Lissu aombe radhi, asijitoe akili

Makupa

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
5,101
2,611
CHADEMA WAMKALIA KOONI LISSU NI MNAFIKI AOMBE RADHI - ASIJITOE AKILI

Kamati kuu CHADEMA imemuhoji Makamu Mwenyekiti na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Tundu Lissu kwa kuudanganya Umma kuwa haku kukubaliana na uamuzi wa kumwalika Rais Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika tarehe 8 Machi mwaka 2023.

Wakati Mwaliko huo kutoka CHADEMA kwenda kwa Mheshimiwa Rais ulijadiliwa na Kamati Kuu ya CHADEMA na Lissu akiwa mjumbe alibariki ujio wa Samia kamati kuu.

Lissu ameulizwa na wana kamati Tarehe 6 Machi, 2023 wakati akihutubia kwenye mtandao wa Clubhouse alipongeza na kusifia kitendo cha BAWACHA kumualika Rais Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho yao ya Siku ya Wanawake Dunian.

Katika mahojiano hayo Tundu Lissu alienda mbali kupongeza kitendo cha Rais Samia kukubali mualiko kwa kusema, “Sikumbuki ni lini mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, ambae siku zote ni rais wa nchi, amewahi kushiriki katika shughuli rasmi ilioandaliwa na chama cha upinzani. Hasa chama kikuu cha upinzani. Wanakamati wanauliza je alikuwa amelewa..?

Tumewasilisha hapa Mawasiliano mbalimbali ya CHADEMA ambayo yamewekwa wazi yanaonyesha kuwa wajumbe pekee wa Kamati Kuu waliopinga rais kupewa mwaliko huo walikuwa John Heche na Godbless Lema.

Tundu Lissu alikuwa katika kundi la wanaokubaliana, ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe. Hivyo wajumbe wameshangaa leo hii Tundu Lissu akitoka hadharani na kudai ya kwamba hakuafiki uamuzi huo. (Ni Mnafiki)

Wajumbe wamehoji Rais Samia Suluhu Hassan alifanya ziara ya kikazi ambayo ilimpeleka hadi Brussels, Ubelgiji, ambapo wakati huo Tundu Lissu alikuwa akipatiwa matibabu zaidi na alifanya kikao na Tundu Lissu kwa ajili ya mazungumzo.

Kikao hicho kilikuwa cha faragha, lakini baada ya mazungumzo yao, Tundu Lissu aliingia kwenye mtandao wa kijamii Twitter na kuelezea mambo sita waliyozungumza na Rais Samia.

Kati ya hayo sita, viwili vilikuwa pamoja na Rais kuhakikisha kwamba Tundu Lissu anapata stahiki zake, kitu ambacho baadaye Tundu Lissu mwenyewe alikiri kilitendeka, pamoja na Rais kuhakikisha usalama wake pale atakaporejea nchini, jambo ambalo sote tumeona likitokea.

Wajumbe wamerejea historia Lengo ni kuweka rekodi sawa na kudhihirisha kwamba Rais Samia Suluhu Hassan hajawahi kuwa na migogoro binafsi na Tundu Lissu.

Tundu Lissu naye hakuwa na matatizo na Rais wakati ambapo rais alikuwa akijibu maombi yake mbalimbali. Hivyo, si ajabu kuona kwamba hadi mwaka jana, wakati CHADEMA ilipokuwa ikijadili kumwalika Rais, hawakuwa na shida yoyote kati yao.

Kilichotokea katikati ambapo Tundu Lissu alianza kumshambulia rais kibinafsi, Jambo ambalo limesemwa jana kuwa alinyimwa gari aina ya Nissan Y62 aliloliomba. (Chuki binafsi)

Tukirejea sasa swala la Tundu Lissu kudanganya umma na kudai kuwa hakuafiki Rais Samia Suluhu Hassan kualikwa kwenye sherehe zile, kwenye uongozi wa taasisi yoyote iwe ya serikali, chama au kampuni binafsi kuna kitu kinaitwa collective responsibility.

Maana ya collective responsibility ni kuwajibika kwa pamoja kwa maana ya kwamba jambo likisha jadiliwa na kukubaliwa kwenye vikao basi wote mnatoka na kauli moja inakuwaje Lissu atoke hadharani aseme hakubaliani walihoji baadhi ya wajumbe.

Uwajibikaji huu wa pamoja ndio sababu ambayo John Heche na Godbless Lema, ambao walikuwa wanapinga rais kualikwa, hawajawahi kutoka hadharani na kukosoa uamuzi huo.

Sasa pale ambapo Tundu Lissu, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa chama, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya chama, na mtu mwenye ndoto za kuwa rais wa nchi hii, haielewi maana ya uwajibikaji wa pamoja, inatia wasiwasi ni aina gani ya rais angekuwa kama angepata ushindi katika uchaguzi wa 2020.

Na utovu huu wa kinidhamu na kuto kuheshimu taasisi ambayo yeye ni kiongozi muandamizi sio tu kwenye swala la mualiko wa rais.

Wanakamati kwa kauli moja wamemtaka Lissu kuandika barua ndani ya masaa 72 ya kuomba radhi.
 
