Just Nana
JF-Expert Member
- Jul 27, 2023
- 500
- 1,001
SEHEMU YA KWANZA:
Nyarugusu- Kigoma, Tanzania
Hofu ilikua imetanda miongoni mwetu, kina mama walikumbatia watoto wao, zaidi ya vilio vya watoto hakuna sauti nyingine iliyosikika, hata ndege pia walihofia kukaa karibu nasi, zilianza kama tetesi zilizofatiwa na hekaheka za wahudumu wa afya waliohudumu kambini pale, palikua na kila dalili kua pana jambo kubwa linaendelea na ni kama lilikua linawashinda nguvu kulidhibiti, baada ya siku chache ndio tunakuja kupata taarifa sahihi, kambi ilikua imevamiwa na gonjwa hatari la kipindupindu, msongamano wa watu ulisababisha huduma mbovu za kijamiii, vyoo vilikua havitoshelezi, maji ya kunywa yalikua ni changamoto, watu mamia kwa mamia walikua wamefululiza kuja ndani ya siku tatu zilizopita kufuatia mgogoro wa kivita uliokua unaendelea huko Kongo. Tahadhari ilitolewa ikiambatana na elimu jinsi ya kujikinga na gonjwa hilo hatari, dalili zikaelezwa pia ili atakapobainika mgonjwa mwenye dalili hizo awahishwe mara moja kwenye hema maalumu. Nilijitahidi kufumba macho japo nipate usingizi lakini kumbukumbu chungu ikapita kwenye fikra zangu, kumbukumbu ya miaka saba iliyoacha makovu mengi yasiyo na idadi mwilini na moyoni mwangu.
Ilikua ni usiku wa kuamkia jumapili, tulikua tumeshafanya maandalizi yote ya kuondoka afajiri ya siku inayofuata, hali ya usalama ilizidi kua mbaya, maelfu na maelfu ya watu walikua wameuawa kwa kukatwa mapanga ama kupigwa risasi. Hofu ilitanda kote, hakuna huduma yoyote ya kijamii iliyokua inapatikana, ni kama tuliachwa tuchinjane tumalizane wenyewe kwa wenyewe, nilikua nina miaka tisa wakati hayo yanatokea, bado naikumbuka ile siku kama ilitokea jana tuu, ni siku iliyonipa jina rasmi la mkimbizi.
Tulikua tumejificha kwa rafiki wa baba ambae alikua mwanajeshi, nyumba za jeshi zilikua hazikaguliwi labda wakipata mashaka na uungaji wako mkono katika kile walichokiita kusafisha nchi dhidi ya uchafu ulioachwa na wabelgiji. Tusingeweza kuendelea kujificha ,ilikua ni lazma tuondoke, rafiki wa baba alitoka usiku ule kwenda kuazima gari ya jeshi la kuweza kutusogeza hadi mpakani , kulikua hakuna namna tungeweza kutoka Rwanda kwa usafiri wa kawaida, magari yote yalikua yanakaguliwa, ilikua nafuu kidogo kama una gari la jeshi.
Tulisubiri kwa zaidi ya masaa manne bila ya dalili ya yule mwanajeshi kurudi, hakukua na namna hata ya kupiga simu maana simu pekee zilikua zinatumika kipindi kile zilikua ni simu za mezani tu, katikati ya kusubiri tukaanza kusikia milio ya risasi, haikua mara ya kwanza kusikia risasi ikilia ila ile siku ilikua tofauti maana milio ya risasi ilikua ni mingi na ikawa inazidi kusogea tulipo, kwa kipindi kile sikumudu kugundua aina gani ya bunduki ilitumika, ila kwa shule ya vitendo ya miaka saba porini ilinitosha kujua kila aina ya bunduki, mataifa zinapotoka na nguvu iliyonayo, kwa sasa naweza sema kua ile milio ilikua ni ya bunduki hatari sana ya kivita inayoitwa AK-47, ugunduzi wa Mrusi Kalashnikov, laiti kama huyu bwana angepata maono ya maafa ambayo bunduki yake ingeyaleta ulimwenguni hasa Africa na Mashariki ya kati , sidhani kama angeendelea na ugunduzi wake.
Tulijikusanya pamoja, mimi na familia yangu pamoja na familia ya yule mwanajeshi ambayo kwa wakati huo alikua amebaki mkewe, watoto wao wakike wawili na kijana wa kazi. Ile familia walikua wahutu, wakati sisi tulikua mchanganyiko, baba Mhutu na mama Mtutsi, watoto wawili kati ya watatu tuliozaliwa na baba na mamangu tulikua na mfanano wa kihutu wakati mdogo wetu wa mwisho alikua ana muonekano wa kitutsi. Haya yalikua ni makabila makubwa na yenye uhasama sana Rwanda.
