TANESCO kuachana na Symbion na Aggreko?

Siku ambayo utaacha kutegemea mawazo ya wanasiasa yakuongoze huko unakotaka kwenda ndiyo siku ambayo utakombolewa kifikra.

Seriously, hatuhitaji mawazo ya mwanasiasa kufahamu matatizo yanayotukumba, hasa hili tatizo sugu la umeme.

Mkuu upepo wa kisiasa usikufanye uchukie wanasiasa wanapoombwa mawazo yao.

Tatizo la umeme halihitaji ufafanuzi wa Mnyika lakini kama waziri kivuli wa wizara husika tena kwa muda mrefu nategemea mawazo mapana zaidi kutoka kwake kama mwanaJF.

Kumtaja mtu humu ni njia tu ya kumualika kwenye mjadala kama ambavyo nimewahi kukutaja wewe sidhani kama maana yake ni kuongozwa kwa kutegemea fikra zako.
 
-Hatma ya TANESCO ni kifo cha mende kama ilivyo kwa mashirika yote ya umma, ni wakati muafaka tukawachia makampuni binafsi yakazalisha, kusafirisha na kuuza umeme. Tumeona tulivyokuwa tunaumizwa na TTCL, ni hivyo hivyo tunaumizwa TANESCO.

-Mbadala tukiutaka tunao. Nakupa siri moja; kuna kampuni ya umeme iliyokuwa tayari kuwekeza kwa fedha zao kujenga damn ya kisasa. wakakubaliwa, baada ya kufanya feasibilty study iliyowagharimu kama dola million 3, walipiwasilisha kwa Mhongo hata hakuitazama wala kuisoma, akasema haifai.

Huo Mkataba waliokuwa nao (Memorandum of Understanding) inabidi Serikali iwalipe Dola Million 4, na wakienda mahakamani watalipwa zaidi kwani damn hiyo hiyo kwa sasa wamepewa Wachina waijenge (sub standard). Huo ndio Muhongo.

- Uhakika wa umeme si kwa gesi tu, gesi ni mojawapo na pia kuna mradi wa Steigler Gorge unaoendeshwa na Wabrazil, kuna mradi huo wa Wachina niliousema (haujaanza) lakini umesha sainiwa na Pinda alivyokuwa China juzi juzi, kuna mradi wa Wacanada na mwingine wa Wachina wa umeme wa Makaa ya mawe. Mbali na hii gesi ambayo bomba ndio linasambazwa.

ukiweka habari za siasa pembeni, uko nondo mama, baasi huwa unaamua kuumiza vichwa vya bavicha tu huku jf wakati unaujua ukweli
cc buku 7 fc@ lumumba
 
Awamu ya nne ilirithi uongozi wakati nchi ikiwa kizani totoroo. Umesahau? au ulikuwa na miaka 7 wakati huo?

Bora hii awamu ya nne leo hii tunaona mikataba ya miradi mikubwa mikubwa ya umeme kuliko wakati wowote ule. Na hilo halipingiki, ukipinga tu, nakuwekea ushahidi humu.

TANESCO ni kama mashirika yote ya umma yalioshindwa kujiendesha na rasilmali wanazo. Libinafsishwe tu au lifanywe kama ilivyofanywa TTCL, lipo kama halipo, lijiendesha lenyewe kifaida au lijifie na huku mashirika binafsi yawekeze kwenye, utafiti, ufuaji, usafirishaji, usambazaji na uuzaji umeme. Uone baada ya miezi 6 tu. Utashangaa.

duu dada yangu we mfanyakazi wa zamani wa TANESCO nini? naona una mawazo yanayoendana na tatizo

ni kweli nakubaliana na wewe shida kubwa ya TANESCO ni siasa za kwenye mashirika ya umma .... uzalishe usizalishe faida mishahara, marupurupu yako pale pale ..... mashirika binafsi, wamiliki au wawekezaji wake wanataka kuona faida tu bila sivyo uongozi na wafanyakazi watakiona cha moto

kwenye huduma yoyote ili kupata faida ni kufanya mojawapo au yote kwa pamoja ya mambo haya mawili
1) uongeze mauzo
2) upunguze gharama za uzalishaji na/au uendeshaji

