TANZANIA: Historia ya Taifa Letu na Sheikh Yahya (RIP!)

Heshima kwako W J Malecela.

Unaweza kumwelezea Sheikh Yahaya Hussen ndani ya jamii yetu kama ifuatavyo.

[1] Mtabiri.

Kazi yake ya utabiri ilifahamika afrika mashariki na maeneo mbali mbali duniani.Alifanya kazi ya utabiri hadi mauti ilipomkuta.Unaweza kumhukumu Sheikh Yahaya kwa kazi ya utabiri lakini wapo wengi waliofaidika na utabiri wake.

[2] Kiongozi wa kiroho [Sheikh]

Sheikh Yahaya Hussein kwa nyakati tofauti aliwahi kushika madaraka makubwa ndani ya BAKWATA taifa.Mara wa mara nimemshuhudia akisoma Quran ndani ya misikiti mbali mbali.Sheikh yahaya Hussein ni mmoja wa mwanzilishi wa mashindano ya usomaji wa Quran Tanzania.Najua wapo wapinzani wake kibao wanaohoji ushiriki wake wa utabiri unaopingana na dini ya kIslamu mara nyingi amekuwa akitoa ufafanuzi fasaha dhidi ya wapinzani wake.

[3] Kachero / Shushu.

Lazima nikiri nilikuwa sijawahi kusikia habari za Sheikh Yahaya Hussein na ushushu lakini baada ya kusoma kitabu cha Mwl Ludovick Mwijage 'The dark side of Nyerere' ndio nikajua kumbe Sheikh alikuwa na kazi nyingine nyuma ya pazia.Enzi za vita baridi ushushu ulikuwa juu sana huwezi kutarajia mtu wa aina ya Sheikh Yahaya aweza kuwa shushu !.

[4] Mbabaishaji.

Nadhani kuelekea mwisho wa maisha yake Sheikh Yahaya Hussein alikuwa amepigikika kimaisha.Kuna baadhi ya mambo yaliashiria Sheikh alikuwa ameishiwa au hakuwa na fedha za kutosha kumudu maisha yake sawa sawa.Utakumbuka kuna kipindi aliugua ikabidi apelekwe India kwa matibabu ya moyo,fedha za matibabu na usafiri alilipiwa na Mheshimiwa B Mkapa.Baada ya safari ya India Sheikh Yahaya Hussein hakuwa yule tuliyemzoea bali alikuwa mganga njaa zaidi.Mfano aliwatisha wanaCCM watakao mpinga Kikwete atakufa,ukiangalia kwa makini utagundua Sheikh alikuwa akijikomba kwa Rais Kikwete.Mfano mwingine ni kujitolea kutoa ulinzi usionekana kwa Rais Kikwete.Kifupi njaa ilimfanya Sheikh Yahaya Hussein abwabwaje chochote mbele ya wenye fedha na madaraka.
 
Kiukweli ni uji mzuri sana kiafya, nami nakubaliana na wewe zinaweza kuwa ni sababu za kisiasa na inawezekana ikawa ni kweli, maana yale mafuta pia yalipatikana na kashfa hivi karibuni kule kwenye kambi za wakimbizi, sina uhakika kama ni Ngara ama lah.
Yale mafuta kama sikosei yalikuwa na chata hii!




Aisee hiyo handshake kwenye picha siyo handshake style ya mafreemason?
 
W. J. William,
Sii wacha Mungu wote hutenda mema , bali watenda mema ndio wacha Mungu!

So strange in my faith the opposite is true. Kwamba alama ya wacha-Mungu ni kutenda 'mema' maana huongozwa na roho wa Mungu lakini si watenda mema wote ni wacha Mungu kwani kutenda kwao mema kunaweza kuwa sababu ya kutaka mafao fulani katika maisha yao na wala si kumwabudu Mungu! Ndiyo maana katika imani yangu huruhusiwi kumhukumu mtu kwani si kwa kazi ya matendo mtu huhesabiwa haki bali kwa moyo uliopondeka (Imani kwa Mungu ambapo bila hiyo kila tendo ni dhambi mbele za Mungu) ambao hakuna awezaye kuupima isipokuwa mtu mwenye hiyo roho na muumba wake!

Labda nitoe mfano wa matendo mema yaambatanayo na imani kama dhabihu ya haki mbele ya Mungu. Kunaweza kuwa na madaktari wawili wa binadamu. Mmoja anatibu kwa lengo lakuondolea watu maumivu na wanatenda hayo yote kwa nguvu akili na uwezo wote kwasababu wanaamini kila mwanadamu anapaswa kuwa na raha na afya njema ili wa mwabudu Mungu. Na mwingine anatenda kazi yake hiyo kwa uaminifu wote kwaakili na nguvu zake zote ili baada ya hayo; apate wagonjwa wengi zaidi wanaoenda kwake kutibiwa kuliko madakatari wenzake ili ama apate pesa nyingi zaidi kama analipwa ama apate sifa zaidi ili jina lake liwe kuu mbele ya jamii.

