SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,275
- Thread starter
- #21
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
22-(Kikosi cha Kunguru weusi)
ILIPOISHIA...
Vita kali inaibuka ndani na nje ya boti iliyokuwa ikienda kwa kasi, ni vita kati ya Tino anayemzuia Jasusi Shadow asiondoke na sanduku lenye vimelea vya V-COBOS wakati huo huo ndani ya boti hiyo mapigano makali kati ya Bosco na Wazari wa afya Dokta Gondwe yalikuwa yakiendela
Upande wa pili Najma anaanza kufuatilia na kuuchimba ukweli kuhusu vimelea vya V-COBOS.
Jez nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
Shadow alikimbia akapanda juu kabisa ya boti Tino naye akamfuata hakutaka kumpa upenyo wa kuondoka na lile sanduku. Sasa walikuwa juu kabisa ya boti hiyo iliyokua ikienda kwa kasi ikipasua mawimbi ya bahari ya hindi. Si Shadow wala si Tino wote walikuwa vizuri kwenye suala zima la mapambano ya bila kutumia siraha.
Mara punde purukushani kati ya Bosco na Waziri wa afya Dokta Gondwe ilihama kutokea ndani ya boti sasa wakahamia nje. Hapo Dokta Gondwe aliweza kumuona Tino akipigana na yule mtu aliyeondoka na sanduku lake lakini cha ajabu Dokta Gondwe hakutaka kushughulika naye yeye akaendelea kukomaa na Bosco.
"Huwezi kuondoka hapa mpaka uniambie ni wapi ilipo dawa ya virusi vya COBOS" Dokta Gondwe aliongea kwa nguvu huku akifuta damu iliyokuwa ikimtoka puani
"Unajisumbua bure Dokta hupati chochote kutoka kwangu, na nitahakikisha nasambaza picha zako chafu mtandaoni" Bosco alijibu huku akitema damu
"Siwezi kukupa hiyo nafasi kijana leo ni ama zako ama zangu" alisema Dokta Gondwe huku akikimbia na kwenda kumvaa Bosco kwa mara nyingine wakaanza tena kupigana. Wakati huo pia juu ya boti bado mpambano kati ya Tino na Jasusi Shadow ulizidi kupamba moto.
Boti iliyokuwa ikienda kwa kasi bila kuongozwa na mtu yeyote sasa ilikuwa ikielekea nchi kavu ikiwa ibakiza mita chache kugusa ardhi mara Jasusi Shadow alilishika lile sanduku kisha akalitupa ndani ya maji kitendo hicho kilimshangaza sana Tino na kwakuwa hakutaka kuvipoteza vimelea vya V-COBOS haraka alijitosa majini kulifuata sanduku lile, sekunde chache baadae Jasusi Shadow naye akajitosa majini kumfuata.
Boti ilienda kwa kasi ikatoka ndani ya maji nakupaa juu mita chache kisha ikatua nchi kavu na kupinduka upande mmoja. Dokta Gondwe na Bosco ambao walikuwa hawelewi hili wala lile wajikuta wakijipigiza vibaya kwenye kuta za boti hiyo
Dokta Gondwe aliumia vibaya mno, aliinuka kwa kujikongoja akatazama pande zote na hapo ndipo alipobaini kuwa boti ilikuwa nchi kavu kwa sasa, aliendelea kuangaza macho yake kila mahali hakumuona Bosco, hakumuona Tino wala Jasusi Shadow.
"Ameenda wapi huyu mpuuzi?" alisema Dokta Gondwe huku akishuka kutoka kwenye boti akazunguuka upande wa pili kuangalia, hakuona mtu lakini mara alisikia vishindo nyuma yake akageuka haraka kuangalia hapo ndipo alimuona Bosco kwa mbali akikimbia kuelekea msituni. Dokta Gondwe hakuwa na nguvu kabisa ya kuendelea kumfuatilia, tayari alikuwa amejeruhiwa na kuchoka karibu kile sehemu ya mwili wake, alikuwa hoi.
Dokta Gondwe aliutazama ule msitu mdogo alikokimbilia Bosco kisha akafungua simu yake akaangalia ramani ya eneo hilo, mara akatabasamu.
