TANESCO kuachana na Symbion na Aggreko?

Ukiamua kutumia akili yako na kuandika kutoka moyoni mwako unaandika yaliyojaa busara na hekima tele, lakini ukiamua kuunga tela la wale Buku 7 basi ni utata mtupu!!!

Huyu FaizaFoxy nitamkaribisha siku yoyote ile nyumbani kwangu aje tule mahanjumati tuongee na kucheka kuhusu mambo mbali mbali ya kuhusu nchi yetu na dunia nzima. Akinialika kwake huyu basi nitafanya kila niwezalo nikanywe hata chai na vitumbua kama siyo pilau la nguvu la binti wa Kariakoo.

Hongera zako na ujue kwamba FaizaFoxy huyu ni kipenzi cha wengi hapa jamvini.

Nakutakia weekend njema


Ikiwa waliisaini na mpaka ifikapo October 2014 itakuwa bado ni mikataba hai, hapo tutajiingiza katika gogoro lingine kama lile tililojiingiza na Dowans ya Al Adawi. Mpaka leo tunalipa kwa gharama kubwa sana, kwa kujidai kwetu kutaka kuvunja mkataba wa Kimataifa. Tutawalipa tu.

Lakini ikiwa mpaka ifikapo hapo October 2014 tutakuwa tumemaliza nao mkataba basi itakuwa ni sawa na hatuna lawama.

Ikumbukwe kuwa mikataba ya Aggreko na Symbion ni mikataba ya dharura mpaka pale tutakapoweza kujikimu na umeme wa uhakika. Kuna miradi mingi ya muda mrefu ambayo inatekelezwa kwa sasa. hakuna sababu kwanini tuendelee na mikataba ya dharura pale tutapokuwa tunajiweza wenyewe.

Isitoshe, ni rahisi sana kwa Symbion na Aggrekko kutuuzia mitambo yao kwa bei nafuu pale tutapokuwa tunajiweza kwa umeme wa uhakika na hiyo mi jenereta yao ikabaki kwetu kwa dharura tu, kwani mpaka wakati huo watakuwa wamesharudisha fedha zao na mifaida kibao.

Waafrika tuone hivi hivi tunajuwa sana kuongea, kupanga na kupangua lakini hatujuwi kutekeleza. Leo mchukuwe Mtanzania yeyote umuulize kuhusu ligi ya mpira wa Uingereza, basi utamkuta anaijuwa hiyo ligi na namna timu inatakiwa iwe kuliko Mourinho. Hiyo si kwenye mpira tu, ni kila pahali, tunajuwa kila kitu kwa midomo yetu lakini kutenda? Ng'oo.

Nchi hii muumba dunia na ardhi alitujaaalia kila kitu chema, maji mengi, madini mengi, ardhi nzuri inayo-limika miezi 12 kwa mwaka, misitu mizuri, mbuga nzuri, milima mizuri, mabonde mazuri, watu wazuri, wanyama wazuri. Kwa ufupi katupa pepo ya duniani, lakini kitu kimoja hatukupewa, nacho ni akili. Akili hatuna.

Binaadam hakosi kasoro na kasoro yetu ni akili.

Wakati sisi tutaanza kuwa na umeme wa uhakika (miaka 50-100 ijayo), kumbuka kuwa mpaka sasa ni 14% tu ya Watanzania wenye umeme tena sio wa uhakika, wenzetu watakuwa hawana haja ya maviwanda ya umeme, majumba na maviwanda yanayohitaji umeme yatakuwa yanajizalishia yenyewe umeme (haya yameshaanza kwa wenzetu, kuna majumba mapya huko yanajizalishia yenyewe umeme na ule wa ziada wanawauzia gridi zao) Hapo sasa.

Self-sufficient Urban Buildings | BETTER WORLD // ENGINEERING

Sosoljip is a Self-Sufficient Net Zero Energy House in South Korea | Inhabitat - Sustainable Design Innovation, Eco Architecture, Green Building

MenoMenoPiu Unveils Plans for Wind-Powered Alvar Aalto Campus Otaniemi | Inhabitat - Sustainable Design Innovation, Eco Architecture, Green Building
 
Mawazo kama haya kutoka kwa wenye nchi ni mfano mzuri kuwa tatizo lipo kwa hao hao wenye nchi.

