SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,275
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.........01
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
UTANGULIZI
Mwanzo ilikuwa ni vita rahisi sana, vita dhidi ya ndugu yangu wa damu aliyeenda kinyume na kanuni za maisha ya utu. Sikujua kwa kufanya hivi ningeamsha vita nyingine kubwa ambayo ipo juu kabisa ya uwezo wangu na uwezo wa nchi yangu. Vita na ndugu yangu imegeuka na kuwa vita ya ulimwengu mzima.
Cha ajabu ni kwamba ili kushinda vita hii haihitaji mtutu wa bunduki wala siraha yoyote. Natamani kuacha kupambana lakini siwezi kwa sababu tayari nimeshaanza. Kuendelea maana yake nimekubali kuwakabili maadui wenye rangi nyeupe ambao wamejipanga kwa zaidi ya miaka 10 kuhakikisha wanashinda.
Hatima ya Dunia yangu, Nchi yangu, Rais wangu, ndugu na familia yangu ipo mikononi mwangu. Kwa bahati mbaya ni kwamba licha ya nchi yangu kuwa na uwezo mdogo wa kupambana lakini imejikuta inatumika kama chungu cha kuandalia vita hii kali bila kujua, isitoshe tunapigana na kitu tusichokiona.
Naweza kusema sasa ni wakati wa mapenzi, sayansi na teknolojia kuipeleka Dunia vile inavyotaka.
Naam kwa mara ya kwanza historia inakwenda kuandikwa, historia ya vita ambayo haijawahi kutokea popote duniani, ndio sababu nasema hii ni VITA YA KISASA (THE MODERN WAR) niite Inspekta Aron"
SEHEMU YA KWANZA- (KIFO CHA SHAHIDI WA MWISHO)
SASA TUANZE SIMULIZI YETU....
"Mume wangu niue mimi, muache mwanangu aishi tafadhali bado ni binti mdogo naomba usimuue"
"Mama naogopa...!"
"Usiogope mwanangu kila kitu kitakuwa sawa, usijali sawa Annah"
"Mheshimiwa, mtihani ulionipa ni mgumu sana hivi nawezaje kumuua mwanangu au mke wangu, naanzaje kumwaga damu zao"
"Kama huwezi basi acha nitakusaidia mimi mwenyewe, nimekwambia chagua moja umuue mtoto wako au mke wako"
"Mheshimiwa siwezi tafadhali nipe adhabu nyingine, waache mke wangu na mwanangu waondoke nitafanya chochote unachotaka, niko chini ya miguu yako mkuu"
Haya yalikuwa ni mazungumzo ya watu zaidi ya watano waliokuwa ndani ya jengo moja chakavu lililokuwa limetelekezwa kabla ya ujenzi kukamilika, jengo hilo lilikuwa limejitenga pembeni kidogo ya mji.
Alikuwepo Dokta Isaack Gondwe ambaye ni waziri wa afya akiwa na vijana watatu nyuma yake ambao wote walikuwa wameziba nyuso zao kwa vitambaa vyeusi. Walikuwa wamesimama mbele ya familia moja ya watu watatu yaani baba mama na binti yao mdogo mwenye umri wa miaka 22 aliitwa Annah.
"Baba Annah nimekukabidhi bastola umuue mmoja kati ya mke au mtoto wako kisha nikuache uende lakini umeshindwa, basi acha vijana wangu wafanye kazi yao" alisisitiza Dokta Gondwe huku akibinua mabega yake kwa kejeri
Kwa mara nyingi tena Baba Annah aliinua juu mkono wake wa kulia ulioshikilia bastola akaielekeza walipokuwa wamesimama mke na binti yake Annah, hali akitetemeka alivuta pumzi ndevu na kuishusha taratibu, kijasho chembamba kikawa kinamtoka mzee huyo.
