ndayilagije
JF-Expert Member
- Nov 7, 2016
- 7,491
- 8,305
Poa tu,kabla hujazungumza ni lazima ufikiri kwanza..kwanini ujifiche kama unajua unachosema?
Dawa hakuna mahospitali mnafunga internet nchi nzima! Seriously ??!!! what a big joke! Hebu fanyeni maendeleo kwa wananchi acheni kukimbizana na kutafuta ubaya na wananchi. North America Europe hawana hili ninyi ndio mtaweza? Acheni kutisha na kudanganya watu. Nchi zilizoendelea internet access zipo kwenye mall, migahawa, Hotel etc. eti tutafunga internet nchi nzima what a crap!
Ogopa sana hadi mmiliki wa internet cafe anaweza kwenda jela kwa matendo yaliyofanywa na mteja wake.Ni ngum kuamini kuwa Nina watu tena viongozi wenye mawazo ya ukija kazi hicho....katika karne hii.
Tutafika ila tutatubu mkuu...Je, TUTAFIKA?
Shida zimedumu nusu karne mkuu. Hawana dhamira ya dhati ya maendeleo.Haya bwana.
Huo muda na rasilimali zilizotumika kudraft huo upupu wangeutumia kutafakari namna ya kuondoa shida ya maji na huduma za afya nchini.
Kweli kabisa mkuu!~~~>>>>Ni jambo gumu sana kupingana na "Nyakati"... ... Kwakuwa tuna wabunge wengi wa CCM ambao ni Mazuzu hii sheria itapita
Lakini naamini hata wao, familia zao na ndugu haimaanishi kuwa wao wapo Salama sana.
Nani alifikiri kuwa Sumaye na Lowasa watakuwa wapinzani???
Endeleeni tu na "Ushamba
Huu ni uoni hafifu wa kiteknolojia ya kupashana habari.Wakati wanafikiria kubana watu kwa hili, wataachwa mbali sana na teknolojia ya kupashana habari.Ina maana hawajifunzi wala kuona mabadiliko ya ajabu ya teknolojia hii? Kila mara kuna updates nyingi tu za kupeana habari kwa speed ya ajabu. Huo utungungaji sheria kandamizi nao utakimbizana na mabadiliko hayo? Leo unatunga sheria kandamizi kesho unaamka imeachwa na teknolojia .Kila siku uvumbuzi mpya.ILANI: Hizi sio kanuni za Sheria ya Makosa ya Mtandao.
Kanuni hizi zinakuja mwezi mmoja baada ya kuambiwa kuna sheria nyingine inakuja pia > Tanzania: Authorities drafting another law targeting the Cyberspace
Zimewekwa hapa: http://habari.go.tz/uploads/documen...ne Content Regulations - 20 January, 2017.pdf
- Kanuni hizi naamini bado ni draft (kama sijakosea)
- Zitagusa karibu kila kitu kinachoandikwa mitandaoni
- Hizi si kanuni za Sheria ya Makosa ya Mtandaoni
![]()
- Vyombo vya Habari vyenye kuwa mtandaoni navyo havitapona!
- Forums kama JF nazo zimeguswa!
![]()
- Social Media Platforms (hadi Makundi ya WhatsApp/Facebook/Instagram/Twitter) nako hakuko salama [emoji1484]
![]()
- Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imepewa nguvu za kutosha kabisa! [emoji1484]
![]()
- Sect 5(1) inamtaka mwenye kumiliki mtandao kuhakikisha anakusanya taarifa za kutosha za wateja wake! (Inalengwa JF?).
- Sect 5(1) pia inamtaka mwenye kumiliki mtandao akiona kitu ambacho wao TCRA wamekwambia hakifai uwe umekiondoa ndani ya saa 12!
- Watanzania walio nje ya Tanzania (diaspora) nao wameguswa!
- Maneno FORUM yametumika mara nyingi kitu kinacholeta picha juu ya nani mlengwa haswa!
![]()
- Kanuni hizi zinakuja wakati JF ikiwa inakabiliwa na kesi 3 mahakama ya Kisutu na mojawapo ya kesi wanaoishtaki JF ni TCRA (kuwa na website yenye .com).
- Internet Cafe zitalazimika kuweka kamera za kunasa kila kinachoendelea ndani
![]()
- Serikali yetu sasa inataka watu kuandika habari za kufikirika!
![]()
Na mwisho, Serikali yetu tukufu kupitia kwa Waziri ambaye ni msomi wa sheria na "Mmoja wa Wapambanaji walio ndani ya CCM" imeweka adhabu kali kwa atakayekiuka taratibu hizi!!!
![]()
Je, TUTAFIKA?
[emoji848]