Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

ES,

Samahani, sijawahi kufanya kazi serikalini hapo bongo. Hapo foreign cheo ni kimoja tu?!? unawezaje kufanya kazi miaka 22 bila kupanda cheo? wakati elimu unaongeza na definetely working experience ipo ya kutosha?

EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
Ministry of Foreign Affairs & International Relations Foreign Affairs Officer 1984 2005

Jamani tutafika kweli namna hii?

FD
 
Mzee Es , Mzee wangu wa kunyumba karibu hapa Songea kama nilivyosema siku za nyuma kuna wakati unakata issue na natamani kukupa mke maana hapa Songea kwa chingwaji ndiyo maisha na si pesa ila pia unapo chemsha ama kuchukua pande mmoja basi lazima tuteme cheche na kwa kukutaja maana unakuwa unajibiwa bro usiogope kutajwa mzee wa Kunyumba ndiyo mambo ya wengi .

Naanza tena kwa kukutaja kwamba Mzee Es Mzee wa kunyumba kwako haki itatendeka pale Charles akapo shinda kesi hiyo ama hata akishindwa ? Maana naona unaenda na uchungu mkubwa ihali ukiwa na ushahidi kwamba kuiba kwa CCM kura ama kutoa rushwa kwa ajili ya yeye Charles kuupata Ubunge basi anashitakiwa kwa rushwa . Shemeji yake kusimama kidete labda yeye anaujua ukweli kwmaba Charles mshikaji wako si mtu wa haki kama umjuavyo ama alikuwa anaweka low profile ili afike huko na akaanza na rushwa huko akiwa anaanza kuonyesha makucha kama ilivyo kwa Rais wetu Dr. Nabii Jakaya Kikwete .

Haya maswala ya kusema ni innocent sis tunayakataa hadi mahakama iamue na pia Mahakama yenyewe itakosa kutenda haki since wewe unaonekena una misimamo kama Mzee JM ambaye alisema Mkuu wa Wilaya akipoteza jimbo kwa Wapinzani basi ajiondoe mwenyewe kazini kama vile Tanzania ni yake Malecela am CCM pekee .
Una usongo na kwa vyeo vyako ndani ya CCM na Serikali na kama unavyo pinga na hamlali kwa kuona Mgombea binafsi anakuwepo mko ama uo tayari kuingia haki tokea kwa Jaji na aseme Charles kashinda since u naonekana kwenya maslahi yako uko tayari kuuacha Utanzania na haki unazo hubiri hapa kila mara.
Je tutafika kweli namna hii Mzee wa Kunyumba ?
 
Mzee umechanganya mambo mengi sana bro, kuanzia CCM, Charles, JM, mgombea binafsi, I mean please!

Nitazungumzia Charles ambaye ndiye the issue hapa, anatuhumiwa kuhusika na kupata ubunge kwa kutumia njia zilizovunja sheria ya nchi, so far ni mtumhumiwa, sasa tunapokuwa kwenye dual process ya kujaribu kisheria kujua kama kweli ana makosa au hana, haivunjwi sheria yoyote kwa mwananchi kama mimi kuchukua sides, na wewe na tafiti kuchukua side mliyoichukua, yaani kumhukumu kuwa tayari ana makosa hata kabla kesi haijaisha!

Ninarudia kuwa so far tumewasikia mashahidi wa upande mmoja tu, bado wa upande wa pili wa mtuhumiwa Charles, ni haki ynagu kuchukua side kama ilivyo ya kwako na wenzako ya kumhukumu Charles kabla ya kesi kuisha,

lakini bado ninaaamini kuwa hii kesi ni kama ile ya Dr. Mlingwa, ya kuonea samaki wadogo, wakati samaki wakubwa wanajulikana na wako huru kufanya as they wish!halafu kuna watu kama wewe na tafiti mmekazania tu kuwa huyu samaki mdogo ana makosa!
 
Huu ndio ukweli wenyewe. Rushwa imefanya viongozi wetu wasijue maana ya kuongoza nchi. Viongozi wamekuwa kama vibaraka tu. Ni kama alivyowahi kusema rais mmoja wa afrika ya kusini ya makaburu kuwa waafrika na viongozi wao ni vipunga tu, ukiwapa kitu kidogo wako tayari hata kuua ndugu zao. Viongozi wetu walithibitisha hilo bila kelele wala mkwaruzo wowote.
 