Mama Annah alimkumbatia binti yake akamziba usoni na kiganja cha mkono wake hakutaka mwanae aone kinachoendelea, naye akafumba macho kwa uchungu akiwa tayari kwa lolote litakalotokea.
Mara ghafula Baba Annah aligeuka kwa kasi akabadilisha uelekeo na kuilekeza bastola yake walipokuwa wamesimama Mheshimiwa dokta Isaack Gondwe na vijana wake, bila kusita akabinya kitufe cha kufyatua risasi huku akiwa amemlenga Dokta Isaack Gondwe kichwani lakini risasi haikutoka ,akajaribu tena mara ya pili na ya tatu lakini hali ikawa ni ile ile, baba Annah akahisi kuchanganyikiwa.
"Hahahah, ha ha ha, ha ha ha haaa" Dokta Gondwe alicheka tena kwa sauti kubwa sana, kisha akaongea
"Nilijuaa...! nilijua tu wewe ni msaliti, unajifanya mjanja sio? ona sasa umeumbuka mbele ya familia yako mzee hii ni mara ya pili unanisaliti, niliwaomba msitoe ushahidi wowote mahakamani lakini mkapanga kunigeuka wewe na familia yako pamoja na kukuhonga pesa nyingi bado ukapanga kunigeuka. Sasa unanisaliti tena kwa mara ya pili unataka kuniua, bahati mbaya bastola niliyokupa haina risasi hahahaha"
"Ulaaniwe Dokta Gondwe, mungu akulaani, utakufa kifo kibaya, wewe na watu wako wote mtakufaa, hata hicho cheo ulichonacho najua ni cha dhuruma, nakwambia utakufa" Baba Annah aliishia kutoa laana kwa mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe mara baada ya kubaini kuwa hana ujanja tena.
"Acha makelele yako, laana kama hizo zilishakuja nyingi sana, hata marehemu mama yangu alinilaani tangu nikiwa tumboni lakini hadi leo hakuna laana iliyofanya kazi" alisema Dkt Gondwe huku akiinamisha kichwa chake chini kutega sikio kumsikiliza kijana wake mwingine ambaye aliingia ndani ya jengo hilo wakati anazungumza.
Kijana huyo hakuwa amefunika sura yake kama wengine, alimnong'oneza maneno kadhaa kwa takribani sekunde 30 hivi, Dokta Gondwe akaonekana kushtuka kiasi kisha akapaza sauti akifoka.
"Kwa nini, kwa nini kila siku yeye tu? hii inawezekanaje? kajuaje tuko hapa? huyu mdogo wako anataka nini? kwa nini unashindwa kumdhibiti? hivi askari ni yeye tu hakuna wengine aah!" Dkt Gondwe alifoka huku akiondoka, akapiga hatua kadhaa kisha akageuka tena.
"Unajua cha kufanya Tino, natangulia kwenye gari" alisema Dkt Gondwe kisha akatoka nje ya lile jengo.
Tino ambaye ndiye aliyeonekana kuwa na mamlaka kuliko vijana wengine wa Dkt Gondwe, alichomoa bastola iliyokuwa kiunoni kwake. Bila kuuliza alimfyatulia risasi Baba Annah, risasi iliyopenya sikio la kushoto ikatokea sikio la kulia, alifanya hivyo pia kwa Mama Annah, kisha akamalizia kumpiga risasi ya kifua Annah. wote wakaanguka chini na kupoteza maisha.
Lilikuwa ni tukio kubwa na zito, kuua watu watatu kwa wakati mmoja. Lakini kwa Tino ilikuwa ni tofauti kabisa, alifanya kwa urahisi sana kama anakunywa maji vile, ilionyesha wazi hii ilikuwa ni kazi aliyoizoea.
Baada ya kufanya hivyo Tino na wale vijana wengine waliandaa mazingira kuonyesha kuwa Baba Annah alimuua mke na mtoto wake kwa kuwapiga risasi kisha na yeye akamalizia kwa kujipiga risasi mwenyewe.