Maoni yangu:
1) Kwenye swala la kwanza mapato ya TANESCO yanatokana na mauzo ya umeme kwa wateja pamoja serikali kutoa ruzuku. Inavyoonekana serikali haitaki kuwekeza vya kutosha au kutoa ruzuku ya kutosha kwa TANESCO ndio maana wao wakachukua uamuzi wa kuongeza bei ya umeme. Kwa sababu za kisiasa serikali haiwezi kukubali ongezeko lote la bei ambalo litawezesha TANESCO kutengeneza faida pamoja na kuwekeza kwenye miundombinu yake iliyochoka. Kwa hiyo hapa ni serikali ichague moja kutoa ruzuku ya kutosha au iruhusu TANESCO ipandishe bei wanavyotaka. Pia TANESCO wapewe rungu la kukusanya madeni yao hasa kwa idara za serikali yenyewe. Bila kusahau watanzania wote walipishwe bei moja ya umeme kulingana na matumizi yao sio Zanzibar wapendelewe kwa bei ndogo.

2) Gharama za uzalishaji na uendeshaji kwa kiwango kikubwa zinaliwa na mikataba ya umeme wa dharura pamoja na ya binafsi (PPP) ambayo TANESCO imeingia na mashirika kama IPTL, SonGAS, na wengineo. Hii mikataba ni wahusika wenyewe walioingia wanajua jinsi itakavyoisha ila kukifanyika siasa tena kwa pupa bila majadiliano yanaweza kuiweka tena TANESCO kwenye hali mbaya kama issue ya DOWANS. Mambo ya ufisadi, ufanisi wa kazi, umakini kwenye manunuzi wa vifaa na miradi ni mambo mengine ya kuangaliwa. Hapa inabidi warudishe tena chuo cha TANESCO ili waweze kutrain wafanyakazi wao kufanya hata matengenezo makubwa ambayo kwa sasa baadhi yanategemea consultants au contractors toka nje ya shirika.

Kumalizia nakuunga mkono kwenye kubinafsisha generation na supply units za TANESCO. Hii kama ulivyosema itaongeza ufanisi (lakini tu kama kutakua na strong regulatory body.... bado na kumbukumbu sana na issue ya ENRON iliyotokea Marekani, nategemea unaijua). ILA NATOFAUTIANA na wewe kwenye kubinafsisha Transmission and Distribution units za TANESCO....hizi zinatakiwa kubakia ndani na serikali for security reasons. Zunguka dunia nzima utakuta transmission units zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali zao. Maana ukiweza kuuweka chali mfumo wa transmission....maana yake nchi nzima iko gizani na kila kitu kitaenda kombo.
 
Inadaiwa Bodi ya wakurugenzi ya TANESCO imepania kuachana na Mikataba ambayo inaonekana kuwa mzigo kwa shirika kati yake na Makampuni ya Symbion Power na Aggreko mwezi Oktoba 2014, kutokana gharama kubwa zisizoshikika toka kwa Makampuni haya.

Nini hatma ya TANESCO?

Tunao mbadala wa makampuni haya?

Tutarajie mgao mkubwa kuelekea 2015?

Tumepata uhakika baada ya kupatikana kwa gesi?
Kuvunja mkataba bila ya maandalizi ni SUICIDE. Watu watafurahia na kuipongeza bodi lakini in a week, wale wale ambao waliifurahia bodi wataanza kurusha makombora.

Kinachotakiwa si kuvunja mkataba kihovyo hovyo bali kuwalazimisha wahusika(Symbion Powe na wenzake) kukaa meza moja within the shortest possible time na kufumua mkataba na kuingia mkataa mpya wenye maslahi kwa wote. Wakati bodi wanatoa agizo hilo kwa akina Symbion, lazima wawaambie wazi kwamba wasipokuwa tayari kwa hilo, basi bodi haitakuwa na namna nyingini zaidi ya kutangaza tenda upya within one month na kwamba existing companies hazitaruhusiwa kushiriki coz' tayari ni failure.

So, either to MINIMIZE their charges or new tender gets advertised within a month. Once new investor(s) start operating, old guys cease doing business with TANESCO instantly.
 
duu dada yangu we mfanyakazi wa zamani wa TANESCO nini? naona una mawazo yanayoendana na tatizo

ni kweli nakubaliana na wewe shida kubwa ya TANESCO ni siasa za kwenye mashirika ya umma .... uzalishe usizalishe faida mishahara, marupurupu yako pale pale ..... mashirika binafsi, wamiliki au wawekezaji wake wanataka kuona faida tu bila sivyo uongozi na wafanyakazi watakiona cha moto

kwenye huduma yoyote ili kupata faida ni kufanya mojawapo au yote kwa pamoja ya mambo haya mawili
1) uongeze mauzo
2) upunguze gharama za uzalishaji na/au uendeshaji

