyonge na mazuri yake yamefutika

Nikiungwa mkono na Shalom, mbingu itakuwa imegeuka na kuwa ardhi kwi kwi kwi!!!. Usijali kuhusu kuunga mkono hoja yangu, wewe changia tu. Nitafurahi zaidi ukinpinga kuliko ukiniunga mkono.

Mrema hata kwasasa bado anafaa kuwa mbunge; unajua paka anayejua kukamata panya, hata meno yakitoka bado anaweza kukamata panya.

Watanzania sisi ni wepesi sana wa kusahau watu ambao wameonyesha uongozi kwa matendo. Tunapenda kukumbuka watu wenye blaah blaah nyingi.

Mrema sasa hata pato hana ni ngumu sana kwa mzee kama yeye kuwa kwenye hali kama hiyo na mawazo yake kuendelea kuwa safi. Ni kumwelewa na kumwombea mungu amsaidie. Ningelikuwa JK, ningempa Mrema kazi angalau asimamie suala la mauaji ya Albino.
 
Mtanzania said:
Ningelikuwa JK, ningempa Mrema kazi angalau asimamie suala la mauaji ya Albino.

Mtanzania,

..kama sijakosea Mrema alikuwa kati ya maofisa usalama waliopatwa na matatizo kutokana na yale mauaji ya Shinyanga yaliyopelekea waziri wa mambo ya ndani Mzee Mwinyi kujiuzulu.

..kama Raisi anataka kumsaidia Mrema basi amteue kuwa mjumbe wa Tume mbalimbali za anazounda. mara nyingi wajumbe wa tume hizo hupata malipo mpaka laki 2.5 kwa siku.
 
Mrema sasa hata pato hana ni ngumu sana kwa mzee kama yeye kuwa kwenye hali kama hiyo na mawazo yake kuendelea kuwa safi. Ni kumwelewa na kumwombea mungu amsaidie. Ningelikuwa JK, ningempa Mrema kazi angalau asimamie suala la mauaji ya Albino.

Mtanzania,


..kama Raisi anataka kumsaidia Mrema basi amteue kuwa mjumbe wa Tume mbalimbali za anazounda. mara nyingi wajumbe wa tume hizo hupata malipo mpaka laki 2.5 kwa siku.


Wakuu apo juu heshima mbele sana, hivi kwani ameshatoka kwenye payroll yao?
 
Nikiungwa mkono na Shalom, mbingu itakuwa imegeuka na kuwa ardhi kwi kwi kwi!!!. Usijali kuhusu kuunga mkono hoja yangu, wewe changia tu. Nitafurahi zaidi ukinpinga kuliko ukiniunga mkono.

Mrema hata kwasasa bado anafaa kuwa mbunge; unajua paka anayejua kukamata panya, hata meno yakitoka bado anaweza kukamata panya.

Watanzania sisi ni wepesi sana wa kusahau watu ambao wameonyesha uongozi kwa matendo. Tunapenda kukumbuka watu wenye blaah blaah nyingi.

Mrema sasa hata pato hana ni ngumu sana kwa mzee kama yeye kuwa kwenye hali kama hiyo na mawazo yake kuendelea kuwa safi. Ni kumwelewa na kumwombea mungu amsaidie. Ningelikuwa JK, ningempa Mrema kazi angalau asimamie suala la mauaji ya Albino.


Hata mimi ukiniuliza leo nitaje waziri bora Tanzania tangia nipate ufahamu nitakutajia Sokoine na mrema. Ila kwa sasa na hasa baada ya kumsikia bihalamulo live nimemtoa kabisa katika group ya watu wanaoweza kuleta tija kwa nchi hii
 
Mrema kaanguka kwa HALBADIRI.
Yote aliyoombewe yameshatokea bado moja tu ambalo haliko mbali ambalo ni "wazimu" na kuokota makopo.mnakumbuka jamani!!!!!
 
maskini mzee wa kiraracha,hana hela,chama akiingizi mshiko duu?na ubunge akikosa mwakani itakuwa soo.
KAMA VIPI washikaji MUKULU JK ampe shavu dogo mrema ili ajikimu kimtind0.
 
Semeni msemavyo lakini Mrema alifanya kazi ambayo tangu aondoke hakuna waziri ambaye amewahi kupata umaarufu kwa kazi kama yeye.Mrema alikuwa mbunifu sana kwani aliweza kuanzisha vituo vidogo vya polisi na ulinzi shirikishi wanaozungumzia kina Mwema sasa hivi. Aliweza kuzuia mali zetu zisiende nje bila mpango. Utakumbuka aliwahi kupiga ambush airport mwenyewe na kudaka madini ya mama Siti Mwinyi. Usisahau mashamba ya mkonge na kusuluhisha mgogoro wa KKKT Arusha uliodumu kwa muda mrefu.
 