Baadae walitoka na kuingia ndani ya gari mbili zilizoegeshwa nje ya jengo hilo, wakaondoka kwa kasi kuwakimbia polisi ambao kwa mujibu wa maelezo ya Dokta Gondwe alimaanisha wapo njiani wanakuja na mmoja kati ya polisi hao ni mdogo wake na kijana wake wa kazi yaani Tino.
⭐⭐⭐
Ni kweli, dakika chache tu baada ya Dokta Gondwe na vijana wake kuondoka, gari za polisi zisizopungua sita zilifika na kufunga breki kali nje ya jengo hilo na punde polisi walishuka na kuanza kumiminika kwa kasi kuingia ndani ya jengo hilo huku siraha zao zikiwa mbele Ilikuwa ni ishara tosha kuwa polisi hawa walikuwa na taarifa kamili ya kile kilichokuwa kinaendelea ndani ya jengo hilo.
Walikagua vyumba vyote vya jengo hilo, hawakupata mtu yeyote zaidi ya miili ya Baba Annah mama Annah na Annah mwenyewe, kwa haraka haraka ilionyesha wazi kuwa Baba Annah ndiye aliyetekeleza mauwaji hayo kwani mkono wake wa kulia alishika bastola iliyotumika.
Lakini hicho sicho alichokuwa akikiona na kukiwaza Inspekta Aron, kijana ambaye ni polisi mpelelezi kutoka kituo cha kati Handeni. Yeye aliyatazama mazingira ya mle ndani kwa utulivu wa hali ya juu, akaitazama ile miili mmoja baada ya mwingine huku akichukua baadhi ya vielelezo muhimu kama ilivyokuwa ada kwa polisi wengine.
"Tumempoteza shahidi mwingine" Alisema Inspekta Jada, polisi ambaye alikuwa akifanya kazi kwa ukaribu sana na Aron. "Yah! tumechelewa kidogo sana, tungewahi tungeweza kuwaokoa pengine" alisema Aron huku akisogea pembeni pamoja na Jada wakiwaacha polisi wengine wakiendelea na kazi.
"Huenda walipata tena taarifa kama tunakuja" Alisema Jada
"Usiseme huenda, huo ndio ukweli wenyewe Inspekta Jada hii serikali ina watu wa hovyo sana" Aron alilalamika "Usijali Aron jitihada zako zitazaa matunda siku moja, ki ufupi unajituma sana, uwe na subra siku moja tutawakamata wote"
"Inshallah iwe hivyo, lazima nitamkamata Tino"
"Mmh! unahisi kaka yako Tino kahusika kwenye hili tukio pia"
" Ndiyo lazima alikuwepo hapa, subiri uone" Alisema Inspekta Aron akachukua simu yake akaitafuta namba aliyoihifadhi kwa jina la 'Bro Tino' akapiga. Simu iliita kwa dakika kadhaa bila kupokelewa mwisho ikakata, akapiga tena.
⭐⭐⭐
Upande wa pili Tino na bosi wake ambaye ni Waziri wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe tayari walishafika mjini. Tino akiwa ndiye dereva alikuwa ameegesha gari pembeni ya barabara na pembeni ya gari hiyo kulikuwa na gari nyingine ya serikali V8 ilikuwa imepaki ikimsubiri Dokta Gondwe ambaye bado alikuwa na mazungumzo na kijana wake tegemezi Tino.
"Tino, kama sikosei hii ni mara ya nne kama sio ya tano nakwambia kuhusu huyu mdogo wako Inspekta Aron unaemlealea sana, hili ni bomu ambalo litakuja kutulipukia baadae" Dkt Gondwe aliongea kwa msisitizo
"Usijali bosi, huyu ni mdogo wangu najua namna ya kumdhibiti niachie mimi, kuwa na amani bosi" Tino aliongea kwa kujiamini huku akipiga jicho pembeni kuitazama simu yake iliyokuwa ikiita mpigaji akiwa ni Aron mdogo wake.
