Tanzania: Ni yapi yaliyojiri 1995?


Mimi kuna kitu kimoja kina nitatiza kuhusu Mkapa. Mimi naamini Nyerere hakua mtu wa kukurupuka. Kama alimchagua Mkapa naamini kabisa Nyerere alidhani anafaa. Je Mkapa ni alikua anaficha makucha yake au kweli alikuwa "Clean" akaja kubadilika baadae?

Mwalimu alimfahamu Mkapa toka siku nyingi, toka Mkapa akiwa Mwanafunzi wa Pugu sekondari,Na Nyerere alikuwa Mwalimu wake na alimpenda pia. Wakati Nyerere akiwa Rais Mkapa amewahi ku-serve kama Waziri wa Mambo ya Nje, na unapokuwa Waziri wa mambo ya nje enzi ya mwalimu siyo kitu kidogo.

Nimewahi kuongea na Mzee Ibrahim Kaduma ambaye pia aliwahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Nyerere, kwa kweli anasema ilikuwa kazi kubwa kwa Muhusika, Mwalimu anaweza kumuita mtu wakati wowote na kutaka taarifa zozote, kwa hiyo ni kazi amabayo ilikuwa inataka muhusika awe na Taarifa nyingi, lakini inahitaji mtu amabye ni HARD WORKING, na Mkapa ni Hardworking, Tofauti na JK Ambaye kwake vitu vingi vinafanyika ki kawaida sana, JK ni mvivu wa kufikiri, kila kitu kwake ni rahisi sana, hata vitu vinavyohitaji umakini uvirahisisha.
 
Mwalimu alimfahamu Mkapa toka siku nyingi, toka Mkapa akiwa Mwanafunzi wa Pugu sekondari,Na Nyerere alikuwa Mwalimu wake na alimpenda pia. Wakati Nyerere akiwa Rais Mkapa amewahi ku-serve kama Waziri wa Mambo ya Nje, na unapokuwa Waziri wa mambo ya nje enzi ya mwalimu siyo kitu kidogo.

Nimewahi kuongea na Mzee Ibrahim Kaduma ambaye pia aliwahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Nyerere, kwa kweli anasema ilikuwa kazi kubwa kwa Muhusika, Mwalimu anaweza kumuita mtu wakati wowote na kutaka taarifa zozote, kwa hiyo ni kazi amabayo ilikuwa inataka muhusika awe na Taarifa nyingi, lakini inahitaji mtu amabye ni HARD WORKING, na Mkapa ni Hardworking, Tofauti na JK Ambaye kwake vitu vingi vinafanyika ki kawaida sana, JK ni mvivu wa kufikiri, kila kitu kwake ni rahisi sana, hata vitu vinavyohitaji umakini uvirahisisha.
So what went wrong with Mkapa mkuu?
 
Moja ya mambo yaliyomchafua Mkapa ni familia yake hasa mkewe na EOTF yake.

So ni the classic blame it on the wife mkuu? Maana Kitine nae walisema mke wake alimuingiza mkenge. Kibaki walisema mke wake alimforce ahakikishe haachii madaraka. Gbagbo nao Ivory Coast inasemekana alikua tayari kuachia ngazi mke akamuambia asi thubutu. Mwinyi nae walidai anaendeshwa na mkewe. Inaelekea hawa mamama wana influence kubwa sana.
 
my head is spinning...i've learned a lesson or two,.while we are busy winning our daily bread,things happen in country,..a bullet can fly at you in the pavement,bust your brains out..next month you are forgotten..that's a damn system..thanks for the info.
 
my head is spinning...i've learned a lesson or two,.while we are busy winning our daily bread,things happen in country,..a bullet can fly at you in the pavement,bust your brains out..next month you are forgotten..that's a damn system..thanks for the info.

Vitu kama hivyo si kwa Tanzania tu.....
 
