TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Mimi bado naona maluweluwe wala majibu ya msingi ya kumtia hatiani sijapata... Navuta subira....
 
Jamani sisi tunaspeculate tu hii habari nafikiri Jerry ni mfanyakazi mwajiriwa wa TBC na kukamatwa kwake -Jerry anadai alikuwa kazini sasa uongozi wa TBC unaweza kusema lolote juu ya hili? Maana si kuwa kachafuliwa Jerry binafsi la hasha hata ofisi yake so ningefurahi kama mwajiri wake TBC angesema lolote au kutoa tamko lolote juu ya tuhuma (sijui shutuma-mtanisamehe sijui tofauti yake) hizi.
 
Eti wamemkamata anapokea rushwa do hii mpya,polisi wanakamata mtu anapokea rushwa inaingia akilini hii kisa wanakijua wenyewe nyie watoto wa mwema hii siyo Tanzania ya mwaka 47, ndio maana tunawashauri mrudi shule muendane na jeshi la kisasa muepukane na fikra za kizamani, embu tukamatieni majambazi huku mitaani achaneni na visasi visivyo ingia akilini
 
jerry(1).jpg


Makachero wa polisi wakichukua nyaraka kutoka kwa Mwandishi wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Jerry Murro (wa pili kushoto) wakati walipopekua gari lake katika kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaama jana.



Utata umeghubika tukio la kukamatwa kwa mshindi wa tuzo ya mwandishi bora kwa mwaka 2009, Jerry Muro, anayefanya kazi katika Shirika la Utangazaji wa Taifa (TBC).
Taarifa zinaeleza kuwa Muro alikamatwa jana asubuhi maeneo ya katikati ya jiji, baada ya askari polisi kulizingira gari lake na kumweka chini ya ulinzi, kisha kumpeleka Kituo Kikuu kwa mahojiano.
Inaelezwa kwamba Muro alifika katika eneo hilo baada ya kupigiwa simu na mtu asiyejulikana, akimtaarifu kuhusu kuwepo tukio lenye umuhimu kwa jamii, ambalo alistahili kuliandika na kulitangaza.
Wakati hayo yakijiri, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, ameshindwa kutoa ufafanuzi wa tukio hilo, licha ya kuthibitisha kushikiliwa kwa Muro.
Kova aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake kuwa, maelezo ya ufasaha kuhusu kukamatwa kwa Muro, atayatoa leo kwa waandishi wa habari.
Hata hivyo, taarifa za ndani kutoka polisi zilieleza kuwa baada ya kufikishwa Kituo Kikuu, Muro alidaiwa kuomba rushwa ya Sh milioni 10 kutoka kwa mtu aliyetambulika kuwa ni Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage.
Muro anadaiwa kuomba rushwa hiyo ili asaidie kushughulikia tatizo la kufukuzwa kazi kwa Mhasibu huyo, kulikofikiwa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Nipashe ilipofika Kituo Kikuu jana mchana, ilimshuhudia Muro akishikiliwa na polisi, huku gari lake aina ya Cresta GX 100 yenye namba T 545 BEH likilindwa na askari kanzu.
Habari za kipolisi zilidai kuwa, baada ya kufikishwa kituoni hapo, Muro alitakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la siku mbili zilizopita, la kumuomba rushwa Wage.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, Wage anayedaiwa kutoa taarifa kuhusu tukio hilo aliiambia polisi kwamba alisahau mawani yake kwenye kiti cha mbele cha gari la Muro, na kwamba aliona pingu za polisi ndani ya gari hilo.
Kutokana na maelezo hayo, Muro alitakiwa kwenda kupekuliwa, lakini alipotakiwa kutoa ufunguo, Muro hakuuona, hali iliyomfanya aombe ruhusa ya polisi kuomba ndugu zake wamletee (ufungo) wa akiba kutoka nyumbani.
Kabla ya ufunguo kuletwa kituoni hapo, inadaiwa kuwa ufunguo wa awali ulionekana katika mazingira ambayo Muro hakuyajua, ndipo aliposhuka kutoka sehemu ya juu kituoni hapo, akiwa chini ya ulinzi wa polisi kwenda kupekuliwa gari lake.
Muro alipokutana na kuzungumza na waandishi wa habari huku akiwa chini ya ulinzi wa polisi, hakuonekana kushtushwa na tukio hilo, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida alisema “nipo hapa kikazi, si mnajua polisi wana ushirikiano mzuri na waandishi wa habari?”
Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kuhusishwa na rushwa, Muro ambaye kuna taarifa kwamba aliachiwa huru kwa dhamana jana jioni, alijibu kwa ufupi, “hakuna kitu kama hicho.”
Kadhalika haikuweza kujulikana kwa nini Wage alivutika kwenda kushitaki kosa la rushwa polisi badala ya Takukuru ambao hutoa pesa za unga ambazo huwa kidhibiti 'murua'.
Muro amewahi kutayarisha vipindi vya televisheni vilivyotangazwa kupitia vituo viwili tofauti vya luninga, zikifichua uovu wa rushwa unaofanywa na polisi wa usalama barabarani, maarufu kama trafiki.
Kwa mara ya kwanza, Muro akiwa mfanyakazi wa ITV, alishirikiana na mpiga picha wake, Idrisa Magomeni, walifichua rushwa inayotolewa kwa trafiki katika maeneo ya kati ya mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro.
Makala hiyo iliyochangia ushindi wa tuzo ya mwandishi bora, ilirushwa kupitia kipindi cha Ripoti Maalum cha ITV. Pia katika siku za hivi karibuni, Muro alishiriki kuandaa kipindi cha Usiku wa Habari kinachorushwa kupitia luninga ya TBC1, ambapo askari wa usalama barabarani mkoani Iringa walionekana wakipokea rushwa.
Makala hizo zilizoonekana kutowafurahisha askari na maofisa kadhaa wa polisi, wahusika katika kadhia hiyo walifukuzwa kazi, ili kulinda heshima ya jeshi hilo.
Inadhaniwa pia kwamba habari hizo hazikuwafurahisha baadhi ya polisi na hivyo kumjengea maadui katika jeshi hilo.