Semeni msemavyo lakini Mrema alifanya kazi ambayo tangu aondoke hakuna waziri ambaye amewahi kupata umaarufu kwa kazi kama yeye.Mrema alikuwa mbunifu sana kwani aliweza kuanzisha vituo vidogo vya polisi na ulinzi shirikishi wanaozungumzia kina Mwema sasa hivi. Aliweza kuzuia mali zetu zisiende nje bila mpango. Utakumbuka aliwahi kupiga ambush airport mwenyewe na kudaka madini ya mama Siti Mwinyi. Usisahau mashamba ya mkonge na kusuluhisha mgogoro wa KKKT Arusha uliodumu kwa muda mrefu.

Hapo umenena MATESO.
Majina mengine bana.
 
WASHKAJI MREMA ANAOMBA USHAURI WENU.mimi ni mtu wake wa karibuuuuuuu sana.
 
Huyu jamaa ameshafulia kisiasa na hata afya yake hivi sasa ni mgogoro. Afadhali Mungu aliepusha ile 1995. Angepata urais huyu hivi sasa wengi wetu tungekuwa wakimbizi kwenye nchi jirani! Ingekuwa chizi kapewa rungu.
 
Namfahamu Augustine Lyatonga Mrema tangu tukiwa wote watoto Marangu. Alihitimu kuwa Mwalimu, lakini baada ya kufundisha kwa muda mfupi,alijiunga na Idara ya Polisi (? Usalama wa Taifa).

Siasa aliingia seriously 1985 alipogombea na kuchaguliwa kuwakilisha Jimbo la Vunjo. Katika kipindi cha pili cha Rais Ali Hassan Mwinyi, Lyatonga aliteuliwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Enthusiasm yake ktk kushughulikia wahalifu, kwa kubuni hata kura za maoni za jamii ilimfanya Rais amteuwe "Naibu Waziri Mkuu", licha ya kwamba wadhifa huo haukuwa katika Katiba. Mrema alikuwa outspoken sana dhidi ya waliokuwa wamepora mashamba ya mkonge (?Chavda?). Ilipodhihirika kwamba alikuwa anataka publicity mno, Rais alimpeleka Wizara ya Kazi na Ustawi wa Jamii ambayo ilikuwa haina haiba kama wizara ya Mambo ya Ndani.

Licha ya kuwa Waziri wa Kazi, Mrema aliendelea na matamshi yake makali. Akiwa Bungeni ktk kipindi ambacho Bunge lilikuwa karibu lifikie kikomo na Uchaguzi Mkuu uandaliwe, alipinga muswada wa Serikali, na Rais Mwinyi akasitisha uteuzi wake kama waziri kwa kukiuka utamaduni wa Cabinet Solidarity.

Bunge lilipovunjwa Agosti 1995, Mrema akatangaza anajiondoa ktk Chama cha Mapinduzi. Vyama kadhaa vya siasa vya upinzani ambavyo ndio mara ya kwanza kuingia ktk kampeni za Uchaguzi Mkuu, vikaanza kumshawishi Mrema ajiunge navyo.

Mrema akaweka masharti kwamba angejiunga na Chama ambacho angekiongoza kama Mwenyekiti Taifa, na ambacho kingemteuwa kuwa Mgombea wa u-Rais ktk Uchaguzi Mkuu wa 1995. Mwishowe akajiunga na NCCR-Mageuzi, akichukua uenyekiti taifa kutoka kwa Mabere Marando, na kuteuliwa Mgombea wa u-Rais kwa tiketi ya NCCR.

Kampeni za Mrema 1995 zlikuwa na vituko vingi: Gari lake likisukumwa na vijana washabiki na Mrema akitandikiwa khanga atembee juu yake na wanawake walioshangilia. Mrema akiwa na uhakika angeshinda alianza kutoa vitisho kwa viongozi wa Serikali aliodai ni wala rushwa. Alitishia k.m. kwamba atamtia mbaroni Mwinyi,na kwamba wiki mbili baada ya kuingia Ikulu, "Mwinyi angekuwa anakunywa maji kwa karai huko Ukonga". Washauri wake walimwomba ku-tone down vitisho walipuuzwa.

Alipotembelea Baba wa Taifa, kijijini Butiama akiwa na timu yake ya kampeni Mkoani Mara, inasemekana Mwalimu alitamka "I shall never allow my country to be thrown to the dogs". Wana NCCR walidai Mwalimu aliwaita mbwa. Lakini baada ya hapo, Mwalimu alijitolea wazi wazi kumfanyia kampeni Benjamin Mkapa. Mrema akashindwa ingawa alipata asilimia 28 ya kura za u-Rais.