So ni the classic blame it on the wife mkuu? Maana Kitine nae walisema mke wake alimuingiza mkenge. Kibaki walisema mke wake alimforce ahakikishe haachii madaraka. Gbagbo nao Ivory Coast inasemekana alikua tayari kuachia ngazi mke akamuambia asi thubutu. Mwinyi nae walidai anaendeshwa na mkewe. Inaelekea hawa mamama wana influence kubwa sana.
Tumenasa wengi kwa wake zetu. Nasikia hata yule mchezaji maarufu wa Argentina na ManCity, Tevez, ni mkewe hataki waishi England pamoja na malipo mazuri anayopata kwa wiki! Maraisi wengi ving'ang'anizi wa madaraka na utafutaji wa utajiri kwa nguvu kisa hasa ni wake zao. Mwalimu aliliona hili. Kuna kipindi Maria huyu alikaa kijijini kwao muda mrefu tu.
 
Yeah, inategemea wewe unautazama vipi Udini kwa sababu Malima alichoandika wala sio kusema ni kuonyesha imbalance ktk elimu na jinsi Waislaam na wanawake walivyokuwa hawapewi nafasi sawa na vijanwa kikristu kuendelea na masomo hata kama wanatoka shule moja.. Na kibaya zaidi yeye alikuwa waziri wa Elimu lakini sisi wote tulimpiga vita pamoja na kwamba alikuwa na report kamili yenye ushahidi wa kuonyesha kutokuwepo uuwiano huo...

Sasa nambie kwa nini hatukufanya hata uchunguzi kuitazama report yake badala yake alikuwa akihojiwa tu ili kuonyesha jionsi gani alivyokuwa mdini ktk kutetea report yake ambayo iliwahusu both waislaam na wanawake..Halafu utawasikia watu kama Boss wanasema nakuja na malalamiko hali It is a report for Christ sake na ndio tunaizungumzia na ndio ilikuwa kazi alopewa Malima kuifanya akiwa kama waziri wa elimu..

Sasa kasema hakuna uuwiano na utafiti anao tayari akapachikwa Udini ipi habari kamili ama malalamiko, besides no one could prove him wrong hadi leo hii tunazungumza hapa JF!

Mind that nafasi za elimu kwa nchi yeyote hazitakiwi kutolewa kwa uwiano bali kwa uwezo. Degeree hazigawiwi kama vitumbua au vyakula vya msaada. Ndiyo sababu walimpuuza. Shule zilikuwa za serikali na kusoma bure halafu anakuja na ripoti ya uchonganishi. No wonder alipigwa kikumbo mpaka akapata pressure iliyomuua.

Kama waziri wa elimu alitakiwa kuja na mkakati wa kuwahamasisha waislamu wasome siyo kugawiwa nafasi za kusoma hata kama hawakuwa na uwezo. Si unajuwa panga la chuo (DISCO...) lilivyokuwa linafagia wazamiaji??
 
Tumenasa wengi kwa wake zetu. Nasikia hata yule mchezaji maarufu wa Argentina na ManCity, Tevez, ni mkewe hataki waishi England pamoja na malipo mazuri anayopata kwa wiki! Maraisi wengi ving'ang'anizi wa madaraka na utafutaji wa utajiri kwa nguvu kisa hasa ni wake zao. Mwalimu aliliona hili. Kuna kipindi Maria huyu alikaa kijijini kwao muda mrefu tu.

Dah kweli Nyerere (R.I.P.) alikua no none sense. Labda muimbaji maarufu wa Kimarekani bibie Beyonce alivyo imba "Who run the world (girls)" alikua ana toa ujumbe mzito sana.
 
Ukweli ni kwamba JK kajiandaa tokea ni mdogo kuja kuwa raisi tokea mahusiano aliyo tengeneza UDSM, jeshini na kwenye chama. Tokea mwanzo alikua na nia ya uraisi na akajiwekea mazingira ya kuuchukua na ukweli ni kapata. Mimi naamini system nzima siyo inayo panga nani awe raisi bali hata system yenyewe ina vikundi mbali mbali. Kundi la JK lilijipanga vizuri na nilitambua kuwa kati ya JK ndiye electable kwa hiyo yeye atashinda na wengine kuchukua nafasi zilizo baki. Hata ukiangalia watu wenye cheo sasa ni watu wamefahamiana at a personal level na JK muda mrefu.
Kwa hili la Kikwete kujiandaa tangu utoto linasemekana kuwa ni kweli na hata ukiwauliza ndugu wa karibu na familia yake.

