Tazama ushahidi huu wa kimahesabu wa Michango ya Lissu Unaothibitisha CHADEMA haifikishi wanachama hata million Moja

We jamaa unahangaika na Chadema sana. Chama chenu mfu

We endelea kung'ang'ana na million10 ukifikiri wanachadema wamekwama! Tambua Kuna ambao hawahitaji kujitangaza! Na kwa taarifa yako wapo wanachadema wenye ukwasi walioupata kihalali na sio Kwa ufisadi kama wa ccm! Na ambao sio ajabu Kwa muda huu unaobwabwaja humu wewe Luka mshamba,gari imeshatolewa order kiwandani tena bullet proof! Na tunatambua ninyi ni wachawi,ikitua tu bandarini tunawekea uchawi proof!
CHADEMA mnaandikaga utafikiri mmepofuka akili.
 
Unafikiri ni Kwanini hao wanachama hawajaguswa na hawaoni sababu ya kuchanga?
Fine, sababu zinaweza kua ni nyingi.

Mfano, Tundu Lisu anaweza kua na maisha mazuri kuliko hao wanachama wanaotakiwa wamchangie. Hivyo wengine wanaweza kudhani sio sawa kumchangia mtu aliekuzidi kimaisha ili anunue kitu kama gari kwa mfano.

Lakini yote ya yote michango ile sio kigezo cha idadi ya wafuasi au wanachama wa Chadema, hakuna uhusiano wa moja kwa moja. Unless labda utumie upeo mfupi kuulazimisha huo uhusiano.
 
Ndugu zangu watanzania,

Ukisikia watu wanafiki,waongo,ndumila kuwili na walaghai basi ni wafuasi wa CHADEMA. Hadharani watakujaza upepo,kukuvimbisha kichwa,kukupa kiburi halafu kumbe nyuma ya pazia wana kucheka tu na kukuona kama sinema tu.

Wafuasi wa Lissu kinafiki na kilaghai walishamuaminisha na kumvimbisha kichwa Lissu kuwa wana mpenda na yeye akakubali kuwa anakubalika sana na anaweza hata kuwa Rais Wa nchi hii wakati hata wafuasi wake tu wanaona kamwe na katu hawezi kuwa Rais wala kiongozi wa ngazi ya juu.

Sasa tangia ameanza kuomba michango ya kununua gari la kifahari kwa ajili ya mizunguko yake imeshangaza na kusikitisha kuona mpaka sasa karibia wiki Ni watu 1673 tuuuuu ndio wameweza kumchangia Lissu hela. Hii ni aibu ,fedheha na jambo la kusikitisha sana tena sana.

Hii inaonyesha wazi na dhahiri Lissu hakubaliki kabisa ndani ya CHADEMA na wengi pengine hawakubaliani kabisa na aina ya siasa zake ,hasa lugha zake mbaya na chafu za kibaguzi na chuki kwa wale ambao hakubaliani nao . kama ambavyo amemshambulia Mheshimiwa Rais kwa lugha za kibaguzi na chuki.

Watanzania na wanachadema wametuma ujumbe bila kujali itikadi zao za kisiasa kuwa hawamuungi mkono lisssu na aina ya siasa zake za chuki na kibaguzi. Jiulize tu ndugu yangu Lissu ana wafuasi wangapi kwenye mitandao yake ya kijamii? Kwanini wamegoma kumchangia? Imekuwaje kati ya mamilioni ya watanzania ndani na nje ya nchi imeshindikana hata watu elfu tano tu yaani 5000 kupatikana kumchangia?

Maana mtu anayekupenda ,kukuunga mkono katika harakati zako na kazi yako ni lazima awe wa kwanza kujitoa na kukuchangia kwa hali na mali. Mfano mimi hapa nilipo ikitokea Rais Samia akasema anahitaji mchango basi ni lazima nitakwenda kuuza hata mahindi yangu ili tu nipate pesa ya kumchangia. Nitafanya hivyo kwa kuwa ninampenda na ninamuunga sana mkono kwa uchapa kazi wake,na utumishi wake unaogusa maisha yetu, mfano kwetu sisi wakulima ambapo tumefaidika na uongozi wake.

Sasa Lissu ndio afahamu ya kuwa hata uchaguzi wa 2020 hakuibiwa kura kama alivyokuwa akidai ,bali ni kuwa watanzania hawampendi na hawamkubali na kumuunga mkono kwa yeye kuwa Rais .kwa kuwa wanaona hatoshi hata chembe kushika nafasi hiyo.anaweza kuwa anafaa kwenye kazi nyingine lakini siyo kazi ya Urais maana hana sifa za Urais zinazohitaji mtu makini,mzalendo,mchapa kazi,mwenye maono,mtulivu,mwenye subira,msikivu,anayejuwa wakati gani aongee na wakati gani akae kimya,wakati gani afanye maamuzi na wakati gani avute subira,nini aongee awapo hadharani na kipi akae kimya.Urais unahitaji mtu mwenye hekima, busara,upendo kwa watu wote.