Hawa ni watu wawili wenye malengo tofauti lakini yajulikanayo ndani ya mioyo yao zaidi japo mwisho wasiku wote wanaonekana kuwa ni watu 'wema'. Mbele ya Mungu kila kazi inayofanywa bila kuamini kuwa ni kazi ya Mungu na sifa na utukufu lazima zirudi kwake ni dhambi. Ndiyo maana sisi kama binadamu hatuwezi kujua yupi katenda 'mema' na yupi mabaya kwa kutumia matokeo ya kazi za binadamu. Lakini sisi katika imani tunaambiwa kila mtu atahukumiwa kwa maneno yake maana mtu hutamka kile kiujazacho moyo. Sasa iwapo hawa wawili tutawafanyia interview kila mtu akatupa sababu zake hatuna budi kuamini watuambiayo na kuwahukumu kwa maneno na si matendo tu bali vyote kwa pamoja maneno na matendo. Wakitudanganya sisi vipo vitu viwili vina washuhudia moyo wake na Mungu mwenyewe aonaye sirini. Akiwa mkweli tutamhubiria kuwa anavyofanya ni kinyume na mapenzi ya Mungu. Akitudanganya atakufa katika dhambi yake na hukumu ya Mungu itakuwa juu yake kwa kusema uwongo.

So ni muhimu kuwa wakweli mbele za binadamu na kwa Mungu kwani ukiwa vuguvugu Mungu atakutapika. Useme kile ambacho moyo wako unaamini kuwa ndiyo ili binadamu wengine wakusaidie kusikia sauti ya Mungu ili uokolewe katika dhambi. Mtu mwovu anaposema uovu wake hata kama anaamini kuwa ni haki ni vizuri na akifungua moyo wake Mungu atampa neema ya kupata ufahamu wa kweli na kuufikia ukweli. Inabidi basi tukubali kusikiliza wanadamu wenzetu wakubwa kwa wadogo maskini ama tajiri wa imani moja na sisi na wale tofauti bila kubagua kwani Mungu huweza kumtumia yeyote kufikisha ujumbe wake wa ukweli kwako. Ndiyo maana neno la Mungu linasema wenye kiburi na majivuono hawata urithi ufalme wa Mungu. Ukimdharau binadamu yeyote ambaye ni kiumbe wa Mungu unadharau kazi ya Mungu ya uumbaji na kujiweka juu yake.

Imetupasa nasi kusema kile kilicho kweli bila kujali sura nafasi ama cheo cha mtu ili Mungu ainuliwe ndani ya mwanadamu. Roho ya Mungu inataka binadamu wote wauujue ukweli kila mtu kwa wakati tofauti tofauti. Wengine bado ni wachanga tunatakiwa kuwachukulia kwa upole na unyenyekevu wote huku tukiangalia wasitu kwaze tukaanguka wote dhambini. Wale walio wabishi tunatakiwa kuwaacha na kukung'uta vumbi miguuni mwetu lakini wale wanaotupokea amani ya Mungu itakuwa pamoja nao hata kuwawezesha kama watanyenyekea na kutii kuinuliwa kutoka mavumbini na kuketishwa na wafalme.
 
Siwezi kuhukumu roho ya Yahya lakini nauwezo wa kuhukumu kazi ya mikono yake kuwa ni batili na uovu kwani kwakututangazia kuwa anamlinda Rais wa nchi ambaye mimi ni raia humo ni kukubali kuwa ulinzi wa Mungu aliye hai hautoshi isipokuwa majini yake ambaye kwake ndiyo miungu kwani anayaamini. Kwavile naamini ninauwezo zaidi ya hayo majini yake na ninaujuzi zaidi ya elimu yake hiyo ya nyota basi ilitupasa sisi wana wa Mungu aliye hai kusimama na kukataa kwa vitendo nasi tulimtangazia vita vya kiroho kuwa ikiwa yeye ana nguvu kuliko sisi basi kama alivyo tabari basi huyo aliye simama kumpinga Rais wa sasa katika uchaguzi atakufa na uchaguzi utaahirishwa kama alivyo sema la hasha basi na sisi tunasimama kutabiri kuwa yeye atakufa kabla ya hao na uchaguzi kamwe hautaahirishwa.

Hapo hatuzungumzi tena tumesema nayo yamekuwa nasi tuna simama tena kwa ujasiri kuliinua jina la Mungu wetu aliye hai aliye julikana kwetu kama Emanueli kabla ya kufa na kufufuka na hata sasa kama Yesu mwana wa Mungu aliye hai mzaliwa wa kwanza wa baba katika ufalme wake na Ame kama mrithi katika huo ufalme (Prince).

Jina hili kuu kupita majina yote tunaliinua na kumshangilia kwani amethibitisha kuwa hakuna awezaye kutenda kinyume na watoto wake ambao wamezaliwa pamoja naye kwa uwezo wa Roho mtakatifu hata kufanyika kuwa Miungu kama baba yetu alivyo ndivyo nasi tulivyo. Ukipenda kuamini utaamini ukitaka kushindana na sisi tutakupisha upige kelele huku sisi tukitoa neno moja tu kwako kwamba tu washindi zaidi ya washindi katika dunia hii nahata ile ijayo. Vita vyetu si vya damu na nyama na silaha zetu si za kimwili bali zina nguvu kwa uwezo wa roho hata kuharibu ngome zote na sultani zote na uweza na mamlaka hata kuzifanya zote ziwe chini ya miguu yetu na kusalimu amri.