Tena ni juzi tu, bi mkubwa wangu alikuwa ananiambia kuwa tangu mimi niko tumboni(1983), mama yangu aliambiwa na dada yake Kikwete aliyekuwa rafiki na mfanyakazi mwenzake bohari kuu, kuwa walikuwa na vikao Bagamoyo,jinsi ya kuweka mikakati kumuandaa Kikwete kuwa rais.

Dada yake huyo alidai kuwa Jakaya alionekana na wazee wa Bagamoyo kuwa na 'nyota' ya uongozi mkubwa ktk Tanzania, hivyo wakajipa jukumu la kumlea kimaadili na kumsaidia kwa hali na mali. Inasemekana ktk ujana mdogo wake Jakaya alipata 'taabu' sana kwa kupigwa mikwaju na wazee kila alipoonekana kushiriki skendo za mitaani.

Hata hivyo, pamoja na simulizi hizo, ni lazima kutakuwa na kitu kingine katika ushiriki wake ktk CCM na serikali kilichomjengea nguvu na ushawishi alioupata.
 
this is a wonderful Thread.....the trend is moving so fast that i couldn't even put my thoughts here.....
by the way namsubiri MKJJ aingie hapa...laiti kama Game theory angekuwepo...hata kwa ID nyingine....
 
Mrema alikubalika Nchi nzima. Wizara ya Mambo ya Ndani ilikuwa imemjenga sana kwa jinsi alivyokuwa akishughulikia kero za Watanzania. Alifahamika na kukubalika zaidi kwa WATANZANIA kuliko wagombea wote wa CCM na vyama vingine. Wakati wa kampeni ndipo yakajitokeza makundi ya ajabu ya Kichagga yakichangishana fedha kwa wingi na kufanya mikutano yao wenyewe utadhani alitakiwa kuwa Rais wao peke yao.

Kukubalika kwa Mrema 1995 ni ushahidi tosha kuwa TZ hatuna viongozi makini hivyo wananchi wanafuta upepo tu ili kutafuta bahati yao imeangukia wapi!!
 
Kwa jinsi mambo yalivyo kwa hawa wazee sometimes tatizo la kutokuwa wabunifu na kutokuamini kuwa urais ni wito toka kwa Mungu,kama alivyo Sheikh,Mchungaji,Padri au kiongozi yoyote wa dini.Kitendo cha kuchukulia kiti cha urais kama just urais kwa ukweli ndio dhambi kubwa ambayo huwa inawaangukia viongozi wetu hawa.

Pata picha ya mtu aliyeingia ikulu kama MR CLEAN kisha anatoka kwenye kiti kama MR UNCREAN,au mwingine aliyeingia ndani ya kiti hicho kwa asilimia 80% na zaidi asilimia hizo nikiwemo mimi kihalali kisha uchaguzi unaofuata baada ya kupanda anashuka chini kwa asilimia 20% kweli ni kwa namna gani wanaiumiza jamii ambayo imekuwa ikiwaamini kwa asilimia kubwa sana na kuwapa madaraka ya kuwatawala ili kuwatoa kwenye rindi la umaskini uliokithiri kupitia maliasili zao.

Sikuona sababu ya BMW kushindwa kunyakua tuzo ya IBRAHIMU MOHAMAED business tycoon wa Misr,lakini Hakuna kitu kizuri kwenye maisha ya kiongozi wa ngazi ya Urais kuishi na kupumzika huku ukiwa umeacha alama [Mark] kwenye mioyo ya Watu na sio majengo na vitu vya kushikika [Material Tangible].