"Huwezi kwenda kokote kijana lazima nikupate" alisema Dokta Gondwe baada ya kubaini kuwa kule alikokwenda Bosco ilikuwa ni Rasi yaani sehemu ya ardhi iliyoingia majini, kwa maana hiyo ili Bosco atoke ilikuwa ni lazima arudi alikotoka kwani alikoenda ilikuwa ni sehemu iliyozunguukwa na maji pande zote tatu.
Dokta Gondwe alibinya simu yake akapiga namba fulani kisha akaweka simu sikioni.
"Hallo"
"Ndiyo bosi nakusikia" sauti nzito ilisikika upande wa pili
"Nahitaji msaada njoo na kikosi chote cha Kunguru weusi nakutumia ramani nilipo, nawahitaji sasa hivi"
"Sawa bosi, lakini Kamanda Tino hayupo aliondoka asubuhi sana aka...."
"Nyie njooni Tino mtamkuta huku"
Aliongea Dokta Gondwe akakata simu kisha akamtumia mtu huyo uelekeo wa mahali alipo. Baada ya hapo alituma ujumbe mfupi wa maandishi kwenda kwa Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa.
,,,,,,,,,,,,Profesa nimefanya kama ulivyonishauri lakini mambo ni mazito sana huku baharini, yaani huwezi kuamini Waziri mkubwa kama mimi nahangaika huku badala ya kukaa bungeni, hawa wamexico wananitesa sana najuta kuchua ofa yao kweli nitafika mbinguni nimechoka sana,,,,,,,,,,
Baada ya kutuma ujumbe huo Dokta Gondwe alipiga hatua akaenda kukaa pembeni ya ile boti kusubiri kikosi cha Kunguru weusi. Jambo la ajabu ni kwamba alikuwa hajali kabisa kuhusu Tino na yule mtu aliyechukua sanduku lake, akili yake yote iliielekeza kwa Bosco
Vita ya Tino na Jasusi Shadow haikuishia kwenye ile boti, bado iliendelea hata ndani ya maji. Wakati Tino akilifuata sanduku lililokuwa linazama kwenye kina kirefu cha bahari Jasusi Shadow naye alikuwa nyuma yake akiogerea kwa kasi kumfuata. Wote walionekana ni wazoefu wa kuogerea na jambo lingine muhimu kila mmoja alikuwa na mtungi wa gesi uliomsaidia kupumua akiwa ndani ya maji.
Waliendelea kuvutana na kugeuzana wakiwa ndani ya maji kila mmoja akitaka kuwa wa kwanza kulifikia sanduku lile. Mwisho walizama mpaka chini kabisa wakagusa ardhi chini ya bahari. Jasusi Shadow alipata mwanya akafanikiwa kumbana vizuri Tino kisha akamchomolea ule mpira unaopitisha gesi kutoka kwenye mtungi akaukata kabisa, hapo Tino alijikuta anaanza kutapatapa baada ya kukosa hewa, mbaya zaidi walikuwa wamezama kwenye kina kirefu cha maji haikuwa rahisi kupata pumzi ya kutosha itakayomuwezesha kufika juu.
Jasusi Shadow alisogea hadi lilipo sanduku akalichukua kisha akaanza kuogerea kupanda juu akimfuata Tino ambaye kwa sasa alikuwa anaelekea kupoteza fahamu baada ya kukosa hewa na kunywa maji mengi.
Shadow alimfikia Tino akamshika na kuogerea naye hadi alipotokeza juu ya maji wakati huo tayari Tino alikuwa amepoteza fahamu hajitambua. Shadow alimbeba na kutoka naye hadi nchi kavu, akamlaza chini kisha akaanza kumminya tumbo kwa nguvu, Tino akawa anayatapika maji mengi aliyokunywa bila kupenda yakatokea mdomoni na puani. Shadow hakutaka kumuacha Tino afe, hilo halikuwa agizo la Sultana bosi wake ambaye pia alikuwa ni mama mzazi wa Tino, licha ya wanafamilia hao wawili kuwa na vita kali wakipigania vimelea vya V-COBOS lakini hakuna siku Sultana alimuagiza Shadow amuue Tino.
Baada ya kutoa huduma hiyo ya kwanza Shadow alimbeba Tino akaingia naye msituni hatua kadhaa kutoka usawa wa bahari akachukua kamba na kumfunga chini ya mti mmoja mkubwa. Wakati huo wote Tino alikuwa hajitambua.