Kichuguu,
Hivi kwa nini Transparency International waliamua kuondoka Bongo?
 
Jamani hizi ripoti sasa imefikia wakati wanahitaji kutupa evidence, au ushahidi, no! Maana kabla hawajandika si wanakutana na ukweli wa maovu yaliyofanyika ndio maana wanatoa conclusion yao mwishoni kuwa Tanzania kuna Rushwa, sasa why not stop generalized things na badala yake wawe blunt, kuwa wamefanya hivi na hivi,

I mean ninaheshimu kuwa wanatupa information, lakini hizi info ni tooo general kuwakaba nazo viongozi wetu, hivi kweli nyinyi mlioko majuu hamuwezi kuwaomba hao watu wawe wana-break down nani amepewa nini na amepewa na nanni?
 
Mzee ES
Hizo info zipo. They know who took what. Ndio maana nimeuliza ni kwa nini TI wameondoka Tanzania? Huenda ikawa hawakupata ushirikiano wa serikali. Si unakumbuka ile ripoti ya Brian Cooksey kuhusu IPTL? Ilimlazimu aondoke nchini.
 
Mzee ES
Hizo info zipo. They know who took what. Ndio maana nimeuliza ni kwa nini TI wameondoka Tanzania? Huenda ikawa hawakupata ushirikiano wa serikali. Si unakumbuka ile ripoti ya Brian Cooksey kuhusu IPTL? Ilimlazimu aondoke nchini.

TI wameondoka nchini lini? Dr Cooksey naye mbona aliendelea kubaki licha ya sakata la IPTL akiendelea na utafiti wake TADREG?

Angalia na hii habari kutoka Mwananchi

Wanasiasa waongoza kwa rushwa

Na Mwandishi Wetu

WANASIASA wametajwa kuwa ni kundi la watu wanaoongoza kwa kujihusisha na rushwa duniani, ripoti ya Transparent International mwaka 2006 imeonyesha.

Ripoti hiyo (Global Corruption Barometer 2006), iliyotolewa mwishoni mwa wiki iliyopita, inaeleza kuwa, vyama vya siasa vinaongoza kwa kupata alama nne katika kipimo ambacho mwenye alama tano ndiye aliyebobea kwa rushwa.

Baada ya vyama vya siasa, Bunge linafuatia likiwa na lama 3.7 na kufuatiwa na wafanyabiashara/sekta binafsi waliopata alama 3.6.

Mtazamo wa wengi unaoonyeshwa katika ripoti hiyo unabainisha kuwa, wanasiasa wamebobea katika rushwa kubwa na pia wawakilishi katika vyombo vya kutunga sheria vya nchi mbalimbali, nao wamesahau majukumu yao na kukumbatia rushwa, hali inayofanya mdudu huyu kuwa hatari kabisa katika sekta za umma.

Ingawa Tanzania haikutajwa moja kwa moja na ripoti hiyo, lakini rushwa kwa wanasiasa, hasa nyakati za chaguzi, hugeuka kigezo muhimu cha kujihakikishia ushindi, eneo ambalo linatazamwa pia katika ripoti hii.

Nchini hapa, serikali iliwahi kupitisha sheria iliyohalalisha takrima katika kipindi cha uchaguzi, ambayo imetenguliwa na Mahakama Kuu baada ya wadau mbalimbali kuilalamikia na kutaka mahakama kuingilia kati baada ya kuichukulia kama rushwa.

Idd Simba, Mbunge wa zamani wa Ilala na mfanyabiashara maarufu, juzi alikaririwa na vyombo vya habari hapa nchini akisema kuwa rushwa inashindikana kutokomea kwa kuwa inawahusisha watu wenye madaraka makubwa serikalini.

Kauli hii ya Simba inaungana na ukweli unaobanishwa na ripoti hii ya Trasparency International, hasa kipengele hiki kinachowahusisha wanasiasa katika rushwa.

