TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Kwa kampuni za ulinzi sawa kumiliki pingu, lakn kwa raia tu wa kawaida sielewi pingu ni za kazi gani!.
Wewe Kachukue changu alafu umfunge za plastic kama hajakimbia ,za chuma bwana hatoki mpkaumalize!!!
 
Hata mimi natamani kufahamu kwa kweli,mwanzoni tulikuwa tunadanganyana kwamba raia wa kawaida haruhusiwi kumiliki lakini baadae wakati sakata la Muro linaendelea nikasikia kwamba pingu zinauzwa kama bidhaa zingine na leo tumeambiwa kwamba jamaa kawasilisha risiti ya manunuzi ya pingu yake..tafadhali wanasheria mtudadavulie jambo hili.

unaniangusha mkuu.. tatizo ni wale ambao waliamini maneno ya serikali! Tulisema mapema siyo kosa kumiliki pingu watu hawataki ati kwa vile Polisei wamesema.
 
kama mtu huitaji kibali kumiliki pingu,je kuna umuhimu wa risiti kweli kwenye hii kesi?


hakuna wanasheria humu JF watuchambulie mpaka hivi sasa au bado wanasubiri more info? kuna mtu ataumbuka kwenye hii kesi.
 
kama mtu huitaji kibali kumiliki pingu,je kuna umuhimu wa risiti kweli kwenye hii kesi?


hakuna wanasheria humu JF watuchambulie mpaka hivi sasa au bado wanasubiri more info? kuna mtu ataumbuka kwenye hii kesi.

Mzee wa emirates, ukweli ni kuwa hakukuwa na haja ya kupeleka risiti ya pingu kwani kumiliki pingu si kosa lakini kwa sababu kwa utambuzi mdogo wa Kova akadai apelekewe risiti, wacha wampeleke tu azidi kunyumbuka vizuri wamezidi kutuwekea vituko. Kama polisi huwa wanasoma somo la sheria basi alikuwa anadoji sana na haya ndo matokeo yake sasa
 
kova utajua kama chachandu ni juisi au?ukisema ndiyo utaletewa na biskuti za mawe
 
risiti hutengenezwa mtaani tu....tusubiri zithibitishwe then tuanze kuhoji

Hata pingu pia huuzwa mitaani. Suala la risiti fake au genuine anayeweza kuthibitisha ni muuzaji tu, sasa uchunguzi uamie Mzinga Corporation. Hili suala limeonesha jinsi gani Jeshi la polisi lilivyo la kizamani limejaa mbumbumbu wengi kama kina Kova. Yule polisi aliyesema limebumbuluka waondoke aliona mbali zaidi japo ni mlinzi wa Bank kuliko Kova anayekaa ofisi huku hawezi kufikria. Sasa hivi Jeshi la polisi limejipatia mzigo wa kumlinda Jerry, maana akidhulika tu tunajua wao ni suspects wa kwanza.
 
kama raia wa kawaida haruhusiwi kumiliki pingu sasa risiti ya nn inahitajika?
duh hapa lazima mtu macho yamtoke coz mkanganyiko wa mambo umezidi!!!!!!!!
 
Wadau habari sana,


Tangu tukio la kukamatwa kwa mwandishi wa habari za uchunguzi JM mambo mengi yamejitokeza na yanaendelea kujitokeza, Lakini kikubwa ambacho nimevutiwa nacho ni kugundua kuwa raia anaruhusiwa kumiliki pingu, sasa wakuu naombeni mnifahamishe taratibu gani nifuate ili ikiwezekana niweze kuwa namiliki pingu.

Mkuu kama unaweza wasiliana na Jerry Muro yeye anazo tayari hivyo atakusaidia kukwambia taratibu za kupata hizo pingu!!! Hivi Jerry mbona hasemi hizo pingu alikuwa nazo kwa nini? Alikuwa anazitumiaje au alikuwa anatarajia kuzitumiaje kwenye maisha/kazi yake?

Tiba
 
.... it is flummoxing to see how many people are into S&M in our society today......!! lol
 
Joji na wengine wote Tanzania, kwa wanaoishi jirani na mkoa wa Morogoro wanaweza kufika pale Mzinga kwenye karakana ya silaha, kuna duka la silaha, kuanzia risasi, bastola na bunduki kadha wa kadha za kuwindia kama ilivyo kwa Tanganyika arms, sasa Pingu huitaji kibali wala barua ya mtendaji kata kuinunua, ila risasi na bunduki ndio unahitaji kua na hati kadha wa kadha.