CHANZO: NIPASHE
 
ni mpango wa kupangwa ukisoma story kamili, eti wanamhoji kwamba alidai rushwa ya mil 10, walimkamata akishuka kwenye gari lake akiingia mgahawa wa city restaurant, je uo ndio utaratibu wa kufuatilia kesi za rushwa? ina maana mimi nikienda polisi kusema karamagi kaniomba rushwa ya ml 10 basi polisi wakurupuke kwenda kumkamata! hivi si vichekesho, kwa nini wasimtegee mtego kama wanavyofanyaga then wamnase on the spot akipokea iyo rushwa? ni kikesi cha kumchafulia jina tu kwani mwisho wa siku hamna ushahidi wowote utaopatikana bali kumchafulia jina tu.
 
Kwa hiyo story hapo juu .. kama anatumia mitandao ya simu kwanza ni rahisi kukamata maongezi kati yake na huyo aliyesema alitakiwa kutoa Rushwa ..
Haya mitandao ya simu na nyie kazi kwenu kusaidia kutoa ushahidi katika utata huu .najua huwa mnakuwa na record yote ya maongezi ...
...ndo hapo tuendelee na mengineyo
 
Swali ni je Muro kama mwandishi wa habari ana uwezo wa kufanya nini juu ya suala la mtu aliyefukuzwa kazi na Waziri mkuu hata aombe rushwa ya kumsaidia katika hilo? Mi ctaki bwana
 
kwa hali hii hakuna haja ya wabongo hasa vijana tulio nje ya mipaka yetu kurudi Tanzania.
 