Jina lako Yesu lihimidiwe milele na milele Amina!
 
Amali njema ndo mkomboz wa marehemu Shekh Yahya,watoto wema ambao watamuombea ni wakomboz wake
 
Amali njema ndo mkomboz wa marehemu Shekh Yahya,watoto wema ambao watamuombea ni wakomboz wake

Imempasa mwanadamu kuzaliwa kuishi mara moja. Baada ya kifo ni hukumu hakuna rehema ama msamaha kwa mtu aliyekufa katika dhambi. Hatuwezi sema Yahya ameenda jehanamu kwani hatujui dakika yake ya mwisho aliimaliza vipi; pengine alikiri haya tunayoyaona sisi kuwa ni uovu lakini Mungu ni zaidi ya sisi wanadamu ni hakimu wa haki naye humpa kila mtu stahili yake. Ninachotaka kusema ni kuwa watoto wake hawawezi kubadili hukumu baada ya kifo cha baba yao. Kama ni kubadili basi ilipaswa kuwa kabla ya kifo, bali yote tunayoyahubiri sasa kuwa si sawa mbele ya Mungu ndiyo tunafanya kazi ya kuwatoa wale wote walio katika hali kama hiyo kabla ya vifo vyao ili nao wapate rehema na msamaha kabla ya mauti; ikitokea wakakataa na kufa katika haya basi hukumu ya Mungu iko juu yao.

Mwandamu hatahukumiwa kwa kosa lolote zaidi ya kukataa neema ya Mungu ya msamaha wa bure ambao unapatikana kwanjia ya kuliamini jina la Yesu ambaye ni pekee alimwaga damu yake msalabani ili sote tuondolewe stahili zetu za hukumu kwa kumwasi Mungu na kumpa utuku wetu shetani baada ya kumdanganya mama yetu Hawa na kisha kumshawishi mumewe Adamu kutokumtii Mungu. Ni bahati mbaya sana hata leo bado twatenda kosa lile lile la kukosa utii kwa neno la Mungu hivyo kumkataa Mungu na kuupenda ulimwengu zaidi. Kwa gene zetu za urithi kutoka kwa babu na bibi yetu Adamu na Hawa hakuna mwanadamu anayeweza kuishi pasipokutenda dhambi. Ili uondoke katika family tree ya Adamu na Hawa lazima ufe na kuzaliwa mara ya pili. Kifo hiki ni kwa kuamini moyoni kuwa Yesu alikufa kwaajili yako na alizikwa akafufuka katika wafu na sasa yupo hai amekaa mkono wa kuume (Mkono wenye nguvu na mamlaka ya kiungu) wa Mungu. Amemtuma roho wake aje duniani kutuwezesha sisi tuzaliwe mara ya pili na hivyo kuhamishwa kutoka ufalme wa shetani na kuwekwa katika ufalme wa Mungu. Ukiamini basi ukiri kwa kinywa chako hiyo imani na kukubali kuongozwa na roho wa Mungu jinsi apendavyo na si jinsi mwili wako upendavyo. Mwili utawaka tamaa ya uzinzi roho wa Mungu atakupa neema ya kukataa kuutii mwili na kutotenda dhambi ya uzinzi kwa mfano. Maisha magumu yatakulazimisha mkono wako uibe ama kwa kalamu au kwa kutumia nguvu; roho mtakatifu atakupa akili ya jinsi ya kupata mahitaji yako bila kuiba kwa njia yeyote. Unaweza ukaomba kwa rafiki yako; ukatafuta kazi unayoiweza hapo atakuongoza wapi inapatikana ama hata kama u mgonjwa ata sababisha mtu akukumbuke na kukupa msaada bila kuomba maana ndiye anayetawala akili za wandamu wote.

Hakuna kitu kinashindikana kwa imani. Ukiona viongozi ni wezi mafisadi, roho wa Mungu ukimwomba wewe uchukue nafasi kwa lengo la kurekebisha atakuwezesha. Lakini kama moyoni unataka ili na wewe ufaidi kamwe hutakaa upate hiyo nafasi na utaishia kuingia katika dhambi ambayo mwisho wako unaweza kuwa mbaya. Si kwamba itakuwa rahisi kama kunywa maji no vipingamizi vitakuwepo lakini mwisho wa siku ukivumilia pasipo kuvunjika moyo utashinda. Hakuna katika historia aliye mtegemea Mungu kwa dogo ama kwa kubwa akashindwa na zaidi sana sasa ambapo shetani hana tena mamlaka kisheria ya kututawala ila kwa hiari yetu. Akikudanganya ukakubali Mungu ni mwenye haki anakukabidhi kwake na kukuondoa katika ufalme wake. Maana umekubali kwa moyo wako na kukiri kwa kinywa chako, mfano mtu anaamini mafisadi lazima washinde na kuchukua uongozi na anaenda mbele zaidi na kukiri kwa mdomo wake; hivyo hiyo inawapa uwezo wao kushinda kwani tumekubali kwa moyo na kwa kukiri Mungu hawezi ingia kati maana ni Mungu wa wabaya na wema. Mimi nikikataa fisadi hawezi kunitawala nikasimama na kuamini kisha kutamka hadharani na kuendelea kufanya hivyo hata kama kwa macho ya kibinadamu nitaonekana naota mwisho wa yote lazima mimi niibuke mshindi kwani ndiyo sababu Yesu alikufa msalabani ili hayo yawezekane.