Usitoe taarifa ambazo hujathibitisha. JWTZ leo wamekanusha kwamba pingu haiuzwi kwa raia. Soma mwananchi. JM yupo katika tanuru la moto. Kama JWTZ wamemkataa sijui nini kinafuata baada ya hapo. Ipo kazi wakubwa. msijifariji, hakuna pingu inauzwa kwa raia. By the way, wewe pingu unanunua kwenda kufanyia nini? Kama siyo kwenda kujifanya polisi na kuwatapeli watu ni nini??? Sina imani na Jerry Muro katika hili.
 
kama mtu huitaji kibali kumiliki pingu,je kuna umuhimu wa risiti kweli kwenye hii kesi?


hakuna wanasheria humu JF watuchambulie mpaka hivi sasa au bado wanasubiri more info? kuna mtu ataumbuka kwenye hii kesi.

2909552.jpg



Mzee hoja ya msingi hapa ni Je, ni halali au si halali kwa mtu binafsi kumiliki pingu?.... Kwa mtazamo wa Kova alijua kuwa pingu ni kama bastola ambayo umilliki wake unasimamiwa na sheria fulani ambayo pamoja na kutoitaja, bado aling'ang'a Jerry apewe uthibitisho polisi kuthibitisha kuwa anamiliki hiyo pingu kihalali. Cha kushangaza, Kova akaibuka mbele ya jamii akisema (tumemtaka alete risiti wakati akijua wazi kuwa hapakuwa na tuhuma zozote zozote kuwa hiyo pingu imeibiwa au ni mali ya Polisi).

Kisheria waweza kuona kuwa Kova alienda chaka kwa kumtaka Jerry alete risti ya maanunuzi ya hiyo pingu kwa maana ya kwamba risti huwa inatumika kuthibitisha uhalali wa umiliki wa mali pale inapotokea ubishani wa watu wawili kuhusu nani ni mmiliki wa mali hiyo, au pale inapotuhumiwa kuwa mali hiyo ni ya wizi na haikupaswa kuwepo mikononi mwa mtuhumiwa. Kwa suala la silaha, risiti ya kununulia silaha, haitoshi kuthibitisha kuwa wewe unamilki kihalali hiyo silaha, mpaka ulete pia "kibali cha Polisi cha Kumilikishwa silaha"...


Hapa Jerry angepaswa kutoa risti kama ingekuwa kuna ubishani kati yake na polisi kuwa ile pingu aliyokutwa nayo sio yake. Hapa Kova anaonyesha kwa upande mwingine kuwa japo alijua hakuna sheria bado alitaka kumkomoa Jerry na kujaribu kuipotosha Jamii toka tuhuma za msingi, kwa kutaka Jerry alete risti ambayo hata kama isingetaja ni wapi hiyo pingu imenunuliwa au hata kama ingetaja jina la mtu mwingine ambaye angekuja kuthuibisha kuwa alimpa Jerry Kihalali, bado Polisi isingekuwa na kesi dhidi yake kwa kuwa hakuna sheria inayozuia kuwa nayo labda kama umeitumia vibaya (hilo sasa lingebaki kwenye kesi ya msingi ya madai ya rushwa kwa nguvu ambapo kama pingu ilitumia ingekuwa ni kielelezo muhimu kwenye ushahidi).
1.JPG
 
Jamani eeh , naomba wasifu wa Kamanda Kovu, kama vile shule, kujiunga Geshi ra Porisi na Kupanda kwake kwa Vyeo. Na mimi nataka jiunga Geshi ra Porisi
 
Jamani eeh , naomba wasifu wa Kamanda Kovu, kama vile shule, kujiunga Geshi ra Porisi na Kupanda kwake kwa Vyeo. Na mimi nataka jiunga Geshi ra Porisi

Moja ya vigezo unatakiwa uwe mbumbumbu kama hawa wa sasa? Unaweza hiyo?
 
Take home message: Nimekuwa nikijiuliza kila siku: Hivi, mtu mwenye akili timamu na raia mwema wa nchii au yoyote ni kwanini ununue Pingu?! Za nini?!!!!!!!