"Haya mimi nakwenda, tayari tumeshaua mashahidi wote nina hakika tutashinda kesi mahakamani na mkwe wangu Osward atakuwa huru, lakini jua vita yetu bado ni kali sana na ndio kwanza tunaanza"
"Sawa mkuu"
Dkt Isaack Gondwe alishuka kwenye gari akapiga hatua na kuingia kwenye gari nyingine ile V8 dereva akawasha gari wakaondoka. Tino aligeuka na kuitazama simu ambayo ilikuwa ikiita kwa mara ya pili sasa, akapokea.
"Nambie dogo"
"Ulikuwa hapa Tino, ni wewe tena si ndiyo?" Inspekta Aron alisikika upande wa pili akiuliza
"Wapi mbona sikuelewi unazungumzia nini?"
"Najua unanielewa vizuri bro, sasa sikia nakuhakikisha kwamba lazima nitakukamata, nitathibitisha uchafu wako wote, mtafungwa wewe pamoja na mtandao wako mzima"
"Come down mdogo wangu, punguza vitisho huna ushahidi wowote wa kunifunga na hautokuja kufanikiwa kamwe, sahau" "Nisikilize kwa makini kaka labda nisiwe hai, yaani kwa mikono yangu nitakupeleke je..."
"Kaa kimya Aron huna faida yoyote wewe, nahangaika usiku na mchana kutafuta mamilioni ya pesa kwa ajili ya matibabu ya mama yetu, lakini wewe unafanya nini? unahangaika kutaka kunizuia, unaakili kweli wewe?"
"Mama yangu hawezi kuendelea kutibiwa kwa pesa zako chafu kaka, hata angekuwa anajitambua ninauhakika asingekubali hili"
"Kwa hiyo unatakaje, nimuache afe?"
"Kufa au kupona kwa mama yangu ni mpango wa Mungu sio wako Tino"
"Ni mama yetu sio mama yako, kumbuka hilo" alisema tino kisha akakata simu kwa hasira
"Vipi amesemaje?" Aliuliza Inspekta Jada mara tu baada ya kukata simu. "Kauli zake ni zile zile za kila siku, anadai anatafuta hela kwa ajili ya mama kule hospitali" Aron alijibu kinyonge.
"Pole Aron, nakuonea huruama sana, mungu akufanyie wepesi ni miezi sita mpaka sasa unapambana kwa ajili ya matibabu ya mama yako gharama ni kubwa lakini bado kaka yako naye anazidi kukuchanganya" alisema Inspekta Jada akionekana kuguswa na hali aliyokuwa akiipitia Inspekta Aron. Kabla Aron hajazunguza chochote mara kuna askari alionekana akikimbia kuwafuata, akafika na kusimama mbele yao huku akihema kwa nguvu.
"Vipi kwema?" aliuliza Aron akionekana mwenye shauku ya kujua kilichomleta, vivyo hivyo kwa Jada.
"Yu..yule binti kule nda..ndani ha..hajafa ni mzima" alisema yule askari kauli iliyowafanya Aron na Jada watazamane.
Je, nini kitafuata?
Nini hatima ya Vita kati ya ndugu hawa wawili yaani Aron na Tino?
Kwa nini Tino yupo karibu na Waziri wa afya?
Annah hajafa ni mzima huu unaweza kuwa ushahidi wa mwisho wa Inspekta Aron?
Kwa nini VITA YA KISASA?
Hii ni sehemu ya kwanza, majibu ya maswali haya utayapata ndani ya simulizi hii maridhawa iliyojaa visa vingi vya kusisimua. Mauaji, tamaa, mapenzi, urafiki, hila,chuki, drama, vita, usaliti, siasa, visasi, mahaba, kushinda na kushindwa pamoja na mambo mengine yasiyotazamiwa bila kusahau LOVE STORY kali ndani yake.
