Tanzania sasa yapata kibali kipya cha kupakua na kupakia mizigo Nairobi. Kenya walitaka tufuate taratibu

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Baada ya maombi ya Tanzania kupata kibali kipya cha kuruhusu kupakia na kupakua mizigo kiitwacho Fifth Freedom Traffic Rights, ndege za ATCL sasa zimeruhusiwa kutua Nairobi.

Ndege za ATCL zikiwa njiani katika safari za kimataifa safari hii zitaruhusiwa kupakua na kupakia mizigo katika katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.

Mapema leo asubuhi mamlaka ya usafiri nchini Tanzania ilitoa tangazo la barua kusitisha kutua kwa ndege za KQ katika viwanja vya ndege vya Tanzania (JNIA na KIA) baada ya mamlaka ya usafiri wa anga ya Kenya kuzuia ndege za ATCL kutua mjini Nairobi na kupakua na kupakia mizigo bila kufuata taratibu au kuwa na kibali cha kufanya hivyo.

Mamlaka hiyo ya Tanzania iliondoa vibali vya Third Right Freedom na kile cha Fourth Right Freedom ambavyo vinaruhusu shirika la ndege kusafirisha abiria na mizigo kupitia Nairobi kuelekea nchi ingine.

Baada ya mazungumzo kati ya pande hizi mbili mamlaka za Kenya zimetoa kibali cha Fifth Freedom Traffic Rights ambacho sasa kitaruhusu ndege za Tanzania zikiwa safarini kwenda Third Party Countries kutua Nairobi ili kupakua, na kupakia mizigo bila shida.

Hatua hii itairuhusu ATCL kuendelea na shughuli zake za kuhudumia mizigo na kuongeza mapato yake katika biashara hiyo ambapo itakuwa ikitumia ndege yake mpya ya mizigo.

Nini maana ya hizi Freedoms?

Kwa mujibu ICAO ambayo ni taasisi ya kimataifa ya umoja wa mataifa inoshughulika na usafiri wowote wa anga za kimataifa, hizi freedom rights mbili za kwanza ni kwa ajili ya transit ambapo mwenye ndege hulipa gharama za kutumia anga la nchi mwenyeji.

Rights ambazo zahusukupanga abiria na kushughulikia mizigo ztwa Traffic Rights.

Hivyo ICAO wametoa hizi freedoms ambazo zipo tisa lakini mbili za kwanza yaani First Freedom ambayo yaruhusu ndege kupita katika anga la nchi ingine bila kutua kwa kutumia anga yake. Second Freedom yaruhusu ndege ya nchi moja kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa nchi ingine kwa matengenezo au kujaza mafuta lakini bila kushusha abiria.

Third Freedom ni ile onoruhusu ndege kutoka nchi moja kwenda nchi ingine ikiwa na abiria au mizigo. Mfano ATCL ikitokea tanzania kwenda Kenya. Fourth Fredom ni ile inoruhusu ndege ilokwenda nchi ingine kurudi katika nchi ilokotoka ikiwa na abiria au mizigo.

Na Fifth Freedom Right ni kibali kinotolewa na nchi moja kwenda kwa nchi ingine kinoruhusu ndege za nchi ilopewa kibali kutua katika nchi mwenyeji na kisha kuruka tena kwenda katika nchi ya tatu au third country.

Zipo freedom rights zingine nne ambazo ama zaziruhusu ndege kutua, na kuondoka katika viwanja zaidi ya kimoja nai ile iitwayo Cabotage ambayo kama fifth freedom right ndege yatua na kufanya shughuli za kupakua na kupakia abiria au mizigo.

Hii ya Fifth Freedom Right yachochea ushindani na kuwawezesha wateja na wasafiri kuwa na uhuru wa kuchagua.
 
sasa mbona hatuelewi tatizo ni hatukufuata taratibu au wao ndiyo hawakufuata makubaliano? Mamlaka itoe maelezo kwa Taifa ili tufahamu ni nani alikurupuka.

Kama barua kama ile inaweza kuandikwa na kuwekwa wazi namna ile halafu inakuja kugundulika kuwa Tanzania tulikurupuka, aliyesaini ile barua anatakiwa awajibishwe mara moja.
 
Hii Jumuiya haina muda unakufa tena
Tatizo ni uswahili.

Tusipende kufanya mambo yetu ya upigaji na kwa mazoea.

