Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Kuhusu mishahara, JPM angekuja kuiongeza mara hata 20 kwakua alikuwa si mbabaishaji, alijua uwezo wa nchi bila kuweka misingi imara ya uchumi haiwezi kukidhi haja ya waliowengi....Kama miradi yote aliyoibuni angeifikisha misho mishahara ni kitu kidogo sana...Tatizo tulitaka awe kama ndiyo Mungu na afanye muujiza ndani ya muda mfupi a solve matatizo yote hata kama sote tunajua uwezo wa nchi zetu una ukomo kwakua kwanza hatuna nguvu za kidola kuwabishia wababe wa dunia hii....Hata hivyo yeye alithubutu kubisha na ishara pekee ni kutokwenda kwao kuwaomba hiyo pia ni legacy...Amekufa kama Mkwawa hajawahi ya rudia matapishi yake....

Tupende au tukatae JPM kila alichokitamka alikifanya iwe ni kibaya au kizuri...Alikitimiza! Hii ni sifa yake kuu
Ange.... ange.... ange...

Jamaa zetu wengine mpaka wajomba zetu, wamestaafu wakiwa na mishahara iliyoongezwa kipindi cha Mheshimiwa JK. wamefanya kazi for 5 years baada ya kuondoka JK bila kuongezwa hata senti Mia mbovu mpaka wamestaafu wewe unasema angekuja kuongeza mara 20??

Hivi wenzetu mnatumia akili kufikiria kweli???
 
Kuna watu wana play victims...Tujiulize kama ingekuwa ni wewe na unajua kuwa kuna mamluki ambao wanataka kuku distract wakati wewe una time limit ungefanyaje?

Alii define democracy kwa namna ambayo siyo ile tunayoimbishwa, ina context yake. Japo in my opinion alienda to the extreme, pengine was justified hapa siwezi sema.

Hata hivyo hakupenda kupingwa hadharani ambayo ni weakness yake kuu na pengine aliichukulia personal na kuwawajibisha wahusika...Lakini je wako wapi watu ambao wakionekana ni confidant wake? Mbona hawakuthubutu hata kumwambia kwa faragha mzee hapo unaenda sivyo? Hawa ndiyo ambao naamini wanapaswa kulaumiwa...I could have told him point blank lakini ki faragha if I were to be one amongst....Hawa wapambe nuksi ndiyo mama yetu Mh. Rais Samia Suluhu Hassan anapaswa kuwa "watch out" Mwl Nyerere aliwang'amua akawawakwepa na kuamua wisely a good fate for him!
Mkuu,

Rais Magufuli hakutaka kuskiliza. Watu waliujua huo udhaifu wa kwamba hakupenda kukosolewa hadharani. Wakafanya jitihada za kumkosoa na kumshauri kisiri Kwa heshima kama kiongozi mkuu, ila je alimsikiliza nani???

Mtume Muhammad juu ya kwamba alikuwa akishushiwa wahyi ila pia alikaa na anaowaongoza na kushauriwa na kukubali kushauriwa ila yeye rais wetu yule alisema hadharani kwamba ukimshauri ndio umeharibu kabisa, au hukumsikia mkuu??

Mheshimiwa Magufuli hakutaka kuamini wala kuambiwa tu kwamba Urais ni taasisi, na sio mtu binafsi. Aliamini yeye anaweza fanya kila jambo kitu ambacho kilikuwa ni udhaifu mkubwa sana, udhaifu ambao unashangaza huyu mtu alipitaje kwenye system za TISS mpaka akafanikiwa kuwa rais??

Hivi ni kweli rais anaweza kutoka hadharani akasema yeye ni kichaa kweri kweri???
 
Wabongo we waone tu! 5-10yrs later utasikia...haya angeweza Magufuli tu...laiti Magufuli angekuwepo... Magufuli ndo alikuwa Rais na bla bla kibao.
Ponapona yenu watanzania wenzangu Mungu aibue mtu mwingine mwenye umagufuli kiasi fulani vinginevyo mtalia kilio kisichoisha na kusahaulika Kwa muda mrefu.
Mungu anaipenda Tanzania.

Mungu wetu ametupa Mama Samia Suluhu Hassan. Tunaona neema zimeanza kutiririka.

Tutamuomba Mama agombee zaidi na zaidi.
 