Kibaya sana unapokuwa Rais yakupasa kuwa ni mtu unaekerwa na matatizo ya watu,na si watu wanao kukera wewe.Daima unakuwa na moyo na dhamila ya kutafuta watu na kujenga watu ambao daima wataendeleza ndoto yako huku nao wakijitayarisha kujiimarisha na kukuza pia ndoto zao.Kwani timu yako ambayo utashirikiana nayo wanakuwa ni wale ambao kama wewe Rais unahakika kuwa ni watu wenye mawazo sawa na wewe pamoja na kuwa mnatoka katika jamii tofauti [Ndege wenye mbawa zinazofana usafiri ama huluka pamoja].Ndio maana BMW alipochukua madaraka akaenda kumwambia Mwalimu amsaidie kuteua Mawaziri Mwalimu akamwambia hilo ni baraza lako sio langu,hakika kwa mwelevu yoyote hilo lilikua ndio jibu kuwa ndege utakao wachagua wewe ndio jinsi ulivyo wewe, vinginevyo ulitudanganya muonekano wako.Wazungu wanasema nionyeshe marafiki zako nitakwambia ulivyo wewe.[Show me your friends and I will tell you who your]

Nyerere alikuwa anakeleka na matatizo na shida za watu haswa Watanzania na Waafrika kwa ujumla.Hata kama Mwalimu alionekana kama dikteta au Mr aambiliki, mimi kama kijana wa kizazi kipya niliyekuja kumjua Mwalimu kwa ufahamu wangu akiwa ameshatoka Madarakani na akiishi kama Rais mstaafu kwa karibu miaka kumi lakini kupitia vitabu,kopi za sauti [Speech] na hadithi simulizi,ameonekana kuwa daima mtetezi wa kweli wa watu wasio kuwa na msemaji.Na hata kama aliwatendea baadhi ya watu ndivyo sivyo alitenda hayo kwa nia ya kutulinda kwa kuwa moja ya sifa ya kiongozi bora ni yule ambae daima uwatetea wasiojiweza.Alitenda yale ambayo baba yoyote mwenye dhamana ya familia angelipaswa kutenda kuikinga familia yake dhidi ya wote wale wenye kusudio baya juu ya familia yake.

Yaliyowasibu Marais wengi kuyumba,baada ya Mwalimu kutoka Madarakani ni Tabia ya Viongozi wengi wa Taifa hili,kupenda kuzungukwa na watu wanaopenda kuwaambia NDIO MZEE.Na yoyote yule ambae anawapinga ama kuwashauri kwenda tofauti nao ni mkosefu wa adabu kwa viongozi na nia adui kwa Taifa.Hivyo kuzungukwa na watu ambao daima watataka kumwambia mambo mazuri tu hata kama kuna jambo baya ambalo lampasa kulipata au limfikie kwake kwa ubaya wake huo huo ili lipate majibu halisi litachakachuliwa mpaka analipata katika picha tofauti na inayohusika.

Kushindwa kuwa wabunifu binafsi nje ya mfumo,wa kupata taarifa halisi kuhusiana na maswali na matatizo ya Wananchi au jamii wanayoitawala katika muda husika.Kuna wakati nilipata kuona picha [movie] ya John Fitzgerald Kennedy Jr. (1917 – 1963) Rais wa Marekani wa 35 na alietumikia Taifa hilo toka mwaka 1961 mpaka 1963.Kupitia Picha hiyo nilipata kuona ni jinsi gani Rais huo alivyokuwa mbunifu binafsi kuokoa Taifa lake lisiingie kwenye vita kati yake na USSR iliyokuwa ikishirikiana kwa siri na Cuba mvutano huo maalufu kama Cuban Missile Crisis au October Crisis in Cuba au Carribean Crisis 1962. Kama vita hiyo isingekuwa uwezo binafsi wa Rais huyo ingesababisha vita ya tatu ya dunia kutokea.

Hakika ukiona Rais huyo anavyojituma kupata taarifa makini na sahihi yeye binafsi na hata pale vyombo ya ulinzi na usalama [Executive Committee of the National Security Council au ECOMM] vikimshurutisha kutoa tamko lasmi wao waingie vitani,lakii Rais huyo hakukubaliana nao mpaka alipoweza kutatua tatizo hilo kubwa la kidunia huku akishirikiana na ndugu yake wa damu Robert Kennedy na kiongozi wa USSR Nikita Khrushchev kutoka ikulu ya Kremlin, kwa siri huku kamati hiyo ya ulinzi na usalama ikiwa aijui zaidi ya kusikia Tangazo la taarifa ya habari ya saa 9:00 AM EDT tarehe 28 October 1962,Kuwa Serikali ya Marekani imetoa Meli ya makombora kaskazini mwa Itaria na Uturuki,baada ya kukubalina na USSR kwa nia ya kutoa Meli ya makombora yake Nchini Cuba.

