TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

TCRA: Wenye akaunti ‘feki’ kukiona

Jamani watueleze vizuri. Mods hebu toenu ufafanuzi ili tuamue kusuka ama kunyoa!
 
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mawasiliano hapa Nchini (TCRA) imewaonya watumiaji wa mitandao ya kijamii wanaojisajili katika mitandao hiyo kwa kutumia majina na taarifa za uongo.


James Kilaba Kaimu Mkurugenzi wa TCRA amesema, vitendo vya watu kujisajili katika mitandao ya kijamii kwa kutumia majina na taarifa zisizo sahihi, ni kosa kisheria na kwamba wanaofanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.


Kilaba ameyasema hayo jana, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuongeza ufahamu kuhusu matumizi sahihi na salama ya mitandao ambayo inasimamiwa na Kitengo cha dharura cha kuitikia matukio ya usalama kwenye mitandao hapa nchini (TZ-CERT).

My take: JF itapoteza maana yake
 
Siyo ajabu anaekataza matumizi ya majina fake anatumia vyeti fake....Hahahahaaa nawaza tu!
 
Tunapoelekea JamiiForums tutaisahau na hatutapata pakusemea tena.
 
Sasa watajuaje kama mhusika sio jina lake?
 
Tupeni mwongozo hapa JF tufanye nini ili tusije kupotezewa muda kwa mashtaka yasiyo ya lazima.Binafsi sitaki kupambana na mambo yanayoepukika na yasiyo na maslahi kwangu kwani vita niliyonayo dhidi ya umaskini ni kubwa mno,inanitosha kwa sasa.
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Mmeshindwa kudili na tigo wanaodanganya watu kua unapewa 10gb uki swap line unakimbilia mjina
 
Katika magazeti kila siku kuna waandishi sijui undugu wao ukoje, lakini wengi wanaitwa NA MWANDISHI WETU. Yaani kila gazeti wapo!
Nanadhani na huyu "Na Mwandishi Wetu" awe wa kwanza kukiona.
 
TCRA wako makini kukamata wanaomtukana mkuu wa kaya tu,lakini mambo ya muhimu yanayogusa jamii wanakaa kimya kama "toothless dog"
Kumtukana mtu yeyote ni kosa hata kama siyo mkuu wa kaya. Kwani wewe ukitukananwa unaona siyo kosa?
 
Hii ni nchi ya matamko. Tulijulikana kama bongoland Sasa tutaitwaje nchi ya matamko. Sijui kiinglish inaitwaje
 
Kuna jina la account na user name..hivi vitu tofauti.
Wengi jamii forum wanatumie user name tofauti lkn taarifa zao ni sahihi.
 
Huyu ni mtu ambaye hata LinkedIn profile hana, technology ilishampita mbali, hawezi kuzuia anonymity hata siku moja kwa kua sio kosa, wameandika wapi kua ni kosa kutumia nickname? Kosa kisheria, sheria ipi?

Wafukuze hawa wazee waweke vijana walio in their 20s au 30s kuendesha hili gurudumu, hawa waliopo wamejaza vyeti tu ila hawana experience yoyote kwenye real industry, miaka yote wamekaa wanafanya kazi ya kuregulate watu tu pamoja na degree zao za science.

Hivi TCRA nzima wamekosa kazi za kufanya? waje JF waombe msaada tutawasaidia kuwaonyesha wapi wapafanyie kazi, ndio kwanza hata internet Tanzania ni ya misukosuko tayari wanaanza kuweka limitations za kijinga, mara mia wangepoteza muda kublock website za ngono, kuzuia freedom of speech hapa tutafukuzana, wakifunga JF nyingine tutafungua ndani ya wiki moja tu ambayo ina complete anonymity. Hawa watu utasema marobot
 
Kuna umuhimu wa kuanzisha Uzi wa kuzungumzia maswala yanayohusu Taasisi za serikali. Maana kuna watu wengi warioajiriwa wanajiona kama miungu watu
 
Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba, salaam!
Ninasikitika kuona kila uchao pamoja na marekebisho ya sheria za mitandao ya mwaka 2015 lakini bado watoaji maoni wengi wanatumia lugha za matusi, kukashifu na kufanya njama za wazi za kuitukana serikali.

Kuficha majina yao halisi wakati wakichangia kwenye mitandao ya kijamii ni ishara tosha kuwa malengo yao si mazuri na hivyo hutumia muda mwingi kutengeneza chuki kwa watu dhidi ya serikali. Kutokana na hali hii mie nashauri mamlaka yako bila kuogopa kulaumiwa na makundi korofi kama haya ichukuwe hatua za makusudi kudhibiti WAHAINI hawa.

Nafahamu kuwa hii ni kazi kubwa kwako lkn ukiishirikisha vizuri TCRA utafanikiwa na nchi yetu inaendelea kuwa mahali salama. Nahitaji kuona watanzania wakifanya siasa zisizowapaka wengine matope wala kuwaweka uchi. TUKIYAACHA MAKUNDI HAYA NI HATATRI KWA USTAWI WA TAIFA LETU.

Vita hii pia iwe jumuishi kwa maana ya kutengeneza mazingira shirikishi ya kupata taarifa za uhalifu mitandaoni toka wadau mbalimbali.

Msakila KABENDE
POLITICAL ACTIVIST
MUNGU AKUBARIKI SANA
 
Back
Top Bottom