Abraham Lincolnn
JF-Expert Member
- Apr 12, 2018
- 3,146
- 6,009
Binafsi nilikuwa mmoja wa waliokuwa wanaipinga sana awamu ya tano na Rais wake Magufuli ila baada ya kutafakari na kujionea hali halisi ilivyo sasa Ninakiri kwamba nilifanya makosa makubwa sana, Ninaomba nisamehewe.Magufuli alikuwa ni nabii aliyepata kuishi ili kuonyesha njia sahihi na miongozo tunayopaswa kuiishi.Leo utumbuaji umekuwa kawaida pale uzembe unapodhihirika zamani haya hayakuwezekana.Kazi alizofanyia Tanzania ni kubwa sana tangu akiwa waziri.Ni kweli alivyosema kuwa amejitolea uhai wake kwa ajili ya Tanzania na sote tumeshuhudia lawama nyingi alizobebeshwa yote hayo yalikuwa ni kwa mapenzi makubwa aliyonayo kwa Tanzania.Magufuli ameitendea haki Tanzania katika nyanja zote, Uchumi,Elimu,Afya,Miundombinu muhimu amani na usalama wa taifa.Kwakweli ni mengi sana aliyoyafanya hayatoshi kuelezea hapa.Ila itoshe tu kusema tumeona ukuu wa Mungu kupitia mtu huyu aliyetumwa kuonyesha njia.Bwana ametoa,Bwana ametwaa.Jina lake lihimidiwe! Amen