TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Jamani Mzinga wamedai kuwa pingu huwa haziuzwi kwa raia- sasa hii risiti ya Jerry ni Genuine? mbona wengi watatumbukia humu kwenye shimo la tewa?
 
mwenyewe hapa nazidi kutatizika na hizi habari ..
Kova nae sijui nini kilimtuma kujitoa kwenye vyomba vya habari na kutangaza pumba zake ..
Hii kama kesi ilitakiwa iendeshe kama kesi zingine mpaka maamuzi yatakapoolea ..sio kila jambo linaanikwa ..
Mie imeshaanza kunichosha
 
Mwanjelwa Mzee Mwanakijiji si ameshalijibu tena mpaka na shairi?.
Maadam sio kosa kisheria kwa raia kumiliki pingu, them, hata akisema pingu zile ni za kujifunga yeye na mwandani, ili asimtoroke usiku.

Naamini Mwanjelwa unazielewa baadhi ya tactics za mapenzi ya 'Masochism' wahusika wakiitwa 'Masochistic', ili wafike, huombwa wafungwe pingu, wachapwe mijeled, wapigwe mangumi, ama waparuliwe mpaka wadoke midamu, ndipo starehe ifuate!.

Pingu sio issue!.

Pasco, Masochism kwetu hapa bado sana kwa kiwango cha kutiana pingu. Huko huko Ulaya na beyond. Ni kweli unavyosema kwamba kuwa na pingu si kosa, lakini nikuulize swali: kuwa na condomu ni kosa? Mbona wewe hujawahi kuzishikilia mkononi zikiwa hazimo kwenye paketi ukapita nazo mitaani watu wakuone nazo!?!

labda unaweza kuwa siyo mfano mzuri sana, lakini pia pingu ni handcuff/kizuizi cha mikono au miguu kinachotumiwa na police kwa wahalifu ili kuwadhibiti. Hakuna sehemu umewahi ona mtu anatumia pingu kwa namna yoyote ile iwayo akili mwako, ukiondoa hiyo masochism; kama unaitumia wewe. Na kama kweli unafanya masochism una sababu gani ya kutembea na pingu kwenye gari badala kuacha eneo lako tukio la hivyo vitendo?!

Ukifikiria kirahisi kirahisi bila kutafakali ndiyo unaweza support huyu kijana kuwa kukutwa na pingu ni halali. hasa akili yako ukiilazia kwenye tuhuma za jeshi la POLICE kama wengi wanavyoingia mtegoni kizembe hapa JF. Anaweza akakamtwa huyu jamaa anapiga miti mkeo au girlfriend wako na ati kwa kuwa hukuona akifanya hilo tendo na pia unamfahamu, ukakimbilia kusema kuwa watu/jeshi la Police linamwonea kwa sababu ya kuripotiwa rushwa!?!!
 
Hii hapa nakala ya stakabadhi ya malipo ya pingu alokutwa nayo Jerry Muro02/04/2010
15 Comment(s)


Kadhia anayoendesha kwa mbwembwe Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, kuhusu mwandishi wa habari za uchunguzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1), Jerry Muro, imezidi kumweka pagumu baada ya risiti ya pingu anayotuhumiwa nayo mwandishi huyo kupatikana.

2909552.jpg
nakala ya stakabathi ya malipo ya pingu alokutwa nayo Jerry Muro

Hali hiyo inajitokeza baada ya kile alichoapa Kova kwamba hakuna raia anayeweza kumiliki pingu, na kwamba alikuwa na hakika kwamba Muro asingeweza kupeleka risiti hiyo. Juzi akiendelea na juhudi zake za kuwakamata watuhumiwa na kuwahukumu huku akisema wengine ni “matapeli sugu”, Kova alisema kwamba Muro aliyekamatwa Jumapili iliyopita na kuachiwa kwa dhamana, alikuwa hajawasilisha risiti hiyo.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kwamba Muro alinunua pingu hiyo kihalali kutoka duka la kuuza silaha la Shirika la Mzinga. Shirika hili ni mali ya serikali. Nipashe imefanikiwa pia kuona risiti aliyopewa Muro kama ushahidi wa ununuzi wa pingu hiyo, ikiwa na namba 34357310. Stakabadhi hiyo ni mali ya serikali pia. Risiti hiyo iliyotolewa Mei 20, mwaka 2008, inaonyesha kuwa Muro alinunua pingu kwa Sh, 25,000. Muro ambaye amejipatia umaarufu kutokana na kufichua aina tofauti za rushwa, Jumapili iliyopita alikutwa na pingu katika gari alilokuwa akilitumia mara baada ya kukamatwa kwa kudaiwa kutaka fedha kwa njia ya vitisho kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage.