Kwa jinsi hiyo hiyo niliposimama na kusema hakuna uchaguzi kuahirishwa ama mtu kufa yote ilikuwa hivyo. Na hata sasa na sema tena kwa sauti kubwa hakuna fisadi atakaye nitawala mimi nikiwa hai ndivyo ilivyo na ndivyo itakavyokuwa no more no less. Keep this post and at the right time will come public in my very ID na you will know why I said this; hukumu imeshatolewa imebaki utekelezaji tu and things will set themselves to obey my voice. A King is not a king if his word does not have power; my word is a decree for what I say is of my father who is the King of Kings and I the prince in His Kingdom!
 
- Well, ya uchawi hayo ni yako Babu wa Loliondo kwa wengine ni mchawi na kwa wengine ni mchumgaji anayeongozwa na Mungu, hapa kila mtu ana dini yake sasa huwezi kujaribu kuhalalaisha yako over za wengine ni dalili za kutokomaa kijamiii, sasa huo unaousema ni utabiri wa kisayansi na mwingine ni uchawi tu kama ue unaouita wa Sheikh, and then unakuja kujisema mwenye who you are na maneno ya anwani utasemaje ya anwani na jina lako la bandia, mimi ninaweka jina langu kamili na mahali nilipoa anza na jina na picha yako hapa jina kamili and then ndio uongelee ya anwani, ulimbukeni ni kulilia kuwa sawa wengine ambao hawakuhusu! na wala huwawezi!

- Kama ni dini mkuu hapa kila mtu ana yake, cha muhimu wewe ni kjaribu ku-relate na mada kwamba Sheikh ana nafasi kwenye historia ya taifa letu au hapana, sasa unasema maneno mengi ambayo ni clear kwamba unakubali kwamba Sheikh alikuwa influencial kwa jamii, sasa onyesha nafasi yake kwenye historia, sio kumhukumu kuhusu dini yake, that is not the idea here mkuu! Kama huna uhakika na kinachosemwa uliza sio ujinga, kuliko kujifanya unajua na huku maneno yako yanakusuta kwamba hujui!

William @ NYC, USA.

mkuu william,nasema tena kuwa ni ulimbukeni kuweka iyo uitayo address. Hata ivo iyo si anuani bali ni sehemu yenye anuani nyingi ila umeleta mjumuliko wake. Hapa sitaki kuwa na mawazo ya kitumwa kuwa najilinganisha nawe,hapana. Na hata nikiamua ivo sioni ulipoelekeza mantiki kwa kuwa jf wapo wengi waliopo hapo ulipo na hawana mambo ayo. Ila ni matter ya umri tu,ukikuwa waweza kuja kujishangaa. Pia nani kakwambia nimeweka jina bandia? Kwanza tambua sijawahi kukuletea birth certificate yangu kujiridhisha kuwa naongopa jina. Usidhani kila umuonaye si mtu wala si jina ila jina liwe lako tu,bwn william malecela. Aya sawa,ni jina zuri na kubwa ila ukumbuke lilianza kama ilo langu ndo sasa unadhani unatamba nalo. Unamhusisha babu wa loliondo na dini yake kwa marehemu yahya ,je uyu marehemu alitumia majini au ndoto,je vipindi vya channel10 ulikuwa unaangalia au ulisubiri afe uje kumsifia? Usihusishe dini ya uislamu na dhana za kichawi ndugu! Najua wewe ni stakeholder mzuri tu jf,ila haitonilimit kuweka ukweli. Naomba uache jazba tukae kwenye mada ya uyo mchawi Yahya,nasema na ntaendelea kumuita yahya kwa kuwa sifa ya u sheikh hana kwa misingi ya dini ya Kiislamu. Sijasema si muislam hapana,nasema usheikh wake mi si uhafiki. Pia nimeeleza kuwa sitokulazima kukubali kuwa uchawi wa Yahya umewanufaisha nyie wachache wala si usemavyo kuwa influencial. Ujue mtu kuwa maarufu si kutenda mema tu,unaweza ukafanya mambo ya ajabu bado ukawa maarufu. Mf.madkiteta,wachawi,mashetani,watakatifu,waadilifu woote wamejenga jina na umaarufu lakini si kwa kukubalika tu. Mfano,Marehemu Yahya nimemjua kwa mabaya,hasa kupitia mambo yake ya kifamilia kule mkwajuni dsm,ni ajabu kumkubali postively,unless and until you were a beneficial partner in his witchcraft! Kama ntakukwaza ntaomba uniweke wazi niombe samahani kwa mawazo yangu yaliyo huru. Nakutakia siku njema ndugu William.
 
Heshima kwako W J Malecela.

Unaweza kumwelezea Sheikh Yahaya Hussen ndani ya jamii yetu kama ifuatavyo.

[1] Mtabiri.

Kazi yake ya utabiri ilifahamika afrika mashariki na maeneo mbali mbali duniani.Alifanya kazi ya utabiri hadi mauti ilipomkuta.Unaweza kumhukumu Sheikh Yahaya kwa kazi ya utabiri lakini wapo wengi waliofaidika na utabiri wake.

[2] Kiongozi wa kiroho [Sheikh]

Sheikh Yahaya Hussein kwa nyakati tofauti aliwahi kushika madaraka makubwa ndani ya BAKWATA taifa.Mara wa mara nimemshuhudia akisoma Quran ndani ya misikiti mbali mbali.Sheikh yahaya Hussein ni mmoja wa mwanzilishi wa mashindano ya usomaji wa Quran Tanzania.Najua wapo wapinzani wake kibao wanaohoji ushiriki wake wa utabiri unaopingana na dini ya kIslamu mara nyingi amekuwa akitoa ufafanuzi fasaha dhidi ya wapinzani wake.

[3] Kachero / Shushu.

Lazima nikiri nilikuwa sijawahi kusikia habari za Sheikh Yahaya Hussein na ushushu lakini baada ya kusoma kitabu cha Mwl Ludovick Mwijage 'The dark side of Nyerere' ndio nikajua kumbe Sheikh alikuwa na kazi nyingine nyuma ya pazia.Enzi za vita baridi ushushu ulikuwa juu sana huwezi kutarajia mtu wa aina ya Sheikh Yahaya aweza kuwa shushu !.

[4] Mbabaishaji.

Nadhani kuelekea mwisho wa maisha yake Sheikh Yahaya Hussein alikuwa amepigikika kimaisha.Kuna baadhi ya mambo yaliashiria Sheikh alikuwa ameishiwa au hakuwa na fedha za kutosha kumudu maisha yake sawa sawa.Utakumbuka kuna kipindi aliugua ikabidi apelekwe India kwa matibabu ya moyo,fedha za matibabu na usafiri alilipiwa na Mheshimiwa B Mkapa.Baada ya safari ya India Sheikh Yahaya Hussein hakuwa yule tuliyemzoea bali alikuwa mganga njaa zaidi.Mfano aliwatisha wanaCCM watakao mpinga Kikwete atakufa,ukiangalia kwa makini utagundua Sheikh alikuwa akijikomba kwa Rais Kikwete.Mfano mwingine ni kujitolea kutoa ulinzi usionekana kwa Rais Kikwete.Kifupi njaa ilimfanya Sheikh Yahaya Hussein abwabwaje chochote mbele ya wenye fedha na madaraka.

- Simple and very clear: Much Respect!

William @ NYC, USA.
 
Jambo ambalo Mkandara ameshindwa kulesma na nahisi ni kutomjua vyema Marehem ni kuwa moja kati ya sifa nyingine ya Marehem ambayo wasio waislam hawaijui ni kuwa Marehem alikuwa ni mooja kati ya wasomaji wakubwa sana wa wa Qur'an na kuna kipindi alishinda mashindano ya kusoma huko Cairo. Ilibidi washindani wake waingine mitini.

How can we forget siku za Ijumaa alipokuwa anasoma pale Mtoro mpaka wakti wa salat Jumaa inapoingia?

Ama kweli msikiti wa Mtoro na K tea shop ya mtaa wa Chagga watakumisss

Mnalikumbuka range la 6 doors la marehem?


Inallillahi wa Inna Illahi Raj'uun
 
mkuu william,nasema tena kuwa ni ulimbukeni kuweka iyo uitayo address. Hata ivo iyo si anuani bali ni sehemu yenye anuani nyingi ila umeleta mjumuliko wake. Hapa sitaki kuwa na mawazo ya kitumwa kuwa najilinganisha nawe,hapana. Na hata nikiamua ivo sioni ulipoelekeza mantiki kwa kuwa jf wapo wengi waliopo hapo ulipo na hawana mambo ayo. Ila ni matter ya umri tu,ukikuwa waweza kuja kujishangaa. Pia nani kakwambia nimeweka jina bandia? Kwanza tambua sijawahi kukuletea birth certificate yangu kujiridhisha kuwa naongopa jina. Usidhani kila umuonaye si mtu wala si jina ila jina liwe lako tu,bwn william malecela. Aya sawa,ni jina zuri na kubwa ila ukumbuke lilianza kama ilo langu ndo sasa unadhani unatamba nalo. Unamhusisha babu wa loliondo na dini yake kwa marehemu yahya ,je uyu marehemu alitumia majini au ndoto,je vipindi vya channel10 ulikuwa unaangalia au ulisubiri afe uje kumsifia? Usihusishe dini ya uislamu na dhana za kichawi ndugu! Najua wewe ni stakeholder mzuri tu jf,ila haitonilimit kuweka ukweli. Naomba uache jazba tukae kwenye mada ya uyo mchawi Yahya,nasema na ntaendelea kumuita yahya kwa kuwa sifa ya u sheikh hana kwa misingi ya dini ya Kiislamu. Sijasema si muislam hapana,nasema usheikh wake mi si uhafiki. Pia nimeeleza kuwa sitokulazima kukubali kuwa uchawi wa Yahya umewanufaisha nyie wachache wala si usemavyo kuwa influencial. Ujue mtu kuwa maarufu si kutenda mema tu,unaweza ukafanya mambo ya ajabu bado ukawa maarufu. Mf.madkiteta,wachawi,mashetani,watakatifu,waadilifu woote wamejenga jina na umaarufu lakini si kwa kukubalika tu. Mfano,Marehemu Yahya nimemjua kwa mabaya,hasa kupitia mambo yake ya kifamilia kule mkwajuni dsm,ni ajabu kumkubali postively,unless and until you were a beneficial partner in his witchcraft! Kama ntakukwaza ntaomba uniweke wazi niombe samahani kwa mawazo yangu yaliyo huru. Nakutakia siku njema ndugu William.