Naam hii ndio MODERN WAR(vita ya kisasa)
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.........01
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
UTANGULIZI
Mwanzo ilikuwa ni vita rahisi sana, vita dhidi ya ndugu yangu wa damu aliyeenda kinyume na kanuni za maisha ya utu. Sikujua kwa kufanya hivi ningeamsha vita nyingine kubwa ambayo ipo juu kabisa ya uwezo wangu na uwezo wa nchi yangu. Vita na ndugu yangu imegeuka na kuwa vita ya ulimwengu mzima.
Cha ajabu ni kwamba ili kushinda vita hii haihitaji mtutu wa bunduki wala siraha yoyote. Natamani kuacha kupambana lakini siwezi kwa sababu tayari nimeshaanza. Kuendelea maana yake nimekubali kuwakabili maadui wenye rangi nyeupe ambao wamejipanga kwa zaidi ya miaka 10 kuhakikisha wanashinda.
Hatima ya Dunia yangu, Nchi yangu, Rais wangu, ndugu na familia yangu ipo mikononi mwangu. Kwa bahati mbaya ni kwamba licha ya nchi yangu kuwa na uwezo mdogo wa kupambana lakini imejikuta inatumika kama chungu cha kuandalia vita hii kali bila kujua, isitoshe tunapigana na kitu tusichokiona.
Naweza kusema sasa ni wakati wa mapenzi, sayansi na teknolojia kuipeleka Dunia vile inavyotaka.
Naam kwa mara ya kwanza historia inakwenda kuandikwa, historia ya vita ambayo haijawahi kutokea popote duniani, ndio sababu nasema hii ni VITA YA KISASA (THE MODERN WAR) niite Inspekta Aron"
SEHEMU YA KWANZA- (KIFO CHA SHAHIDI WA MWISHO)
SASA TUANZE SIMULIZI YETU....
"Mume wangu niue mimi, muache mwanangu aishi tafadhali bado ni binti mdogo naomba usimuue"
"Mama naogopa...!"
"Usiogope mwanangu kila kitu kitakuwa sawa, usijali sawa Annah"
"Mheshimiwa, mtihani ulionipa ni mgumu sana hivi nawezaje kumuua mwanangu au mke wangu, naanzaje kumwaga damu zao"
"Kama huwezi basi acha nitakusaidia mimi mwenyewe, nimekwambia chagua moja umuue mtoto wako au mke wako"
"Mheshimiwa siwezi tafadhali nipe adhabu nyingine, waache mke wangu na mwanangu waondoke nitafanya chochote unachotaka, niko chini ya miguu yako mkuu"
Haya yalikuwa ni mazungumzo ya watu zaidi ya watano waliokuwa ndani ya jengo moja chakavu lililokuwa limetelekezwa kabla ya ujenzi kukamilika, jengo hilo lilikuwa limejitenga pembeni kidogo ya mji.
Alikuwepo Dokta Isaack Gondwe ambaye ni waziri wa afya akiwa na vijana watatu nyuma yake ambao wote walikuwa wameziba nyuso zao kwa vitambaa vyeusi. Walikuwa wamesimama mbele ya familia moja ya watu watatu yaani baba mama na binti yao mdogo mwenye umri wa miaka 22 aliitwa Annah.
"Baba Annah nimekukabidhi bastola umuue mmoja kati ya mke au mtoto wako kisha nikuache uende lakini umeshindwa, basi acha vijana wangu wafanye kazi yao" alisisitiza Dokta Gondwe huku akibinua mabega yake kwa kejeri
Kwa mara nyingi tena Baba Annah aliinua juu mkono wake wa kulia ulioshikilia bastola akaielekeza walipokuwa wamesimama mke na binti yake Annah, hali akitetemeka alivuta pumzi ndevu na kuishusha taratibu, kijasho chembamba kikawa kinamtoka mzee huyo.
Mama Annah alimkumbatia binti yake akamziba usoni na kiganja cha mkono wake hakutaka mwanae aone kinachoendelea, naye akafumba macho kwa uchungu akiwa tayari kwa lolote litakalotokea.