Kilisikika kishindo cha nguvu ,gari la jeshi liliingia kwa fujo pale ndani likiwa limelizoa geti kubwa la kuingilia, yaani hawakuona kama palikua na uhitaji wa kugonga geti wakamua kuingia nalo. Kwa akili ya utoto tuliona kelele zingetusaidia, kila mtu alikua amepanick, mama alitukumbatia kwa nguvu, bado nalikukumbuka like kumbatio, bado nalikumbuka, lilikua ni kumbatio la mwisho kukumbatiwa kwa upendo wa ndani kabisa. Teke moja lilitosha kuusambaratisha mlango wa kuingilia ndani , waliingia wanajeshi wasiopungua nane wakiwa wameongozana na kundi la wanajeshi wasio rasmi maarufu Kama interahamwe.
Tuliamuliwa wote tupige magoti, mama mwenye nyumba alimtambua mmoja kati ya wale wanajeshi kua ni kati ya marafiki wakubwa wa mumewe, akawa anajitahidi kumchangamkia ili atusaidie, alipigwa teke moja takatifu akaangukia sakafu, alifikia mdomo, Sina hakika kama bado anamiliki meno yake ya mbele kama alifanikiwa kunusurika.
Walitoa amri moja tuuu, inyenzi wote kaa upande wa kulia, tukawa tunavutana na kung'ang'aniana, hakuna aliekua tayari kumuachia mwenzie, aliyempiga kofi mke wa yule mwanajeshi alietupa hifadhi kwake alikuja hadi tuliposimama na mama angu, akamnyakua mdogo angu wa mwisho wa miezi nane, alimrusha ukutani kwa nguvu ,damu ya moto ilinirukia usoni, mdogo angu alitoa sauti hafifu na kukaa kimya. Utulivu pale ndani ulipotea, ile kauli ikarudiwa tena, inyenzi pita upande wa kulia, kifo kisikie tu kwa mbali, yule kijakazi wa mwenye nyumba akawa anatusukuma mimi na familia yangu, hawa hapa inyenzi...hawa hapa inyenzi...
Ilitolewa amri ya kua mimi na kakangu tukabidhiwe mapanga, sikuwahi hata kuchinja kuku hapo kabla, nilikua naogopa sana damu, eti leo nakabidhiwa panga niue binadamu, hapana...tena mamangu mzazi,mama alikua ananisitiza nifanye wanavyotaka ili mimi na kakangu tupone, machozi hayakuacha kunitoka. Nikiwa katika kushangaa nini kinaendelea , kuipa mda akili ikubaliane na uhalisia, yule kijakazi wa mwenye nyumba alininyang'anya lile panga, kwa kasi akamrukia mama angu na kuanza kumcharanga kama nyama buchani....
Nyarugusu- Kigoma, Tanzania
Hofu ilikua imetanda miongoni mwetu, kina mama walikumbatia watoto wao, zaidi ya vilio vya watoto hakuna sauti nyingine iliyosikika, hata ndege pia walihofia kukaa karibu nasi, zilianza kama tetesi zilizofatiwa na hekaheka za wahudumu wa afya waliohudumu kambini pale, palikua na kila dalili kua pana jambo kubwa linaendelea na ni kama lilikua linawashinda nguvu kulidhibiti, baada ya siku chache ndio tunakuja kupata taarifa sahihi, kambi ilikua imevamiwa na gonjwa hatari la kipindupindu, msongamano wa watu ulisababisha huduma mbovu za kijamiii, vyoo vilikua havitoshelezi, maji ya kunywa yalikua ni changamoto, watu mamia kwa mamia walikua wamefululiza kuja ndani ya siku tatu zilizopita kufuatia mgogoro wa kivita uliokua unaendelea huko Kongo. Tahadhari ilitolewa ikiambatana na elimu jinsi ya kujikinga na gonjwa hilo hatari, dalili zikaelezwa pia ili atakapobainika mgonjwa mwenye dalili hizo awahishwe mara moja kwenye hema maalumu. Nilijitahidi kufumba macho japo nipate usingizi lakini kumbukumbu chungu ikapita kwenye fikra zangu, kumbukumbu ya miaka saba iliyoacha makovu mengi yasiyo na idadi mwilini na moyoni mwangu.
Ilikua ni usiku wa kuamkia jumapili, tulikua tumeshafanya maandalizi yote ya kuondoka afajiri ya siku inayofuata, hali ya usalama ilizidi kua mbaya, maelfu na maelfu ya watu walikua wameuawa kwa kukatwa mapanga ama kupigwa risasi. Hofu ilitanda kote, hakuna huduma yoyote ya kijamii iliyokua inapatikana, ni kama tuliachwa tuchinjane tumalizane wenyewe kwa wenyewe, nilikua nina miaka tisa wakati hayo yanatokea, bado naikumbuka ile siku kama ilitokea jana tuu, ni siku iliyonipa jina rasmi la mkimbizi.
