TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Hata mimi natamani kufahamu kwa kweli,mwanzoni tulikuwa tunadanganyana kwamba raia wa kawaida haruhusiwi kumiliki lakini baadae wakati sakata la Muro linaendelea nikasikia kwamba pingu zinauzwa kama bidhaa zingine na leo tumeambiwa kwamba jamaa kawasilisha risiti ya manunuzi ya pingu yake..tafadhali wanasheria mtudadavulie jambo hili.
 
Haya kale karisiti ka ile pingu kamepatikana na wananchi mnakaribishwa kujipatia pingu zenu kwa Tshs 25,000/= tu.Kova leta sinema nyingine maana wewe na cheo chako hata hujui sheria za nchi sijui cheo hiki ulukipataje.Kama kuna fisadi alikutuma umnyamazishe Jerry Muro amechemsha na wewe unadhlilsha cheo hicho unastahili kuwa mkuu wa mgambo kule Manyoni.Nenda shule angalau ujuejue sheria acha longolongo ulizozoea kule Mbeya.


Naombeni kufahamu hivi kazi ya Pingu ni nini kwa raia wa kawaida?
 
Joji na wengine wote Tanzania, kwa wanaoishi jirani na mkoa wa Morogoro wanaweza kufika pale Mzinga kwenye karakana ya silaha, kuna duka la silaha, kuanzia risasi, bastola na bunduki kadha wa kadha za kuwindia kama ilivyo kwa Tanganyika arms, sasa Pingu huitaji kibali wala barua ya mtendaji kata kuinunua, ila risasi na bunduki ndio unahitaji kua na hati kadha wa kadha.
 
Tanzania ni nchi ya amani na utulivu....wazee mnataka kumiliki silaha na pingu za nini?

"The LORD is on my side; I will not fear. What can man do to me?" Psalms 118:6
 
You are absolutely right, la kuomba radhi kwa Mhando silijui, ila Jerry ni mla rushwa sana tu.

Na toka apewe tuzo amevimba kichwa sana kama yule wa Chadema. Hasikii ushauri wala nini anajiona yupo juu sana.
ukimwangalia tu anavyoongea na kujitetea na anavyopepesa macho unajua tu kwamba hilo soo kalifanya na ndio zake hizo,anyway hilo analo.
 
You are absolutely right, la kuomba radhi kwa Mhando silijui, ila Jerry ni mla rushwa sana tu.

Na toka apewe tuzo amevimba kichwa sana kama yule wa Chadema. Hasikii ushauri wala nini anajiona yupo juu sana.
ukimwangalia tu anavyoongea na kujitetea na anavyopepesa macho unajua tu kwamba hilo soo kalifanya na ndio zake hizo,anyway hilo analo.
 
Let us wait and see what is going to happen on this issue, thamani ya risiti tutaiona mwisho wa sakata hili, wangapi tunatumia mobile phone handsets tulizonunua kwa wamachinga? Hii iwe tahadhari siku kukitokea issue risiti itakutoa knockout!!
 
hii ndio risiti aliyopewa jerry muro baada ya kununua pingu.
1.JPG
 
Kufuatana na kilichoripotiwa katika magazeti yote mawili (Nipashe na Tanzania Daima), inaelekea Jerry aliwapelekea risiti hiyo moja kwa moja kwenye newsrooms zao, lakini siyo polisi kwenyewe (hata copy). Kwa nini? Masuali yazidi kuongezeka bila majibu kamili. Did he solicit, or didn't he? - the plot thickens.
 
Hii nchi bwana utafikiri imeshuka leo toka kuzimu. Huyu Muro mbona anaumiza watu vichwa namna hii. Sasa waziri mkuu kweli anaona jambo la Muro ni muhimu zaidi kuliko mafisadi walichukua pesa zetu walala hoi? Ukiamka Muro mkilala Muro what the hell is going on. Mnaacha kupambana na majambazi wanaochukua uhai wa wananchi nyie mmekazania Muro Muro mpaka jua linazama. Hebu tatueni matatizo muhimu ya wananchi sio Muro,Polisi, Rushwa n.k
 
Tanzania ni nchi ya amani na utulivu....wazee mnataka kumiliki silaha na pingu za nini?