Mara ghafula Baba Annah aligeuka kwa kasi akabadilisha uelekeo na kuilekeza bastola yake walipokuwa wamesimama Mheshimiwa dokta Isaack Gondwe na vijana wake, bila kusita akabinya kitufe cha kufyatua risasi huku akiwa amemlenga Dokta Isaack Gondwe kichwani lakini risasi haikutoka ,akajaribu tena mara ya pili na ya tatu lakini hali ikawa ni ile ile, baba Annah akahisi kuchanganyikiwa.
"Hahahah, ha ha ha, ha ha ha haaa" Dokta Gondwe alicheka tena kwa sauti kubwa sana, kisha akaongea
"Nilijuaa...! nilijua tu wewe ni msaliti, unajifanya mjanja sio? ona sasa umeumbuka mbele ya familia yako mzee hii ni mara ya pili unanisaliti, niliwaomba msitoe ushahidi wowote mahakamani lakini mkapanga kunigeuka wewe na familia yako pamoja na kukuhonga pesa nyingi bado ukapanga kunigeuka. Sasa unanisaliti tena kwa mara ya pili unataka kuniua, bahati mbaya bastola niliyokupa haina risasi hahahaha"
"Ulaaniwe Dokta Gondwe, mungu akulaani, utakufa kifo kibaya, wewe na watu wako wote mtakufaa, hata hicho cheo ulichonacho najua ni cha dhuruma, nakwambia utakufa" Baba Annah aliishia kutoa laana kwa mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe mara baada ya kubaini kuwa hana ujanja tena.
"Acha makelele yako, laana kama hizo zilishakuja nyingi sana, hata marehemu mama yangu alinilaani tangu nikiwa tumboni lakini hadi leo hakuna laana iliyofanya kazi" alisema Dkt Gondwe huku akiinamisha kichwa chake chini kutega sikio kumsikiliza kijana wake mwingine ambaye aliingia ndani ya jengo hilo wakati anazungumza.
Kijana huyo hakuwa amefunika sura yake kama wengine, alimnong'oneza maneno kadhaa kwa takribani sekunde 30 hivi, Dokta Gondwe akaonekana kushtuka kiasi kisha akapaza sauti akifoka.
"Kwa nini, kwa nini kila siku yeye tu? hii inawezekanaje? kajuaje tuko hapa? huyu mdogo wako anataka nini? kwa nini unashindwa kumdhibiti? hivi askari ni yeye tu hakuna wengine aah!" Dkt Gondwe alifoka huku akiondoka, akapiga hatua kadhaa kisha akageuka tena.
"Unajua cha kufanya Tino, natangulia kwenye gari" alisema Dkt Gondwe kisha akatoka nje ya lile jengo.
Tino ambaye ndiye aliyeonekana kuwa na mamlaka kuliko vijana wengine wa Dkt Gondwe, alichomoa bastola iliyokuwa kiunoni kwake. Bila kuuliza alimfyatulia risasi Baba Annah, risasi iliyopenya sikio la kushoto ikatokea sikio la kulia, alifanya hivyo pia kwa Mama Annah, kisha akamalizia kumpiga risasi ya kifua Annah. wote wakaanguka chini na kupoteza maisha.
Lilikuwa ni tukio kubwa na zito, kuua watu watatu kwa wakati mmoja. Lakini kwa Tino ilikuwa ni tofauti kabisa, alifanya kwa urahisi sana kama anakunywa maji vile, ilionyesha wazi hii ilikuwa ni kazi aliyoizoea.
Baada ya kufanya hivyo Tino na wale vijana wengine waliandaa mazingira kuonyesha kuwa Baba Annah alimuua mke na mtoto wake kwa kuwapiga risasi kisha na yeye akamalizia kwa kujipiga risasi mwenyewe.
Baadae walitoka na kuingia ndani ya gari mbili zilizoegeshwa nje ya jengo hilo, wakaondoka kwa kasi kuwakimbia polisi ambao kwa mujibu wa maelezo ya Dokta Gondwe alimaanisha wapo njiani wanakuja na mmoja kati ya polisi hao ni mdogo wake na kijana wake wa kazi yaani Tino.
⭐⭐⭐
Ni kweli, dakika chache tu baada ya Dokta Gondwe na vijana wake kuondoka, gari za polisi zisizopungua sita zilifika na kufunga breki kali nje ya jengo hilo na punde polisi walishuka na kuanza kumiminika kwa kasi kuingia ndani ya jengo hilo huku siraha zao zikiwa mbele Ilikuwa ni ishara tosha kuwa polisi hawa walikuwa na taarifa kamili ya kile kilichokuwa kinaendelea ndani ya jengo hilo.
Walikagua vyumba vyote vya jengo hilo, hawakupata mtu yeyote zaidi ya miili ya Baba Annah mama Annah na Annah mwenyewe, kwa haraka haraka ilionyesha wazi kuwa Baba Annah ndiye aliyetekeleza mauwaji hayo kwani mkono wake wa kulia alishika bastola iliyotumika.
Lakini hicho sicho alichokuwa akikiona na kukiwaza Inspekta Aron, kijana ambaye ni polisi mpelelezi kutoka kituo cha kati Handeni. Yeye aliyatazama mazingira ya mle ndani kwa utulivu wa hali ya juu, akaitazama ile miili mmoja baada ya mwingine huku akichukua baadhi ya vielelezo muhimu kama ilivyokuwa ada kwa polisi wengine.
"Tumempoteza shahidi mwingine" Alisema Inspekta Jada, polisi ambaye alikuwa akifanya kazi kwa ukaribu sana na Aron. "Yah! tumechelewa kidogo sana, tungewahi tungeweza kuwaokoa pengine" alisema Aron huku akisogea pembeni pamoja na Jada wakiwaacha polisi wengine wakiendelea na kazi.
"Huenda walipata tena taarifa kama tunakuja" Alisema Jada
"Usiseme huenda, huo ndio ukweli wenyewe Inspekta Jada hii serikali ina watu wa hovyo sana" Aron alilalamika "Usijali Aron jitihada zako zitazaa matunda siku moja, ki ufupi unajituma sana, uwe na subra siku moja tutawakamata wote"
"Inshallah iwe hivyo, lazima nitamkamata Tino"
"Mmh! unahisi kaka yako Tino kahusika kwenye hili tukio pia"
" Ndiyo lazima alikuwepo hapa, subiri uone" Alisema Inspekta Aron akachukua simu yake akaitafuta namba aliyoihifadhi kwa jina la 'Bro Tino' akapiga. Simu iliita kwa dakika kadhaa bila kupokelewa mwisho ikakata, akapiga tena.
⭐⭐⭐
Upande wa pili Tino na bosi wake ambaye ni Waziri wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe tayari walishafika mjini. Tino akiwa ndiye dereva alikuwa ameegesha gari pembeni ya barabara na pembeni ya gari hiyo kulikuwa na gari nyingine ya serikali V8 ilikuwa imepaki ikimsubiri Dokta Gondwe ambaye bado alikuwa na mazungumzo na kijana wake tegemezi Tino.
"Tino, kama sikosei hii ni mara ya nne kama sio ya tano nakwambia kuhusu huyu mdogo wako Inspekta Aron unaemlealea sana, hili ni bomu ambalo litakuja kutulipukia baadae" Dkt Gondwe aliongea kwa msisitizo
"Usijali bosi, huyu ni mdogo wangu najua namna ya kumdhibiti niachie mimi, kuwa na amani bosi" Tino aliongea kwa kujiamini huku akipiga jicho pembeni kuitazama simu yake iliyokuwa ikiita mpigaji akiwa ni Aron mdogo wake.