Shadow alichukua lile sanduku akamtazama Tino kwa sekunde kadhaa kisha akageuka na kuondoka zake, akatokomea msituni.
Upande wa pili ndani ya gereza la Kanondo, gereza ambalo wafungwa walikuwa wakiishi maisha malaini sana tofauti kabisa na magereza mengine. Hapo ndipo alipokuwa ameifadhiwa kijana Osward mtoto wa kigogo mmoja maarufu kama mzee Matula, alikuwa hapo kwa zaidi ya miezi mitatu akisubiri kesi yake ya mauaji iliyokuwa bado inaendelea kuunguruma mahakamani.
Najma alifika kwa ajili ya kufanya mazungumzo nyeti na Osward ambaye alifurahi sana baada ya kumuona kwa mara nyingine tangu alipomuona siku iliyopita.
"Siamini kama umekuja kuniona tena Najma, nilipoambiwa na askari kuwa kuna mwanamke amekuja kuniona nikawa najiuliza ni nani huyo kumbe ni wewe mpenzi" Alisema Osward huku furaha yake ikionekana wazi kwa nuru iliyokuwa inang'aa usoni kwake, hakika alikuwa akimpenda sana Najma.
"Hebu kaa nina mazungumzo muhimu na wewe" Alisema Najma huku akionekana kutofurahiswa hata kidogo na maneno ya Osward.
"Sawa nimekaa, nambie mguu wako unaendeleaje?"
"Salama nilishapona"
"Kwa nini jana ukakubali kuondoka na inspekta Aron hujui kama yule ni adui yetu mkubwa na ndio sababu ya mimi kuendelea kuwa humu hadi leo?"
"Anafanya kazi yake acha kumlaumu, kama hukuua basi ukweli utajulikana tu kuwa mpole"
"Mmh mbona leo wewe ni mkali hivyo, uko sawa kweli Najma wangu?"
"Ki ukweli siko sawa, nitakuwa sawa kama utanijibu kwa uaminifu maswali yote nitakayokuuliza Osward" alisema Najma huku akikaa vizuri kwenye kiti
"Swali gani? uliza tu"
"Nataka kujua zile Safari ambazo baba alikuwa akikuagiza kwenda Mexico ulikuwa unaenda kufanya nini?" Najma aliuliza swali lililomfanya Osward ashtuke lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake
"Kwani kuna nini mbona ghafula?"
"Ghafula nini si unijibu tu"
"Aah! Ni..nimambo mambo fulani fulani tu ee...lakini sana nilikuwa naenda kusimamia biashara zake kule Mexico"
"Biashara gani? nazijua bishara zote anazofanya baba sijawahi sikia hata siku moja akasema anabiashara Mexico unanidanganya Osward"
"Ni kweli anabi..."
"Sikia acha nikurahisishie swali naona unataka kuzunguuka sana, ni hivi unaelewa nini kuhusu virusi vya COBOS?" Najma alibadilisha swali lililomfanya Osward ashtuke sana hakuweza kuficha mshtuko wake tena.
"Nambie unajua nini ku..."
"Shiii!! Shiii! Najma tulia hutakiwi kutaja hilo neno hapa" alisema Osward huku akimtaka Najma anyamaze
"Kwa nini?"
Osward aliangaza macho huku na huku kisha akamsogelea Najma na kuongea kwa sauti ya chini
"Kuwa makini na hilo neno, utajitafutia matatizo"
"Kwa nini?"
"Najma nakuomba nakuomba sana kama umeanza au unataka kufuatilia kuhusu virusi vya COBOS basi acha sasa hivi kabla hujafika mbali, hili ni suala nyeti sana, kuna watu wakubwa na wazito wako nyuma ya hii ishu Najma sitaki kupoteza mpenzi wangu naomba acha na hili suala mara moja" Osward aliongea kwa msisitizo tena kwa kumaanisha sana huku akiwa ameikukutanisha mikono yake kama mtu anayeomba toba.
Najma alibaki katika hali ya mshangao, hakuelewa ni kwa nini Osward aliongea kwa uzito kiasi kile hapo akili yake ikafunguka akaamini kuwa suala la virusi vya COBOS ni kweli lipo na nizito sana, baba yake Dokta Gondwe anahusika pia.
Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA...