Maoni yangu:
1) Kwenye swala la kwanza mapato ya TANESCO yanatokana na mauzo ya umeme kwa wateja pamoja serikali kutoa ruzuku. Inavyoonekana serikali haitaki kuwekeza vya kutosha au kutoa ruzuku ya kutosha kwa TANESCO ndio maana wao wakachukua uamuzi wa kuongeza bei ya umeme. Kwa sababu za kisiasa serikali haiwezi kukubali ongezeko lote la bei ambalo litawezesha TANESCO kutengeneza faida pamoja na kuwekeza kwenye miundombinu yake iliyochoka. Kwa hiyo hapa ni serikali ichague moja kutoa ruzuku ya kutosha au iruhusu TANESCO ipandishe bei wanavyotaka. Pia TANESCO wapewe rungu la kukusanya madeni yao hasa kwa idara za serikali yenyewe. Bila kusahau watanzania wote walipishwe bei moja ya umeme kulingana na matumizi yao sio Zanzibar wapendelewe kwa bei ndogo.

2) Gharama za uzalishaji na uendeshaji kwa kiwango kikubwa zinaliwa na mikataba ya umeme wa dharura pamoja na ya binafsi (PPP) ambayo TANESCO imeingia na mashirika kama IPTL, SonGAS, na wengineo. Hii mikataba ni wahusika wenyewe walioingia wanajua jinsi itakavyoisha ila kukifanyika siasa tena kwa pupa bila majadiliano yanaweza kuiweka tena TANESCO kwenye hali mbaya kama issue ya DOWANS. Mambo ya ufisadi, ufanisi wa kazi, umakini kwenye manunuzi wa vifaa na miradi ni mambo mengine ya kuangaliwa. Hapa inabidi warudishe tena chuo cha TANESCO ili waweze kutrain wafanyakazi wao kufanya hata matengenezo makubwa ambayo kwa sasa baadhi yanategemea consultants au contractors toka nje ya shirika.

Kumalizia nakuunga mkono kwenye kubinafsisha generation na supply units za TANESCO. Hii kama ulivyosema itaongeza ufanisi (lakini tu kama kutakua na strong regulatory body.... bado na kumbukumbu sana na issue ya ENRON iliyotokea Marekani, nategemea unaijua). ILA NATOFAUTIANA na wewe kwenye kubinafsisha Transmission and Distribution units za TANESCO....hizi zinatakiwa kubakia ndani na serikali for security reasons. Zunguka dunia nzima utakuta transmission units zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali zao. Maana ukiweza kuuweka chali mfumo wa transmission....maana yake nchi nzima iko gizani na kila kitu kitaenda kombo.

Hilo la security, ni mawazo ya kizamani sana.

Hivi likiwa au lisiwe chini ya Serikali, security inahusu nini hapo? Watendaji wote si binaadam? tena nje ya Serikali kunaweza kuwa ni secure zaidi kuliko ndani ya Serikali.
 
Kwa kweli ni uamuzi wa hekima na unaozingatia kuwatua watanzania mzigo mkubwa wa bei ya nishati hii muhimu kwa maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Hongera sana whoever brought up such a wonderful idea.
 
Hawawezi kujitoa kwa Symbion kwani tayari wameenda mbali kwa kuunda kampuni ya pamoja baina yao inaitwa SOUTHERN ELECTRIC COMPANY LTD , Kwa ajili ya kuuza umeme wa gesi nchi za Msumbiji na Malawi na tayari walishasaini mikataba , Tanesco ina mialiko asilimia 40 na Symbion 60 .....Someni hotuba ya Mnyika Bunge la bajeti mtaona kwa kina kilichopo ndani .......
 
Hilo la security, ni mawazo ya kizamani sana.

Hivi likiwa au lisiwe chini ya Serikali, security inahusu nini hapo? Watendaji wote si binaadam? tena nje ya Serikali kunaweza kuwa ni secure zaidi kuliko ndani ya Serikali.

