The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Hii habari inafurahisha sana na inasikitisha sana. Katika habari hii ndio mtaona uzuzu wa viongozi wa CCM. Aliyoyasema Shibuda yalitakiwa yasemwe na Chiligati maana yeye ni Katibu wa Uenezi na Itikidai wa CCM. Au na yeye hana nguvu kama katibu wao?au hajijui kama yeye ni Katibu wa Uenezi na Itikidai wa CCM? Au anadhani watanzania tumelala statment yake iatufanya na sisi tuwe mazezeta?Kuna mtu aliwahi kuniambia ukiwa CCM inakubidi uwezuzu ndio utakaa ndani ya CCM sasa naamini maneno yake. Wewe ni Katibu wa Uenezi na Itikidai wa CCM na Waziri wa Serikali tena ya chama chenu! hujui kama ni kosa kwa kiongozi kushutumiwa?nilitegemea ungesema inabidi Chenge ajiuzulu ili ufanye uchunguzi huo ndio uwajibikaji. Huo ndio utawala bora. Lakini badala yake mnatufanya sisi mazuzu. Jueni hizo zama zimeshapitwa na ndio maana mnazomewa!
 
Looh! tayari wanaanza kurukana. Muhimu ni kuendelea kumvizia mmoja mmoja.

Linalosikitisha ni kwamba SFO wamefukua kidogo tu na tayari wakawa wamemnasa Chenge. TAKUKURU yetu imewanasa wangapi tokea imepewa majukumu!

Kuna umhimu wa kuwakodi hawa SFO na wengineo, kama akina Kroll ili watufukulie kwa ukamilifu kabisa pesa za waTanzania zilipofichwa duniani kote.
 
Hata vitu vibaya hawajui kuvifanya vizuri.

Of all places, unaenda kuweka hela ulizokwiba Tanzania kwenye a British Crown dependant island barely 100 kms from the shores of England.Despite all the extradition treaties and Commonwealth ties?

Smart lawyer indeed, hakusikia kilichompata Professor? Hakuwa hata na hesabu za kujua Liechenstein, Luxembourg Switzerland au Monaco ambako sheria za privacy ni ngumu zaidi ya UK?

Ujinga wake ndoyo faida yetu, maana sasa waingereza wamemuaibisha kashindwa hata kukataa imebaki anasema hizo pesa sio za BAE.

With AG's like these, no wonder we have such horrible contracts.

Na bado anatumia muda wake mwingi binafsi kusifia degree yake ya sheria .. what a .......

Mara ya mwisho alitishia magazeti ya nyumbani kuwa yakiandika habari zake angewashitaki. Sasa moto umeanza kuwaka na nasubiri kumwona mwizi Chenge in court!
 
Sijui mheshimiwa rais ataunda tume ya kumchunguza Chenge na the usual blah blah blah ifuate...
 
Looh! tayari wanaanza kurukana. Muhimu ni kuendelea kumvizia mmoja mmoja.

No hawarukani wanaendeleza kile wanachokifanya kina Kada Mpinzani na wezake. Kurukaruka na kukosa hoja. Mtu na akili yako huwezi kusema eti wewe ni bubu! Bubu anatamani kusema wewe unaombea ububu!

Haya tutaona bubu kama hatasema mwaka huu.
 
Sijui mheshimiwa rais ataunda tume ya kumchunguza Chenge na the usual blah blah blah ifuate...

Oya we mwakilishi mganga wa kienyeji nini?Rais lazma aunde tume ichunguze tena anaweza kuipa miaka mitatu ili Chenge agombee ubunge na 2010! Nani hamjui JK? Rais anaeongoza kwa usanii mwingiii tume nyiiingi na vicheko vya kimzahamzaha. Yaani hata yeye Mwenye hajiamini anajiundia tume! hivi wewe ni Rais wa kuchaguliwa una washauri wako nje ya mawaziri wewe kwa nafasi yako ya Urais hapa ulimwenguni ni wapili kutoka Mungu ni Rais wewe ndio unae appoint na wewe ndio mwenye uwezo wa kumfukuza mtu iweje uunde tume eti kutathmini utendaji wa baraza la mawaziri? Haki ya Mungu awamu hii tumempata Rais wajukuu wa wajukuu zetu watakuja kucheka sana wakija kusoma historia ya huyu jamaa.
 