Kukosa fadhila kwa Mrema kulianza kujionyesha zaidi pale alipoanza kugombana na Mabere Marando. Mwisho akitaka kumfukuza Mabere toka NCCR, mambo yalimgeukia akatoka NCCR-Mageuzi na kujiunga na Tanzania Labour Party iliyokuwa inaongozwa na Lwekama. Ktk Tanzania Labour Party nako alikaribishwa kuwa Mwenyekiti Taifa. Lakini soon afterwards, mgogoro baina ya Mrema na viongozi wa awali wa T.L.P. ukaanza.

Uchaguzi Mkuu wa 2000, T.L.P. ikamsimamisha Mrema kama mgombea wao, lakini licha ya kukiimarisha chama, Mrema alikuwa mgombea wa tatu, Profesa Lipumba akichukua nafasi ya pili baada ya Mkapa. Hakujifunza kwa vile migogoro ndani ya T.L.P. iliendelea na ktk Uchaguzi Mkuu wa 2005, Mrema aliambulia kura chache sana kama mgombea wa U-Rais, chama chake kikipata kiti kimoja tu cha Ubunge huko Biharamulo Magharibi.

Mrema ameendelea kulumbana na wanachama viongozi ktk T.L.P. na mwaka huu alipokuwa na Mkutano Mkuu wa T.L.P., aliwafukuza wajumbe akabakia na wajumbe 163 tu, waliomchagua Mwenyekiti wa Taifa kwa miaka mitano ijayo. Tumeshuhudia kusambaratika kwa chama chake kule Biharamulo wiki iliyopita, ambako yeye mwenyewe alikwenda kumkampenia mgombea wake aliyeambulia kura 187, zikiwa ni asilimia 0.57 za kura zilizopigwa.

Mrema amechoka na amekwisha kisiasa. Bora arudi Kiraghacha, Marangu kunywa mbege. Tutamkaribisha.
hukugusia mafanikio aliyopata katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini mwaka 1995 kwa kupata kura asilimia 30%, wabunge 55, mwitikio wa mageuzi wa kihistoria katika taifa letu.

1996 kushinda ubunge wa jimbo la temeke katika uchaguzi mdogo uliotokana na uamuzi wa mahakama baada ya upinzani kupinga ushindi wa CCM mahakamani..

kosa la Mrema ni kukosekana kwa mfumo imara wa kitaasisi katika vyama vya upinzani na undumilakuwili mwingi wa viongozi wengi katika vyama vya siasa vya upinzani..

Bado ninaamini mchango wa ALM katika siasa za mageuzi ya nchi hii ni za kuuungwa mkono na wapenda mabadilko wote katika jamii..

kuanguka kwake kuwe chachu ya kuzaliwa mageuzi imara katika taifa la tanzania.
 
He was once warned by Mwalimu against those who stood above him in terms of not only academic qualifications but also what very quickly proved to be basis reasoning and strategic planning. His political career was built on flagile foundations, on bricks of ice in the desert which gave him an artificial bubbly life at the time when he was allowed to carry the huge freezers from CCM to NCCR-Mageuzi. As they started rusting, his strategic plans let him down - he sat watching them fall to pieces and along them he fell too.
 
Ndugu pamoja na mapungufu yote ambayo tunayaona kwa sasa lakini tukubali kuwa enzi za Mrema alifanya kazi ambazo kama kweli mawaziri tulionao kwa sasa wangefanya hata robo yake nchi yetu isingekwa kama ilivyo kwa sasa. Tizama mambo ya ndani, tunao wageni wachina kiasi gani ambao hawana hata residence and work permits na wanafanya biashara za kipuuzi, hapo ndiyo tunawaita wawekezaji?? Angekuwepo mrema siamini wala kudhani kungekuwa na uozo kama huo. Huo ni mfano mdogo tu.
 
ndugu pamoja na mapungufu yote ambayo tunayaona kwa sasa lakini tukubali kuwa enzi za mrema alifanya kazi ambazo kama kweli mawaziri tulionao kwa sasa wangefanya hata robo yake nchi yetu isingekwa kama ilivyo kwa sasa. Tizama mambo ya ndani, tunao wageni wachina kiasi gani ambao hawana hata residence and work permits na wanafanya biashara za kipuuzi, hapo ndiyo tunawaita wawekezaji?? Angekuwepo mrema siamini wala kudhani kungekuwa na uozo kama huo. Huo ni mfano mdogo tu.