Wage pamoja na maofisa wa juu wa Halmashauri hiyo mwezi uliopita walifutwa kazi na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwa tuhuma za ufisadi wa kutisha. Bado wanachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Miongoni mwa rushwa ambazo Muro alizifichua ni zile zilizohusu askari wa usalama barabarani kupokea rushwa.

8772229.png
Jerry Muro​
Kwa mara ya kwanza Muro alifanya kipindi maalum akiwa mfanyakazi wa ITV na kuwanasa askari hao katika barabara kuu ya Morogoro, kati ya Dar es Salaam na Morogoro. Mara ya pili alifanya kipindi cha usiku wa habari katika barabara kuu mkoani Iringa na kilionyeshwa na TBC1 anakofanya kazi Muro kwa sasa.

Mwaka jana Muro alishinda tuzo ya mwandishi bora wa mwaka na kipindi cha ITV ambacho kilisababisha askari kadhaa walioonekana wakipokea rushwa kufukuzwa, ndicho kilimpandisha ngazi.

Kadhalika kipindi cha TBC1 nacho kimepeleka kilio kwa askari waliomulikwa, na sasa wanachunguzwa kabla ya kufukuzwa kazi kwa kula rushwa.

Kamanda Kova tangu kuibuka kwa kadhia ya Muro ambayo imeacha maswali mengi kutokana na kuendeshwa mno kwa mizengwe, amekuwa akikanyaga sheria ambazo kama kiongozi wa juu wa Jeshi la Polisi anapaswa kuzisimamia. Kwa mfano Jumatatu Kova alionyesha hadharani bastola anayomiliki Muro kama ambavyo polisi wengi wamekuwa wakionyesha silaha walizokamata kwa watu wanatuhumiwa kwa ujambazi. Ingawa Kova alikiri kwamba Muro alikuwa anamiliki bastola hiyo kihalali, hakueleza umma ilikuwa na umuhimu gani basi kiutaalam na kiusalama kutoa taarifa za kina za silaha ya raia, ikiwa ni pamoja na uwezo wake wa kubeba risasi na ilikotengenezwa. Kadhalika, Kova alionekana akijenga hoja kwamba pingu aliyokuwa anamiliki Muro ilikuwa inatiliwa shaka na kukiwa hakuna sheria yoyote Tanzania inayomzuia mtu kumiliki pingu, kifaa hicho si silaha wala hakina ukiritimba wowote wa kukimiliki. Kova pia anadaiwa kuvunja sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 kwa kuwataja watu waliotoa taarifa za rushwa, hivyo kuweka suala zima katika mtihani mkubwa wa kisheria. Kifungu cha 51(1) (a) cha sheria hiyo, kinazuia kutajwa kwa jina, makazi na anuani ya mtu aliyetoa taarifa kuhusu vitendo vya rushwa au aliyesaidia mamlaka inayohusika kufanikisha kukamatwa kwa mhusika.

Juzi Kova aliwaanika watu wengine wawili aliodai kuwa ni washirika wa Muro katika kutenda uhalifu, na aliwatangaza kwamba ni “mapateli sugu wasiostahili kupewa dhamana”. Kova aligeuka kuwa Polisi na Hakimu wa kuhukumu papo hapo. Kadhia ya Muro imekuwa ikibadili mwelekeo kila uchao, awali polisi walikuwa wanamtuhumu kwamba alidai rushwa ya Sh. milioni 10, lakini wameshindwa kueleza ni kwa nini hawakuweka mtego ili kumshikisha na pia ni kwa nini suala hilo halikupelekwa Takukuru ambao kisheria ndio mahali hasa pa kushughulikia makosa ya rushwa.

