Wanne Wafariki dunia, Sita Wajeruhia ajali ya Noah Handeni

Kikwajuni One

JF-Expert Member
Mar 18, 2013
13,142
6,947
20230929165624_835396986_8815267908605915839_640_321_85_webp.webp


Watu wanne wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya BM Coach kugongana na Toyota Noah katika eneo la Manga Wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jioni ya leo Ijumaa, Septemba 29, 2023 na kusema ilihusisha Noah na basi la Kampuni ya BM Coach ambalo lilikuwa likitokea Barabara ya Segera.

"… Kweli imetokea ajali watu wanne wamefariki dunia na wengine sita wamejeruhiwa katika eneo la Manga wilayani Handeni," amesema Kamanda Mchunguzi.

Mganga Mfawidhi Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya Handeni, Abdulmajid Makoye amekiri kupokea miili ya marehemu hao pamoja na majeruhi wengine sita ambao kutokana na majeruhi yao walisafirishwa.

Amewataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Amina Zuberi (50) mkazi wa Lushoto, Badru Hinda (4) na Nicolaus Mahimu (32) wa Dar es Salam, Joseph Joachim (39), Mariam Hamis (23) mkazi wa Kwamsisi na majeruhi wa mwisho ni Mwinjuma Hemed (23) mkazi wa Kabuku.

"Katika watu waliofariki wapo watoto wawili, mmoja wa miezi 9 na mwingine miaka mitatu ambapo mmoja amefia hapa hapa hospitali na mwingine amefia kwenye ajali pamoja na wanaume wengine wawili," amesema
 
Uandishi habari wa kitanzania unazidi ku advance yani hata chanzo cha ajali hakitajwi na habari inachapishwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom