TANZANIA: Historia ya Taifa Letu na Sheikh Yahya (RIP!)

- Mkuu Bob, sawa sawa sana mimi sasa hivi namuona Sheikh Yahaya RIP Mnajimu representing a hope kwa wananchi wengi wanyonge nje ya the life system tuliyokuwa nayo under siasa za Utawala wa Awamu wa kwanza, infact kune recorded facts kwamba watwala wa wa Awamu ya kwanza hawakumtaka kabisa hapa nchini ndio maana alikuwa akiishi kama mkimbizi Kenya, na alirudi pale tulipobadili siasa zetu, ndio maana ninasema kwamba Nationally he was very influencial in his own way, infact ingekua nchi za wenzetu angeweza hata kuwa a National hero, even though matokeo ya utabiri wake siku zote ulikuwa debatable, lakini huwezi kukataa au ku-igonre his infulencial socially kwa taifa.

William @ NYC, USA.

Hivi kule Kenya hakuwa kikazi zaidi na akizuga kama amefukuzwa? Mbona he played big role in the arrest of people accused of masterminding the failed attempt to ovethrow Nyerere in 1983?
 
poleni sana ..... mmepoteza muda mwingi kumjadili mchawi na ufugaji wa majini...... amepoteza watu wengi... wamejenga umwoga kwa watanzania na imani za kijini.... hope God will punish him for this....!!

- Unajua maongezi ya ufugaji wa majini ni very low kwa sababu you have to know something na hayo mambo haat uweze kuyaongea mimi sijui majini na wala siamini kwamba yapo, ndio maana siwezi kumhukumu bin-adam mwingine na maneno ya majini, I mean duh! Majini tena na Great Thinkers! kweli!

William @ NYC, USA.
 
Hivi kule Kenya hakuwa kikazi zaidi na akizuga kama amefukuzwa? Mbona he played big role in the arrest of people accused of masterminding the failed attempt to ovethrow Nyerere in 1983?

- Historia mara nyingi huandikwa na watawala, sasa inategemea unasoma kitabu kilichoandikwa na wakati wa watawala wa awamu gani!

William @ NYC, USA.
 
- Pole sana Mwalimu, kama kawaida yako ikishaguswa Awamu ya kwanza ni lazima uje na mapovu, nenda kule kwenye facebook yangu uone Balozi wetu mmoja aliyeko nje alivyo-comment kuhusu Sheikh Yahya na Awamu ya kwanza, kwamba walimfukuza kwa sababu angekwua kikwazo kwa siasa za the times! sio mimi mkuu wanajua zaidi ndio wamesema, ameishi maisha yake yote Kenya, mimi nimeshinda sana kwenye banda lake Uwanja wa Maonyesho ya Saba Saba enzi hizo, anatuonyesha Video za Super Mazembe na Mfuweni Lipua Lipua, alikuwa akitokea Kenya, infact he had a Porshe!

- Sasa magazeti ya Kenya yaliyokuwa yakiheshimiwa sana wakati ule yaliwezaje kuweka articles za mwizi na mtapeli, I mean mkuu zile mambo ya Awamu ya kwanza ya zidumu fikra za other imperfect human beings ziliisha sasa tuko huru kufikiri na kuchambua facts!


William @ NYC, USA

Kwamba marehemu sheikh Yahya hakupendwa ktk awamu ya kwanza kwangu mm ni news maana ktk kitabu cha Ludovick Mwijage (The dark side of Nyerere legacy) ameelezewa kama informer wa serikali ya Nyerere. Aliwa-expose kina Mwijage, watu ambao walikuwa wanampinga na hata kufikiria kumpindua nyerere miaka ya mwanzoni mwa 80. Ndo maana mm sikushangaa niliposikia sheikh akitoa utabiri tata kuhusiana na siasa za Tanzania.

Halafu ndugu Malecela, nimenusa kama una "unsettled score" na mwalimu nyerere.. Vp unahusiana na ambitions za urais za baba? Samahani, labda naota ndoto za mchana...
 
Kaka William, hivi ile bulga ya USAID ndio Oatmeal ?

- Well, almost the same isipokuwa tofauti ni kwamba ile ilikuwa soft sana, as opposed na otameal ya sasa ingawa pia inategemea na upishi maana sisi kule bongo shuleni, ilikuwa inapikwa hasa kwenye majiko ya kuni na inakorogwa sana, I mean I miss it! Kwa wale ambao hawakusoma enzi hizo poleni sana mlikosa mengi sana muhimu ya historia ya taifa letu!

William @ NYC, USA.
 