Kundi la wafanyabiashara katika ripoti hiyo ya TI linaelezwa kuwa linatumia rushwa kuziba mazingira ya kulipa kodi.

Polisi wamefuatia wakiwa na alama 3.5 na mahakama ikifuatia kwa kukamata nafasi ya tano ikiwa na pointi 3.5. taasisi hizi zinahusishwa na rushwa katika kazi zake za kusimamia sheria za nchi.

Taasisi za mwisho katika upokeaji rushwa ni taasisi za dini ambazo zimepewa alama 2.8 na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yalipata alama 2.9.

Maeneo ya huduma za jamii kama elimu na afya yamegusiwa na ripoti hiyo, huku ikielezwa kuwa maeneo haya yanaawathiri zaidi raia maskini ambao hupaswa kutoa rushwa ili wapate huduma ambazo ni haki yao kisheria.

Sababu ya raia hawa kutoa rushwa inatokana na kukithiri kwa urasimu katika vitengo vya huduma mbalimbali za jamii, urasimu unaojengwa ili kurahisisha rushwa kutolewa au kutokana na kuwepo kwa huduma duni.

Kufuatia kuongezeka kwa rushwa, hasa barani Afrika na ulimwenguni kote, maisha ya familia mbalimbali katika bara hili yanaonyesha kuathirika zaidi ukilinganisha na familia katika mabara mengine.

Ukitupilia mbali tatizo la rushwa, bado maisha ya Afrika yanakabiliwa na kukosekana kwa huduma muhimu kama maji, afya na elimu, vita visivyokatika na pia ukosefu wa chakula katika nchi mbalimbali.

Ripoti hii inaonyesha pia kuwa, wananchi wengi hawana imani na serikali zao juu ya namna ya kupambana na rushwa na uchunguzi uliofanyika katika nchi za Marekani na Uingereza unaonyesha kuwa, wananchi wanaziona serikali zao kama taasisi zinazochochea rushwa na sio kupambana nayo.

Akizungumza na Mwananchi, Mkurugenzi wa TI nchini, Willy Kitima, alisema utafiti huo ulifanyika kwa kutumia baadhi ya nchi kikanda, ambapo Afrika iliwasilishwa na Kenya, na baadhi ya watu walikuwa wanaulizwa ni makundi gani wanayodhani yanajihusisha na rushwa zaidi.

Mamlaka ya kupambana na rushwa nchini (Takuru) imekuwa ikilalamika mara kwa mara kushindwa kupambana na rushwa kutokana na kutokuwapo sheria zinazoilinda mamlaka hiyo na kuipatia nguvu.

Hata hivyo jana wakati wa sherehe za siku ya Maadili, Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, alisema sheria mpya ya rushwa itakayotoa mwanya zaidi kwa Takuru kufanya kazi zake vizuri zaidi, iko jikoni.

Eneo ambalo linalalamikiwa sana na mamlaka hiyo ni mikataba ya serikali na zabuni mbalimbali. Hili ni eneo linaloambatana na rushwa kubwa zinazoathiri taifa na kauli za serikali ya Tanzania mara nyingi zimekuwa zikikumbatia sheria za sasa ambazo zinataka mikataba mbalimbali inayotiwa saini na serikali kubakia siri kati ya viongozi wa serikali na wawekezaji.

Ripoti hii inaonyesha pia kuwa wengi wa wanaotoa rushwa hulenga katika kupata huduma za msingi ambazo ni haki yao kupata au kwa lengo la kupambana na urasimu wa serikali au ikiwa ni lengo la hofu ya sheria mbalimbali kandamizi dhidi yao.

Uzoefu unaonyesha pia kuwa, rushwa inawatafuna na kuwaumiza zaidi raia maskini hasa inapotokea kuwa baadhi ya kodi zinapunguzwa kwa walio na uwezo wa kuzilipa na kuziweka kwa wasio na uwezo wa kufanya hivyo.

Wakati huo huo, serikali jana ilizindua mkakati mpya wa kupambana na rushwa, mpango unaoipa taasisi ya Kuzuia Rushwa nchini (Takuru) mbinu mpya za kupambana na kutokomeza tatizo hilo nchini.