Mpaka sasa sina data za uhakika kwamba Waziri Chenge anakosa gani? Nadhani kilichoonekana ni hela... source bado haijajulikana tusubiri tutajua.

Tunajenga taifa la kipumbavu sana kwa mtu kama Chenge kuwa/kumiliki TZS 1.2 Billion ni hela ndogo sana!!! Huu umaskini ndio unatusumbua...

Of course nikifa bila kumiliki utajiri usiozidi hapo... nitakuwa nimekufa nikiwa maskini...
 
Mpaka sasa sina data za uhakika kwamba Waziri Chenge anakosa gani? Nadhani kilichoonekana ni hela... source bado haijajulikana tusubiri tutajua.

Tunajenga taifa la kipumbavu sana kwa mtu kama Chenge kuwa/kumiliki TZS 1.2 Billion ni hela ndogo sana!!! Huu umaskini ndio unatusumbua...
Of course nikifa bila kumiliki utajiri usiozidi hapo... nitakuwa nimekufa nikiwa maskini...

Mhh ....

Siamini kama hii umeitoa wewe mkuu!

Hebu isome tena kwa sauti usikie vile inasound!
 
Mpaka sasa sina data za uhakika kwamba Waziri Chenge anakosa gani? Nadhani kilichoonekana ni hela... source bado haijajulikana tusubiri tutajua.

Tunajenga taifa la kipumbavu sana kwa mtu kama Chenge kuwa/kumiliki TZS 1.2 Billion ni hela ndogo sana!!! Huu umaskini ndio unatusumbua...

Of course nikifa bila kumiliki utajiri usiozidi hapo... nitakuwa nimekufa nikiwa maskini...

Tatizo siyo hela,

Chenge atueleze ameipataje kwa kazi yake na mshahara wake.

Atueleze kwa nini yeye kama ofisa mkubwa wa serikali ameshindwa kuiweka hiyo hela nchini isaidie kukuza uchumi wetu na kuamua kuiweka nje, je alikuwa ana nia ya kuificha? Kwa nini?

Atueleze kama katika declarations wanazofanya katika tume ya maadili ya viongozi alitaja mali hizi.

Ni hayo tu kwa sasa, hamna mtu anayekataa Chenmge kuwa na hela, ila maswali yetu ayajibu.
 
Mpaka sasa sina data za uhakika kwamba Waziri Chenge anakosa gani? Nadhani kilichoonekana ni hela... source bado haijajulikana tusubiri tutajua.

Tunajenga taifa la kipumbavu sana kwa mtu kama Chenge kuwa/kumiliki TZS 1.2 Billion ni hela ndogo sana!!! Huu umaskini ndio unatusumbua...

Of course nikifa bila kumiliki utajiri usiozidi hapo... nitakuwa nimekufa nikiwa maskini...

Mkuu tatizo sio hizo pesa bali amezipata wapi maana kwa mfanyakazi wa serikali ya Tanzania 1B ni kubwa hata kama akifanya kazi miaka 50, ila ukizungumzia kwenye context ya mafisadi wenzake hiyo hela ni ndogo sana wala hamna haja ya kumuuliza, ambavyo ndo atakavyofanya JK
 
Tatizo siyo hela,

Chenge atueleze ameipataje kwa kazi yake na mshahara wake.

Atueleze kwa nini yeye kama ofisa mkubwa wa serikali ameshindwa kuiweka hiyo hela nchini isaidie kukuza uchumi wetu na kuamua kuiweka nje, je alikuwa ana nia ya kuificha? Kwa nini?

Atueleze kama katika declarations wanazofanya katika tume ya maadili ya viongozi alitaja mali hizi.

Ni hayo tu kwa sasa, hamna mtu anayekataa Chenmge kuwa na hela, ila maswali yetu ayajibu.