Ha ha ha labda nikueleze kwa njia tofauti

nachotofautiana na wewe ni hili swala la serikali kuachia mwekezaji kuendesha kila kitu jinsi anavyotaka yeye na serikali haijui chochote......kwa nchi yetu hili si jambo geni, tumechemsha kwenye madini, na sasa tunachemsha kwenye gas pia.....gharama za kutumia mobile phones ni kubwa wakati reliability haiendani na gharama hizo......hii ni hatari kwa transmission network ... uliza wataalam wowote wa electrical transmission engineering watakueleza

kunaweza kufanyika ubinafsishaji au ushirikiana na makampuni binafsi kwa lengo la kuongeza ufanisi .... ila serikali iwe na shares za kutosha, uwezo wa kutoa maamuzi na kuelewa nini kinaendelea ndani ya kampuni kwa maana ya kuweka wataalam wazalendo (pamoja na mashushu) ili kulinda usalama wa nchi .... ukileta biashara ya makampuni ya simu kwenye swala hili nyeti la transmission network itakula kwetu muda si mrefu! .... sasa hivi hao wazungu wa songo songo wakikohoa tu mgao kila kona itakua grid ya taifa?....acha masihara dada yangu!

na nikasisitiza kuna umuhimu wa kuwa na regulatory body yenye nguvu za kisheria na wataalam wa kutosha wa kudhibiti hayo maeneo yanayobinafsishwa ....si umeme tu....SUMATRA, TTCRA, EWURA, etc wajengewe uwezo na kupewa nguvu...waache kuingiliwa na wanasiasa!
 
Katika hili ni muhimu sana tukajifunza kutokana na historia, waTz kwa ujumla wetu tunaendekeza sana siasa, hata wasomi wetu nao wamekuwa ni wapiga siasa, fitna na majungu. Wote tunakumbuka mwaka 2008/2009 Ngeleja akiwa Waziri wa Nishati na Madini walikubaliana na Tanesco wanunue ile mitambo ya iliyokuwa Dowans (sasa Symbion) kwa bei ya USD 59.7mil (Megawatt 112.5) lakini kwa mshangao mkubwa Spika Sitta na wenzake waliokuwa wanajifanya wapambanaji wa ufisadi wakakwamisha mpango huo.

Baadaye mitambo hiyo iliponunuliwa na Symbion kwa zaidi ya USD 100mil, na Tanesco kunendelea kulipia mkataba wa umeme tunaonunua Symbion hakuna mtu anapiga kelele tena, ni ajabu na kweli!

Pia ni vyema kuelewa kwamba kwa sasa mikataba waliyonayo Tanesco na makampuni ya Symbion, Aggreko na IPTL, mkataba ulio nafuu zaidi kwa capacity charge ni huo wa IPTL!
 
Ninawasapoti wakurugenzi nikiwa na uhakika ni watu wanaoelewa wanachofanya.Kama watavunja mikataba huku terms za mikataba yenyewe zikiiumiza Tanesco kwa kuvunja mikataba,then nitakuwa wa kwanza kuwageuka hawa wakurugenzi na kutaka wapelekwe mahakamani kwa kosa la kuhujumu uchumi maana watakuwa wanatumika kuwatafutia mafisadi hela za bure tu.Haiwezekani uwe mkurugenzi Tanesco halafu usijue mambo ya kisheria kama hayo.Haiwezekani mkataba uwe umebakiza miezi miwili kuisha halafu wewe msomi unayejua mambo vizuri tu,ulazimishe kuuvunja kabla huku ukijua kufanya hivyo kutakupelekea kulipa fidia.Huo utakuwa ufisadi kwa kutumia sheria na hawa wakurugenzi watakuwa timu moja na wamiliki wa hizo kampuni wakituhadaa watanzania kwa michezo yao ya njama za kishetani ya thesis x antithesis= synthesis!
 
Kwa kiasi fulani kupanda kwa bei ya umeme kunachangiwa sana n mikataba hiyo oliyoingiwa kati ya TANESCO na makapuni hayo ya kitapeli.

Mkuu siyo kiasi fulani hicho ndicho chanzo cha msingi cha gharama ya umeme ku[anda mengine ni inefficiency ya TANESCO kwa bahati mbaya ushoga uliyopo kati TANESCO na EWURA haitaruhusu UKWELI huu uwekwe wazi tutalipishwa tu mpaka tukome
 
Kama wataweza kuvunja mikataba hiyo,watakuwa wameliokoa taifa.
Inadaiwa Bodi ya wakurugenzi ya TANESCO imepania kuachana na Mikataba ambayo inaonekana kuwa mzigo kwa shirika kati yake na Makampuni ya Symbion Power na Aggreko mwezi Oktoba 2014, kutokana gharama kubwa zisizoshikika toka kwa Makampuni haya.

Nini hatma ya TANESCO?

Tunao mbadala wa makampuni haya?

