Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Tunahitaji Rais mwenye maono ya kuthubutu kama Obama, mbishi na mbwatukaji kama Ahmedinajad, asiyetishiwa na wawekezaji kama Hugo Chavez, mwenye kuzungukwa na watu wenye uwezo kama Lula na mwenye mvuto kwa watu wa kawaida kama Zuma. Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kidogo (au sana kutegemea na kipimo) ambaye hatopiga magoti kwa kila mtu anayejiita "mwekezaji" na ambaye hatozungukwa na wenye kuimba sifa zake.

Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kama Mrema!
Aisee haya maombi siku Ingine tuachane nayo .

Nadhani mnaelewa kilichotokea
 
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa. Wakati wa Magufuli ulikuwa supporter wake. Nashangaa now ni kama umemgeuka
Itakuwa kumbukumbu zako haziko sawa.

Hayati rais Magufuli alifanya baadhi ya mambo ambayo najivunia mpaka kesho kwayo. Nimehojiwa na baadhi ya Taasisi za kimataifa kuhusu Tanzania's approach on COVID-19 na mahojiano hayo yamerikodiwa (reference zipo), katika mahojiano hayo nimejivunia kuwa naongozwa na rais Magufuli. Namna serikali yake ilivyoliendea suala la COVID basi kwangu alistahili na anastahili pongezi za hali ya juu. Sitokutajia hayo mahojiano kwa sababu za privacy.

Ila pia hayati rais Magufuli alifanya mambo ya ajabu sana ambayo hakuna mtu au Mtanzania mwenye akili timamu, mpambanuzi na mwenye uelewa wa mambo atayakubali. Bahati mbaya mambo hayo mabaya yalikuwa mengi kuliko mema aliyoyafanya. Na hata hayo mema ukiyaangalia kwa undani basi kuna ukakasi wa hali ya juu.

Mfano, ununuzi wa ndege za Atcl kwa cash na bila kupitia bungeni lilikuwa ni suala linamlomtia doa sana.

Ujenzi wa airport ya chato lilikuwa ni suala baya sana ambalo kiongozi mwenye busara hakutakiwa hata kulifikiria.

Namna ya suala la korosho mwaka 2018 liligubikwa na ghiliba na sintofahamu nyingi sana.

Jaribio la mauaji ya Tundu Lissu akiwa kama kiongozi bungeni, na namna ambavyo serikali ililiendea suala lile ilikuwa haikubaliki.

Kupotea/kutekwa kwa baadhi ya watu prominent ambapo hali hiyo ilikuwa ina public interests na serikali yake kutofanikiwa kutoa majibu mazuri kwa wananchi ilionyesha udhaifu mkubwa sana. Mfano Mohamed Dewji.

Suala la wateule wake kufanya mambo kinyume na muongozo wa viongozi wa Umma halafu yeye kuamua kunyamaza iliichafua picha yake.

All in all, mimi sikuwa supporter wake kama unavyosema lakini alikuwa rais wangu niliyemheshimu. Nilimpongeza alipopatia na alipostahili pongezi na kumkosoa na kumshauri alipokosea.

Usinichukie mkuu!
 
Wakuu tuache kufikiria tawala za kijeshi.Mimi nadhani tupate raia mmoja tu mzalendo mwenye vision na uchungu wa kweli na maendeleo ya nchi hii.Hawa watu wapo isipokuwa bado hawajapewa nafasi au wanabaniwa au wanavurugwa na system isiyoitakia mema nchi.
Embu tuchukulie mfano tumpe urais Pombe Magufuli leo hii,hivi hatutaweza kusonga kweli?
Hongera aseeh!ametunyoosha ingawaa as a human being alikua na flaws lakini alisimama kiume!
 
Itakuwa kumbukumbu zako haziko sawa.

Hayati rais Magufuli alifanya baadhi ya mambo ambayo najivunia mpaka kesho kwayo. Nimehojiwa na baadhi ya Taasisi za kimataifa kuhusu Tanzania's approach on COVID-19 na mahojiano hayo yamerikodiwa (reference zipo), katika mahojiano hayo nimejivunia kuwa naongozwa na rais Magufuli. Namna serikali yake ilivyoliendea suala la COVID basi kwangu alistahili na anastahili pongezi za hali ya juu. Sitokutajia hayo mahojiano kwa sababu za privacy.

Ila pia hayati rais Magufuli alifanya mambo ya ajabu sana ambayo hakuna mtu au Mtanzania mwenye akili timamu, mpambanuzi na mwenye uelewa wa mambo atayakubali. Bahati mbaya mambo hayo mabaya yalikuwa mengi kuliko mema aliyoyafanya. Na hata hayo mema ukiyaangalia kwa undani basi kuna ukakasi wa hali ya juu.

Mfano, ununuzi wa ndege za Atcl kwa cash na bila kupitia bungeni lilikuwa ni suala linamlomtia doa sana.

Ujenzi wa airport ya chato lilikuwa ni suala baya sana ambalo kiongozi mwenye busara hakutakiwa hata kulifikiria.

Namna ya suala la korosho mwaka 2018 liligubikwa na ghiliba na sintofahamu nyingi sana.

Jaribio la mauaji ya Tundu Lissu akiwa kama kiongozi bungeni, na namna ambavyo serikali ililiendea suala lile ilikuwa haikubaliki.

Kupotea/kutekwa kwa baadhi ya watu prominent ambapo hali hiyo ilikuwa ina public interests na serikali yake kutofanikiwa kutoa majibu mazuri kwa wananchi ilionyesha udhaifu mkubwa sana. Mfano Mohamed Dewji.

Suala la wateule wake kufanya mambo kinyume na muongozo wa viongozi wa Umma halafu yeye kuamua kunyamaza iliichafua picha yake.

All in all, mimi sikuwa supporter wake kama unavyosema lakini alikuwa rais wangu niliyemheshimu. Nilimpongeza alipopatia na alipostahili pongezi na kumkosoa na kumshauri alipokosea.

Usinichukie mkuu!
Umeandika mawazo yangu
 
Kwa level ya Urais huwezi kupendwa na kila mtu mkuu, Unasahau pia nature ya binadamu Kupenda Varieties vitu vipya, Mama aendelee kujenga Taifa huku akifahamu wapo watakaomchukia tena wataenda far na kuanza harakati awe imara zaidi JPM vinginevyo hujuma zitakuwa juu sana kwa waliobanwa mirija yao ivo kupelekea vitu kama maandamano ambayo ivo kukutoa kwenye Power ni haraka sana
Asitake kuridhisha kila mtu tena katika Kundi ambalo hata ulibebe mgongoni hariridhiki ni hao waliojificha kwenye miavuli wa investors, Mwendezake alilijua ilo ndio mana mtaji wake ukabaki kwa hawa low na medium Class
Exactly huku mitaani ambako ndo wapiga kura wapo mama kashapoteza credit haraka sana...ingawa wafanyakazi tulokua tunaminywa tunamfurahia Ila 2025 uchaguzi mama ajipange wapiga kura ambao ndo Tabaka la chini na kati Maza washamchokaa mnooo na hivi hatumbui ndo kabisaa yaani,hasikilizi shida za wananchi kwenye mikutano hiloo ndo kabisaa yaani
 
Exactly huku mitaani ambako ndo wapiga kura wapo mama kashapoteza credit haraka sana...ingawa wafanyakazi tulokua tunaminywa tunamfurahia Ila 2025 uchaguzi mama ajipange wapiga kura ambao ndo Tabaka la chini na kati Maza washamchokaa mnooo na hivi hatumbui ndo kabisaa yaani,hasikilizi shida za wananchi kwenye mikutano hiloo ndo kabisaa yaani
Muongo sana ww. Hiyo survey umeifanya wapi? Chato na kwa wasukuma? Huku kwetu mama anakubalika 100%. Tukutajie mazuri aliyoyafanya kwa muda mfupi kila mmoja anamsifu?
 
rais fyatu huyu awe na ujasiri wa kutimua na kupitia upya mikataba ya wawekezaji wanaoneemesha makwao kwa kutumia rasilimali zetu na kutuacha hohe hahe! asile meza moja na mafisadi, ambaye yuko tayari na uwezo wa kujiuliza ni kwa nini pamoja na utajiri wote tuliobarikiwa na mungu bado tumeendelea kuwa masikini, mwenye utayari wa kutoa upofu huu uliotugubika...................nani sasa?! ..........labda mm

Tulimpata, tukamchukulia for granted, ameondoka zake leo imepita miezi saba!
 
Back
Top Bottom