ni mpango wa kupangwa ukisoma story kamili, eti wanamhoji kwamba alidai rushwa ya mil 10, walimkamata akishuka kwenye gari lake akiingia mgahawa wa city restaurant, je uo ndio utaratibu wa kufuatilia kesi za rushwa? ina maana mimi nikienda polisi kusema karamagi kaniomba rushwa ya ml 10 basi polisi wakurupuke kwenda kumkamata! hivi si vichekesho, kwa nini wasimtegee mtego kama wanavyofanyaga then wamnase on the spot akipokea iyo rushwa? ni kikesi cha kumchafulia jina tu kwani mwisho wa siku hamna ushahidi wowote utaopatikana bali kumchafulia jina tu.

Mkuu nakubaliana na wewe,mi nachoshangaa ni hiki TAKUKURU walikuwa wapi mpaka polisi wakamkate mtu anaetuhumiwa kwa rushwa? kwa sababu nijuavyo TAKUKURU ndo haswa walipaswa kumkamata jamaa na kumhoji,sasa polisi imekuwaje wao ndo wakamkamata? KULIKONI?
 
Inaelezwa kwamba Muro alifika katika eneo hilo baada ya kupigiwa simu na mtu asiyejulikana, akimtaarifu kuhusu kuwepo tukio lenye umuhimu kwa jamii, ambalo alistahili kuliandika na kulitangaza.


Mchezo ndipo ulipoanzia hapa- mpigie simu jifanye kuna habari- akija tu we tuachie kazi. Jerry unayo namba ya simu uliyopigiwa -atafutwe huyo mpigaji wa simu then tujue kama ni kweli kulikuwa na habari au ndo ulikuwa unaambiwa 'baby come?'

Muro anadaiwa kuomba rushwa hiyo ili asaidie kushughulikia tatizo la kufukuzwa kazi kwa Mhasibu huyo, kulikofikiwa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


Nauliza tena hapa Jerry angesaidia namna gani?-Kumrudisha kazini au?

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, Wage anayedaiwa kutoa taarifa kuhusu tukio hilo aliiambia polisi kwamba alisahau mawani yake kwenye kiti cha mbele cha gari la Muro, na kwamba aliona pingu za polisi ndani ya gari hilo.

Kwa nini akimbilie kutoa ushahidi wa vitu alivyovikuta kwenye gari mapema hivi? Je Jerry wakati unatoka nyumbani kwako uliviona vidhibiti hivi garini kwako?

Kutokana na maelezo hayo, Muro alitakiwa kwenda kupekuliwa, lakini alipotakiwa kutoa ufunguo, Muro hakuuona, hali iliyomfanya aombe ruhusa ya polisi kuomba ndugu zake wamletee (ufungo) wa akiba kutoka nyumbani.
Kabla ya ufunguo kuletwa kituoni hapo, inadaiwa kuwa ufunguo wa awali ulionekana katika mazingira ambayo Muro hakuyajua,

CHANZO: NIPASHE

Jerry wakati wa kukamatwa hakukuwa na purukushani yoyote iliyowapa nafasi police kupossess ufunguo wako wa gari? Ulipopatikana mara ya pili ulipatikanajepatikanaje? sio kuwa waliuchukua na kwenda kuplace hivyo vidhibiti?

ah geshi ra borisi mnabaka haki yangu ya kuwaamini, mi ctaki kabisa bana
 
kwa hali hii hakuna haja ya wabongo hasa vijana tulio nje ya mipaka yetu kurudi Tanzania.

