TCRA: Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji

View attachment 2047592
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imemtaka aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa (CCM) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole kusimamisha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi kinachoruka kupitia Humphrey Polepole Online TV.

Uamuzi huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Hans Gunze ambapo amesema uamuzi huo unakuja baada ya kutenda makosa matatu ikiwemo kuzungumzia Deni la Taifa, Virusi vya Corona na suala la Machinga (Kwamba Wakuu wa Mikoa hawakufuata utaratibu).

"Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole Online Tv kinaamriwa kusimamishwa kwa muda hadi Mmiliki atakapohakikisha anakuwa na Wafanyakazi wenye taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji ili kuleta ufanisi na tija katika vipindi vyake, pili kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, kanuni, misingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari na leseni yake"

"Pia baada ya kutekeleza maelezo hayo kipindi cha Humphrey Polepole Online kitatakiwa kutoa taarifa TCRA kuwa maelekezo yote yamezingatiwa na kuwa kipindi kitarejea chini ya Uangalizi wa TCRA kwa miezi 6, haki ya kukata rufaa ipo wazi ndani ya siku 21 Kisheria kuanzia siku ya kutolewa uamuzi"
#MillardAyoUPDATES
Tunajua kwa nini TCRA wamemfungia: Pia na wao hawana makosa kwa sababu TCRA haiko huru ulitaka boss TCRA afanyeje amfungie Polepole au afukuzwe kazi? kwa kifupi tunahitaji katiba mpya ila kila taasisi iwajibike kwa wananchi badala ya kwa Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala.

1. Lkn kafungiwa kisa kutetea wamachinga
2. Kafungiwa kisa kuwakosoa wakuu wa mikoa hasa wa Dar es salaam, Rais hajui kinachoendela huku chini, Tanzania tulishasahau habari za Mgambo lkn sasa wana nguvu km polisi tena, wiki iliyopita walakamaa vijana wakifanya biashara mgambo walichkua laki moja moja kuttoka kila kijana, rushwa inatumika katika zoezi hili. Pale jogoo barabara ya kwenda mbezi juu wenye viwanda wametoa rushwa na kubolewa.
 
Tunajua kwa nini TCRA wamemfungia: Pia na wao hawana makosa kwa sababu TCRA haiko huru ulitaka boss TCRA afanyeje amfungie Polepole au afukuzwe kazi? kwa kifupi tunahitaji katiba mpya ila kila taasisi iwajibike kwa wananchi badala ya kwa Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala.

1. Lkn kafungiwa kisa kutetea wamachinga
2. Kafungiwa kisa kuwakosoa wakuu wa mikoa hasa wa Dar es salaam, Rais hajui kinachoendela huku chini, Tanzania tulishasahau habari za Mgambo lkn sasa wana nguvu km polisi tena, wiki iliyopita walakamaa vijana wakifanya biashara mgambo walichkua laki moja moja kuttoka kila kijana, rushwa inatumika katika zoezi hili. Pale jogoo barabara ya kwenda mbezi juu wenye viwanda wametoa rushwa na kubolewa.
Siku chache zilizopita Polepole alikuwa na uwezo wa kumpigia simu boss wa TCRA na kumtaka ajieleze. Ni vizuri kufahamu kuwa madhara ya katiba mbovu anayapata kila mmoja wetu.
 
Pole yake huyo polepole! Maskini, hakujua kuwa kamba aliyoshiriki kuisuka itamnyonga siku moja! Ama kweli akili za mchimba kisima huingia mwenyewe kwanza zimeanza kufanya kazi yake!
Namshauri tena Kwa mara ya mwisho kuwa Kama huo mpango wake na vipindi vyake vilikuwa haviandaliwi na tiss ili kuwadissmantal wananchi kwenye kadhia ya Mbowe basi ajiengue taratiiibu huko aliko kwani siyo mahali salama Sana kwake Kwa Sasa!
 
I get your point but kinyozi akinyolewa tunahamaki hatufurahi.

Nakubaliana nawe dadaangu. Watu hawa kama kina Muzorewa, Sithole, Buthelezi na wenzao ni liability tu:

 
Polepole alikua mbunge?
Najua huwezi kunielewa na wala siyo wewe tu ambae utashindwa kunielewa.

Sheria inapotungwa alietunga sheria ni pamoja na yule alieiunga mkono sheria hiyo.Polepole alikuwa kinara wa kuunga mkono sheria kandamizi enzi zile za utawala wa Bwana Chato.