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
22-(Kikosi cha Kunguru weusi)
ILIPOISHIA...
Vita kali inaibuka ndani na nje ya boti iliyokuwa ikienda kwa kasi, ni vita kati ya Tino anayemzuia Jasusi Shadow asiondoke na sanduku lenye vimelea vya V-COBOS wakati huo huo ndani ya boti hiyo mapigano makali kati ya Bosco na Wazari wa afya Dokta Gondwe yalikuwa yakiendela
Upande wa pili Najma anaanza kufuatilia na kuuchimba ukweli kuhusu vimelea vya V-COBOS.
Jez nini kitafuata?
SASA ENDELEA....
Shadow alikimbia akapanda juu kabisa ya boti Tino naye akamfuata hakutaka kumpa upenyo wa kuondoka na lile sanduku. Sasa walikuwa juu kabisa ya boti hiyo iliyokua ikienda kwa kasi ikipasua mawimbi ya bahari ya hindi. Si Shadow wala si Tino wote walikuwa vizuri kwenye suala zima la mapambano ya bila kutumia siraha.
Mara punde purukushani kati ya Bosco na Waziri wa afya Dokta Gondwe ilihama kutokea ndani ya boti sasa wakahamia nje. Hapo Dokta Gondwe aliweza kumuona Tino akipigana na yule mtu aliyeondoka na sanduku lake lakini cha ajabu Dokta Gondwe hakutaka kushughulika naye yeye akaendelea kukomaa na Bosco.
"Huwezi kuondoka hapa mpaka uniambie ni wapi ilipo dawa ya virusi vya COBOS" Dokta Gondwe aliongea kwa nguvu huku akifuta damu iliyokuwa ikimtoka puani
"Unajisumbua bure Dokta hupati chochote kutoka kwangu, na nitahakikisha nasambaza picha zako chafu mtandaoni" Bosco alijibu huku akitema damu
"Siwezi kukupa hiyo nafasi kijana leo ni ama zako ama zangu" alisema Dokta Gondwe huku akikimbia na kwenda kumvaa Bosco kwa mara nyingine wakaanza tena kupigana. Wakati huo pia juu ya boti bado mpambano kati ya Tino na Jasusi Shadow ulizidi kupamba moto.
Boti iliyokuwa ikienda kwa kasi bila kuongozwa na mtu yeyote sasa ilikuwa ikielekea nchi kavu ikiwa ibakiza mita chache kugusa ardhi mara Jasusi Shadow alilishika lile sanduku kisha akalitupa ndani ya maji kitendo hicho kilimshangaza sana Tino na kwakuwa hakutaka kuvipoteza vimelea vya V-COBOS haraka alijitosa majini kulifuata sanduku lile, sekunde chache baadae Jasusi Shadow naye akajitosa majini kumfuata.
Boti ilienda kwa kasi ikatoka ndani ya maji nakupaa juu mita chache kisha ikatua nchi kavu na kupinduka upande mmoja. Dokta Gondwe na Bosco ambao walikuwa hawelewi hili wala lile wajikuta wakijipigiza vibaya kwenye kuta za boti hiyo
Dokta Gondwe aliumia vibaya mno, aliinuka kwa kujikongoja akatazama pande zote na hapo ndipo alipobaini kuwa boti ilikuwa nchi kavu kwa sasa, aliendelea kuangaza macho yake kila mahali hakumuona Bosco, hakumuona Tino wala Jasusi Shadow.
"Ameenda wapi huyu mpuuzi?" alisema Dokta Gondwe huku akishuka kutoka kwenye boti akazunguuka upande wa pili kuangalia, hakuona mtu lakini mara alisikia vishindo nyuma yake akageuka haraka kuangalia hapo ndipo alimuona Bosco kwa mbali akikimbia kuelekea msituni. Dokta Gondwe hakuwa na nguvu kabisa ya kuendelea kumfuatilia, tayari alikuwa amejeruhiwa na kuchoka karibu kile sehemu ya mwili wake, alikuwa hoi.
Dokta Gondwe aliutazama ule msitu mdogo alikokimbilia Bosco kisha akafungua simu yake akaangalia ramani ya eneo hilo, mara akatabasamu.