Urais unahitaji mtu mwenye chujio la maneno,mtu mwenye muunganiko mzuri wa akili na mdomo wake,mwenye kufikiri kabla ya kuzungumza na siyo kuzungumza ndio ufikiri,mtumweye uwezo wa kuwaunganisha watu wote bila kujali dini zao,makabila yao,kanda zao na hata jinsia zao. Urais unahitaji mtu mwenye kifua cha chuma japo ana moyo wa nyama na damu.

Urais hauhitaji mtu mropokaji, mkurupukaji,mwenye mihemuko,jazba,hasira,mwenye kuongea neno lolote lile linalomjia mdomoni pake au mtu mwenye kujiona ana akili kuliko watu wote,mtu asiye shaurika wala kukubali ushauri wa watu wengine. Urais hauhitaji mtu wakuwagawa watu kwa kusema hawa ni Maccm au Mapoliccm. Huyo hatufai hata kidogo.

Lissu amepelekewa ujumbe mzito sana na mchungu sana ambao utampa somo zitoo sana kama atahitaji kujifunza. Ni lazima sasa ajifunze na kubadilika.asijione ana akili sana kupita watu wote .

Lissu anazidiwa ushawishi na nguvu ya kukubalika hata na msemaji wa club ya Simba Ahmed Ally achilia mbali Ally Kamwe wa Yanga, ambaye huhamasisha mashabiki wake kuujaza uwanja wa Benjamini mkapa unaobeba mashabiki elfu sitini kwa viingilio vya kuanzia Elfu tano kwa viti vya mzunguko mpaka laki mbili kwa VIP A?

Ole wake apitishwe na CHADEMA kugombea Urais uchaguzi ujao kushindana na mama yetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hasssan ataona aibu atakayovuna katika sanduku la kura. Lissu Akipata kura hata laki moja Basi akachinje kuku ale.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Tulia weye, riwaya ndefuu pumba.
CHADEMA naona mmeamua kumpelekea ujumbe mzito na mchungu sana Lissu .ambapo mpaka sasa haamini kwa kile kinachoendelea.maana alijiona ni mkubwa sana.matokeo yake imeonyesha Lissu ni mdogo kiushawishi kuliko hata msemaji wa Simba Ahmed Ally. Au Ally Kamwe wa Yanga.
 
Ndugu zangu watanzania,

Ukisikia watu wanafiki,waongo,ndumila kuwili na walaghai basi ni wafuasi wa CHADEMA. Hadharani watakujaza upepo,kukuvimbisha kichwa,kukupa kiburi halafu kumbe nyuma ya pazia wana kucheka tu na kukuona kama sinema tu.

Wafuasi wa Lissu kinafiki na kilaghai walishamuaminisha na kumvimbisha kichwa Lissu kuwa wana mpenda na yeye akakubali kuwa anakubalika sana na anaweza hata kuwa Rais Wa nchi hii wakati hata wafuasi wake tu wanaona kamwe na katu hawezi kuwa Rais wala kiongozi wa ngazi ya juu.

Sasa tangia ameanza kuomba michango ya kununua gari la kifahari kwa ajili ya mizunguko yake imeshangaza na kusikitisha kuona mpaka sasa karibia wiki Ni watu 1673 tuuuuu ndio wameweza kumchangia Lissu hela. Hii ni aibu ,fedheha na jambo la kusikitisha sana tena sana.

Hii inaonyesha wazi na dhahiri Lissu hakubaliki kabisa ndani ya CHADEMA na wengi pengine hawakubaliani kabisa na aina ya siasa zake ,hasa lugha zake mbaya na chafu za kibaguzi na chuki kwa wale ambao hakubaliani nao . kama ambavyo amemshambulia Mheshimiwa Rais kwa lugha za kibaguzi na chuki.

Watanzania na wanachadema wametuma ujumbe bila kujali itikadi zao za kisiasa kuwa hawamuungi mkono lisssu na aina ya siasa zake za chuki na kibaguzi. Jiulize tu ndugu yangu Lissu ana wafuasi wangapi kwenye mitandao yake ya kijamii? Kwanini wamegoma kumchangia? Imekuwaje kati ya mamilioni ya watanzania ndani na nje ya nchi imeshindikana hata watu elfu tano tu yaani 5000 kupatikana kumchangia?

Maana mtu anayekupenda ,kukuunga mkono katika harakati zako na kazi yako ni lazima awe wa kwanza kujitoa na kukuchangia kwa hali na mali. Mfano mimi hapa nilipo ikitokea Rais Samia akasema anahitaji mchango basi ni lazima nitakwenda kuuza hata mahindi yangu ili tu nipate pesa ya kumchangia. Nitafanya hivyo kwa kuwa ninampenda na ninamuunga sana mkono kwa uchapa kazi wake,na utumishi wake unaogusa maisha yetu, mfano kwetu sisi wakulima ambapo tumefaidika na uongozi wake.