Tutarajie mgao mkubwa kuelekea 2015?

Tumepata uhakika baada ya kupatikana kwa gesi?
 
Narudia tena,nawasapoti directors kuvunja hiyo mikataba only kama wameona loop holes za kisheria na kama mikataba bado ina muda mrefu wa kuwepo.Kama imebakiza muda mfupi ni bora tu wasubiri iishe manake wakivunja hatutawaelewa,hata pasipokuwa na madhara ya kisheria bado wengine tutajiuliza walikuwa wapi siku zote hizo?
 
Katika hili ni muhimu sana tukajifunza kutokana na historia, waTz kwa ujumla wetu tunaendekeza sana siasa, hata wasomi wetu nao wamekuwa ni wapiga siasa, fitna na majungu. Wote tunakumbuka mwaka 2008/2009 Ngeleja akiwa Waziri wa Nishati na Madini walikubaliana na Tanesco wanunue ile mitambo ya iliyokuwa Dowans (sasa Symbion) kwa bei ya USD 59.7mil (Megawatt 112.5) lakini kwa mshangao mkubwa Spika Sitta na wenzake waliokuwa wanajifanya wapambanaji wa ufisadi wakakwamisha mpango huo.

Baadaye mitambo hiyo iliponunuliwa na Symbion kwa zaidi ya USD 100mil, na Tanesco kunendelea kulipia mkataba wa umeme tunaonunua Symbion hakuna mtu anapiga kelele tena, ni ajabu na kweli!

Pia ni vyema kuelewa kwamba kwa sasa mikataba waliyonayo Tanesco na makampuni ya Symbion, Aggreko na IPTL, mkataba ulio nafuu zaidi kwa capacity charge ni huo wa IPTL!

na baada ya kelele zile za Sitta kuna mtu alijiuzulu lakini hadi leo nikitafuta ushahidi wa kina wa huyu mtu kuhusishwa na hizi kampuni kama walivyoimba akina six siupati.Bado najiuliza hivi kujiuzulu kwa mamvi ulikuwa uwajibikaji wa kikazi,kuwa na maslahi na kampuni hizi au alikuwa anamlinda mtu mwingine?waungwana nisaidieni!
 
Ha ha ha labda nikueleze kwa njia tofauti

nachotofautiana na wewe ni hili swala la serikali kuachia mwekezaji kuendesha kila kitu jinsi anavyotaka yeye na serikali haijui chochote......kwa nchi yetu hili si jambo geni, tumechemsha kwenye madini, na sasa tunachemsha kwenye gas pia.....gharama za kutumia mobile phones ni kubwa wakati reliability haiendani na gharama hizo......hii ni hatari kwa transmission network ... uliza wataalam wowote wa electrical transmission engineering watakueleza

kunaweza kufanyika ubinafsishaji au ushirikiana na makampuni binafsi kwa lengo la kuongeza ufanisi .... ila serikali iwe na shares za kutosha, uwezo wa kutoa maamuzi na kuelewa nini kinaendelea ndani ya kampuni kwa maana ya kuweka wataalam wazalendo (pamoja na mashushu) ili kulinda usalama wa nchi .... ukileta biashara ya makampuni ya simu kwenye swala hili nyeti la transmission network itakula kwetu muda si mrefu! .... sasa hivi hao wazungu wa songo songo wakikohoa tu mgao kila kona itakua grid ya taifa?....acha masihara dada yangu!

na nikasisitiza kuna umuhimu wa kuwa na regulatory body yenye nguvu za kisheria na wataalam wa kutosha wa kudhibiti hayo maeneo yanayobinafsishwa ....si umeme tu....SUMATRA, TTCRA, EWURA, etc wajengewe uwezo na kupewa nguvu...waache kuingiliwa na wanasiasa!

Unakuwa hujafanya kitu. Ukisha iingiza Serikali kuwa na share nyingi, umeshaharibu kila kitu. Kwani kudhibiti na kutengeneza sera za usimamiaji ni lazima Serikali iwe na shares? shares wanaweza kuwa nazo lakini chache tu na sikubaliani na wao kuwa major shareholders, inakuwa hujafanya kitu na hakuna mwekezaji ataekubali. Hao hao walioharibu leo mimi kama mwekezaji nikatumbukize fedha zangu wakazi-control wao? haiji.
 
Na kwa kiwango kikubwa watanzania wenyewe tunachangia kwa kukomaa na siasa ambazo zinatuondoa kwenye mambo ya msingi na kuacha mambo yaende kama yanavyokwenda.