Sakata la Jerry Muro: Jeshi sasa lakuna vichwa

DUKA LA MZINGA LASEMA PINGU HAZIUZWI KWA RAIA






SAKATA la Mwandishi wa habari Jerry Muro, anayetuhumiwa kujihusika na vitendo vya kutaka fedha kwa nguvu pamoja na kukutwa na pingu, limezidi kufumuka baada ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) kujadili sababu za kuingizwa katika kadhia hiyo huku Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiahidi kushughulikiwa kwa haraka.

Muro, mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji (TBC) na ambaye amejipatia umaarufu kutokana na kufichua aina tofauti za rushwa, Jumapili iliyopita alikutwa na pingu katika gari alilokuwa akilitumia baada ya kukamatwa kwa kudaiwa kutaka fedha kwa njia ya vitisho kutoka kwa aliyekuwa mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage.

Juzi, Muro aliwaonyesha waandishi risiti ya kumiliki pingu, alizodai kuzinunua katika duka la silaha la Mzinga lililo Upanga jijini Dar es Salaam, lakini hakuwa amewasilisha risiti hiyo kwa Jeshi la Polisi ambalo linaendelea kumpa muda wa kutafuta kidhibiti hicho.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, afisa habari na mawasiliano wa JWTZ, Luteni Kanali Mgawe Kapambala alisema wameshangazwa na suala la raia kuruhusiwa kununua pingu wakati hana matumizi nayo na kwamba tayari wamefanya vikao kujadili suala hilo.

"Sisi wenyewe tumeshangazaa baada ya kuona taarifa ile kwenye vyombo vya habari, lakini tunachojiuliza ni kwamba inakuwaje raia anauziwa pingu wakati hana matumizi nayo,” alisema Kanali Mgawe.

"Duka lile linauza hadi silaha za moto ndio maana tunashindwa kuelewa."

Kwa mujibu wa uchunguzi ambao gazeti dada la The Citizen liliufanya jana kwenye duka la silaha la Mzinga, raia hawaruhusiwi kununua pingu isipokuwa vyombo vya dola tu tena kwa shughuli maalum tu.

Mwandishi aliyejaribu kununua pingu kwenye duka hilo, aliambiwa: "Hatuwezi kukuuzia wewe kwa kuwa hautoki jeshini. Tunauza kwa polisi na magereza. Na silaha tunauza kwa watu kwa sababu maalum, lakini si pingu."

Suala la Muro pia liliibuka bungeni wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu.

Akijibu swali kuhusu mkasa huo wa Muro, Waziri Pinda alisema suala hilo litafanyiwa uchunguzi wa kina na kumalizwa kwa haraka kwa kuwa linaweza kusababisha mkanganyiko na kuzua hisia mbaya miongoni mwa wananchi.

Waziri mkuu alilazimika kulitolea maelezo hayo baada ya kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed kuhoji serikali inalifikiriaje juu ya sakata hilo.

Katika swali lake, Hamad alitaka kujua iwapo misukosuko anayopata Muro ambaye ni mwandishi wa kituo cha TBC1, kama ni sehemu ya misukosuko wanayopata waandishi wa habari wanaofuatilia mambo mazito duniani hasa barani Afrika.

Kabla ya kuuliza swali mbunge huyo alieleza ameshuhudiwa kwa muda mrefu waandishi wengi wa habari wanaofuatilia mambo mazito ya nchi, hupata misukosuko sehemu mbalimbali duniani hasa katika Bara la Afrika.

Na kabla ya majibu ya Waziri Pinda, Naibu Spika Anna Makinda alisema "bahati yako, halijaenda mahakamani".

Lakini katika majibu yake Waziri Mkuu Pinda alionyesha ugumu wa swali hilo akisema: "Hili suala lingekwenda mahakamani, jibu lingekuwa rahisi kweli."

Akaongeza:"Labda niseme kwanza kwamba, binadamu alivyoumbwa ni kiumbe mwenye mapungufu mengi tu, hata kama angekuwa ana sifa nyingine zote, tukubali tu kwamba atakuwa na mapungufu. Waziri mkuu anayo; Hamad anayo; kwa hiyo na waandishi wa habari vile vile wanayo mapungufu yao kama binadamu."

Alisema ndio sababu ziliwekwa sheria, kanuni na taratibu ili kusaidia kufanya mambo kwa kuzingatia sheria na kanuni.

"Sasa yaliyompata Jerry... niseme tu kwamba kama binadamu na kama mtumishi mwingine yoyote, ni jambo ambalo linawezekana kabisa. Yale anayotuhumiwa yanawezekana yakawepo, vile vile yasiwepo," alisema Pinda.