Tulikua tumejificha kwa rafiki wa baba ambae alikua mwanajeshi, nyumba za jeshi zilikua hazikaguliwi labda wakipata mashaka na uungaji wako mkono katika kile walichokiita kusafisha nchi dhidi ya uchafu ulioachwa na wabelgiji. Tusingeweza kuendelea kujificha ,ilikua ni lazma tuondoke, rafiki wa baba alitoka usiku ule kwenda kuazima gari ya jeshi la kuweza kutusogeza hadi mpakani , kulikua hakuna namna tungeweza kutoka Rwanda kwa usafiri wa kawaida, magari yote yalikua yanakaguliwa, ilikua nafuu kidogo kama una gari la jeshi.
Tulisubiri kwa zaidi ya masaa manne bila ya dalili ya yule mwanajeshi kurudi, hakukua na namna hata ya kupiga simu maana simu pekee zilikua zinatumika kipindi kile zilikua ni simu za mezani tu, katikati ya kusubiri tukaanza kusikia milio ya risasi, haikua mara ya kwanza kusikia risasi ikilia ila ile siku ilikua tofauti maana milio ya risasi ilikua ni mingi na ikawa inazidi kusogea tulipo, kwa kipindi kile sikumudu kugundua aina gani ya bunduki ilitumika, ila kwa shule ya vitendo ya miaka saba porini ilinitosha kujua kila aina ya bunduki, mataifa zinapotoka na nguvu iliyonayo, kwa sasa naweza sema kua ile milio ilikua ni ya bunduki hatari sana ya kivita inayoitwa AK-47, ugunduzi wa Mrusi Kalashnikov, laiti kama huyu bwana angepata maono ya maafa ambayo bunduki yake ingeyaleta ulimwenguni hasa Africa na Mashariki ya kati , sidhani kama angeendelea na ugunduzi wake.
Tulijikusanya pamoja, mimi na familia yangu pamoja na familia ya yule mwanajeshi ambayo kwa wakati huo alikua amebaki mkewe, watoto wao wakike wawili na kijana wa kazi. Ile familia walikua wahutu, wakati sisi tulikua mchanganyiko, baba Mhutu na mama Mtutsi, watoto wawili kati ya watatu tuliozaliwa na baba na mamangu tulikua na mfanano wa kihutu wakati mdogo wetu wa mwisho alikua ana muonekano wa kitutsi. Haya yalikua ni makabila makubwa na yenye uhasama sana Rwanda.
Kilisikika kishindo cha nguvu ,gari la jeshi liliingia kwa fujo pale ndani likiwa limelizoa geti kubwa la kuingilia, yaani hawakuona kama palikua na uhitaji wa kugonga geti wakamua kuingia nalo. Kwa akili ya utoto tuliona kelele zingetusaidia, kila mtu alikua amepanick, mama alitukumbatia kwa nguvu, bado nalikukumbuka like kumbatio, bado nalikumbuka, lilikua ni kumbatio la mwisho kukumbatiwa kwa upendo wa ndani kabisa. Teke moja lilitosha kuusambaratisha mlango wa kuingilia ndani , waliingia wanajeshi wasiopungua nane wakiwa wameongozana na kundi la wanajeshi wasio rasmi maarufu Kama interahamwe.
Tuliamuliwa wote tupige magoti, mama mwenye nyumba alimtambua mmoja kati ya wale wanajeshi kua ni kati ya marafiki wakubwa wa mumewe, akawa anajitahidi kumchangamkia ili atusaidie, alipigwa teke moja takatifu akaangukia sakafu, alifikia mdomo, Sina hakika kama bado anamiliki meno yake ya mbele kama alifanikiwa kunusurika.
Walitoa amri moja tuuu, inyenzi wote kaa upande wa kulia, tukawa tunavutana na kung'ang'aniana, hakuna aliekua tayari kumuachia mwenzie, aliyempiga kofi mke wa yule mwanajeshi alietupa hifadhi kwake alikuja hadi tuliposimama na mama angu, akamnyakua mdogo angu wa mwisho wa miezi nane, alimrusha ukutani kwa nguvu ,damu ya moto ilinirukia usoni, mdogo angu alitoa sauti hafifu na kukaa kimya. Utulivu pale ndani ulipotea, ile kauli ikarudiwa tena, inyenzi pita upande wa kulia, kifo kisikie tu kwa mbali, yule kijakazi wa mwenye nyumba akawa anatusukuma mimi na familia yangu, hawa hapa inyenzi...hawa hapa inyenzi...
Ilitolewa amri ya kua mimi na kakangu tukabidhiwe mapanga, sikuwahi hata kuchinja kuku hapo kabla, nilikua naogopa sana damu, eti leo nakabidhiwa panga niue binadamu, hapana...tena mamangu mzazi,mama alikua ananisitiza nifanye wanavyotaka ili mimi na kakangu tupone, machozi hayakuacha kunitoka. Nikiwa katika kushangaa nini kinaendelea , kuipa mda akili ikubaliane na uhalisia, yule kijakazi wa mwenye nyumba alininyang'anya lile panga, kwa kasi akamrukia mama angu na kuanza kumcharanga kama nyama buchani....