Sasa Lissu ndio afahamu ya kuwa hata uchaguzi wa 2020 hakuibiwa kura kama alivyokuwa akidai ,bali ni kuwa watanzania hawampendi na hawamkubali na kumuunga mkono kwa yeye kuwa Rais .kwa kuwa wanaona hatoshi hata chembe kushika nafasi hiyo.anaweza kuwa anafaa kwenye kazi nyingine lakini siyo kazi ya Urais maana hana sifa za Urais zinazohitaji mtu makini,mzalendo,mchapa kazi,mwenye maono,mtulivu,mwenye subira,msikivu,anayejuwa wakati gani aongee na wakati gani akae kimya,wakati gani afanye maamuzi na wakati gani avute subira,nini aongee awapo hadharani na kipi akae kimya.Urais unahitaji mtu mwenye hekima, busara,upendo kwa watu wote.

Urais unahitaji mtu mwenye chujio la maneno,mtu mwenye muunganiko mzuri wa akili na mdomo wake,mwenye kufikiri kabla ya kuzungumza na siyo kuzungumza ndio ufikiri,mtumweye uwezo wa kuwaunganisha watu wote bila kujali dini zao,makabila yao,kanda zao na hata jinsia zao. Urais unahitaji mtu mwenye kifua cha chuma japo ana moyo wa nyama na damu.

Urais hauhitaji mtu mropokaji, mkurupukaji,mwenye mihemuko,jazba,hasira,mwenye kuongea neno lolote lile linalomjia mdomoni pake au mtu mwenye kujiona ana akili kuliko watu wote,mtu asiye shaurika wala kukubali ushauri wa watu wengine. Urais hauhitaji mtu wakuwagawa watu kwa kusema hawa ni Maccm au Mapoliccm. Huyo hatufai hata kidogo.

Lissu amepelekewa ujumbe mzito sana na mchungu sana ambao utampa somo zitoo sana kama atahitaji kujifunza. Ni lazima sasa ajifunze na kubadilika.asijione ana akili sana kupita watu wote .

Lissu anazidiwa ushawishi na nguvu ya kukubalika hata na msemaji wa club ya Simba Ahmed Ally achilia mbali Ally Kamwe wa Yanga, ambaye huhamasisha mashabiki wake kuujaza uwanja wa Benjamini mkapa unaobeba mashabiki elfu sitini kwa viingilio vya kuanzia Elfu tano kwa viti vya mzunguko mpaka laki mbili kwa VIP A?

Ole wake apitishwe na CHADEMA kugombea Urais uchaguzi ujao kushindana na mama yetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hasssan ataona aibu atakayovuna katika sanduku la kura. Lissu Akipata kura hata laki moja Basi akachinje kuku ale.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Bichwa kubwa akili kamasi
Wee umeambiwa wapiga kula wanaishi twita. Je niwananchi wangapi walio jiunga na huo mtandao x nimtandao wa wana alakati na wana siasa


Sisi wananchi kula yetu nikwenye Box na anayebisha asubili 2025 muone tofauti ya nguvu ya uma na dola
 
Bichwa kubwa akili kamasi
Wee umeambiwa wapiga kula wanaishi twita. Je niwananchi wangapi walio jiunga na huo mtandao x nimtandao wa wana alakati na wana siasa


Sisi wananchi kula yetu nikwenye Box na anayebisha asubili 2025 muone tofauti ya nguvu ya uma na dola
Kwani michango inachangwa twitter au kupitia simu na benki? Kwani michango inahusu watu wa twitter pekee yake? Mbona unaonyesha udogo wa akili kiasi hicho?
 
Kama kuna members wanakufuatilia hapa JF na wamekuwa wakikuona kama wewe ni Kichwa Chao!,Aisee nawaonea huruma!
Hoja hujibiwa kwa hoja na siyo viroja. Wafuasi wa Lissu mpo wapi? Mbona mmegoma na kumkataa kiasi hicho kumuunga mkono?
 
1673 ni wiki, Je ikifika mwezi itakuwaje?

Unawajua na wasiopenda kuonekana hadharani wako wangapi na wamechanga ngapi?

Lakini kama Mtu ananitaka mchango na siko katika Hali nzuri kiuchumi na sijamchangia so far, ndio simpendi?
Hadharani wapi? Kwani pesa hizo zinawekwa kwenye kapu lililo wekwa uwanjani au unachanga kwa siri kupitia simu au benki? Mbona unashindwa kuwaza vizuri na kujenga hoja Kiutu uzima?
 
Back
Top Bottom