Si juzi tuu mlivunja mkataba na Dowans? Humjamaliza hata kuwalipa kumbe tayari ulishaingia kwenye mikataba mingine ambayo unataka kuivunja tena.



Kama ni nafuu kwa nini mlikuwa hamtaki kuilipa Dowans? You think it is just simple like that kuvunja mikataba eh?

Juzi hapa tuu uliambiwa kuwa kama huwezi kumudu gharama za umeme ni vema ukaamua kuwasha kibatari au ukae gizani halafu bado unatarajia mikataba hiyo ivunjwe?



Sasa ukivunja hivyo mikataba ndiyo umeme utapatikana? Ndiyo watu wataacha kulamba hiyo 86 per cent?

Unless you address the root cause of the problem hata kama ukivunja hiyo mikataba bado wataendelea kulamba hizo per cent.

Hili tatizo halikuanza baada ya kuingia kwenye mikataba na hayo makampuni.

Sasa mbona umenichambua kama vile unamjibu Prof. Muhongo?
Mfuate ofisini kwake umpe majibu haya!
 
Tunaomba ushahidi wa hilo, isiwe wewe ndio unatupa takwimu hewa.

FaizaFoxy, nahisi utakuwa umesoma shule za kata! Nimetumia mahesabu ya kitakwimu kwa akubalisha ujumbe wa Invisible! Msome hapo chini!

Wakiweza kuvunja hii mikataba tutafungua ukurasa mpya, lakini wasiwasi wangu ni kama tunao mbadala wa makampuni haya ambayo kiukweli yanatia hasara kubwa sana japo yanasaidia.

Kumbuka, ni mwaka jana tu tuliambiwa kuwa TANSECO wanailipa kila siku Symbion Power milioni 152 na katika kila sh.100 zinzoingia TANESCO, sh.86 inaelekwzwa kwenye malipo hayo!
 
Tunaomba ushahidi wa hilo, isiwe wewe ndio unatupa takwimu hewa.

Hata kama kama wakimiliki hayo majenereta na kununua gesi ya kuzalishia umeme wao wenyewe bado utakuwa haujatatua the underlying problem.

Sana sana itakuwa ni sawa na kubadilisha Division 0 kuwa Division 5 ili uweze kumiliki cheti.

Wewe unadhani tatizo liko wapi?
 
Haya ndiyo mambo ya msingi ya kujadili.. Invisible EMT BAK my sis FaizaFoxy nae kavua gamba..Safi..Ifike sehemu tuseme inatosha..

Ningependekeza Tanesco wanunue hiyo mitambo baada ya kumaliza mkataba..Ila kuvunja mkataba hapana..Tunaweza kuingia kwenye matatizo zaidi..
 
Last edited by a moderator:
Panya anakawaida ya Kula na kupuliza HIYO mipango ya kuvunja mikataba ni uongo na kupuliza maumivu ya ongezeko la umeme tuu. Wasomi gani wanaleta changamoto bila mbadala wake, yaani umeme uwe bei juu huku unataka kuvunja mikataba inayokulazimu kupandisha HIYO bei? Na majigambo ya gesi kupunguza gharama za umeme yameyeyuka tena..??
 
Ukoloni wa kiuchumi unaweza kuwa hatari kwa mustakabali wa jamii kuliko hata ukoloni wa kisiasa. Mikataba yote hiyo ni muendelezo wa ukoloni wa kiuchumi unaotokana na ujuha wa waliopewa dhamana ya kuongoza unaowafanya kuwa mawakala!
 
Kwani biashara ya utumwa ilikuwa na mkataba kwamba kuna siku ingekuja kukoma? Ukoloni ulikuwa na mikataba kwamba ungeisha miaka ya 1960s?

Ni uamuzi tu. Gharama za kuvunja mikataba ni nafuu kuliko kuendelea kuteseka hivi!

Fikiria nchi haina umeme, lakini katika kila 100% ya mapato, wamiliki wa mikataba hewa wanalamba 86%.

Nani alikudanganya kuwa biashara ya Utumwa imeisha? jisomee hapa kuhusu utumwa uliopo leo hii duniani, kuna watumwa wengi leo hii duniani kuliko wakati mwingine wowote ule: https://www.freetheslaves.net/sslpage.aspx?pid=301

Pia usijidanganye kuwa ukoloni umeisha, wazungu walitu-koloni kimadaraka lakini leo hii wanatu-koloni ki uchumi, kiteknolijia na kimabavu. Unakumbuka maneno ya George Bush Jr.? "You're either with us or you are against us". Kama sio kutu-koloni kimabavu ni nini?