Ukiona hatua na mwenendo mzima wa tukio hilo unatamani kuona picha hiyo kwa viongozi wetu.Najiuliza maswali yasiyo na majibu nafsi zao zinataka nini hapa duniani.Ni kuwa tajiri zaidi ya matajiri wengine Nchini huku ukiwa Rais au Kiongozi wa kitaifa au nikutenda mambo mema na kuona kuwa umebadilisha maisha ya watanzani walio wengi kujisikia kuwa wanahaki sawa na wanafurahi na kushukuru Mungu kwa kuwapa nchi yenye maziwa na asali na Viongozi wenye kuwajari.

Hatimae wakisharimbikiza wanakutana na hakuna chochote cha maana katika nafsi zao tena, zaidi ya vilio na sauti za umma zinazowaombea mabaya baada ya kuwaombea mema wao na vizazi vyao kwa kuwanyua wao na Nchi yao.Hakika Urais sio Biashara Urais ni Maisha ya Watu na hatima ya vizazi vyao,Ukipewa dhamana jua kunasiku Watanzania watukuuliza uliwatumikiaje na kama sie wewe utakaejibu familia au kizazi chako kitajibu.Haya sio maneno yangu ni maneno ya Mwalimu,Anasema yeye amekaa ikulu miaka 25 na hakuna Rais atakae kuja kukaa huko miaka hiyo labda tu kwa njia ya Kidikteta.Mwalimu anasema Ikulu ni Mzigo ukipita barabarani ukaona watu wanashida huo ni mzigo wako wewe kama Rais.
 
So what went wrong with Mkapa mkuu?

Kwa Mtizamo wa Mwalimu Mkapa alikuwa mmoja kati ya waumini wazuri wa Siasa za Nyerere, Na ukizingatia kwamba Mkapa alikuwa mmoja wa Wahariri wa Habari alikuwa na Nafasi nzuri sana ya kuweza kupembua Kiuhalisia Siasa za Nyerere.

Kwenye miaka ya Themanini kulikuwa na Fununu kuwa Mkapa alikuwa Bepari, na Alihusishwa sana na Jamaa mmoja ambaye ni Tajiri toka kusini anajulikana kama
AMWENYE( Tajiri wa Biashara ya usafirishaji), Nakumbuka wakati wa Kampeni ilikuwa moja kati ya Tuhuma ambazo zilimuandama sana, Na wakati fulani alilazima kumualika Amwenye kwenye kampeni na kukanusha hayo.

Miaka ya Mwanzo Ofisini Mkapa alifanya Vizuri sana, lakini Baada ya Kifo cha JKN,Mkapa alibadilika , hakuwa Mkapa yule Mwanafunzi na muumini wa Siasa za JKN.

Inawezekana kuwa wakati wa Nyerere sio wote walikuwa wanapenda Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, bali walilazimika kwa kuwa hawakuwa na namna ya kufanya na Pia JKN alikuwa mkali sana na anawafuatilia, Leadership Code ilifuatwa na kufuatiliwa.

Kwahiyo basi baada ya kifo cha JKN, Ilikuwa nafasi nzuri kwa kuwa hakukuwa na mtu mwingine wa kuwapigia kelele.


Hivyo basi kwa ushawishi na Tamaa ya mali waliona ni nafasi nzuri kujilimbikizia Mali.
 