hapo umenena mkulu
 
Kushuka kwa Mrema kulianzia kileleni kwake. Aliingia mkenge baada ya kujiunga na NCCR Mageuzi. Wana CCM walishusha pumzi baada ya kuona amejiunga na NCCR Mageuzi(Kama alivyofanya Kolimba), maana hicho chama kilianzishwa na mashushushu na lengo kubwa lilikuwa kuwachota wale wapinzani halisi na kuwazuga donor community waliokuwa wanataka mabadiliko Tanzania. Kosa la pili alipohamia TLP akaenda kuwafuata walewale mashushushu na wakawa wanammaliza kila kukicha (aliendelea kufanya kosa lilelile).
Lakini yote aliyokuwa anayasema Mrema yalikuwa ni kweli alikuwa anasema nchi inatafunwa, tutakuja mkumbuka ni kweli, kama angekuwa ameenda shule kama kina Slaa na wenzake basi angekuwa na impact mapema zaidi. Lakini kilikuwa kipindi tofauti watanzania tulikuwa bado tuko kwenye lepe zito la usingizi walau sasa tunasikia sauti za upinzani, na wapinzani hawaonekani useless kama kipindi kile.
 
Napata mitizamo tofauti, nahisi ni kwa sababu kila aliyechangia hakuwa mweyewe ama alikuwa na MAPENZI au CHUKI. Ambao hawakutanguliza hayo wameeleza vizuri.

Ni ukweli ulio dhahiri kwamba utatenda na kusema kuendana na wakati wako. Wote waliotajwa na slaa pale mwembe yanga walisema watamshitaki lakini baada ya miaka mitatu wamepelekwa wao mahakamani kwa vitu vilevile alivyovitamka. Nimekumbusha haya ili kuwarejesha kwenye hoja za mrema mara nyingi akirudia kuwa nchi inaibiwa/inaliwa.

Angali.
Vituo vidogo vya polisi kila mahali.
Majambazi yalirudisha Bunduki.
Ni yeye aliyesababisha kurusiwa kwa biashara ya bureau de change.
Ni yeye aliyetufanya tufahamu kuwa kuna watu wanahamisha dhahabu.
Ni yeye aliyetujuza juu ya import support ambayo mpaka leo inapigiwa kilele.

Na mengineyo mengi, huo ulikuwa wakati wake

Kwa sasa anahangaikia tu mlo wake, akiachia chama ataishije? mimi nahisi ni haki yake kuupigania uhai wake.

Yanayomkuta mkapa leo ni laana ya yale aliyowafanyia wapinzani na Siku moja lazima atafika tu mahakamani.
 
Watanzania tuna matatizo mengi yanayochangia kuturudisha nyuma mojawapo ya matatizo makubwa yanayoendelea kulitafuna taifa letu ni usahaulifu [kumbukumbu fupi].Ukweli wa jambo hili utaliona kila mara uchaguzi unapowadia,wakinamama waliopata taabu ya matibabu duni mahospitali,wanafunzi waliopata taabu ya kupata mikopo,wananchi walioumizwa na tatizo la rushwa na nk wote kwa pamoja wanasahau masahibu yote wanairejesha tena CCM.Kumbukumbu fupi ni mtaji mkubwa sana kwa chama cha mapinduzi.Leo tunawasikia waislam wakilalamikia mahakama ya kadhi hata wasipopewa kipindi cha uchaguzi utashangaa wanakuwa wapiga debe wazuri wa CCM.

Wanajamvi nimeanzia mbali kidogo pengine muweze kuelewa msingi wa hoja yangu.Bwana Mrema pamoja na mapungufu yake mengi lakini bado anaendelea kuwa mmoja wa wanasiasa wachapakazi wakubwa ambao taifa letu limewahi kuwapata.Bwana Mrema wakati alipokuwa waziri wa mambo ya ndani na baadaye naibu waziri mkuu aliweza kuzuia wimbi kubwa la ujambazi hata akafika mahali majambazi walirejesha silaha wenyewe.Bwana Mrema alikuwa ni waziri wa wananchi hasa wanyonge si kama mawaziri tunaowaona leo.Nina hakika Bwana Mrema kama angekuwa bado waziri wa mambo ya ndani mauaji ya ndugu zetu maalbino tusingeyasikia.Huyu Bwana alikuwa mchapakazi na mbunifu wa hali ya juu sana,hakuwa waziri wa kukaa maofisini tu bali alikuwa anakwenda hata kwenye matukio.Kipindi cha Mzee Ruksa kulikuwa na ule mgogoro wa KKKT Meru watu waliuwawa,mali kama nyumba,mifugo na nk viliteketezwa ni huyu huyu Bwana Mrema aliweza kumaliza mgogoro uliokuwa unalitia aibu taifa letu nje na ndani.Watu wanaoweza kubeza uwezo wa Bwana Mrema ni vijana wadogo ambao kipindi cha Mzee Ruksa hawakuwa na ufahamu wa kuweza kupambanua mambo.