Pundit;
Kutokuwa na uzalendo wa kuweka hela ndani nadhani ndio moja ya hoja nzito dhidi ya Chenge. Vinginevyo, hana mzigo wa kuthibitisha aliko zipata, mpaka labda ashitakiwe. Na mzigo bado uko kwetu kuangalia kama alitangaza hizi mali, sio yeye akafungue daftari la Serikali atusomee.
 
Pundit;
Kutokuwa na uzalendo wa kuweka hela ndani nadhani ndio moja ya hoja nzito dhidi ya Chenge. Vinginevyo, hana mzigo wa kuthibitisha aliko zipata, mpaka labda ashitakiwe. Na mzigo bado uko kwetu kuangalia kama alitangaza hizi mali, sio yeye akafungue daftari la Serikali atusomee.

Hapa mkuu utaona umuhimu wa watu kama hawa kuspeak up, lakini atakaa kimya bila kusema kitu, kama aliziorodhesha kwenye commission ya maadili ya umma sioni kama kuna tatizo, kama aliziorodhesha atatwambia tu amezipata vipi then let the man be, lakini atakaa kimya na hatachukuliwa hatua zozote.
 
Looh! tayari wanaanza kurukana. Muhimu ni kuendelea kumvizia mmoja mmoja.
Hapana kaka unakosea!!, mmojaX2 hatutowaweza hawa!!dawa sasa ni Kurusha 'KOTA' kwenye matawi yote,bila shaka zitaanguka nyingi tu mchanganyiko,zile mbivu basi twafyonza,zile mbichi twavundika kwa ajili ya kesho.
 
Mpaka sasa sina data za uhakika kwamba Waziri Chenge anakosa gani? .

Tunajenga taifa la kipumbavu sana kwa mtu kama Chenge kuwa/kumiliki TZS 1.2 Billion ni hela ndogo sana!!! Huu umaskini ndio unatusumbua...
Of course nikifa bila kumiliki utajiri usiozidi hapo... nitakuwa nimekufa nikiwa maskini...
Naelekea Kufikiri umaskini upo wa aina mbaliX2,sina uhakika unazungumzia umaskini upi haswa?
**umasikini wa Hali??,Aki....?? sijui!
 
Mhh ....

Siamini kama hii umeitoa wewe mkuu!

Hebu isome tena kwa sauti usikie vile inasound!

Yaani wewe Mwafrika wa kike humjui Kasheshe? au unaota? mie tangu niingie humu JF sijaona watu kadhaa wakisema Njano ni Njano wao lazma waseme opposite wapo wengi Kasheshe ni mmoja wapo. Yeye mwenyewe atakufa hata kuwa na reserve ya 1 million dollar yapo anasema ni pesa kidogo sana.

Kasheshe hizo million dollar zingekuwa hapa bongo japo zingekuwa Benk lakini zingekuwa zinazunguka kama watu wangekopeshwa na mabenk yanayo hodhi hizo pesa na dollar ingekuwa sio strong kama ilivyo sasa. Shilling inakuwa weak kutokana na uhaba wa USD.
 
Chenge akija na maelezo ya jinsi alivyoipata hiyo hela yakiwa tofauti na tunavyotaka tutaendelea kuhoji na kunung'unika..kilichobaki tusubiri mpaka uchunguzi utakapokamilika.
 
Chenge akija na maelezo ya jinsi alivyoipata hiyo hela yakiwa tofauti na tunavyotaka tutaendelea kuhoji na kunung'unika..kilichobaki tusubiri mpaka uchunguzi utakapokamilika.

Kaka wale jamaa wanachunguza kwa manufaa yao chenge hashitakiwi hapo ila yeye ni shahidi, ila sasa ni zamu yetu kumuomba atupe maelezo yake sisi kama wapiga kura wake.
 
kwani ile fomu ya kutaja mali aliziweka na hizo pesa au hazimo na ni nani anatunza hizo fomu.
 
kwani ile fomu ya kutaja mali aliziweka na hizo pesa au hazimo na ni nani anatunza hizo fomu.

Hicho ndo kinasubiliwa wakuu hapa wakachungulie kwenye commission ya maadili na kujua kama halitaja hizo $ 1000000 au vipi, lakini hata kama alizitaja atuambie tu alizipata vipi only that, maana kuwa na pesa sio tatizo
 
Back
Top Bottom