Mkakati huo ujulikanao kama Mpango wa Pili wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (Nascap II), ulizunduliwa na Makamu wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein wakati wa maadhimisho ya siku ya maadili, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Mkakati huo ni mahususi kwa ajili ya kuongeza uwezo wa kuratibu sekta binafasi, wizara na idara za serikali, serikali za mitaa na asasi zisizo za serikali katika mapambano dhidi ya rushwa.

Mpango huo wa miaka minne, unalenga kuongeza ushiriki wa asasi za kiraia, NGOs na sekta binafsi katika kupambana na rushwa ili kuongeza mafanikio katika mapambano dhidi ya rushwa.

Hata hivyo alisema jana kuwa pamoja na juhudi za serikali katika vita dhidi ya rushwa kuonyesha mafanikio, hasa kwa kupungua kwa kiasi kikibwa rushwa za wazi, bado kuna upungufu mkubwa wa wafanyakazi katika taasisi zote zinazojishughulisha na vita hiyo.

Alisema pia kuna udhaifu katika usimamizi wa utawala bora kutokana na sheria zilizopitwa na wakati na ushirikishwaji mdogo wa vyama vya hiari na mamlaka za serikali za mitaa.

Alisema sheria mpya ya rushwa inaandaliwa, ili kuhakikisha kuwa Takuru inapewa uwezo mkubwa ikiwemo kushughulikia vitendo vya rushwa nje ya mipaka ya Tanzania na kushirikiana na nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa zilizosaini Mkataba wa Kimataifa wa Kupambana na Rushwa mwaka 2003, Tanzania ikiwa mojawapo.

Marekebisho hayo yanayotarajiwa kupelekwa bungeni Aprili mwakani, yanaingiza kifungu kinachowalinda watoa taarifa za rushwa pamoja na mashahidi wa kujitolea, wanaojitokeza katika vita hiyo.
 
Mzee ES,

Sina uhakika kama TI wameondoka Tanzania, ila najua kuwa wana ofisi kila nchi duniani; ofisi yao hapa Tanzania ilikuwa pale Samora Avenue ikiongozwa na Bwana Wilbert Kiduwaa Kitima. Wasiwasi wangu ni kuhusu huyu mkurugenzi ambaye alitoka Business Care Services asijekuwa naye ameshawekwa mfukoni na system ya serikali ili awe anaficha uozo mwingine.

Hata hivyo, TI huwa wana barometer nyingi za kupima kiwango cha rushwa bila hata kutegemea hawa local coordinators. Kwa mfano, huwa wanafuatlia details zote za contracts kubwa kubwa za makampuni ya kimataifa (multinationals) zinazofanywa na serikali zote duniani kuangalia kama kuna rushwa imetumika; hawawezi kusema nani kala rushwa ila watasema kuwa rushwa imetumika katika contract hiyo.
 
"...ofisi yao hapa Tanzania ilikuwa pale Samora Avenue..."

Kwa ajili ya kumbukumbu tu, ofisi yao iko Seaview, Protea Courtyard Hotel.
 
"...ofisi yao hapa Tanzania ilikuwa pale Samora Avenue..."

Kwa ajili ya kumbukumbu tu, ofisi yao iko Seaview, Protea Courtyard Hotel.

Kumbe; basi sawa inaonyesha kuwa bado TI ipo Tanzania. Je wako active vya kutosha au wanaogopa 'superstructure.'
 
Kichuguu,
Waliondoka 2 months ago. Oktoba. Nimepata habari kutoka Bongo hawapo tena.
 
Duh...sasa hawa TI nao wanaondoka kimya kimya kwa nini...?? Kama hawakupata ushirikiano kutoka serikalini kwa nini wasitoe tamko kwa wananchi kuomba support maana kuwepo kwao ni muhimu kwa wananchi kwa ujumla.

Tunapowa na serikali yenye madaraka ya kumuondoa yoyote nchini hata kama anafanya kazi kwa manufaa ya umma naona kuna hatari kubwa madaraka hayo yakawa mis-used. Kusema hivyo sina maana kuwa TI wamefukuzwa na serikali ila nashindwa kupata jibu kwa nini wameondoka.