"Huwezi kwenda kokote kijana lazima nikupate" alisema Dokta Gondwe baada ya kubaini kuwa kule alikokwenda Bosco ilikuwa ni Rasi yaani sehemu ya ardhi iliyoingia majini, kwa maana hiyo ili Bosco atoke ilikuwa ni lazima arudi alikotoka kwani alikoenda ilikuwa ni sehemu iliyozunguukwa na maji pande zote tatu.
Dokta Gondwe alibinya simu yake akapiga namba fulani kisha akaweka simu sikioni.
"Hallo"
"Ndiyo bosi nakusikia" sauti nzito ilisikika upande wa pili
"Nahitaji msaada njoo na kikosi chote cha Kunguru weusi nakutumia ramani nilipo, nawahitaji sasa hivi"
"Sawa bosi, lakini Kamanda Tino hayupo aliondoka asubuhi sana aka...."
"Nyie njooni Tino mtamkuta huku"
Aliongea Dokta Gondwe akakata simu kisha akamtumia mtu huyo uelekeo wa mahali alipo. Baada ya hapo alituma ujumbe mfupi wa maandishi kwenda kwa Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa.
,,,,,,,,,,,,Profesa nimefanya kama ulivyonishauri lakini mambo ni mazito sana huku baharini, yaani huwezi kuamini Waziri mkubwa kama mimi nahangaika huku badala ya kukaa bungeni, hawa wamexico wananitesa sana najuta kuchua ofa yao kweli nitafika mbinguni nimechoka sana,,,,,,,,,,
Baada ya kutuma ujumbe huo Dokta Gondwe alipiga hatua akaenda kukaa pembeni ya ile boti kusubiri kikosi cha Kunguru weusi. Jambo la ajabu ni kwamba alikuwa hajali kabisa kuhusu Tino na yule mtu aliyechukua sanduku lake, akili yake yote iliielekeza kwa Bosco
Vita ya Tino na Jasusi Shadow haikuishia kwenye ile boti, bado iliendelea hata ndani ya maji. Wakati Tino akilifuata sanduku lililokuwa linazama kwenye kina kirefu cha bahari Jasusi Shadow naye alikuwa nyuma yake akiogerea kwa kasi kumfuata. Wote walionekana ni wazoefu wa kuogerea na jambo lingine muhimu kila mmoja alikuwa na mtungi wa gesi uliomsaidia kupumua akiwa ndani ya maji.
Waliendelea kuvutana na kugeuzana wakiwa ndani ya maji kila mmoja akitaka kuwa wa kwanza kulifikia sanduku lile. Mwisho walizama mpaka chini kabisa wakagusa ardhi chini ya bahari. Jasusi Shadow alipata mwanya akafanikiwa kumbana vizuri Tino kisha akamchomolea ule mpira unaopitisha gesi kutoka kwenye mtungi akaukata kabisa, hapo Tino alijikuta anaanza kutapatapa baada ya kukosa hewa, mbaya zaidi walikuwa wamezama kwenye kina kirefu cha maji haikuwa rahisi kupata pumzi ya kutosha itakayomuwezesha kufika juu.
Jasusi Shadow alisogea hadi lilipo sanduku akalichukua kisha akaanza kuogerea kupanda juu akimfuata Tino ambaye kwa sasa alikuwa anaelekea kupoteza fahamu baada ya kukosa hewa na kunywa maji mengi.
Shadow alimfikia Tino akamshika na kuogerea naye hadi alipotokeza juu ya maji wakati huo tayari Tino alikuwa amepoteza fahamu hajitambua. Shadow alimbeba na kutoka naye hadi nchi kavu, akamlaza chini kisha akaanza kumminya tumbo kwa nguvu, Tino akawa anayatapika maji mengi aliyokunywa bila kupenda yakatokea mdomoni na puani. Shadow hakutaka kumuacha Tino afe, hilo halikuwa agizo la Sultana bosi wake ambaye pia alikuwa ni mama mzazi wa Tino, licha ya wanafamilia hao wawili kuwa na vita kali wakipigania vimelea vya V-COBOS lakini hakuna siku Sultana alimuagiza Shadow amuue Tino.
Baada ya kutoa huduma hiyo ya kwanza Shadow alimbeba Tino akaingia naye msituni hatua kadhaa kutoka usawa wa bahari akachukua kamba na kumfunga chini ya mti mmoja mkubwa. Wakati huo wote Tino alikuwa hajitambua.