.......no no no...usichanganye mambo hapa mkubwa, na usitake kujustify kukosa uzalendo wako kwa tukio hili, niambie ni nchi gani hapa duniani mambo yao ni mswano 100%? Rudini home tusaidiane kuijenga nchi kimaadaili na ''kimwili'' mzee!
 
ni mpango wa kupangwa ukisoma story kamili, eti wanamhoji kwamba alidai rushwa ya mil 10, walimkamata akishuka kwenye gari lake akiingia mgahawa wa city restaurant, je uo ndio utaratibu wa kufuatilia kesi za rushwa? ina maana mimi nikienda polisi kusema karamagi kaniomba rushwa ya ml 10 basi polisi wakurupuke kwenda kumkamata! hivi si vichekesho, kwa nini wasimtegee mtego kama wanavyofanyaga then wamnase on the spot akipokea iyo rushwa? ni kikesi cha kumchafulia jina tu kwani mwisho wa siku hamna ushahidi wowote utaopatikana bali kumchafulia jina tu.

kumjenga!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
jerry(1).jpg


Taarifa zinaeleza kuwa Muro alikamatwa jana asubuhi maeneo ya katikati ya jiji, baada ya askari polisi kulizingira gari lake na kumweka chini ya ulinzi, kisha kumpeleka Kituo Kikuu kwa mahojiano.

Alikamatwa katikati ya jiji ama sea clif??? vyanzo vingine ninasema seaclif wengine katikati ya jiji tuelewe kipi??????

Inaelezwa kwamba Muro alifika katika eneo hilo baada ya kupigiwa simu na mtu asiyejulikana, akimtaarifu kuhusu kuwepo tukio lenye umuhimu kwa jamii, ambalo alistahili kuliandika na kulitangaza.
hapa ni mtego tu, mwandishi aliebobea hawezi kukurupuka tu kutoka pila kuwa na uhakika wa tukio lenyewe

Muro alidaiwa kuomba rushwa ya Sh milioni 10 kutoka kwa mtu aliyetambulika kuwa ni Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage.

Hapa napo kizunguzungu mara mfayabiashara mara mhassibu wa bagamoyo tuelewe kipi vyanzo vya habari kuweni makini

Muro anadaiwa kuomba rushwa hiyo ili asaidie kushughulikia tatizo la kufukuzwa kazi kwa Mhasibu huyo, kulikofikiwa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Ataomba rusha kwa mtu aliyetimuliwa kazo na PM ili iweje??.

Nipashe ilipofika Kituo Kikuu jana mchana, ilimshuhudia Muro akishikiliwa na polisi, huku gari lake aina ya Cresta GX 100 yenye namba T 545 BEH likilindwa na askari kanzu.
Kwaniani gari lake lilindwe na askari kanzau likiwa kituoni?? inamaana watu wanokwenda na magari kuhojiwa polisi magari yao yanalindwa na akari kanzu eneo la kituo ili iweje??

Habari za kipolisi zilidai kuwa, baada ya kufikishwa kituoni hapo, Muro alitakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la siku mbili zilizopita, la kumuomba rushwa Wage.
kama walikuwa wanataarifa kuwa aliomba rushwa siku bili zilizopita walikuwa wapi hadi wamkamate baada ya siku 2??

, Muro alitakiwa kwenda kupekuliwa, lakini alipotakiwa kutoa ufunguo, Muro hakuuona,
nani alichukuwa ufunguo wa gari la muro na kwanini aliuchukuwa

hali iliyomfanya aombe ruhusa ya polisi kuomba ndugu zake wamletee (ufungo) wa akiba kutoka nyumbani.

mchezo mchafu umefanyika hapo

Kabla ya ufunguo kuletwa kituoni hapo, inadaiwa kuwa ufunguo wa awali ulionekana katika mazingira ambayo Muro hakuyajua, ndipo aliposhuka kutoka sehemu ya juu kituoni hapo, akiwa chini ya ulinzi wa polisi kwenda kupekuliwa gari lake.
kama funguo ulipotea iweje upatikane kwenye mazingira ya kutatanisha.... kuna jambo limejificha hapo


Muro alipokutana na kuzungumza na waandishi wa habari huku akiwa chini ya ulinzi wa polisi, hakuonekana kushtushwa na tukio hilo, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida alisema “nipo hapa kikazi, si mnajua polisi wana ushirikiano mzuri na waandishi wa habari?”