- Well, nje ya mada unaonekana una tatizo sana na mimi binafsi basi fungua mada inayonihusu maana kwenye hii mada ya Sheikh Yahaya RIP, siwezi kukusaidia.

- Kuhusu hoja yako ya msingi, ni kwamba mimi nimeweka picha, jina langu kamili na anwani yangu ninapoishi, sasa na wewe kwanza fanya hivyo ndio utakuwa na haki ya kuongelea anything of that lines otherwise naona unajaribu sana kuiharibu mada, lakini huwezi maana wengi hapa tunazo akiliza kutosha kukuelewa.


- Kama Sheikh Yahya alikuwa ni mchawi kwako, sio tatizo isipokuwa alikuwa mwananchi mwenye uwezo wa tofauti sana na wananchi wengine kama mimi, ndio maana hata Rais wa jamhuri jana alienda kuhudhuria mazishi yake, ukisoma vizuri sana hii topic utaona sio wote wenye mawazo kama yako na ndio Demokrasia!

- karibu sana ila jitahidi next time kufungua topic inayonihusu badala ya kujaribu kuharibu mjadala muhimu sana kama huu.

William @ NYC, USA.
 
Kiongozi wa kiroho Sheikh Yahaya Hussein kwa nyakati tofauti aliwahi kushika madaraka makubwa ndani ya BAKWATA taifa.Mara wa mara nimemshuhudia akisoma Quran ndani ya misikiti mbali mbali.Sheikh yahaya Hussein ni mmoja wa mwanzilishi wa mashindano ya usomaji wa Quran Tanzania.Najua wapo wapinzani wake kibao wanaohoji ushiriki wake wa utabiri unaopingana na dini ya kIslamu mara nyingi amekuwa akitoa ufafanuzi fasaha dhidi ya wapinzani wake.[/COLOR]

Moja kati ya sifa nyingine ya Marehem ambayo wasio waislam hawaijui ni kuwa Marehem alikuwa ni mooja kati ya wasomaji wakubwa sana wa wa Qur'an na kuna kipindi alishinda mashindano ya kusoma huko Cairo. Ilibidi washindani wake waingine mitini

Ama kweli msikiti wa Mtoro na K tea shop ya mtaa wa Chagga watakumisss
Inallillahi wa Inna Illahi Raj'uun
 
RIP Sheikh Yahya Hussein...........in addition kwa yaliyosemwa hapo juu kuhusu Hayati Sheikh Yahya alikuwa Kiungo Mkubwa sana.....na hasa kwa jamiii ya walionacho na wasiokuwa nacho...........
 
PHP:
 [IMG]https://www.jamiiforums.com/template/JamiV1/default/misc/quote_icon.png[/IMG] Originally Posted by W. J. Malecela [IMG]https://www.jamiiforums.com/template/JamiV1/default/buttons/viewpost-right.png[/IMG] - Well, ya uchawi hayo ni yako Babu wa Loliondo kwa wengine ni mchawi na kwa wengine ni mchumgaji anayeongozwa na Mungu, hapa kila mtu ana dini yake sasa huwezi kujaribu kuhalalaisha yako over za wengine ni dalili za kutokomaa kijamiii, sasa huo unaousema ni utabiri wa kisayansi na mwingine ni uchawi tu kama ue unaouita wa Sheikh, and then unakuja kujisema mwenye who you are na maneno ya anwani utasemaje ya anwani na jina lako la bandia, mimi ninaweka jina langu kamili na mahali nilipoa anza na jina na picha yako hapa jina kamili and then ndio uongelee ya anwani, ulimbukeni ni kulilia kuwa sawa wengine ambao hawakuhusu! na wala huwawezi!

Ndungu William Malecela, wote ambao wapo hapa jamii forums na wanaweza kuchangia kuwe na kuchangia mada wamekuwa registered. Hili suala la kwamba wengine wanajificha majina, wewe umeandika jina kamili na anuani ulipo ni uamuzi wako kwa upo huru kufanya utakavyo.
Huenda mimi naishi hapo NY City karibu na United Nations, block chache kutoka Uganda House, tukitazamana na ngambo ya bruklin. Hakuna sababu ya kufanya mtu ajikamue, ila wewe uliyejikamua hivyo umefanya kwa sababu zako. Pole ila kwa sasa niko kijijini kwangu kamji kadogo Mtombu nawafungulia gate waendao kuangalia wanyama mbuga za wanyamapori huko Ngorongoro, serengeti na seronera.
 