Kupanga mipango na Watanzania ni kupoteza muda

Awali kila mmoja tulikuwa tukikubaliana kwamba, Tungelipenda kupata Rais atayetupeleka mputamputa, baada ya kumpata, Sasa kila mmoja analia lia tu na huwezi kuwatambua tena iwapo walikuwa wakimaanisha kutaka mtu isiyocheka na nyani, mutu jasiri ambayo inaweza kudhibiti hata marais wastaafu na wake zao

Mtu isiyoogopa hata watu wa chama chake, mtu isiyoogopa kampuni za kidunia zilizo na mitaji mikubwa kuipita hata nchi yetu kwa makusanyo ya miaka nane

Hii inamaana, Wengi wa Wabongo ndio wanaupenda uwoga uwoga na wanapenda maisha ya starehe bila kuyatolea jasho, na ndio maana ofsi nyiingi zimejaa wapigaji, wabongo utamkuta kajenga nyumba nzuuuri ya mamilioni ya fedha, lakini pesa ya jasho lake iliyotumika hapo, Haifiki hata laki moja! zingine zoote ni za wizi!!

Sasa kama ni waoga, mlitaka Rais asiye muoga wa nini awafanyie nini sasa??

Pumbavu zenu
Jamani imekuwaje tena???

Mbona tunatukana tu??
 
Mnakera bwana ifikie mahala mkae kwa pattern
Mkuu let's be fair, hata kama tulitaka mtu strong na mwenye uthubutu flani hivi lakini mwendazake alizidi aisee duh!!!

Watu wakamshauri mzee punguza kidogo namna hii hatutofika, kilichowakuta ni aliwaramba vichwa.
 
Pata picha tungefanikiwa kumwezesha miaka 15....Tungekuwa tumenyooka kama stari wa ruler....

Kwa tulivyokuwa tumelegea nadhani tumepata sindano za moto za kutosha tuharibu wenyewe sasa....Yohana alishatengeneza njia nyikani acha wapakwa mafuta waje kutupeleka Caanan😂😂😂
Kwani mkuu mlikuwa na mipango ya kumuwezesha mengine 15??
 
Mkuu let's be fair, hata kama tulitaka mtu strong na mwenye uthubutu flani hivi lakini mwendazake alizidi aisee duh!!!

Watu wakamshauri mzee punguza kidogo namna hii hatutofika, kilichowakuta ni aliwaramba vichwa.
Nyie mnataka mtu wa vugu vugu hamnaga kitu cha namna hio its either warm or cold! SSH ni warm na ndio atavumilia upuuzi mwingi tu ambao mnautaka wabongo! Ila itafikia mahala mtamkumbuka tu Hayati Jiwe
 
Hatumhitaji Ahmedinajad. Hatumhitaji Chavez. Na zaidi ya yote, hatuhitaji Rais kama Mrema.

Tunahitaji Rais mwenye vision, commitment, integrity kama Lee wa Singapore. Tunahitaji Rais kama Castro atakaewekeza katika kuboresha hali ya maisha ya watu wake kwa kutumia alichonacho.

Hatuhitaji Rais atakayetupa vijisifa visivyo na maana bali tunahitaji rais atakayeweza kutumia mazingira yaliyokuweko kutuongoza kuelekea kwenye hali bora zaidi ya kudumu.

Hapana, hatuhitaji Rais fyatu maana tumeishapoteza muda kiasi cha kutosha.

Amandla.........
Sasa huyu ndio genius.

Heko mkuu
 
Dikteta Joseph Stalin wa Urusi aliua mamilioni ya watu na alizikwa na mamilioni ya watu pia.
Hao watu ni wa jamuhuri ya twiter wale wa Jamuhuri ya Muungano uliwaona siku ile ya kumuuaga walivyozuiwa wakavamia airport...Hao ndiyo sauti ya Mungu sauti ya watu...Utateseka sana....Pole, roho mbaya mzigo!
 
Alizungukwa??????!!!!!!!

Mimi nlidhani alikuwa akiwateua waliomzunguka kumbe wote wale walijiteua wenyewe?!

Alijizungushia watu aliojizungushia akiwa na akili timamu na lengo maalum.
Why was he hiring and firing? Au na yenyewe utabisha? Hakuwa Mungu kumbuka, he was a humanbeing, ambaye alikuwa na limitations za kujua roho za watu, ila pale walichemsha hakujali ni rafiki au siyo, kwake Tanzania na watanzania was his first priority
 
Kwani mkuu mlikuwa na mipango ya kumuwezesha mengine 15??
Kabisa nilikuwa wakwanza ku propose aongezewe muda....Basi tu nikagundua kumbe Mungu alimwonea huruma akampumzisha mapema....Maana hawa wenye chuki wangebajatika kumpata wangemdhalilisha sana...Mungu kamlinda; So bad for them!
Kwake lile neno la kuishi ni Kristo kufa ni faida limethibithwa mbele ya macho yetu...
Dikteta Joseph Stalin wa Urusi aliua mamilioni ya watu na alizikwa na mamilioni ya watu pia.
Kwahiyo unataka kutuambia hadithi gani!

