TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

I'll tell you why I'm laughing (if you didn't notice); Muro ameitwa kwenda mahali ambapo ameahidiwa kukatiwa kitu kidogo.. anatoa taarifa kwa vyombo husika (in this case, say TAKUKURU) na anaandaa watu wake wa kurekodi kitu hicho. Yule mtu mwingine anatoa taarifa kwa vyombo husika (lets assume ni Polisi); Polisi wanaandaa mtego wa kumtia matatani Muro, na mura anaandaa mtego kumtia matatani jamaa ili amrushe katika kipindi chake.

Well.. anaenda pale anakabidhiwa mzigo (polisi wanachekelea wamemnasa). Na mara moja wanaanza kujitamba kuwa jamaa anayepiga vita rushwa ndiyo huyo kakamatishwa. Habari zinaruka haraka haraka na wanamkimbiza Muro kituoni, sms zinaenea, na hadithi kolea.

Muro anafikishwa kituoni anapigishwa mkwara na maneno kibao. Anapewa nafasi ya kujitetea. Anawaambia "mna wazimu".. wanashangaaa..

should I tell you how the story end?[/QUOTE]



ooooooooooooooooooooooooooooooops please go ahead MKJJ
 
on the day that Jerry was airing ile issue ya Iringa, nilichonga na mkulu mmoja wa hilo jeshi letu .... akaniambia huyu dogo watamtenda tu ... kama sio kummaliza then watamshikisha adabu .... nikamuuliza why?? akasema sasa amezidi ... amefukuzisha sana watu kazi na haelekei kubadilika.

I was kinda puzzled!! kwamba ndivyo usalama wetu wa raia bongo walivyo?? ina maana hii move haiko supported kabisa na police .... to them wao wanaona kama wanadhalilishwa!

so MKJJ, hiyo ni first attempt tu, i believe there are more to come! Why serikali yetu isimpe ulinzi?? sababu the the guy is now a clear target! .... sitoshangaa kuona taa hii mpya ya matumaini ya uadilifu wa uandishi wa habari ikitokomezwa .... coz tumeshuhudia sehemu nyingi tu police wetu wakihusishwa na ujambazi na maovu mengineyo!

jamani tusingojee hilo litokee!

MDBD
Serikali ipi impe ulinzi na wakati wote ni mafisadi na hawapendi ishu zao zitoke nje kama hivi?
 
haya yote yana gharama jamani; kama kweli ameamua kuingia kwenye mapambano ni lazima awe tayari kulipa gharama yake. Hii ndio maana inaitwa vita. Kama kweli ni mpiganaji wa dhati, my story hapo juu has an ending made for the movie.
 
JAmani sasa wewe unaomba rushwa halafu unatumia nguvu (kumfunga pingu ili atoe rushwa si kutumia nguvu?) huo ni ujambazi sasa si kuomba rushwa . Nafikiri hii ni hadithi ili kuhalalisha uwepo wa pingu ndani ya gari la Muro

Jerry has alikuwa framed... lakini bahati nzri, framer wake hakujua kwamba jamaa yuko kazini....
 
Huo ni mtego wa kutumaliza waaandishi kwa hiyo msifurahie hiyo ishu ya jeri kukamatwa wanalipiza kisasi cha wenzao iringa. Lazima tuwe makini katika hili. polisi wametangaza vita na media kwasababu habari zao za rushwa zimeingia maji machafu. Ila hawatawezi kina jeri topo wengi wataisha tu kama IGP mwema hajui uozo wa jeshi lake Jk avunje aunde kikosi kingine. Aluta Kontinwa.

No, nyie waandishi wa habari mnaongoza katika kupokea rushwa. Tatizo hakuna mwandishi ambaye yuko tayari kulisema hili hadharani kwa maana ya kuandika. Sina haja ya kueleza jinsi ambavyo mnatia aibu kwa kuomba rushwa na kujifanya maofisa usalama.
Jerry hayuko juu ya sheria na hawezi kuepuka kutuhumiwa kama binadamu wa kawaida. Hii si vita ya Polisi na waandishi bali ni vita ya kupambana na rushwa, haina macho kwamba itamwacha hata yule anaepiga kelele za kukata rushwa MCHANA ilhali usiku ANAMULIKA.
Jerry ana haki ya kushtakiwa kwa tuhuma zozote zile na kujitetea mbele ya mahakama. Iki nchi yetu ipate mafanikio ni lazima tuache longolongo kwamba huyu mwandishi mwenzetu yuko katika mapambano ya rushwa kwahiyo asituhumiwe au kushtakiwa.
Kwa kuongezea kama mimi na wewe hatupokei rushwa si rahisi kuwatambua wapokea rushwa.
Jerry akifanya kazi nzuri tutampongeza, akiharibu tutamsema.
WALA RUSHWA WOTE HUJUANA.
 