RIP Sheikh Yahya Hussein...........in addition kwa yaliyosemwa hapo juu kuhusu Hayati Sheikh Yahya alikuwa Kiungo Mkubwa sana.....na hasa kwa jamiii ya walionacho na wasiokuwa nacho...........

- Strong sana safi sana!

Es!
 
Moja kati ya sifa nyingine ya Marehem ambayo wasio waislam hawaijui ni kuwa Marehem alikuwa ni mooja kati ya wasomaji wakubwa sana wa wa Qur'an na kuna kipindi alishinda mashindano ya kusoma huko Cairo. Ilibidi washindani wake waingine mitini

Ama kweli msikiti wa Mtoro na K tea shop ya mtaa wa Chagga watakumisss
Inallillahi wa Inna Illahi Raj'uun

- Hoja nzito sana, sawa sawa mkuu!

William @ NYC, USA.
 
Ame,
Mkuu wangu imani za dini zinatofautiana na hakika sii lazima nifuate dini kuamini jambo fulani..Na pengine nikwambie tu kwamba hata Uislaam haukubaliani na mtazamo wangu kwani bila kuamini Mungu na mitume wake huwezi kuwa mcha Mungu na wala sii rahisi ukatenda mema. Hivyo sikutumia dini yeyote ila mtazamo wangu ktk kuamini kwamba ktk kila jema litendwalo huongozwa na baraka za Mwenyezi Mungu na kila baya huongozwa na Shetani..Haya ya daktari kutaka fedha au kutotana fedha hayahusiani kabisa na ucha Mungu kwa sababu hakuna mahala mwenyezi Mungu amekataza watu kudai malipo zaidi kwa kazi nzuri inayofanywa na mmoja...

Licha ya hivyo, udakari sio ktk kutenda mema bali ni ibada, ni ibada kama kula kunywa na mengine yote ambayo yanampatia uhai binadamu. Ni moja ya nguzo za kujitafutia riziki kama kazi nyingine zozote zilizohalilishwa iwe kubeba zege au umanamba na hakuna uchache wa fedha unaohalalisha ucha Mungu. Na kifupi daktari hawezi kuwa mbora na mcha Mungu kuliko kuli mbeba zege kwa sababu tu daktari anaponya wagonjwa..Je kama kashindwa kumponyesha mgonjwa tutamweka kundi gani?..

Kisha hizi habari za kutohukumu hata sikubaliani nazo kwa sababu dunia nzima na imani zetu za dini tunapokea na kukubali kuwepo kwa mahakama ambao wanatoa hukumu za wahalrfu. Hakuna Mkristu anayeweza nambia dunia hii ingekuwa vipi pasipo kuwepo mahakama na jela ila tusubiri Mungu awahukumu waharifu..Nachoajua mimi na kukiamini ni matumizi ya sheria ya hukumu kama hizi tunazotumia leo kinyume cha hukumu ambazo Mwenyezi Mungu alisisitiza kuzitumia..Ktk imani ya dini sheria zetu hizi zinaitwa kujichukulia sheiria mkononi...Sasa ukiniuliza ni hukumu gani ambazo Mwenyezi Mungu aliziweka? hapo ndipo tunarudi ktk mjadala mkali wa kiimani ambao wewe utaaamini unachoamini na mimi nintaamini nachoamini.

Ila sote kwa pamoja tunafanya makosa makubwa kumhukumu Sheikh Yahya kabla hajafikishwa mbele ya sheria iwe ya kidini au ya kidunia... Na hakika watu wengi humu wametoa verdict ya guilty kwa marehemu hali hata sheria ya kidunia inasema mtuhumiwa huwa Innocent Until proven guilty in THE COURT of LAW..
 
Ame,
Mkuu wangu imani za dini zinatofautiana na hakika sii lazima nifuate dini kuamini jambo fulani..Na pengine nikwambie tu kwamba hata Uislaam haukubaliani na mtazamo wangu kwani bila kuamini Mungu na mitume wake huwezi kuwa mcha Mungu na wala sii rahisi ukatenda mema. Hivyo sikutumia dini yeyote ila mtazamo wangu ktk kuamini kwamba ktk kila jema litendwalo huongozwa na baraka za Mwenyezi Mungu na kila baya huongozwa na Shetani..Haya ya daktari kutaka fedha au kutotana fedha hayahusiani kabisa na ucha Mungu kwa sababu hakuna mahala mwenyezi Mungu amekataza watu kudai malipo zaidi kwa kazi nzuri inayofanywa na mmoja...

Licha ya hivyo, udakari sio ktk kutenda mema bali ni ibada, ni ibada kama kula kunywa na mengine yote ambayo yanampatia uhai binadamu. Ni moja ya nguzo za kujitafutia riziki kama kazi nyingine zozote zilizohalilishwa iwe kubeba zege au umanamba na hakuna uchache wa fedha unaohalalisha ucha Mungu. Na kifupi daktari hawezi kuwa mbora na mcha Mungu kuliko kuli mbeba zege kwa sababu tu daktari anaponya wagonjwa..Je kama kashindwa kumponyesha mgonjwa tutamweka kundi gani?..