Jana nipashe iliwasiliana na uongozi wa Shirika la Mzinga ambalo linauza pingu hapa nchini, na ulisema upo tayari kumuuzia hata mwandishi kama anazo fedha. "Wewe kama una hela njoo tutakuuzia pingu, haina shida tatizo lipo katika silaha," alisema Mary Peter, mfanyakazi wa shirika hilo alipoulizwa na Nipashe, jana jioni. Mary alipoulizwa kama anakumbuka Muro aliwahi kununua pingu kwao, alijibu kwa kifupi kuwa yeye sio msemaji wa shirika hilo.



 
NAKALA YA RISITI YA PINGU HII HAPA CHINI, MAMBO HAYO......!

2909552.jpg
 
Mimi nadhani Jerry anatakiwa kulindwa hasa wakati huu. Kuna watu wengi sana ambao wana potential ta kuathiriwa na uchunguzi wa Muro na hasa kuhusiana na investment za GWAMI kule Moro. Nasikia....wengine mtanikosoa, bwana "GWAMI" amenunua mtaa wa Ghorofa moja, kakodisha floor nzima ya ofisi ya CCM vijana Moro kwa ajili ya hotel, amejenga Ghorofa Msamvu kwa muda mfupi. Napenda kujiuliza hivi mfanyakazi gani wa serikali anaweza kufanya yote hayo haraka na kwa ufanisi mkubwa. Ukithaminisha miradi yote hiyo utapata kichaa kwa mfanya kazi wa halmashauri maskini kama Bagamoyo. JM was about to spoil the air and it seems some of us will fight hard to prevent that from happening hata kama ni kwa gharama yoyote.
 
Mimi nadhani Jerry anatakiwa kulindwa hasa wakati huu. Kuna watu wengi sana ambao wana potential ta kuathiriwa na uchunguzi wa Muro na hasa kuhusiana na investment za GWAMI kule Moro. Nasikia....wengine mtanikosoa, bwana "GWAMI" amenunua mtaa wa Ghorofa moja, kakodisha floor nzima ya ofisi ya CCM vijana Moro kwa ajili ya hotel, amejenga Ghorofa Msamvu kwa muda mfupi. Napenda kujiuliza hivi mfanyakazi gani wa serikali anaweza kufanya yote hayo haraka na kwa ufanisi mkubwa. Ukithaminisha miradi yote hiyo utapata kichaa kwa mfanya kazi wa halmashauri maskini kama Bagamoyo. JM was about to spoil the air and it seems some of us will fight hard to prevent that from happening hata kama ni kwa gharama yoyote.


Wacha habari zako wewe! Kuna watu wanamiliki mitaa hawajachunguzwa ndiyo iwe Gwami?! Acha kauli yako. Jerry anataka ku-spoil air kwa kutumia pingu, yeye kama nani?
 
Pingu zinafaa sana nyumbani kwa mkeo unapohitaji maximum satisfaction kutoka kwa mama watoto.
 
Mwanjelwa Mzee Mwanakijiji si ameshalijibu tena mpaka na shairi?.
Maadam sio kosa kisheria kwa raia kumiliki pingu, them, hata akisema pingu zile ni za kujifunga yeye na mwandani, ili asimtoroke usiku.

Naamini Mwanjelwa unazielewa baadhi ya tactics za mapenzi ya 'Masochism' wahusika wakiitwa 'Masochistic', ili wafike, huombwa wafungwe pingu, wachapwe mijeled, wapigwe mangumi, ama waparuliwe mpaka wadoke midamu, ndipo starehe ifuate!.

Pingu sio issue!.

Pamoja na kuwa sheria haimkatazi raia kuwa na pingu, jamani tujiulize hasa pingu hizi Jerry alikuwa anamiliki kwa sababu gani hasa kiundani, na zaidi ya yote kwa nini alitembea nazo kwenye gari siku hiyo? je katika kazi yake ya uandishi wa habari huwa wanakutana na purukushani ambazo huwenda zingehitaji matumizi ya pingu hizo?