Ni matumaini yangu kuwa sasa umeelewa.
 
View attachment 2047592
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imemtaka aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa (CCM) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole kusimamisha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi kinachoruka kupitia Humphrey Polepole Online TV.

Uamuzi huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Hans Gunze ambapo amesema uamuzi huo unakuja baada ya kutenda makosa matatu ikiwemo kuzungumzia Deni la Taifa, Virusi vya Corona na suala la Machinga (Kwamba Wakuu wa Mikoa hawakufuata utaratibu).

"Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole Online Tv kinaamriwa kusimamishwa kwa muda hadi Mmiliki atakapohakikisha anakuwa na Wafanyakazi wenye taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji ili kuleta ufanisi na tija katika vipindi vyake, pili kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, kanuni, misingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari na leseni yake"

"Pia baada ya kutekeleza maelezo hayo kipindi cha Humphrey Polepole Online kitatakiwa kutoa taarifa TCRA kuwa maelekezo yote yamezingatiwa na kuwa kipindi kitarejea chini ya Uangalizi wa TCRA kwa miezi 6, haki ya kukata rufaa ipo wazi ndani ya siku 21 Kisheria kuanzia siku ya kutolewa uamuzi"
#MillardAyoUPDATES
Akome...

Tulimwambia asishangilie sheria za kipuuzi walizozitunga na Mwendazake na Kabudi wakiamini watatawala milele
 
kwamba wananchi sisi ni hatuna akili mpaka tuchukiane kisa polepole !!!, hicho kipindi hakina tofauti na mtu kupiga story vijiweni hayo ni maoni ya polepole hivo aachwe aongee
 
Nashangaa na wapinzani nao wanafurahia hawakumbuki sheria hizo hizo zinatumika kuwapiga pini na wao, akili ya bora tukose wote bila kukumbuka anayepata kila siku ni CCM.

Polepole akitimiza matakwa ya TCRA wamuache aongee, wasimletee visa kwenye ofisi zao kisa anawapinga mabosi wao, wajue hili taifa sio la mabubu na wajinga, ni la watu wanaohoji na kutaka majibu.
 
Tunajua kwa nini TCRA wamemfungia: Pia na wao hawana makosa kwa sababu TCRA haiko huru ulitaka boss TCRA afanyeje amfungie Polepole au afukuzwe kazi? kwa kifupi tunahitaji katiba mpya ila kila taasisi iwajibike kwa wananchi badala ya kwa Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala.

1. Lkn kafungiwa kisa kutetea wamachinga
2. Kafungiwa kisa kuwakosoa wakuu wa mikoa hasa wa Dar es salaam, Rais hajui kinachoendela huku chini, Tanzania tulishasahau habari za Mgambo lkn sasa wana nguvu km polisi tena, wiki iliyopita walakamaa vijana wakifanya biashara mgambo walichkua laki moja moja kuttoka kila kijana, rushwa inatumika katika zoezi hili. Pale jogoo barabara ya kwenda mbezi juu wenye viwanda wametoa rushwa na kubolewa.
N wao wana makosa ya kutoa rushwa
 
View attachment 2047592
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imemtaka aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa (CCM) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole kusimamisha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi kinachoruka kupitia Humphrey Polepole Online TV.

Uamuzi huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Hans Gunze ambapo amesema uamuzi huo unakuja baada ya kutenda makosa matatu ikiwemo kuzungumzia Deni la Taifa, Virusi vya Corona na suala la Machinga (Kwamba Wakuu wa Mikoa hawakufuata utaratibu).

"Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole Online Tv kinaamriwa kusimamishwa kwa muda hadi Mmiliki atakapohakikisha anakuwa na Wafanyakazi wenye taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji ili kuleta ufanisi na tija katika vipindi vyake, pili kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, kanuni, misingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari na leseni yake"

"Pia baada ya kutekeleza maelezo hayo kipindi cha Humphrey Polepole Online kitatakiwa kutoa taarifa TCRA kuwa maelekezo yote yamezingatiwa na kuwa kipindi kitarejea chini ya Uangalizi wa TCRA kwa miezi 6, haki ya kukata rufaa ipo wazi ndani ya siku 21 Kisheria kuanzia siku ya kutolewa uamuzi"
#MillardAyoUPDATES
Hivi kwa nini haka kajamaa wasikavue tu ubunge ndondo au kuna ugumu gani wadau kisheria?
 
Back
Top Bottom