Kisha hizi habari za kutohukumu hata sikubaliani nazo kwa sababu dunia nzima na imani zetu za dini tunapokea na kukubali kuwepo kwa mahakama ambao wanatoa hukumu za wahalrfu. Hakuna Mkristu anayeweza nambia dunia hii ingekuwa vipi pasipo kuwepo mahakama na jela ila tusubiri Mungu awahukumu waharifu..Nachoajua mimi na kukiamini ni matumizi ya sheria ya hukumu kama hizi tunazotumia leo kinyume cha hukumu ambazo Mwenyezi Mungu alisisitiza kuzitumia..Ktk imani ya dini sheria zetu hizi zinaitwa kujichukulia sheiria mkononi...Sasa ukiniuliza ni hukumu gani ambazo Mwenyezi Mungu aliziweka? hapo ndipo tunarudi ktk mjadala mkali wa kiimani ambao wewe utaaamini unachoamini na mimi nintaamini nachoamini.

Ila sote kwa pamoja tunafanya makosa makubwa kumhukumu Sheikh Yahya kabla hajafikishwa mbele ya sheria iwe ya kidini au ya kidunia... Na hakika watu wengi humu wametoa verdict ya guilty kwa marehemu hali hata sheria ya kidunia inasema mtuhumiwa huwa Innocent Until proven guilty in THE COURT of LAW..

Respect mkuu Mkandara!

Mine was a reaction to what u said; imani yako mimi siifahamu ila nilihukumu kauli yako in reference to what u said so kama kauli yako inashabihiana na imani yako ama ni tofauti sifahamu maana hata imani yako siifahamu.

Kuhusu kuhukumu simaanishi hukumu ya kidunia na hata hiyo hutolewa baada ya mtu kujitetea so hahukumiwi kwasababu katenda bali kwa kutenda na kwa kuthibitisha kwa neno lake (kiujazacho moyo) mbele ya sheria kama kweli katenda ama laa!

Kuhusu mema this is a very subjective term na hapa hakuna standard ya what is mema ila kama kuna kitu kinachotuongoza kuhusu hayo tunayoyaita mema mfano katiba ama neno la Mungu thru Quran ama Bible ama kitabu kingine cha imani. Kwahiyo kwa mfano kwa Osama ni vyema na nikutenda mema kufanya terorism na kwetu wengine ni jambo baya; sasa niambie hapo nani yuko sahihi na yupi yuko wrong? Nikisema yuko wrong basi na mimi niwe tayari kukubali ni wrong kuwa cast out demons and their urgents wakija kwenye anga zangu maana what is gud to me is bad to those who are in opposite side. Mfano kwenye kabila langu kupiga goti kumsalimia mtu ni kukosa adabu wakati kwa wenzetu wa kanda ya ziwa ndiyo hasa adabu. So linapokuja kuhukumu basi kwa habari ya imani kuhani ni Mungu na mwenye moyo unao hukumiwa na yeye haangalii (Kwa habari ya imani yangu ninayoifahamu zaidi) uliyoyatenda tu bali dhamira ya kilichokupelekea wewe kutenda.

Jambo linaloweza kuwa baya sana machoni mwa wanadamu hilo ndilo la weza kuwa takatifu sana mbele ya Mungu mfano kwenye Biblia Mfalme Sauli alipewa agizo na Mungu kuua waamaleki wote asibakize hata kitu kimoja chenye uhai kikaishi; mfalme akamwonea huruma mfalme wao na kuchagua vile vilivyo vinono na kuvipeleka katika himaya yake. Nabii alipokuja na kumuuliza umetimiza kama alivyosema Mungu? Naye akajibu ndiyo; lakini nabii alsikia sauti ya wanyama ikitokea katika hema yake ndipo alipomuuliza tena kwa msisitizo jee hizi sauti ni za nani; naye mfalme kwa kujua aligundulika akajitetea hao niliwaacha kwasababu niliona watatusaidia katika mahitaji yetu. Kwa logic ya kibinadamu ni kosa kuua na pia kuangamiza kile ambacho waweza kukitumia kama faida; lakini hili lilimsababisha huyo mfalme ku nyang'nywa crown yake; showing wema wetu waweza kuwa uovu mbele za Mungu na infact kwa habari ya ukristo ni kuwa matendo yetu hata kama yawe mema kiasi gani mbele za Mungu ni machafu na yenye kunuka kama dekio la chooni. Inamaana bila roho mtakatifu hakuna awezaye kumpendeza Mungu. Kwamba hii ni sawa ama siyo anajua yeye kwani ndiye kuhani na ndiye mwenye kudai kuwa ni almighty na wewe unaingia katika hiyo hukumu kama standard yako kama una amini hicho; wale wasioamini hatuna hakika vipi wataikwepa hii standard ya hukumu ya almighty na sisi hatuna common values nao so wako out of our group tunaheshimu imani yao.
 
Back
Top Bottom