jerry muro akiwa kituo cha kati cha polisi dar leo
Jerry Muro akiingia sentro leo
Akiwa amezingirwa na makachero wa polisi, mwandishi wa TBC Jerry Muro akiwasiliana na ndugu na jamaa baada ya kufikishwa kituo cha kati jijini Dar leo akituhumiwa kupokewa rushwa toka kwa mhasibu mkuu wa zamani wa wilaya ya Bagamoyo, Bw. Michael Wage

Jerry Muro akihojiwa na waandishi wenzie kituo kikuu cha polisi jijini Dar leo ambako anashikiliwa kwa tuhuma za kupokea rushwa ya shilingi milioni 10. Jerry Muro akijiandaa kukabidhi vitu vyake
kwa makachero wa polisi baada ya kufikishwa sentro leo

JERRY MURO MATATANI

Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Mtangazaji wa Shirika la Habari Tanzania (TBC) Jerry Muro (pichani juu kulia) kwa tuhuma za kudai fedha kwa njia ya vitisho.

Muro anadaiwa kumtisha aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo Michael Wage ambaye hivi karibuni alisimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa tuhuma za ubadhilifu pamoja na viongozi wengine wa Halmahauri ya Wilaya Bagamoyo.

Akithibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo Suleimani Kova alikiri jeshi lake kumshikilia Muro na kuwa alimtishia Wage kuwa yeye ni Ofisa wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na kumtaka atoe fedha Sh milioni 10.

"Polisi inamhoji Muro dhidi ya tuhuma hizo na mahojiano yakikamilika taratibu za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na maelezo zaidi nitayatoa kesho wakati wa mazungumzo yangu na waandishi wa habari" Kova alisema.

Bingwa huyo wa Tuzo za Uandishi wa Habari 2009 Tanzania alionekana akiwa sentro na mkononi ameshikilia bahasha tatu pamoja na kamera ya Video.

Alipohojiwa na wenzie juu ya kuhusika na tuhuma hizo alikana na kudai kushangazwa kuwekwa chini ya ulinzi kwa madai kuwa alipigiwa simu na mtu kupewa taarifa kuwa kuna kazi katika Hoteli ya City Garden.

"Kaka nilitaarifiwa tu kama ujuavyo kazi zetu kuwa kuna kazi City Garden niakaamua kwenda. Lakini baada ya kufika tu nilishangaa nawekwa chini ya ulinzi na askari kanzu ambao ndiyo walionifikisha kituoni hapa bila ya kunitajia kosa lanmgu. " alilonga Muro.

Kwa upande wake Wage alidai kuwa mtuhumiwa anatumiwa na watu wengine ambapo juzi alimpandisha katika gari lake na kumfunga pingu kisha kumtaka atoe Sh milioni 10 na kwa kuthibitisha kuwa alikuwa ndani ya gari hilo alidai kuacha miwani yake yenye mikanda myeusi.

Polisi ilipomhoji Muro kama anazo pingu alikiri kumiliki pingu pamoja na bastola ambapo baada upekuzi katika gari lake lenye namba za usajili T 545 BEH polisi walikuta pingu hizo pamoja miwani iliyosemwa na mlalamikaji.

Muro alishinda tuzo ya Mwandishi bora wa mwaka kupitia vipindi vyake vya Televisheni vya "Usiku wa Habari" vinavyorushwa katika kituo cha TBC1 kila siku na kabla ya kuhamia hapo alikuwa kituo cha ITV na aliendesha kipindi cha "Ripoti Maalum".


Miongoni mwa mambo aliyokuwa akirusha katika vipindi hivyo ni pamoja na rushwa, matumizi mabaya ya madaraka pamoja na ukiukwaji wa sheria.

Polisi wamekuwa ni waathirika wakuu katika vipindi hivyo kwani mara mbili amewatoa Polisi Usalama barabarani wakiomba na kupokea rushwa hadharani kutoka kwa madereva wa malori na mabasi ya mikoani.