Tusikimbilie kusema sheria haikatazi yeye kama raia kuwa na pingu but tukumbuke kuwa pingu si sawa na maji ya kunywa kuwa ni muhimu kuwa nazo (unless alikuwa na specific matumizi nazo) na atueleze matumizi hayo, na kwa nini siku hiyo zilikuwa garini?
 
HIvi Watanzania tuna matatizo gani jamani? Siyo kosa kukutwa na pinguu!!! Hakuna jaji mwenye akili timamu anayeweza kumkuta mtu na hatia ya kosa la kukutwa na pingu!
 
HIvi Watanzania tuna matatizo gani jamani? Siyo kosa kukutwa na pinguu!!! Hakuna jaji mwenye akili timamu anayeweza kumkuta mtu na hatia ya kosa la kukutwa na pingu!

Mwanakijiji hakuna aliyesema ni kosa tumeelewa kuwa si kosa. Lakini mtu yeyote akiwa na kitu chake atakwambia kuwa anacho kwa sababu flani, silaha mtu anamiliki kwa kuwa anajilinda kwa usalama wake na pingu ni kwa ajili ya kufanyia nini? Sawa umesema kuna matumizi mengine ambayo pingu zinatumika huwenda sababu za Jerry zinaangukia ndani ya kundi hilo la sababu nyinginezo but why zilikuwa garini siku ile ya tukio? Sisemi kuwa Jerry ana makosa la hasha but najaribu kuwaza zaidi why atembee nazo siku hiyo? au huwa zinakaa ndani ya gari lake daima? Yeye mwenyewe anasemaje?

Mi bado haijaniingia akilini huwenda ni kwa sababu ya upeo wangu mfupi wa haya mambo lakini ninaamini kama ambavyo mmenijuza mengi hata hili mtanisaidia tu.
 
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, afisa habari na mawasiliano wa JWTZ, Luteni Kanali Mgawe Kapambala alisema wameshangazwa na suala la raia kuruhusiwa kununua pingu wakati hana matumizi nayo na kwamba tayari wamefanya vikao kujadili suala hilo.
"Sisi wenyewe tumeshangazaa baada ya kuona taarifa ile kwenye vyombo vya habari, lakini tunachojiuliza ni kwamba inakuwaje raia anauziwa pingu wakati hana matumizi nayo,” alisema Kanali Mgawe
Kwa mujibu wa uchunguzi ambao gazeti dada la The Citizen liliufanya jana kwenye duka la silaha la Mzinga, raia hawaruhusiwi kununua pingu isipokuwa vyombo vya dola tu tena kwa shughuli maalum tu.
Huyu Kanali angetutajia basi kifungu cha sheria kinachosema ivyo.....
 
Huyu Kanali angetutajia basi kifungu cha sheria kinachosema ivyo.....

Kaka hii kesi itaibua mengi sana ndugu yangu -maana risiti ile ni ya serikali na ina muhuri wa Mzinga Morogoro. Yetu macho

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, afisa habari na mawasiliano wa JWTZ, Luteni Kanali Mgawe Kapambala alisema wameshangazwa na suala la raia kuruhusiwa kununua pingu wakati hana matumizi nayo na kwamba tayari wamefanya vikao kujadili suala hilo.
"Sisi wenyewe tumeshangazaa baada ya kuona taarifa ile kwenye vyombo vya habari, lakini tunachojiuliza ni kwamba inakuwaje raia anauziwa pingu wakati hana matumizi nayo,” alisema Kanali Mgawe
Kwa mujibu wa uchunguzi ambao gazeti dada la The Citizen liliufanya jana kwenye duka la silaha la Mzinga, raia hawaruhusiwi kununua pingu isipokuwa vyombo vya dola tu tena kwa shughuli maalum tu......
hii ndiyo concern yangu- tuyajue hayo matumizi ya pingu kwa raia wa kawaida ndipo tujadili kwa kina. Ninayoyajua mimi ni
- kumfungia mhalifu (police)
-na yale aliyoelezea Mwjj kwenye chumba cha mapenzi

Kama kuna mengine please nijuzeni mwenzenu.
 