"Damned if you do damned if you don't".
 
Haya ndiyo mambo ya msingi ya kujadili.. Invisible EMT BAK my sis FaizaFoxy nae kavua gamba..Safi..Ifike sehemu tuseme inatosha..

Ningependekeza Tanesco wanunue hiyo mitambo baada ya kumaliza mkataba..Ila kuvunja mkataba hapana..Tunaweza kuingia kwenye matatizo zaidi..

Wachana na FaizaFoxy jibu hoja zake. Hapa zinaongelewa facts, tunajikumbusha enzi zetu za Jambo Forums tukijibizana kwa hoja bila kujali nani gamba nani gwanda. Kama mjadala unakushinda bila kuleta ufataani wako ni bora uwe msomaji tu.
 
Wewe unadhani tatizo liko wapi?

Tatizo ni kuwa na shirika la umma lenye kumiliki na kuendesha biashara kubwa kuliko zote Tanzania ambalo linaendeshwa na watu wasio na uchungu na hiyo biashara wala hawajui umuhimu wa hiyo biashara wala hawana ujuzi wa biashara zaidi ya kusoma madarasani.

Ni wakati muafaka Shirika hili nalo likawa la watu binafsi wenye uchungu, ujuzi na wanaojuwa umuhimu wa biashara.

Niliwahi kupendekeza miaka iliyopita, shirika hili libinafsishwe na wauziwe matajiri, kipaumbele wapewe matajiri wa Kitanzania, nilipendekeza hisa kubwa apewe SS Bakhressa na apewe kuliendesha, ambae ana CV nzuri ya kuendesha biashara kubwa kubwa na zinazokuwa kila kukicha. uone jinsi shirika litavyobadilika ndani ya miezi 6 tu na umeme utavyokuwa ni kitu cha ajabu kutokuwepo.
 
FaizaFoxy, nahisi utakuwa umesoma shule za kata! Nimetumia mahesabu ya kitakwimu kwa akubalisha ujumbe wa Invisible! Msome hapo chini!

Iwe za kata au za mtungi. Bado hujaleta ushahidi wa uyasemayo, hayaingii akilini. Invisible ameandika kitu tofauti na wewe umekibadilisha maana, sijui kwa faida ya nani? ya kujiridhisha au kujidanganya nafsi yako?

Pia hapo juu nimekuwekea ushahidi wa kukujulisha kuwa utumwa upo leo hii na haujaisha kama unavyojidanganya tena ndio umeshamiri na ukoloni pia upo leo hii na hauna ubavu wa kuuondoa.
 
Shida sio TANESCO .... ni siasa kuingilia TANESCO ... hii imetokea kwenye maeneo mengi tu hasa awamu hii ya nne ...sio TANESCO tu,...elimu, TANROADS, etc

Awamu ya nne ilirithi uongozi wakati nchi ikiwa kizani totoroo. Umesahau? au ulikuwa na miaka 7 wakati huo?

Bora hii awamu ya nne leo hii tunaona mikataba ya miradi mikubwa mikubwa ya umeme kuliko wakati wowote ule. Na hilo halipingiki, ukipinga tu, nakuwekea ushahidi humu.

TANESCO ni kama mashirika yote ya umma yalioshindwa kujiendesha na rasilmali wanazo. Libinafsishwe tu au lifanywe kama ilivyofanywa TTCL, lipo kama halipo, lijiendesha lenyewe kifaida au lijifie na huku mashirika binafsi yawekeze kwenye, utafiti, ufuaji, usafirishaji, usambazaji na uuzaji umeme. Uone baada ya miezi 6 tu. Utashangaa.
 
Nani alikudanganya kuwa biashara ya Utumwa imeisha? jisomee hapa kuhusu utumwa uliopo leo hii duniani, kuna watumwa wengi leo hii duniani kuliko wakati mwingine wowote ule: https://www.freetheslaves.net/sslpage.aspx?pid=301

Pia usijidanganye kuwa ukoloni umeisha, wazungu walitu-koloni kimadaraka lakini leo hii wanatu-koloni ki uchumi, kiteknolijia na kimabavu. Unakumbuka maneno ya George Bush Jr.? "You're either with us or you are against us". Kama sio kutu-koloni kimabavu ni nini?

