TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

Baada ya kuangaika na wizi wa voucher zetu... wanaingilia majina fake.
 
Huku sasa ni kutafuta kiki, hivi mnaweza kufuatilia watu kwenye twitter na facebook to that extent?
 
Watu wanaweza kuishi bila mtandao Wa internet ila Internet haiwezi kuishi bila watu , Ni kwanini kila siku TCRA mnatufanya kafara? Kiasi cha bundle mnapanga nyinyi bei, nyinyi muda Wa matumizi , nyinyi SAA ya ku-expire nyinyi ,na sasa mnataka kukumata aah haya
 
Kuna kiongozi mmoja alisema kuwa waandishi wa habari msipopiga kelele kuhusu unyanyasaji unaofanywa na serikali kwa vyama vya upinzani, wakimaliza huko wanaamia kwenu. Sasa naona wameamia na kwetu sasa....
 
Tupeni mwongozo hapa JF tufanye nini ili tusije kupotezewa muda kwa mashtaka yasiyo ya lazima.Binafsi sitaki kupambana na mambo yanayoepukika na yasiyo na maslahi kwangu kwani vita niliyonayo dhidi ya umaskini ni kubwa mno,inanitosha kwa sasa.
 
Kuzima simu feki tu zimewashinda ndo wataweza hili?? Huo ni muendelezo wa episodes tu tushazoea hayo
 
Jamaa zangu wa mtaa wa Pili wako kimya kama vile hawalioni hili bandiko wao wako bize na UKUTA. Kweli tunaelekea kuishi maisha ya Pyongyang na Kiongozi Mkuu atakuwa hakosolewi!!
 
TCRA badala wajikite ktk matatizo ya msingi sana wana deal na majina ya watu... yaani hadi kero..
.
1: Nilitegemea wa deal na FREE TV channels ziwe free... ila wako tu

2: VAT ktk miamala ya simu... wamekaa tu... watu wanaibiwa sana ktk mitandao ya simu kwa kutumiwa sms na kuunganishwa ktk huduma bila kujiunga na kukata fedha kihuni hasa tigo... nimewapa taarifa TCRA kwa kuwapigia mara nyingi na kuwatumia e-mail hakuna lolote....

Sasa wanahangaika na majina ya watu... watapeleka wapi...?

TCRA fanyeni ya msingi, achaneni na mambo yasiyo ya msingi
 
Back
Top Bottom