"Ndiyo maana kwa sababu hiyo inabidi uchunguzi ufanyike, tena wa kina ili kuweza kubaini ukweli wa yale wanayomtuhumu ni kiasi gani na kiasi gani si kweli."

Hata hivyo alisema tatizo ni namna jambo hilo lilivyoanza kushughulikiwa na vyombo husika vya usalama na Jerry mwenyewe. Alisema wote wamekimbilia kwenye vyombo vya habari na kujenga picha tofauti kwa wananchi.

"Tatizo ninalolitapa, Mheshimiwa Hamad, ni pengine namna jambo hili lilivyoanza kushughulikiwa... tumekimbilia kwenye vyombo vya habari sisi tunaochunguza, na yeye kama mtuhumiwa ametafuta vyombo vya habari na kuvitumia. Kwa hiyo sasa ujumbe tunaowapa wananchi kwa ujumla unaweza ukatuchanganya sana.

"Kwa hiyo mimi rai yangu ni kuwa uchunguzi fanyeni kama mnavyofanya uchunguzi mwingine wowote. Utakapofikia mwisho, itajulikana kama ni kesi ya kwenda mahakamani au hapana," alisema Pinda.

Katika swali lake la nyongeza Hamad, ambaye ni mbunge wa Wawi (CUF), alitaka kujua kama waziri mkuu anaweza kutumia nafasi yake kuhakikisha suala hilo linakwenda na kumalizika haraka.

Akijibu swali hilo Pinda alisema yeye binafsi hapendi suala hilo liendelee kwa muda mrefu kwa kuwa linaweza kuanza kuibua hisia zisizo nzuri kwa wananchi.

Alidokeza kuwa tayari amezungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) ambao wamempa majibu ya uhakika kuwa suala hilo halitachukua muda mrefu kumalizika.

Wakati huo huo Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeeleza kuwa halitaki kulumbana na Muro kwa kujibizana kwenye vyombo vya habari na kuwataka wananchi kuliachia jeshi hilo lifanye kazi yake ili sheria ichukue mkondo wake mahakamani. Habari hii imeandikwa Exuper Kachenje, Dodoma, Sadick Mtulya, Patricia Kimelemeta, Boniface Meena na Festo Polea
 
Hizi kutoka nipashe

http://www.wavuti.com/4/post/2010/02/jerry-muro-aonesha-risiti-ya-pingu-alokutwa-nayo.html

Eti wanadai wameongea na wauzaji na kuambiwa kuwa pingu unanunua tu kama bamia
 
Hizi kutoka nipashe

http://www.wavuti.com/4/post/2010/02/jerry-muro-aonesha-risiti-ya-pingu-alokutwa-nayo.html

Eti wanadai wameongea na wauzaji na kuambiwa kuwa pingu unanunua tu kama bamia


Achana na wanasheria wa Bongo. Ila pia nina wasi wasi na msemajiwa jeshi. Anaweza kuwa anaongea ukweli ambao haupo. Kwamba ilikuwaje jamaa akauziwa pingu na kwa sababu ipi!? Maana mimi binafsi aiingii akilini kabisa: hizi pingu kwa Jerry Muro zilikuwa za nini hasa! Maelezo hayawezi tosheleza hapa
 
JAmamni hii kesi ya Jerry itaibua mengi sasa Mzinga wanasema kwa kawaida Pingu huwa haziuzwi kwa raia. Sasa swali ni je risiti aliyoitoa Jerry ni Genuine? Nani kamwuuzia Jerry Pingu hizo? Movie inaendelea.....
 
Take home message: Nimekuwa nikijiuliza kila siku: Hivi, mtu mwenye akili timamu na raia mwema wa nchii au yoyote ni kwanini ununue Pingu?! Za nini?!!!!!!!
Mwanjelwa Mzee Mwanakijiji si ameshalijibu tena mpaka na shairi?.
Maadam sio kosa kisheria kwa raia kumiliki pingu, them, hata akisema pingu zile ni za kujifunga yeye na mwandani, ili asimtoroke usiku.

Naamini Mwanjelwa unazielewa baadhi ya tactics za mapenzi ya 'Masochism' wahusika wakiitwa 'Masochistic', ili wafike, huombwa wafungwe pingu, wachapwe mijeled, wapigwe mangumi, ama waparuliwe mpaka wadoke midamu, ndipo starehe ifuate!.

Pingu sio issue!.
 
Back
Top Bottom