Kwamba marehemu sheikh Yahya hakupendwa ktk awamu ya kwanza kwangu mm ni news maana ktk kitabu cha Ludovick Mwijage (The dark side of Nyerere legacy) ameelezewa kama informer wa serikali ya Nyerere. Aliwa-expose kina Mwijage, watu ambao walikuwa wanampinga na hata kufikiria kumpindua nyerere miaka ya mwanzoni mwa 80. Ndo maana mm sikushangaa niliposikia sheikh akitoa utabiri tata kuhusiana na siasa za Tanzania.

Halafu ndugu Malecela, nimenusa kama una "unsettled score" na mwalimu nyerere.. Vp unahusiana na ambitions za urais za baba? Samahani, labda naota ndoto za mchana...

- Unajua ni kawaida kwa mtu kama nikitoa maoni yangu on anything kwamba lazima iwe inahusu wazazi depending na who is listening, so siku zote nina a choice to make of either kutoa maoni kama wananchi wengine wote wa taifa hili walio huru kama mimi, au kuogopa hukumu za wasioyataka na kufyata mkia, not so sorry mkuu, I choose to speak my mind on any issue and let the chips fall where they may!

William @ NYC, USA.
 
Mi najua huyu bwana SHEIKH YAHAYA alikuwa mganga wa kienyeji na mchawi,ikiwezekana maiti yake wangeitupa baharini kama OSAMA BIN LADEN
 
Kumbukumbu pekee inayoijua mpaka leo kuhusu huyu bwana ni utabiri wake wa mwaka 1984 kama sikosei baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan akasema kuwa Tanzania nzima aliyefunga ni mtu mmoja tu tena ni mtoto wa chini ya miaka 18. Yaani waliokuwa wakifunga wote walikuwa wakishinda na njaa na yeye pia Lol!, ila alifanikiwa sana kuwaandaa watanzania kisaikolojia pale serikali ipodhamiria kufanya mambo makubwa ya kushitusha.

RIP, Sheikh Yahya. Mwenyezi mungu akuweke panapokustahili.
 
- Unajua maongezi ya ufugaji wa majini ni very low kwa sababu you have to know something na hayo mambo haat uweze kuyaongea mimi sijui majini na wala siamini kwamba yapo, ndio maana siwezi kumhukumu bin-adam mwingine na maneno ya majini, I mean duh! Majini tena na Great Thinkers! kweli!

William @ NYC, USA.

Teh ajabu waafrika tunaweza kuogopa kuzungumiza majini lakini tusiogope kuzungumzia UFOs kumbe inaweza kuwa kitu kile kile just bcs kimoja ni cha mzungu kingine cha mwafrika.

Nadhani imefika wakati zifanyike tafiti za kitaalamu za haya mambo ya uchawi na majini waafrika tunaweza kunufaika........


May be Officialy we can have a Tanzanian made Aircraft wich does not need na expensive Airport to land or take off
 
Mi najua huyu bwana SHEIKH YAHAYA alikuwa mganga wa kienyeji na mchawi,ikiwezekana maiti yake wangeitupa baharini kama OSAMA BIN LADEN
Mkuu,pamoja tupo nyakati nyingine lakini ni vema kuheshimu tamaduni zetu za kuheshimiana.Sheikh tulimjadili mara nyingi huko nyuma akiwa hai kwa sasa hasira hazitusaidii tena.tuwe na staha maana ana familia ambayo haijakukosea na watasoma maandiko kama haya na kuwaongezea uchungu.leteni mazuri yake kwa wanaofahamu ili tujifunze.
 
pumba tupu....
kutaka tu kumkweza sheikh yahaya kuwa alikuwa significant kwa watanzania...
labda kwako na wale wanaoamini mapete yake...majority ya watanzania he was nothing but mchawi!!!!!
 
- Wanaume tumeumbwa kutafuta maisha, huko kote nilikuwa natafuta maisha, nikaishia kuyapata hapa New york City, ambako nimeishi since 1987 na toka 1988 ninafanya kazi kwenye kampuni moja mpaka leo, nikitoka hapa ninarudi bongo home Kinyerezi kwenye kibanda changu nilichojenga kwa jasho langu, so angalia tena maneno yako kama yako sawa, samahani kwa kutoka nje ya mada ila ni vyem kurekebishana mtu anapokuwa hajui anachosema!

William @ NYC, USA.

Kwanza nafurahi kwa mmoja wa agent wa Ibilisi kuondoka, alivuta na kupotosha watu wengi kwa shughuli zake za kupiga lamli na kutumia majini! Kama mjumbe wa shetani kafa nimefurahi, je siku nikisikia shetani mwenyewe kafa si furaha yangu itapidukia?