Shadow alichukua lile sanduku akamtazama Tino kwa sekunde kadhaa kisha akageuka na kuondoka zake, akatokomea msituni.
Upande wa pili ndani ya gereza la Kanondo, gereza ambalo wafungwa walikuwa wakiishi maisha malaini sana tofauti kabisa na magereza mengine. Hapo ndipo alipokuwa ameifadhiwa kijana Osward mtoto wa kigogo mmoja maarufu kama mzee Matula, alikuwa hapo kwa zaidi ya miezi mitatu akisubiri kesi yake ya mauaji iliyokuwa bado inaendelea kuunguruma mahakamani.
Najma alifika kwa ajili ya kufanya mazungumzo nyeti na Osward ambaye alifurahi sana baada ya kumuona kwa mara nyingine tangu alipomuona siku iliyopita.
"Siamini kama umekuja kuniona tena Najma, nilipoambiwa na askari kuwa kuna mwanamke amekuja kuniona nikawa najiuliza ni nani huyo kumbe ni wewe mpenzi" Alisema Osward huku furaha yake ikionekana wazi kwa nuru iliyokuwa inang'aa usoni kwake, hakika alikuwa akimpenda sana Najma.
"Hebu kaa nina mazungumzo muhimu na wewe" Alisema Najma huku akionekana kutofurahiswa hata kidogo na maneno ya Osward.
"Sawa nimekaa, nambie mguu wako unaendeleaje?"
"Salama nilishapona"
"Kwa nini jana ukakubali kuondoka na inspekta Aron hujui kama yule ni adui yetu mkubwa na ndio sababu ya mimi kuendelea kuwa humu hadi leo?"
"Anafanya kazi yake acha kumlaumu, kama hukuua basi ukweli utajulikana tu kuwa mpole"
"Mmh mbona leo wewe ni mkali hivyo, uko sawa kweli Najma wangu?"
"Ki ukweli siko sawa, nitakuwa sawa kama utanijibu kwa uaminifu maswali yote nitakayokuuliza Osward" alisema Najma huku akikaa vizuri kwenye kiti
"Swali gani? uliza tu"
"Nataka kujua zile Safari ambazo baba alikuwa akikuagiza kwenda Mexico ulikuwa unaenda kufanya nini?" Najma aliuliza swali lililomfanya Osward ashtuke lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake
"Kwani kuna nini mbona ghafula?"
"Ghafula nini si unijibu tu"
"Aah! Ni..nimambo mambo fulani fulani tu ee...lakini sana nilikuwa naenda kusimamia biashara zake kule Mexico"
"Biashara gani? nazijua bishara zote anazofanya baba sijawahi sikia hata siku moja akasema anabiashara Mexico unanidanganya Osward"
"Ni kweli anabi..."
"Sikia acha nikurahisishie swali naona unataka kuzunguuka sana, ni hivi unaelewa nini kuhusu virusi vya COBOS?" Najma alibadilisha swali lililomfanya Osward ashtuke sana hakuweza kuficha mshtuko wake tena.
"Nambie unajua nini ku..."
"Shiii!! Shiii! Najma tulia hutakiwi kutaja hilo neno hapa" alisema Osward huku akimtaka Najma anyamaze
"Kwa nini?"
Osward aliangaza macho huku na huku kisha akamsogelea Najma na kuongea kwa sauti ya chini
"Kuwa makini na hilo neno, utajitafutia matatizo"
"Kwa nini?"
"Najma nakuomba nakuomba sana kama umeanza au unataka kufuatilia kuhusu virusi vya COBOS basi acha sasa hivi kabla hujafika mbali, hili ni suala nyeti sana, kuna watu wakubwa na wazito wako nyuma ya hii ishu Najma sitaki kupoteza mpenzi wangu naomba acha na hili suala mara moja" Osward aliongea kwa msisitizo tena kwa kumaanisha sana huku akiwa ameikukutanisha mikono yake kama mtu anayeomba toba.
Najma alibaki katika hali ya mshangao, hakuelewa ni kwa nini Osward aliongea kwa uzito kiasi kile hapo akili yake ikafunguka akaamini kuwa suala la virusi vya COBOS ni kweli lipo na nizito sana, baba yake Dokta Gondwe anahusika pia.
Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA...