Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Tunahitaji Rais mwenye maono ya kuthubutu kama Obama, mbishi na mbwatukaji kama Ahmedinajad, asiyetishiwa na wawekezaji kama Hugo Chavez, mwenye kuzungukwa na watu wenye uwezo kama Lula na mwenye mvuto kwa watu wa kawaida kama Zuma. Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kidogo (au sana kutegemea na kipimo) ambaye hatopiga magoti kwa kila mtu anayejiita "mwekezaji" na ambaye hatozungukwa na wenye kuimba sifa zake.
Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kama Mrema!
Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kama Mrema!