Haya basi amekufa wewe umebaki, unahoja?
 
Ange.... ange.... ange...

Jamaa zetu wengine mpaka wajomba zetu, wamestaafu wakiwa na mishahara iliyoongezwa kipindi cha Mheshimiwa JK. wamefanya kazi for 5 years baada ya kuondoka JK bila kuongezwa hata senti Mia mbovu mpaka wamestaafu wewe unasema angekuja kuongeza mara 20??

Hivi wenzetu mnatumia akili kufikiria kweli???
Mawazo ya masikini ni leo tu kesho anawapelekea wengine wasio na nafasi....Na hao ambao hawana kabisa mishahara unawachukuliaje?

Kwahiyo tukiongezewa sasa tukala.mbegu badala ya kuzipanda zitasaidia kitu gani?


Si ajabu, kwakua mwenzetu mawazo yake yalikuwa mbele sana...Sikulaumu tatizo maono yako mafupi....Basi ongezewa tuone kama hizo shida zitapungua!

Hizo tulizoongezewa enzi hizo mbona wengine tulikuwa tunapokea tarehe ya 35? Tena zina kopwa kwa wabarikiwa kundi fulani? Au hilo nalo utabisha?

Ukiwa mchonganishi usiwe msahaulifu....Alafu kulikoni mbona kama kuna mashindano ya JK na JPM? Kwani enzi za JK JPM hakuwa sehemu ya maamuzi? Maana mnatumia nguvu sana kuwapambanisha...
 
Waziri aliyekuwa na hiyo portifolio alikuwa nani vile, nikumbushe tafadhali...Utateseka sana...Yupo kama maji kila ukitaja mafanikio kuanzia awamu ya tatu mpaka ya tano jina lake limo kwenye list....Acha husuda, mpe haki anayestahili haki yake...Legacy ya JPM haipunguzi wala haigombani na ya JK tatizo mnataka kulazimisha mambo!
Na sijui kwa nini kuna wengi sana humu mitandanoni wako kwenye denial ya legacy ya Magufuli ila kiuhalisia wanamkumbuka sana na wangependa kuwa naye what Magufuli did in his short-lived service is now so entrenched in the fabric of the Tanzanian society to the extent whether we like it or not he will still live with us, though posthumously, for a very long time to come. Hata watoto waliokuwa na miaka 5 wakati wa utawala wake walimjua na ndiyo watakaokuja kumtetea na kumsafisha
 
Kabisa nilikuwa wakwanza ku propose aongezewe muda....Basi tu nikagundua kumbe Mungu alimwonea huruma akampumzisha mapema....Maana hawa wenye chuki wangebajatika kumpata wangemdhalilisha sana...Mungu kamlinda; So bad for them!
Kwake lile neno la kuishi ni Kristo kufa ni faida limethibithwa mbele ya macho yetu...

Kwahiyo unataka kutuambia hadithi gani!

Haya basi amekufa wewe umebaki, unahoja?
At times Huwa binafsi nasema ma kufarijika kuwa Bora Mungu aliamua kumpumzisha Mzee wa watu, maana siyo kwa chuki na upinzani aliopambana nao wakati akijitahidi kujenga nchi. Alikuwa na maono ya mbali wakati waliomzunguka waliwaza Leo tu na ndiyo tunawasikia huko bungeni wakijionesha rangi halisi. Wanayemsifia Leo kesho watamsema tena. Magufuli alilijua Hili na hakuangahika nao. Maybe he knew he had so little time left and fought to ensure he started core infrastructural development projects ambazo alijua zingechelewa sana kuanzishwa kwani zilohitaji maamuzi magumu na yenye lawama. Alitimiza wajibu wake na sasa amepumzika.
 
ukweli kwa nchi Kama tz,ambayo inabahati mbaya Sana ya kupata viongozi wasio na maono yenye tija, except mwal.nyerere na jpm.kama jpm amepata upinzani mkubwa mno ,nadhani Sasa kilichobaki aje maraika tu awaongoze hawa viumbe wa tz ambao ni viumbe complex kwakweli.Si unajua huwez kumfanyia fitina malaika.
 
Back
Top Bottom