Taken from: http://issamichuzi.blogspot.com/
 
No, nyie waandishi wa habari mnaongoza katika kupokea rushwa. Tatizo hakuna mwandishi ambaye yuko tayari kulisema hili hadharani kwa maana ya kuandika. Sina haja ya kueleza jinsi ambavyo mnatia aibu kwa kuomba rushwa na kujifanya maofisa usalama.
Jerry hayuko juu ya sheria na hawezi kuepuka kutuhumiwa kama binadamu wa kawaida. Hii si vita ya Polisi na waandishi bali ni vita ya kupambana na rushwa, haina macho kwamba itamwacha hata yule anaepiga kelele za kukata rushwa MCHANA ilhali usiku ANAMULIKA.
Jerry ana haki ya kushtakiwa kwa tuhuma zozote zile na kujitetea mbele ya mahakama. Iki nchi yetu ipate mafanikio ni lazima tuache longolongo kwamba huyu mwandishi mwenzetu yuko katika mapambano ya rushwa kwahiyo asituhumiwe au kushtakiwa.
Kwa kuongezea kama mimi na wewe hatupokei rushwa si rahisi kuwatambua wapokea rushwa.
Jerry akifanya kazi nzuri tutampongeza, akiharibu tutamsema.
WALA RUSHWA WOTE HUJUANA.

tuwasikiliza Polisi kama wana kesi yenye ushahidi utakaoweza kusimama mahakamani; kama hawana na wameboronga wawe tayari kuomba msamaha.
 
kama kweli kala rushwa au kapakaziwa time will tell
 
haki ya mtu haipotei ila inachelewa sanaaaaaaaa,time will tell
 
tuwasikiliza Polisi kama wana kesi yenye ushahidi utakaoweza kusimama mahakamani; kama hawana na wameboronga wawe tayari kuomba msamaha.

Mhh, kwani hapa kuna kitu kitawekwa hewani (public)? Nahisi kama kweli mtego ume-abort, basi polisi wataomba yaishe kimya kimya - kiutu uzima! Bado naelea hewani mwenzenu!
 
Mzee Mwanakijiji;

Kuna vitu havi TALLY hapo.

1. Pingu ya nini kwa mtu kama yeye??
2. Kama alipigiwa simu na kwenda eneo la tukio, Je alipokea hiyo hela?
3. Kwanini hela itoke polisi na sio TAKUKURU?
4. Wage alijuaje Jerry ana pingu kwenye gari lake?


Kuna dots zina miss kwenye hii movie..

FP
 
Mzee Mwanakijiji;

Kuna vitu havi TALLY hapo.

1. Pingu ya nini kwa mtu kama yeye??
2. Kama alipigiwa simu na kwenda eneo la tukio, Je alipokea hiyo hela?
3. Kwanini hela itoke polisi na sio TAKUKURU?
4. Wage alijuaje Jerry ana pingu kwenye gari lake?


Kuna dots zina miss kwenye hii movie..

FP

FP,

Nimesema sana kwamba bado nyota ni nyingi kichwani mwangu! Ni maluwe luwe tu. Sioni mwanga wowote ili akili yangu ndogo iweze kuunda story. Labda majinias ndo wanaweza kuelewa vizuri hiki kitu! Mimi nimetoka kapa!
 
Na swali la mwisho ambalo ni GUMU ni kuwa, Jamaa wa Bagamoyo tayari kazi kasimamishwa/kufukuzwa.......sasa alikua anatoa rushwa ili iweje?
 
FP,

Nimesema sana kwamba bado nyota ni nyingi kichwani mwangu! Ni maluwe luwe tu. Sioni mwanga wowote ili akili yangu ndogo iweze kuunda story. Labda majinias ndo wanaweza kuelewa vizuri hiki kitu! Mimi nimetoka kapa!

Aisee Dark City..mi mwenyewe nipo katika Dark City.

Giza tupu. Ila source yangu flani ananinyetisha kuwa jamaa ni zake kudai mshiko.

Sasa tusubiri.
 
FP,

Nimesema sana kwamba bado nyota ni nyingi kichwani mwangu! Ni maluwe luwe tu. Sioni mwanga wowote ili akili yangu ndogo iweze kuunda story. Labda majinias ndo wanaweza kuelewa vizuri hiki kitu! Mimi nimetoka kapa!


Na kuwa kuna watu wengine watajitokeza leo kutoa ushahidi jinsi jamaa alivyowatoa hela.

Vitha ni vitha Mura
 
Mwandishi Jerry Muro aingia matatani Dar

Boniface Meena na Sadick Mtulya.



SIKU chache baada ya kutoa habari zilizoanika rushwa zinazofanywa na askari wa kikosi cha usalama barabarani, mwandishi wa habari za uchunguzi, Jerry Muro ameingia matatani baada ya kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa.

Muro, mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji (TBC) na ambaye amejipatia umaarufu kutokana na kufichua aina tofauti za rushwa, anashikiliwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi ambayo imeeleza kuwa habari zaidi kuhusu mkasa wake zitatolewa leo.