"Damned if you do damned if you don't".

Iwe za kata au za mtungi. Bado hujaleta ushahidi wa uyasemayo, hayaingii akilini. Invisible ameandika kitu tofauti na wewe umekibadilisha maana, sijui kwa faida ya nani? ya kujiridhisha au kujidanganya nafsi yako?

Pia hapo juu nimekuwekea ushahidi wa kukujulisha kuwa utumwa upo leo hii na haujaisha kama unavyojidanganya tena ndio umeshamiri na ukoloni pia upo leo hii na hauna ubavu wa kuuondoa.

Shukran!
 
Hata kama kama wakimiliki hayo majenereta na kununua gesi ya kuzalishia umeme wao wenyewe bado utakuwa haujatatua the underlying problem.

Sana sana itakuwa ni sawa na kubadilisha Division 0 kuwa Division 5 ili uweze kumiliki cheti.
Tatizo nini nini na wafanye nini?
 
Invisible

Tatizo sio Tanesco kama Tanesco, tatizo ni that web which surrounds tanesco deeds kwasababu ya political na mega corruptions penetration which has already been institutionalized
 
Inadaiwa Bodi ya wakurugenzi ya TANESCO imepania kuachana na Mikataba ambayo inaonekana kuwa mzigo kwa shirika kati yake na Makampuni ya Symbion Power na Aggreko mwezi Oktoba 2014, kutokana gharama kubwa zisizoshikika toka kwa Makampuni haya.

Nini hatma ya TANESCO?

Tunao mbadala wa makampuni haya?

Tutarajie mgao mkubwa kuelekea 2015?

Tumepata uhakika baada ya kupatikana kwa gesi?

mitambo ya kuzalishia umeme kutoka gesi yenye kutosheleza mahitaji yetu itanunuliwa lini au tunaendekeza zimamoto?
 
Inadaiwa Bodi ya wakurugenzi ya TANESCO imepania kuachana na Mikataba ambayo inaonekana kuwa mzigo kwa shirika kati yake na Makampuni ya Symbion Power na Aggreko mwezi Oktoba 2014, kutokana gharama kubwa zisizoshikika toka kwa Makampuni haya.

Nini hatma ya TANESCO?

Tunao mbadala wa makampuni haya?

Tutarajie mgao mkubwa kuelekea 2015?

Tumepata uhakika baada ya kupatikana kwa gesi?
Inawezekana bodi ya wakurugenzi imepanga hivyo, kwa kuwa inatarajiwa, hadi kipindi hicho, lile bomba kubwa la gesi, linalotandazwa toka Mtwara, litakuwa limekamilika.

Kwa maana hiyo, hatutakuwa na haja sana ya kutumia mitambo hiyo ya kukodi, ya design ya akina Symbion na Aggreko, kwa kuwa pale Ubungo na Kinyerezi, kunatarajiwa kufungwa mitambo ya kuzalisha umeme, kwa kutumia gesi hiyo, mitambo ambayo itakuwa, kwa asilimia 100, inamilikiwa na serikali yetu.

Lakini bado tatizo litakuwa, hiyo mitambo ya Symbion na Aggreko na akina IPTL, wenye hisa wengi, ni vigogo wetu wa serikali yetu ya CCM.

Si mnakumbuka, wakati wa skandali ya Richmond, ambayo baadaye ilijigeuza jina na kujiita Dowans, na hivi sasa, ndiyo inayotambulika kama Symbion, namna kampuni hiyo ilivyokuwa ikitukamua, kupitia kodi tunazolipa watz, ambapo, kila siku, TANESCO walikuwa wakiwalipa Richmond, shilingi milioni 150 kwa siku, hata kama siku hiyo, matambo huo, haujazalisha hata uniti moja ya kuwauzia TANESCO!!

Vile vile, si tunakumbuka, jinsi Tume ya Mwakyembe, ilivyofichua kuwa wamiliki wenye hisa nyingi kwenye mtambo huo wa Richmond, ni vigogo wazito, akiwemo RA na mzee wa mamvi?!!