"The LORD is on my side; I will not fear. What can man do to me?" Psalms 118:6

Kweli Tanzania ni nchi ya amani...au watu mnataka kuwafunga mapingu wakezenu ana watoto wenu wanapowakosea?
 
Acha majungu wewe, watu kama ninyi ndio manachangia kwa kiasi kikubwa sana kuisambaratisha hii jamhuri....unaweza kuweka ushahidi hapa hata wa kusikia vijiweni kuwa huyu bwa'mdogo JM ni mla rushwa? Tafadhali weka ushahidi, vinginevyo acha majungu.

Usihangaike mimi ilishasituka kuwa huyu ni majeruhi wa Jerry manake usidhani kuwa hawamo humu, JF ni kubwa hii?
 
Mh, hata makampuni ya ulinzi yanapingu pia, je mwandishi wa habari pingu za nini!
 
Tanzania Daima wanasema mwaka wa kutolewa risiti umefutikafutika.,nipashe wao wamesema ni 2008. Which is which?
Utata juu ya utata!
 
Tanzania Daima wanasema mwaka wa kutolewa risiti umefutikafutika.,nipashe wao wamesema ni 2008. Which is which?
Utata juu ya utata!
hAYO YOTE NI MAGAZETI,LAKINI KUMBUKA KUWA kOVA KAMA BOSI WA JESHI LA POLISI KASEMA MTU BINAFSI HAWEZI KUMILIKI PINGU, SWALI LILE DUKA LINAMUUZIA HIZO PINGU NANI? JE POLISI WANANUNUA PINGU KWENYE HILO DUKA NA SIO RAIA?. JE KOVA HAKUJUA KUWA KUNA MADUKA YANAUZA PINGU?
 
Mnafikiri Polisi watafanya uchunguzi huru hapo?
Tunaomba iundwe Tume tumechoka ifanye kazi mtasikia tu imeundwa wanakula 100mil.

Mkuu Fidel,

Sitashangaa kusikia imeundwa tume na imetumia zaidi ya millioni 100. Lakini je, katika mazingira yaliyopo tunatarajia polisi kutenda haki katika sakata hili kama wakiachiwa wao kufanya huo uchunguzi?

Tiba
 
TATIZO LA KOVA ANAFIKIRI PINGU NI SILAHA LOL kumbe wenzie huku tunazitumia kufanyia malavidavi, i mean kuongeza manjonjo kwenye shughuli, na zinauzwa kwenye masex shops!!!kwa nini JM hakuwaambia kazinunua nje ya nchi.... easy.
 
Mh, hata makampuni ya ulinzi yanapingu pia, je mwandishi wa habari pingu za nini!

Kwa kampuni za ulinzi sawa kumiliki pingu, lakn kwa raia tu wa kawaida sielewi pingu ni za kazi gani! Kama kwa ajili ya mapenzi zipo za plastic na hata kamba zinatosha. Lakini kwa kutembea na pingu pamoja na bastola, mmh...
 
Wadau habari sana,


Tangu tukio la kukamatwa kwa mwandishi wa habari za uchunguzi JM mambo mengi yamejitokeza na yanaendelea kujitokeza, Lakini kikubwa ambacho nimevutiwa nacho ni kugundua kuwa raia anaruhusiwa kumiliki pingu, sasa wakuu naombeni mnifahamishe taratibu gani nifuate ili ikiwezekana niweze kuwa namiliki pingu.

Tuambie kwanza unataka pingu za kazi gani au mapambo nyumbani au kumfunga ng'ombe wakati wa kumkamua au...za kufanyia ujamb.........
 
Back
Top Bottom