Habari za kupambana na kero ya rushwa na ufisadi jana zilimwingiza mwandishi huyo mikononi mwa polisi.

Habari zaidi zinasema kuwa Muro, ambaye alishinda tuzo ya Mwanahabari Bora wa mwaka 2009 kutokana na habari yake ya rushwa inayofanywa na askari wa usalama barabarani, alikumbwa na mkasa huo jana majira ya saa 6:00 jijini Dar es Salaam.

Alikamatwa wakati akiwa hoteli ya Sea Cliff.

Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata, Muro alikamatwa baada ya kuwekewa mtego na polisi mara baada ya kuarifiwa na mfanyabiashara mmoja, ambaye jina halijawekwa bayana na polisi, kuwa mwandishi huyo amedai rushwa ya Sh10 milioni.
Habari zinadai kuwa mwandishi huyo alikamatwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa fedha hizo.

"Muro alikuwa ameahidiana na mfanyabiashara mmoja kuwa angepewa Sh10 milioni kama hongo, lakini mfanyabiashara huyo alitoa taarifa polisi na ndio leo (jana) wamefanikiwa kumkamata. Walimkamata mara baada ya kupokea fedha hizo," alisema mtoa taarifa.

Kamanda wa polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alikiri jeshi lake kumshikilia mwandishi huyo kwa mahojiano, lakini hakutaka kuelezea zaidi mkasa huo.

"Ni kweli yuko hapa na anahojiwa na mimi ndo ninapewa taarifa hivyo nitatoa taarifa kamili kesho (leo) saa 6:00,"alisema Kova.
Alisema kuwa Muro amekamatwa kutokana na tuhuma za kutaka kuchukua fedha kutoka kwa mlalamikaji ambaye hakumtaja jina lake.

Kukamatwa kwa mwandishi huo ni mwendelezo wa wimbi la matukio ya kukamatwa kwa waandishi mara baada ya kuripoti uozo katika taasisi za serikali. Mwaka 2004, mwandishi mwandamizi wa IPP, Zephania Musendo alikamatwa kwa tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa kigogo wa Taasisi ya Kupambana na Rushwa (Takuru).

Alikamatwa baada ya kutoa habari mfululizo kuhusu uozo uliokuwa unaihusu taasisi hiyo, hasa migongano ya vigogo wa Takuru, ambayo kwa sasa imeongezewa majukumu na kuitwa Takukuru. Mwandishi huyo alitiwa hatiani mwaka 2005 na kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela.

Mwaka 2002, mwandishi wa Mwananchi, George Maziku alikamatwa na polisi kwa madai ya ya kuingilia uhuru wa Bunge baada ya kuandika habari kuwa baadhi ya mabadiliko ya sheria yalilenga kukipa upendeleo chama tawala na kwamba suala la takrima lingechochea rushwa.

Maziku alihojiwa na polisi kwa saa kadhaa na baadaye kuachiwa bila ya kufunguliwa mashtaka.

Mwaka 1996, mwandishi wa IPP mkoani Ruvuma, Adam Mwaibabile alikamatwa kwa tuhuma za kukutwa na nyaraka za serikali. Mwandishi huyo alikuwa anachukiwa na uongozi wa mkoa kutokana na kuripoti uozo uliokuwa ukifanywa na viongozi wa juu wa serikali ya mkoa.

Inadaiwa alikutwa na nyaraka kutoka kwa mkuu wa mkoa ambayo ilikuwa ikimuelekeza mkurugenzi kutompa mwandishi huyo leseni ya biashara.

Alipatikana na hatia na kuhukumiwa kwenda jela mwaka mmoja, lakini juhudi za wanaharakati na wadau wa habari zilimrejesha mahakamani kupinga hukumu hiyo na akashinda na kuachiwa huru.

Katika taarifa yake iliyotingisha Jeshi la Polisi, Muro, wakati huo akiwa kituo cha televisheni cha ITV, alionyesha jinsi askari wa usalama barabarani wanavyoomba na kupokea rushwa kutoka kwa madereva wa magari kwenye Barabara ya Morogoro.

Mapema mwaka huu akiwa TBC1, Muro alionyesha rushwa kama hiyo ya askari wa usalama barabarani mkoani Iringa wakiomba na kuchukua rushwa kutoka kwa madereva. Habari hizo mbili zilisababisha askari zaidi ya 20 kutimuliwa kazi.

Mbali na tuzo ya Mwandishi Bora wa Mwaka, Muro alitunukiwa pia tuzo mbili tofauti; moja ikihusu uandishi mzuri wa habari zinazohusu utawala bora na nyingine VVU na Ukimwi kwa upande wa televisheni.
 
Back
Top Bottom