Je Benjamin Mkapa alipo shinda uraisi alimpa JK kama compromise ili wafuasi wa JK wasikatae kuisaidia CCM wakati wa kampeni? Kwa maana naamini JK kupewa uwaziri na Mkapa haikuwa bahati mbaya.

mkuu jk huyu wa leo na wa 1995 ni vitu viwili tofauti

jk wa 1995 alikuwa na sifa nyingi tu
kwanza alishiriki kuunda tra baada ya nchi kuwa na sifa ya kusamehe kodi ovyo ovyo

jk alipopewa uwaziri wa fedha aliunda tra

na hakum favour kighoma malima
kwenye skendo ya kodi
so watu walimuona hana ukabila wala udini
na mchapakazi pia
 
nina ndugu ni ccm insiders
hata la kikwete kuhamia chadema 2005 ni la ukweli na mbowe alipewa bilioni tatu za kuandaa mazingira
but leo ukilisema hilo utaoonekana unazusha

Kwani tatizo ni nini? Kwani kama Mbowe alipewa tatizo ni nini? Kwani ni dhambi? Ukichukua fedha za fisadi ili ufanye A. Lakini wewe ukichukua fedha hizo ukazitumia kufanya B. Basi hiyo siyo Rushwa, bali mpewa fedha ana Busara. Heko Mbowe, tumia fedha hizo kuijenga Chadema.
 
mkuu jk huyu wa leo na wa 1995 ni vitu viwili tofauti

jk wa 1995 alikuwa na sifa nyingi tu
kwanza alishiriki kuunda tra baada ya nchi kuwa na sifa ya kusamehe kodi ovyo ovyo

jk alipopewa uwaziri wa fedha aliunda tra

na hakum favour kighoma malima
kwenye skendo ya kodi
so watu walimuona hana ukabila wala udini
na mchapakazi pia

So what changed mkuu and why?
 
So what changed mkuu and why?

kuna sababu nyingi
but mimi naona baada ya kukaribia kuwa rais 1995
alijiona ana yeye ni entitled
na most qualified kwa hiyo akawa corrupt mentally

hakujiona ana mengi ya kujifunza au hiyo kazi ni kubwa kwake
 
The Boss said:
mkuu jk huyu wa leo na wa 1995 ni vitu viwili tofauti

jk wa 1995 alikuwa na sifa nyingi tu
kwanza alishiriki kuunda tra baada ya nchi kuwa na sifa ya kusamehe kodi ovyo ovyo

jk alipopewa uwaziri wa fedha aliunda tra

na hakum favour kighoma malima
kwenye skendo ya kodi
so watu walimuona hana ukabila wala udini
na mchapakazi pia

The Boss,

..TRA ilianzishwa kutokana na mapendekezo ya Tume ya Raisi iliyoongozwa na Edwin Mtei.

..JK hana mchango wowote ule zaidi ya kuwa he was the Minister in Charge of Finance wakati wa utekelezaji wa mapendekezo ya Tume hiyo.

..JK ana sifa nyingi sana ikiwemo kuwa mtu asiye na makuu au asiyependa kujikweza etc etc.

..sijawahi kusikia JK akipewa sifa ya uchapa kazi na mtu yeyote yule aliyepata kufanya naye kazi.



The Presidential Commission on Taxation


Tax reform commenced in 1989 with the appointment of the Presidential Commission of Enquiry into Public Revenues, Taxation and Expenditure (hereafter called 'the Mtei Commission') (GOT, 1991). According to the Commission, its appointment was compelled by the 'serious economic and financial problems' (sic) that the government faced at the time.

It is however notable that the government was not poised immediately to undertake such reforms because the problematic tax system and the rampant corruption it had engendered through the 'ruksa'1politics of the former President Ali Hassan Mwinyi were beneficial to business interests that supported the ruling political cadre. 'Ruksa' politics had eroded respect for law and order and accelerated corruption and the incursion of business interests into the decision-making machinery for public affairs (GOT, 1996a; Hyden, 1999). A point was reached when the tax system had reached astounding fiscal irresponsibility2.

International donors and aid institutions took serious exception to the problem and after the Danish study on the fiscal system in 19903, donor countries agreed to suspend further aid and assistance to the economic recovery programmes unless sound measures are taken to revive the tax system and restore its respectability. This is the background to the Commission's appointment.

 
Back
Top Bottom