TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

MTU ukikosa kazi unaanza kuwaza ujinga.
Basi hata password zisiwe encrypted liwe jina tu lionekane kawaida
 
Unajua hii nchi watu wanatumia nguvu kubwa sana kupambana na vitu vya kijinga sana..

Sasa kama mtu anatumia utambulisho fake na wala hajihusishi na vitendo vya kitapeli au kuvunja sheria unahangaika naye wa nini??
Lengo lao ni kuingilia tu faragha za watu, just to silence the mass. Kuna kila dalili uhuru wa habari unachimbiwa kaburi.
 
Hivi Jamii forum Wana capture device information? Ukiacha email.

Nafikiria tu jinsi watakavyo tu trace
 
Hii serikali ya Hapa kazi tu, hv inaendeshwa vipi? Kila mtu ni kujikomba kwa kutoa matamko yasiyokuwa na kichwa wala miguu
 
Mmeshindwa tu kuyasimamia Makampuni ya simu kwenye usajili wa line tu, ije kwenye mitandao? Facebook wenyewe wameshindwa hayo Ndio maana kuna account fake, sasa tuambieni Sheria ya JF inaruhusu watu kutumia majina fake, nyinyi mmasema ni kosa kisheria, ina maana mnampango Jf ikate roho?
Siku mkianza kukamata fake account basi ndio itakuwa mwisho wangu kutumia mitandao
Kweli kabisa kiongozi,tupo wengi
 
TCRA TRCA....Mbona hua hamdeal na inshu strategic wazee?Vingamuzi,dstv,etc mbona hamuongelei?
 
Jamani sikilizeni mbona hawazungumzi wizi unaofanywa na vijana wanaotembe mtaani wanasajili laini haya makampuni yapigwe marufuku kutembeza laini mtaani
 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) James Kilaba amewataka wadau wa mawasiliano nchini kujiepusha na sheria za ukiukwaji wa mitandao kwa kutokusambaza ujumbe ulio na maudhui ya uchochezi na uzushi.

James Kilaba ameyasema hayo wakati akizungumza na wahandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya matumizi sahihi na salama ya mitandao mbapo amesema kuwa watumiaji wa mitandao wanatakiwa kutotoa maudhui ya uchochezi pindi wanapo pokea ujumbe huo kwa mtu mwingine.

“Nina wataka mfute maramoja pindi mnapopokea taarifa za uchochezi na kutoa taarifa kwa wanaohusika mnazipokea taarifa hizo” Alisema Kilaba.

Kilaba ameongeza kuwa watuamiaji wa mitandao wasitengeneze akaunti kwa lengo la kufanya utapeli au kutumia taarifa zisizo za kwao na kusisitiza kuwa wanatakiwa kutunza vifaa wanavyohifadhia kumbukumbu zao.

Kufuatia hali hiyo TCRA wamezindua kampeni ya TZ-CERT(Tanzania Computer Emergency Response Team) kwa lengo la kuongeza ufahamu kwa watumiaji wote wa mtandao baada ya kubaini kuwepo kwa changamoto kwa watumiaji wa mitandao, hivyo kampeni hiyo itadumu kwa muda wa miezi mitatu kupitia mtandao wa Facebook, Twitter.
 
Ndio tabu ya kufanya maamuzi kwa mwendo kasi.!
 
Kusitumike neno uchochezi bali munakimbia ukweli na mabadiliko kwa kutumia media ,mitandao.
Time will tell
 
Hivi,lile zoezi la sim fake wamesha maliza?,au ndo yaleyaleeew
 
Wanataka kuzima kimbunga cha ukuta,hatuwezi kuacha kuwa tunaripoti ya msingi ila tu isije kuwa yale yatakayowachoma wakayaita ya uchochezi au uzushi wakati ni ya kweli.
 
Huu ndio ujinga wenye kiwango cha juu zaidi ya lami[emoji34] [emoji34] [emoji34]
 
Uchochezi ni kuiambia ukweli serikali na kuwa na mawazo kinzani na wao.
 
Back
Top Bottom