"Haya mimi nakwenda, tayari tumeshaua mashahidi wote nina hakika tutashinda kesi mahakamani na mkwe wangu Osward atakuwa huru, lakini jua vita yetu bado ni kali sana na ndio kwanza tunaanza"
"Sawa mkuu"
Dkt Isaack Gondwe alishuka kwenye gari akapiga hatua na kuingia kwenye gari nyingine ile V8 dereva akawasha gari wakaondoka. Tino aligeuka na kuitazama simu ambayo ilikuwa ikiita kwa mara ya pili sasa, akapokea.
"Nambie dogo"
"Ulikuwa hapa Tino, ni wewe tena si ndiyo?" Inspekta Aron alisikika upande wa pili akiuliza
"Wapi mbona sikuelewi unazungumzia nini?"
"Najua unanielewa vizuri bro, sasa sikia nakuhakikisha kwamba lazima nitakukamata, nitathibitisha uchafu wako wote, mtafungwa wewe pamoja na mtandao wako mzima"
"Come down mdogo wangu, punguza vitisho huna ushahidi wowote wa kunifunga na hautokuja kufanikiwa kamwe, sahau" "Nisikilize kwa makini kaka labda nisiwe hai, yaani kwa mikono yangu nitakupeleke je..."
"Kaa kimya Aron huna faida yoyote wewe, nahangaika usiku na mchana kutafuta mamilioni ya pesa kwa ajili ya matibabu ya mama yetu, lakini wewe unafanya nini? unahangaika kutaka kunizuia, unaakili kweli wewe?"
"Mama yangu hawezi kuendelea kutibiwa kwa pesa zako chafu kaka, hata angekuwa anajitambua ninauhakika asingekubali hili"
"Kwa hiyo unatakaje, nimuache afe?"
"Kufa au kupona kwa mama yangu ni mpango wa Mungu sio wako Tino"
"Ni mama yetu sio mama yako, kumbuka hilo" alisema tino kisha akakata simu kwa hasira
"Vipi amesemaje?" Aliuliza Inspekta Jada mara tu baada ya kukata simu. "Kauli zake ni zile zile za kila siku, anadai anatafuta hela kwa ajili ya mama kule hospitali" Aron alijibu kinyonge.
"Pole Aron, nakuonea huruama sana, mungu akufanyie wepesi ni miezi sita mpaka sasa unapambana kwa ajili ya matibabu ya mama yako gharama ni kubwa lakini bado kaka yako naye anazidi kukuchanganya" alisema Inspekta Jada akionekana kuguswa na hali aliyokuwa akiipitia Inspekta Aron. Kabla Aron hajazunguza chochote mara kuna askari alionekana akikimbia kuwafuata, akafika na kusimama mbele yao huku akihema kwa nguvu.
"Vipi kwema?" aliuliza Aron akionekana mwenye shauku ya kujua kilichomleta, vivyo hivyo kwa Jada.
"Yu..yule binti kule nda..ndani ha..hajafa ni mzima" alisema yule askari kauli iliyowafanya Aron na Jada watazamane.
Je, nini kitafuata?
Nini hatima ya Vita kati ya ndugu hawa wawili yaani Aron na Tino?
Kwa nini Tino yupo karibu na Waziri wa afya?
Annah hajafa ni mzima huu unaweza kuwa ushahidi wa mwisho wa Inspekta Aron?
Kwa nini VITA YA KISASA?
Hii ni sehemu ya kwanza, majibu ya maswali haya utayapata ndani ya simulizi hii maridhawa iliyojaa visa vingi vya kusisimua. Mauaji, tamaa, mapenzi, urafiki, hila,chuki, drama, vita, usaliti, siasa, visasi, mahaba, kushinda na kushindwa pamoja na mambo mengine yasiyotazamiwa bila kusahau LOVE STORY kali ndani yake.
Naam hii ndio MODERN WAR(vita ya kisasa)