Pili, kwa jinsi unavyoelekea, siku ukirudi nyumbani utataka ugombee ubunge! ndugu dizaini ya kina-Lau Masha kwa sasa hawana nafasi tena. Tumeshuhudia watu mliokaa nje ya nchi kwa muda mrefu, mnapoteza uzalendo na mnakuwa mnajipendekeza kwa wakubwa waliowaweka bila kujali matatizo ya wananchi! Kaa hukohuko, huku tunajitosheleza kwani kuna vijana wengi tu wenye uchungu na Taifa lao!
 
Wakuu wote JF, heshima mbele sana:-

- Kifo cha Sheikh Yahaya jana, kimetushitua wananchi wengi sana hasa wale tuliomzoea toka enzi za Utawala wa Awamu Ya Kwanza, I mean you wanted to ignore the guy lakini he was all over the map coming from Kenya, enzi hizo kwenye mabazeti ya Taifa na Baraza, ambayo kuwa nayo Tanzania ilikuwa ni very luxurious.

- Ninakumbuka ukiyaona hayo magazeti, hasa kwa kuomba kwa waliokuwa nayo, the first thing you wanted ilikuwa ni kukimbilia kwenye ukurasa wa Nyota na Utabiri wa Sheikh Yahaya, as opposed na miaka ya karibuni na hadi kuelekea kutangulia kwake kwenye haki.

- Ni muhimu wana-hisstoria wa taifa hili wakampa nafasi Marehemu, of his role either positive au negative katika maisha ya wananchi hasa enzi za Cold War: Je Historia imuhukumu vipi ndugu zangu?


William @ NYC, USA.
Ni kweli Marehemu alikuwa mtu mwenye umaharufu wake, si enzi ya awamu ya kwanza tu, ila awamu zote za Urais wa nchi hii.

Kusema kweli kwa habari ambazo mimi nazijuwa, Mrehemu Yahaya Hussein, si kuwa alikuwa mtabiri tu, aliyekuwa na sifa mbali mbali ndani na nje ya nchi ya Tanzania, pia alikuwa ni mfanyakazi wa serikali, ukipenda unaweza kumuita shushu.

Uko Kenya ambako alikwenda, si kwa ajili ya mambo ya utabiri peke yake, bali ilikuwa ni mbinu mojawapo ya yeye kuweza kufunguliwa ofisi ili haweze kufanyakazi ya ushushu bila ya kushtukiwa, na uku akiwa kwenye undercover ya utabiri. Nadhani Kenya walipopata hizo tetesi ndio ikawa sababu ya yeye kuondolewa uko.

Kuhusu kazi yake ya Utabiri, kuna watu wenye kumuunga mkono kuwa alichokuwa anakifanya ni sawa na kuna wale ambao kina sisi, tunajuwa kuwa alichokuwa akikifanya si katika imani ya Uislam.

Uislam unapinga ilo jambo kwa nguvu zote.

Uislam unatufahamisha kuwa Mtabiri wa nyota, kusoma viganja vya watu vya mikono na kuwaeleza hivyo wanavyosema ameona, huyu mtu ana tofauti na mpiga ramri.

Na hii ni tofauti na zile tabiri za hali ya hewa ambazo watu wengi wenye kushabikia utabiri wa kinyota, ufananisha nazo.

Watu wengi wameshindwa kutofautisha dini yake na kazi yake ya utabiri, na wachache wnafikiria ndio Uislam unafundisha hayo mambo, na wapo wengine wakamuhusisha na mambo ya majini.

Uislam upo wazi kabisa, wla haujaficha kitu...! Kinachobakia ni mtu, mwenyewe kuchagua wapi pa kukamata.

Tunasoma kwenye Qur'an:
“Enyi Mlioamini! Bila shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli ni uchafu katika kazi za shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa”
Al-Maaida: 90

Na vile vile Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza jambo hilo, hivyo inatakiwa tujiweke kando kabisa.

Mambo yote haya ni haramu na yeyote mwenye kuamini kuwa jambo fulani limetokea kwa sababu ya nyota kadhaa na kadhaa amemkanusha Mwenyezi Mungu kama Alivyosema katika Hadiyth ifuatayo:

Yeyote atakayejimai (kufanya kitendo cha ndoa) na mwanamke mwenye hedhi, au kwa kutumia njia ya nyuma, au kumkaribia mtabiri na kuamini aliyoambiwa, basi amekufuru yale aliyoteremshiwa Muhammad.
[Hadiyth Sahiyh imesimuliwa na AsWhabus-Sunnan na wengineo]

Na kufanya hivyo ni humpeleka mtu kuingia katika shirk. Na Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) humghufuria mtu dhambi zote ila shirk kama Alivyosema:

"Hakika Mwenyezi Mungu Hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa"
An-Nisaa: 48

Tunachotakiwa sisi wengine ni kuangalia kile ambacho tunakiona kinafaa na kuyawacha yale ambayo si katika Uislam.