Ujenzi wa vituo vidogo vya polisi ni ubunifu wa Bwana Mrema baada ya kubaini msongamano katika vituo vikubwa.Bwana Mrema aliwasaidia wakulima wa kahawa kulipwa bei nzuri kulingana na mauzo katika soko la dunia.

Tusisubiri Bwana Mrema afe ndiyo tumwage sifa zake,tumpatie sifa akiwa hai kwasababu anastahili.


Tatizo kubwa analokumbana nalo Bwana Mrema ni kufanyakazi na watu wa system bila yeye kujua,watu wa system wako pale kuhakikisha hapigi hatua yoyote ya kisiasa.Bwana Mrema akiweza kupanga safu nzuri ya viongozi bado anaweza kuleta chachu ya mageuzi hapa nchini.
 
Watanzania tuna matatizo mengi yanayochangia kuturudisha nyuma mojawapo ya matatizo makubwa yanayoendelea kulitafuna taifa letu ni usahaulifu [kumbukumbu fupi].Ukweli wa jambo hili utaliona kila mara uchaguzi unapowadia,wakinamama waliopata taabu ya matibabu duni mahospitali,wanafunzi waliopata taabu ya kupata mikopo,wananchi walioumizwa na tatizo la rushwa na nk wote kwa pamoja wanasahau masahibu yote wanairejesha tena CCM.Kumbukumbu fupi ni mtaji mkubwa sana kwa chama cha mapinduzi.Leo tunawasikia waislam wakilalamikia mahakama ya kadhi hata wasipopewa kipindi cha uchaguzi utashangaa wanakuwa wapiga debe wazuri wa CCM.

Wanajamvi nimeanzia mbali kidogo pengine muweze kuelewa msingi wa hoja yangu.Bwana Mrema pamoja na mapungufu yake mengi lakini bado anaendelea kuwa mmoja wa wanasiasa wachapakazi wakubwa ambao taifa letu limewahi kuwapata.Bwana Mrema wakati alipokuwa waziri wa mambo ya ndani na baadaye naibu waziri mkuu aliweza kuzuia wimbi kubwa la ujambazi hata akafika mahali majambazi walirejesha silaha wenyewe.Bwana Mrema alikuwa ni waziri wa wananchi hasa wanyonge si kama mawaziri tunaowaona leo.Nina hakika Bwana Mrema kama angekuwa bado waziri wa mambo ya ndani mauaji ya ndugu zetu maalbino tusingeyasikia.Huyu Bwana alikuwa mchapakazi na mbunifu wa hali ya juu sana,hakuwa waziri wa kukaa maofisini tu bali alikuwa anakwenda hata kwenye matukio.Kipindi cha Mzee Ruksa kulikuwa na ule mgogoro wa KKKT Meru watu waliuwawa,mali kama nyumba,mifugo na nk viliteketezwa ni huyu huyu Bwana Mrema aliweza kumaliza mgogoro uliokuwa unalitia aibu taifa letu nje na ndani.Watu wanaoweza kubeza uwezo wa Bwana Mrema ni vijana wadogo ambao kipindi cha Mzee Ruksa hawakuwa na ufahamu wa kuweza kupambanua mambo.

Ujenzi wa vituo vidogo vya polisi ni ubunifu wa Bwana Mrema baada ya kubaini msongamano katika vituo vikubwa.Bwana Mrema aliwasaidia wakulima wa kahawa kulipwa bei nzuri kulingana na mauzo katika soko la dunia.

Tusisubiri Bwana Mrema afe ndiyo tumwage sifa zake,tumpatie sifa akiwa hai kwasababu anastahili.


Tatizo kubwa analokumbana nalo Bwana Mrema ni kufanyakazi na watu wa system bila yeye kujua,watu wa system wako pale kuhakikisha hapigi hatua yoyote ya kisiasa.Bwana Mrema akiweza kupanga safu nzuri ya viongozi bado anaweza kuleta chachu ya mageuzi hapa nchini.

Kweli kijana wastahili pongezi.washkaji tumpongeze na kumsifia mrema akiwa bado hai,sijaona waziri mfano wake hadi leo........washkadau TOENI maoni
 
Back
Top Bottom