CHADEMA WAMKALIA KOONI LISSU NI MNAFIKI AOMBE RADHI - ASIJITOE AKILI

Kamati kuu CHADEMA imemuhoji Makamu Mwenyekiti na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Tundu Lissu kwa kuudanganya Umma kuwa haku kukubaliana na uamuzi wa kumwalika Rais Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika tarehe 8 Machi mwaka 2023.

Wakati Mwaliko huo kutoka CHADEMA kwenda kwa Mheshimiwa Rais ulijadiliwa na Kamati Kuu ya CHADEMA na Lissu akiwa mjumbe alibariki ujio wa Samia kamati kuu.

Lissu ameulizwa na wana kamati Tarehe 6 Machi, 2023 wakati akihutubia kwenye mtandao wa Clubhouse alipongeza na kusifia kitendo cha BAWACHA kumualika Rais Samia Suluhu Hassan kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho yao ya Siku ya Wanawake Dunian.

Katika mahojiano hayo Tundu Lissu alienda mbali kupongeza kitendo cha Rais Samia kukubali mualiko kwa kusema, “Sikumbuki ni lini mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, ambae siku zote ni rais wa nchi, amewahi kushiriki katika shughuli rasmi ilioandaliwa na chama cha upinzani. Hasa chama kikuu cha upinzani. Wanakamati wanauliza je alikuwa amelewa..?

Tumewasilisha hapa Mawasiliano mbalimbali ya CHADEMA ambayo yamewekwa wazi yanaonyesha kuwa wajumbe pekee wa Kamati Kuu waliopinga rais kupewa mwaliko huo walikuwa John Heche na Godbless Lema.

Tundu Lissu alikuwa katika kundi la wanaokubaliana, ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe. Hivyo wajumbe wameshangaa leo hii Tundu Lissu akitoka hadharani na kudai ya kwamba hakuafiki uamuzi huo. (Ni Mnafiki)

Wajumbe wamehoji Rais Samia Suluhu Hassan alifanya ziara ya kikazi ambayo ilimpeleka hadi Brussels, Ubelgiji, ambapo wakati huo Tundu Lissu alikuwa akipatiwa matibabu zaidi na alifanya kikao na Tundu Lissu kwa ajili ya mazungumzo.

Kikao hicho kilikuwa cha faragha, lakini baada ya mazungumzo yao, Tundu Lissu aliingia kwenye mtandao wa kijamii Twitter na kuelezea mambo sita waliyozungumza na Rais Samia.

Kati ya hayo sita, viwili vilikuwa pamoja na Rais kuhakikisha kwamba Tundu Lissu anapata stahiki zake, kitu ambacho baadaye Tundu Lissu mwenyewe alikiri kilitendeka, pamoja na Rais kuhakikisha usalama wake pale atakaporejea nchini, jambo ambalo sote tumeona likitokea.

Wajumbe wamerejea historia Lengo ni kuweka rekodi sawa na kudhihirisha kwamba Rais Samia Suluhu Hassan hajawahi kuwa na migogoro binafsi na Tundu Lissu.

Tundu Lissu naye hakuwa na matatizo na Rais wakati ambapo rais alikuwa akijibu maombi yake mbalimbali. Hivyo, si ajabu kuona kwamba hadi mwaka jana, wakati CHADEMA ilipokuwa ikijadili kumwalika Rais, hawakuwa na shida yoyote kati yao.

Kilichotokea katikati ambapo Tundu Lissu alianza kumshambulia rais kibinafsi, Jambo ambalo limesemwa jana kuwa alinyimwa gari aina ya Nissan Y62 aliloliomba. (Chuki binafsi)

Tukirejea sasa swala la Tundu Lissu kudanganya umma na kudai kuwa hakuafiki Rais Samia Suluhu Hassan kualikwa kwenye sherehe zile, kwenye uongozi wa taasisi yoyote iwe ya serikali, chama au kampuni binafsi kuna kitu kinaitwa collective responsibility.

Maana ya collective responsibility ni kuwajibika kwa pamoja kwa maana ya kwamba jambo likisha jadiliwa na kukubaliwa kwenye vikao basi wote mnatoka na kauli moja inakuwaje Lissu atoke hadharani aseme hakubaliani walihoji baadhi ya wajumbe.

Uwajibikaji huu wa pamoja ndio sababu ambayo John Heche na Godbless Lema, ambao walikuwa wanapinga rais kualikwa, hawajawahi kutoka hadharani na kukosoa uamuzi huo.

Sasa pale ambapo Tundu Lissu, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa chama, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya chama, na mtu mwenye ndoto za kuwa rais wa nchi hii, haielewi maana ya uwajibikaji wa pamoja, inatia wasiwasi ni aina gani ya rais angekuwa kama angepata ushindi katika uchaguzi wa 2020.

Na utovu huu wa kinidhamu na kuto kuheshimu taasisi ambayo yeye ni kiongozi muandamizi sio tu kwenye swala la mualiko wa rais.

Wanakamati kwa kauli moja wamemtaka Lissu kuandika barua ndani ya masaa 72 ya kuomba radhi.
tena alisifia sana kuwa CHADEMA imepata coverage kwenye media kwa rais kuhudhuria.
huyu wakati mwingine ni mwehu.
 
Lissu is not worthy credible afadhali Mtikila alifahamika alichokisimamia hadi mauti yanamkuta.
 
Back
Top Bottom