Na hakuna miongoni mwetu, mwenye kujua kama Marehemu aliomba Toba kwa Mola wake kabla ajafariki au lah au aliwacha madhambi yote na kujuta kwa kila dhambi aliyoifanya, pamoja na kuwa na azma ya kutorudia tena kutenda dhambi hiyo. Hapo ni yeye na Mungu wake ndio wenye kujua na si sisi.


"Al-Ladhīna 'Idhā 'Aşābat' hum Muşībatun Qālū 'Innā Lillāhi Wa 'Innā 'Ilayhi Rāji`ūna".
Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.
Baqarah: 156
 
Kwanza nafurahi kwa mmoja wa agent wa Ibilisi kuondoka, alivuta na kupotosha watu wengi kwa shughuli zake za kupiga lamli na kutumia majini! Kama mjumbe wa shetani kafa nimefurahi, je siku nikisikia shetani mwenyewe kafa si furaha yangu itapidukia?

Pili, kwa jinsi unavyoelekea, siku ukirudi nyumbani utataka ugombee ubunge! ndugu dizaini ya kina-Lau Masha kwa sasa hawana nafasi tena. Tumeshuhudia watu mliokaa nje ya nchi kwa muda mrefu, mnapoteza uzalendo na mnakuwa mnajipendekeza kwa wakubwa waliowaweka bila kujali matatizo ya wananchi! Kaa hukohuko, huku tunajitosheleza kwani kuna vijana wengi tu wenye uchungu na Taifa lao!

- Ha! ha! ha! ha! yaani JF ndio wanatoa ubunge? Yale yale! wakiwa na mawazo tofauti na yako basi wanatafuta ubunge JF1 ha! ha! ha!

Es!
 
pumba tupu....
kutaka tu kumkweza sheikh yahaya kuwa alikuwa significant kwa watanzania...
labda kwako na wale wanaoamini mapete yake...majority ya watanzania he was nothing but mchawi!!!!!

Hahah watu wana hasira. So kwamba naunga mkono Tiba zake but kama ni uchawi basi alikuwa mchawi developed mpaka anarusha na kuonyesha ujuzi wake kwenye TV na radio.

Kuna mwingine yule dogo alikuwa anaitwa dr Manyau nyau. sijui yuko wapi siku hizi. Kweli haya mambo yanahitaji kufanyiwa reseach sio kuhukumu tu. Sasa mtu kama Dr manyau nyau alikuwa anakubali kufutanana camera za TV akifanya vitu vyake bila kificho.

Aiseee nilishngaa sana. Hata kwenye uchawi au kwa mchawi Kuna vitu unaweza kujifunza na kurekebisha au kuviondoa kabisa kwenye jamii.

We should not be afraid kuogelea some of our culture, belief na taboos .
 
- Wanaume tumeumbwa kutafuta maisha, huko kote nilikuwa natafuta maisha, nikaishia kuyapata hapa New york City, ambako nimeishi since 1987 na toka 1988 ninafanya kazi kwenye kampuni moja mpaka leo, nikitoka hapa ninarudi bongo home Kinyerezi kwenye kibanda changu nilichojenga kwa jasho langu, so angalia tena maneno yako kama yako sawa, samahani kwa kutoka nje ya mada ila ni vyem kurekebishana mtu anapokuwa hajui anachosema!

William @ NYC, USA.

Ndugu Malecele sikuteleza ulimi ila niko wazi na unielewe hivyo. Nimefurahi ulivyotetea hoja hiyo kwenye maandishi mekundu hayo ndiyo tunayotaka, maana jasho lako lina thamani zaidi kuliko urithi. Pia maisha si kama hesabu za computation tu, mtu anatakiwa kuwa tayari kwa challenge ambayo ndiyo kihunzi ukikivuka ujue tayari uko ng'ambo ya daraja.
 
Kaka William, hivi ile bulga ya USAID ndio Oatmeal ?

Nilipoona mara ya kwanza nilifikiri Oatmeal ndiyo ile tuliyokuwa tunapata lunch tuliyozoea kuiita bulga, lakini kwa uchunguzi zaidi ni tofauti maana Oatmeal maji moto yanatosha kuchanganya mkoroga na mlo umekamilika, lakini ile bulga ilihitajika kupikwa kweli kweli kwa wenye miraba minne kuchochea kuni. Na ukila mtu wajisikia umetulia class room ya extended, upper primary, na hata kule secondary level education.

Unimekumbusha niwapate hawa wa USAID niwaulizie ile kitu iko wapi, maana wanafunzi na wanachuo wa siku hizi wakiipata ile hata maandamano yatatoweka.
 
Back
Top Bottom