Kuna watu walitaka wawe wapitisha tu mizigo Nairobi wakidhani ni rahisi hivyo.

Kuna mambo mengi khasa usalama vyapewa kipaumbele.

Tufuate taratibu.
 
sasa mbona hatuelewi tatizo ni hatukufuata taratibu au wao ndiyo hawakufuata makubaliano? Mamlaka itoe maelezo kwa Taifa ili tufahamu ni nani alikurupuka. Kama barua kama ile inaweza kuandikwa na kuwekwa wazi namna ile halafu inakuja kugundulika kuwa Tanzania tulikurupuka, aliyesaini ile barua anatakiwa awajibishwe mara moja.
Kama tumepewa kibali kipya, hiyo yamaanisha kwamba hatukufuata taratibu.
 
Kwa nini hawakuwasiliana ndani kwa ndani kabla hawajatoka hadharani? Wanadiplomasia wana kazi gani? Ni aibu nchi zenye viongozi wenye akili kufanya mambo kama watoto.
Huwezi kudeal na muhuni kwa njia ya kistaarabu. Muhuni unadeal naye kihuni. Wakenya ni wahuni.
 
Kwa nini hawakuwasiliana ndani kwa ndani kabla hawajatoka hadharani? Wanadiplomasia wana kazi gani? Ni aibu nchi zenye viongozi wenye akili kufanya mambo kama watoto.
Walikurupuka.

Hata mtu fulani maarufu alitaka atumie mwanya huo kujijenga kisiasa.

Ila Johari na yule mkenya wamemzidi kete.
 
Huwezi kudeal na muhuni kwa njia ya kistaarabu. Muhuni unadeal naye kihuni. Wakenya ni wahuni.
Wakenya ni wapumbavu sana.
Wameitwa kwenye meza ya mazungumzo mara kibao lakini wakawa wanapiga chenga...hii ñdio namna ya ku-deal nao.
Akikufinya kidogo unampelekea ngumi...hapo mtaelewana.
 
Mradi "Reconciliation" imefanyika sasa ifatie "Resilience".

Tuchape kazi.

Yaani ufanye Reconciliation na nyang’au? How many times we did this kuwafungia na kuwatisha na still wanaendelea na uhuni? Au ni mara yako ya kwanza kusikia kuhusu KQ kufungiwa na kuwatishia ndio wanakubali kuwa wanafanya makosa? Nyang’au sio mtu wa kuaminika hata kidogo, hapo hakuna reconciliation, ni ubabe wetu umesaidia wakubali sbb wao wangepata hasara zaidi, nyang’au ni nyang’au tu, huwezi kumuamini au kufanya reconciliation nae kamwe, nyoka atabakia nyoka, ndivyo ilivyo kwa nyang’au ni kuwa nao makini sana.
 
Yaani ufanye Reconciliation na nyang’au? How many times we did this kuwafungia na kuwatisha na still wanaendelea na uhuni? Au ni mara yako ya kwanza kusikia kuhusu KQ kufungiwa na kuwatishia ndio wanakubali kuwa wanafanya makosa? Nyang’au sio mtu wa kuaminika hata kidogo, hapo hakuna reconciliation, ni ubabe wetu umesaidia wakubali sbb wao wangepata hasara zaidi, nyang’au ni nyang’au tu, huwezi kumuamini au kufanya reconciliation nae kamwe, nyoka atabakia nyoka, ndivyo ilivyo kwa nyang’au ni kuwa nao makini sana.

Kama kibali kimeombwa ni ubabe upi umetumika hapo?

Wao wazileta ndege na sie twapata watalii lukuki zaidi ya milioni moja kwa mwaka.

Kwahiyo sisi ni soko lao kubwa na sisi pia ni wateja wao.

Cha msingi ni kwamba ingawa sisi ndo tumeanza kunyanyuka kwenye biashara hii ya usafiri wa ndege bado twapaswa kuwa waangalifu pale tunapotafuta njia zaidi ya kujipanua ili nasi tupate mapato mazuri khasa ukanda huu wa Afrika.

Hakuna nyang'au wala ubabe, tutumie akili zetu.
 
Resilience and continuity very important.

Ila tusipende kukurupuka na kuhemka tutumie elimu zetu uzuri kutatua vikwazo vya hapa na pale.
Nashangaa sana kuona mtu haelewi kabisa inconvenience iliyotokana na barua ile! Actually there are unnecessary costs involved.
 
Back
Top Bottom