Huyu Kanali angetutajia basi kifungu cha sheria kinachosema ivyo.....
kiko kichwani mwake hatuwezi kukiona, labda hakimu/jaji aufungue ubongo wake? by the way nao jeshi kwani nini wanaziuza? maana kwa tafsiri ya Kova ni magereza na Polisi tu sasa JWTZ nao ni za nini Jeshi huwa wanashikilia wahalifu?? au za kuwafunga Mateka? kama ni hivyo kwanini ziwe bidhaa zinazoonyeshwa kwenye Duka Lao? wana mtangazia nani hiyo Biashara? Magereza Au Polisi? au Serikali yote kwa Jumla.
 
kiko kichwani mwake hatuwezi kukiona, labda hakimu/jaji aufungue ubongo wake? by the way nao jeshi kwani nini wanaziuza? maana hiyo kwa tafsiri ya Kova ni magereza na Polisi tu sasa JWTZ nao kwa ni za nini? au za kuwafunga Mateka? kama ni hivyo kwanini ziwe bidhaa zinazoonyeshwa kwenye Duka Lao? wana mtangazia nani hiyo Biashara? Magereza Au Polisi? au Serikali yote kwa Jumla.
Labda yale makampuni binafsi ya ulinzi -si huwa wanawalinzi wao- kwa kuwakamatia wahalifu sehemu wanazolinda.
 
Kaka hii kesi itaibua mengi sana ndugu yangu -maana risiti ile ni ya serikali na ina muhuri wa Mzinga Morogoro. Yetu macho
Hata Jerry Nae katika clip zake zote alizoongea hajagusia swala la matumizi ya pingu yake sijui kwa nn!! naona anawaonyesha risit tu matumizi yaa pingu hasemi!!
 
Usitoe taarifa ambazo hujathibitisha. JWTZ leo wamekanusha kwamba pingu haiuzwi kwa raia. Soma mwananchi. JM yupo katika tanuru la moto. Kama JWTZ wamemkataa sijui nini kinafuata baada ya hapo. Ipo kazi wakubwa. msijifariji, hakuna pingu inauzwa kwa raia. By the way, wewe pingu unanunua kwenda kufanyia nini? Kama siyo kwenda kujifanya polisi na kuwatapeli watu ni nini??? Sina imani na Jerry Muro katika hili.
Ningeshauri wote wanaoshabikia kesi hii waisome hii post. Just because hakuna sheria inayokataza mtu kumiliki pingu does it mean kuwa inaruhusiwa? We mwananchi wa kawaida pingu za kazi gani? Hata kama za mapenzi unatembea nazo kwenye gari za nini? Jerry hapa una kitu tujuze tukuelewe
 
Mwanakijiji hakuna aliyesema ni kosa tumeelewa kuwa si kosa. Lakini mtu yeyote akiwa na kitu chake atakwambia kuwa anacho kwa sababu flani, silaha mtu anamiliki kwa kuwa anajilinda kwa usalama wake na pingu ni kwa ajili ya kufanyia nini? Sawa umesema kuna matumizi mengine ambayo pingu zinatumika huwenda sababu za Jerry zinaangukia ndani ya kundi hilo la sababu nyinginezo but why zilikuwa garini siku ile ya tukio? Sisemi kuwa Jerry ana makosa la hasha but najaribu kuwaza zaidi why atembee nazo siku hiyo? au huwa zinakaa ndani ya gari lake daima? Yeye mwenyewe anasemaje?

Mi bado haijaniingia akilini huwenda ni kwa sababu ya upeo wangu mfupi wa haya mambo lakini ninaamini kama ambavyo mmenijuza mengi hata hili mtanisaidia tu.
Hivi alikuwa na pingu kwenye gari lake siku hiyo tu na siyo anakuwa nazo mara zote kwenye gari ?
 
Pingu zinatumika hasa kwa wazungu na wengineo katika kufanya mapenzi, kuna wanawake mpaka watiwe pingu ndiyo wanasikia raha, hali kadhalika wanaume wengine pia hivyo hivyo. Kwa hiyo pingu zina matumizi ya kila namna.

Lakini pia Jerry kazi aliyoifanya dhidi ya polisi ni ya hatari sanaaa, kuwa na pingu ni kitu kizuri tuu.
And who knows my be Jerry ni mtu wa USALAMA WA TAIFA!!!! Yoteee yawezekana.
 
Back
Top Bottom