Tanga: Ajali ya Fuso yaua sita wilayani Lushoto, wengine wajeruhiwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Watu sita wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 239 AFB walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kutumbukia kwenye korongo katika eneo la barabara ya Soni/Mombo wilayani Lushoto mkoani Tanga.

RPC wa Tanga, Safia Jongo amesema ajali hiyo imetokea asubuhi ya leo Jumanne Machi 29, 2022.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto na majeruhi wapo Hospitalini hapo wakiendelea kupata matibabu.

RPC Jongo ametoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya moto mkoani humo kuendelea kufuata sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.

fuso1.JPG


Chanzo: MillardAyo
 
Mwenyezi Mungu sidhani anahusika, accident ni kosa la mtu!,barabara zetu ni mbovu mno, magari yetu lini yalifanyiwa proper roadworthy?major service?,tusimlaumu Mwenyezi Mungu
 
Ajali zimefunguliwa na mama hana cha kufanya maana hataki kuwasema wahusika watakasirika na watamjibu.
Kwa sasa kuna sehemu kuna shida hali ilipofikia lazima mama afanye mabadiriko tu kwenye jeshi la polisi, na kupewa majukumu upya kwa kila RTO.

Akiteua IGP, mpya akampa majukumu mapya tunaweza kuona mabadiriko!

Leo namsikia kamanda anashangaa eti inakuwaje lori linabeba container bila kufunga lock?!! wakati nenda kurasini pale kila leo makontena yanadondoka barabarani na ni hapa mjini!
 
Polisi wenyewe ndio wanaongoza kwa kuendesha ovyo.

Mnamkumbuka mwaka Jana wilaya ya Handeni huko huko Tanga, gari la policcm liligongana na lorry la TJL Kisha mabasi ya polisi zaidi ya manne yakaenda kuligonga lile Lori la polisi lililopata ajali.

Wake policcm hawakuchukuliwa hatua yoyote badala yake tuliona wakuu wao wa kazi wakiwatetea.

Halafu unakuja kuona RPC anatoa wito watu wawe waangalifu. Lini policcm watajua kwamba CHARITY BEGINS AT HOME?

Hilo Lori limeoita Soni, pale Soni pana trafik, ameona kabisa watu wamepanda Lori badala ya Basi, badala ya kuwashusha wapande magari ya abiria si ajabu amechujua rushwa ya elfu mbili na kuliachia Lori libebe abiria.

Mimi ningekua rpc tanga ningeanza na trafik wa Soni.

Lkn itakua business as usual. Trafik akipangiwa kituo anapewa hesabu ya kupeleka kwa wakubwa. Kwani Nani asiyejua......?
 
Watu sita wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 239 AFB walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kutumbukia kwenye korongo katika eneo la barabara ya Soni/Mombo wilayani Lushoto mkoani Tanga.

RPC wa Tanga, Safia Jongo amesema ajali hiyo imetokea asubuhi ya leo Jumanne Machi 29, 2022.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto na majeruhi wapo Hospitalini hapo wakiendelea kupata matibabu.

RPC Jongo ametoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya moto mkoani humo kuendelea kufuata sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.

View attachment 2168006

Chanzo: MillardAyo
Hivi madereva siku hizi wanavita bangi na kulewa kabla ya kuendesha magari au?

Ndani ya mwezi huu itakuwa takribani watu 50 wamefariki kwa mambo ya ajali.
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya nyumba ambayo baba/mama anamtegemea Mungu na nyumba ambayo baba/mama asiyemtegemea Mungu
 
Back
Top Bottom