Kwa hiyo itabidi TANESCO ifanye kazi ya ziada, kama kweli wanataka kweli kuachana na mikatamba ya mitambo hiyo, ya dharura,ya akina Symbion na wenzake, kwa kuwa upo uwezekano mkubwa, pesa hizo zinazopatikana kwenye mitambo hiyo, upo uwezekano mkubwa, ndizo zitakazotumika, kwenye kampeni ya urais, kwenye uchaguzi wa mwaka 2015!!
 
Ikiwa waliisaini na mpaka ifikapo October 2014 itakuwa bado ni mikataba hai, hapo tutajiingiza katika gogoro lingine kama lile tililojiingiza na Dowans ya Al Adawi. Mpaka leo tunalipa kwa gharama kubwa sana, kwa kujidai kwetu kutaka kuvunja mkataba wa Kimataifa. Tutawalipa tu.

Lakini ikiwa mpaka ifikapo hapo October 2014 tutakuwa tumemaliza nao mkataba basi itakuwa ni sawa na hatuna lawama.

Ikumbukwe kuwa mikataba ya Aggreko na Symbion ni mikataba ya dharura mpaka pale tutakapoweza kujikimu na umeme wa uhakika. Kuna miradi mingi ya muda mrefu ambayo inatekelezwa kwa sasa. hakuna sababu kwanini tuendelee na mikataba ya dharura pale tutapokuwa tunajiweza wenyewe.

Isitoshe, ni rahisi sana kwa Symbion na Aggrekko kutuuzia mitambo yao kwa bei nafuu pale tutapokuwa tunajiweza kwa umeme wa uhakika na hiyo mi jenereta yao ikabaki kwetu kwa dharura tu, kwani mpaka wakati huo watakuwa wamesharudisha fedha zao na mifaida kibao.

Waafrika tuone hivi hivi tunajuwa sana kuongea, kupanga na kupangua lakini hatujuwi kutekeleza. Leo mchukuwe Mtanzania yeyote umuulize kuhusu ligi ya mpira wa Uingereza, basi utamkuta anaijuwa hiyo ligi na namna timu inatakiwa iwe kuliko Mourinho. Hiyo si kwenye mpira tu, ni kila pahali, tunajuwa kila kitu kwa midomo yetu lakini kutenda? Ng'oo.

Nchi hii muumba dunia na ardhi alitujaaalia kila kitu chema, maji mengi, madini mengi, ardhi nzuri inayo-limika miezi 12 kwa mwaka, misitu mizuri, mbuga nzuri, milima mizuri, mabonde mazuri, watu wazuri, wanyama wazuri. Kwa ufupi katupa pepo ya duniani, lakini kitu kimoja hatukupewa, nacho ni akili. Akili hatuna.

Binaadam hakosi kasoro na kasoro yetu ni akili.

Wakati sisi tutaanza kuwa na umeme wa uhakika (miaka 50-100 ijayo), kumbuka kuwa mpaka sasa ni 14% tu ya Watanzania wenye umeme tena sio wa uhakika, wenzetu watakuwa hawana haja ya maviwanda ya umeme, majumba na maviwanda yanayohitaji umeme yatakuwa yanajizalishia yenyewe umeme (haya yameshaanza kwa wenzetu, kuna majumba mapya huko yanajizalishia yenyewe umeme na ule wa ziada wanawauzia gridi zao) Hapo sasa.

Self-sufficient Urban Buildings | BETTER WORLD // ENGINEERING

Sosoljip is a Self-Sufficient Net Zero Energy House in South Korea | Inhabitat - Sustainable Design Innovation, Eco Architecture, Green Building

MenoMenoPiu Unveils Plans for Wind-Powered Alvar Aalto Campus Otaniemi | Inhabitat - Sustainable Design Innovation, Eco Architecture, Green Building

Kuna siku ukiamua kuwa impartial (kusema ukweli bila kutawaliwa na fikra za udini) unaongea busara sana!
Ndio maana Watanzania wenzio hapa tunahitaji mabadiliko ili hii hali iliyopo sasa ya "zilongwa mbali zitendwa mbali" ikome!
 
Ni aibu kwa nchi yetu kuwa
na taasisi mbovu kama TANESCO. Viongozi wake wapo, wanajua mikataba
mibovu ilivyo,wamekaa kimya tu.

Ulichoandika hata hukijui; Ni MD wa TANESCO anayesaini mikataba au viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini?
 
Back
Top Bottom