anajijua anawindwa kwa udi na uvumba na anamaadui wengi sana ktk jamii inayomzunguka hapo nadhani alielewa nini kinachofanyika.
Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kuhusishwa na rushwa, Muro ambaye kuna taarifa kwamba aliachiwa huru kwa dhamana jana jioni, alijibu kwa ufupi, “hakuna kitu kama hicho.”
rushwa ya milioni 10 uachiwe kwa dhamani jioni tena jana ni j2 inakuja akilini kweli

Kadhalika haikuweza kujulikana kwa nini Wage alivutika kwenda kushitaki kosa la rushwa polisi badala ya Takukuru ambao hutoa pesa za unga ambazo huwa kidhibiti 'murua'.

hela zote za rushwa za kukamatisha watu huwa zinatoka takukuru haya huyo muhasibu why aende polisi kuchukua pesa.... kunamchezo unachezwa hapo tena wakitoto kabisa.

Hivi mtu kama muro anajijua wazi kuwa amewasababishiwa watendaji wengi sana wa serikali kukamatwa kwa rushwa sasa leo hii yy aombe rushwa ya 10 milion tena aletewe mkononi inmaana hana akili alishindwa kuwaambia wamwekee ktk account tena ya mtu sio yake bado narudia hii ni njama ningeomba polisi wajipange upya kumuwinda jerry mur hapo wamechemka

 
kumbe uzushi tu akuna lolote kuchafuana tu jerry kuwa makini maadui ni wengi kuliko marafiki ucfe moyo
 
Nasikitika, bado ukweli juu ya jambo hili haujulikani. Tumebaki kikisia na kunukuu vyombo vya habari ambavyo katika hili nao sio makini, hawana uchambuzi na kwa vyovyote vile hawawezi kuaminika. Nasubiri taarifa za baadaye leo.
 
Kama Jerry angeomba rushwa si angewekewa mtego na PCCCB? Lakini ikumbukwe kuwa wanasema yeye ameomba rushwa akijitambulisha kuwa in officer wa PCCCB, hii hapa imekaaje? Yamkini kuna kitu hapa, either ka ukweli fulani au malipuano.
http://issamichuzi.blogspot.com/2010/01/jerry-muro-akiwa-kituo-cha-kati-cha.html.
Ninahisi kuwa Jerry anaweza pia kuwa intelligence agency na polisi hawafahamu. Maana yuko equipped kuliko nilivyomdhania.........Let give it time, we will soon learn something from here.
 
Tatizo la Watanzania ni kwamba hatuna standard moja inapokuja kwenye uhalifu. Tunatetea/kupinga kulingana na mhusika ni nani.

Kama Muro amechukua rushwa inabidi ashughulikiwe sawa na raia mwingine yeyote bila kujali yeye huko nyuma kafanya nini.

Masaula ya kwamba kwanini polisi na si TAKUKURU naona ni kutafuta mchawi bure.

Muhimu ni kusubiri ukweli wote ujulikane.

Kilicho wazi ni kwamba kwa tanzania waandishi wa habari huwa wanachukua rushwa ili waandike habari nzuri au wamtetea mhusika.
 
Jamani wadau hakuna mwenye updates na suala hili jamani mpaka sasa??? Kova si alisema anafanya press conference on this issue hajafanya bado kwa wale ambao wako karibu zaidi na vyanzo vya habari????
 
Jerry pingu unasema ni zako???? mwandishi wa habari au kuna kingine tusichokijua babangu?
 
Source: Daily News 01 Feb 2010:

Mr Kova said Muro posed as an official with the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) and attempted to extort the money from Mr Wage.

Police told reporters at Central Police Station in Dar es Salaam that Muro was brandishing a pair of handcuffs when threatening to arrest Mr Wage in Bagamoyo.

The former district accountant reported the matter to police leading to Muro's arrest. Police found the pair of handcuffs and a pistol in his car during a search.

At least now, I can now understand the police on this saga!
 
Back
Top Bottom