Kwa kuangalia Mission Statement yao (see below), organisation kama hii ni ya kukumbatiwa na wanyonge hasa Africa; maana huenda ndiye mkombozi aliyebaki...(hasa baada ya RA and Co kuonyesha nia yao ya kununua media zote bongo)

FYI

Transparency International, the global civil society organisation leading the fight against corruption, brings people together in a powerful worldwide coalition to end the devastating impact of corruption on men, women and children around the world. TI's mission is to create change towards a world free of corruption.

Transparency International challenges the inevitability of corruption, and offers hope to its victims. TI plays a lead role in improving the lives of millions around the world, by building momentum for the anti-corruption movement, raising awareness and diminishing apathy and tolerance of corruption, as well as devising and implementing practical actions to address it.

Transparency International is a global network including more than 90 locally established national chapters and chapters-in-formation. These bodies fight corruption in the national arena in a number of ways. They bring together relevant players from government, civil society, business and the media to promote transparency in elections, in public administration, in procurement and in business. TI's global network of chapters and contacts also use advocacy campaigns to lobby governments to implement anti-corruption reforms.

Politically non-partisan, TI does not undertake investigations of alleged corruption or expose individual cases, but at times will work in coalition with organisations that do.

TI has the skills, tools, experience, expertise and broad participation to fight corruption on the ground, as well as through global and regional initiatives.

Now in its second decade, Transparency International is maturing, intensifying and diversifying its fight against corruption.
 
Kama habari zilizoandikwa na gazeti la Mwananchi zina ukweli basi wala rushwa wakubwa wa Tanzania hawana budi kubugia bia kwa wingi na nyama choma za moto!! Imenukuliwa kuwa, Mkuu mpya wa PCB Bw. Edward Hosea amefanya kile ambacho mtu anayetaka kuondoa rushwa hapaswi kufanya!! Amewapa wala rushwa muda wa kusubiri kukamatwa!!!

soma habari hapa: http://www.mwananchi.co.tz/mwananchisite/Mwananchi/Habari/Habari0.asp

Katika habari hiyo Mkuu huyo mpya ameamua kufanya mambo yafuatayo:

a. Wala Rushwa wafurahia X'mass na Mwaka Mpya hawatakamatwa ili wasije kupata Kiharusi

b. Amesema taasisi yake ina uwezo wa kuchunguza rushwa hivyo itafanya hivyo. Lakini uwezo wa kukamata vigogo haina. Kwa hiyo watanzania watarajie uchunguzi wa kila aina ya rushwa! Kufikishwa watu mahakamani ni ndoto kwa mujibu wa mkuu huyo!!

c. Ofisi yake haitakamata viongozi kama majaji kwani ita"paralayze system". Sasa majaji, mawaziri, Wakuu wa Polisi endeleeni kula! Tanzania pasipo nyinyi haiendi!!

d. Sijui kwa misingi gani, anasema kutaja anayechunguzwa ni uvunjwaji wa haki za binadamu!

Sikilizeni matangazo yangu ya kesho nina ujumbe kwa bosi wetu huyu!! Labda bado mgeni, ndo maana kamba bado iko mguuni!!
 
PCB ilianzishwa kwa ajili ya matakwa ya Mataifa ya nje. Aipo mioyoni mwa viongozi wetu wakuu wa Serikali.Itaishia kuwakamata walalahoi.
 
Serikali yenye nia ya dhati ya kumaliza rushwa haitaji PCB. PCB ni mzigo usio wa lazima kwa walipa kodi. Kipindi cha PCB rushwa ndo imezidi kuliko kabla ya hapo.
 
Nyerere aliimba rushwa ni adui wa haki, lakini wapi! Inabidi kuiongeza rushwa kwenye amri kumi za Mungu, yaani watoto kuanzia chekechekea na msingi wafundishwe rushwa nini na inakuwaje mtu anashawishika kutoa au kupokea rushwa hata kama alikuwa hataki (ripoti ya warioba wanaoisoma tayari wameshakuwa deformed). Itawaongezea kidogo nguvu ya kukataa kuwa deformed na adult society watakayoikuta
 
Back
Top Bottom