Ni kama siasa zipi hizo mkuu?. Hivi kweli Tanzania ni nchi kweli yakuwa na uhaba wa umeme kweli?

Imagine, 152million kila siku kisha zidisha kwa siku 365 na hapo ni Symbion Power tu!

Hawa symbion power ndiyo kina nani? hivi siyo wale wale wenye Richmond? na je ni kwa uzarishaji umeme hauruhusiwi ufanywe na watu/kampuni binafsi?
 
Ulichoandika hata hukijui; Ni MD wa TANESCO anayesaini mikataba au viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini?

Wewe ndiyo haujui nilichokiandika mimi! MD wa TANESCO yuko pale kwa maslahi ya nani, TANESCO au Waziri wa nishati na madini?

Ndiyo maana mimi niligenerelize kwa kusema "viongozi".

MD wa TANESCO, kama anakubali kuifanyia kazi mikataba mibovu na akakubali bila kulalamika ni majanga! Kama anajua kabisa kwamba waziri amesaini mkataba mbovu; kwanini MD aendelee kung'ang'ania madaraka?

Kwanini asitokelezee na kusema hapa hapana?
 
Tatizo ni kuwa na shirika la umma lenye kumiliki na kuendesha biashara kubwa kuliko zote Tanzania ambalo linaendeshwa na watu wasio na uchungu na hiyo biashara wala hawajui umuhimu wa hiyo biashara wala hawana ujuzi wa biashara zaidi ya kusoma madarasani.

Ni wakati muafaka Shirika hili nalo likawa la watu binafsi wenye uchungu, ujuzi na wanaojuwa umuhimu wa biashara.

Niliwahi kupendekeza miaka iliyopita, shirika hili libinafsishwe na wauziwe matajiri, kipaumbele wapewe matajiri wa Kitanzania, nilipendekeza hisa kubwa apewe SS Bakhressa na apewe kuliendesha, ambae ana CV nzuri ya kuendesha biashara kubwa kubwa na zinazokuwa kila kukicha. uone jinsi shirika litavyobadilika ndani ya miezi 6 tu na umeme utavyokuwa ni kitu cha ajabu kutokuwepo.

agreed,

Serikali inatakiwa kuacha kuhodhi mashirika yanayoneemesha wachache na kuibebesha mzigo serikali yenyewe na wanachi maskini... kazi kuu ya serikali iwe kwenye kutunga sera na miongozo (kwa kushirikiana na wadau), kusimamia, kutoa adhabu na kukusanya stahili yake

Mfano mzuri ni makampuni ya simu na mawasiliano kwa ujumla - TCRA imebaki na jukumu kuu tu.... we can do it kwa maji, umeme, nk. na nakubali kabisa, wapewe wazawa wenye uchungu na wanaojua biashara, kuwepo hata na motivational effort za successful indigenous businessmen kuwa majority shareholders wa mashirika hayo

JK AKIWEZA KUWEKA HUO MSIMAMO HATASAHAULIKA HADI GENERATIONS NNE AU TANO ZIJAZO

naamini kabisa anaweza kuamua na kusimamia hilo
 
Tatizo ni kuwa na shirika la umma lenye kumiliki na kuendesha biashara kubwa kuliko zote Tanzania ambalo linaendeshwa na watu wasio na uchungu na hiyo biashara wala hawajui umuhimu wa hiyo biashara wala hawana ujuzi wa biashara zaidi ya kusoma madarasani.

Ni wakati muafaka Shirika hili nalo likawa la watu binafsi wenye uchungu, ujuzi na wanaojuwa umuhimu wa biashara.

Niliwahi kupendekeza miaka iliyopita, shirika hili libinafsishwe na wauziwe matajiri, kipaumbele wapewe matajiri wa Kitanzania, nilipendekeza hisa kubwa apewe SS Bakhressa na apewe kuliendesha, ambae ana CV nzuri ya kuendesha biashara kubwa kubwa na zinazokuwa kila kukicha. uone jinsi shirika litavyobadilika ndani ya miezi 6 tu na umeme utavyokuwa ni kitu cha ajabu

Biashara kubwa ya Bakhresa ni ipi huyu kanjanja mkwepa kodi maarufu? Biashara ya kutembeza Ice cream kwa baiskeli na kuuza unga? Boti zake zinasifika kubeba magendo kati ya dar na zanzibar na makampuni yake yanaogopa kutia mguu soko la hisa kukwepa uwazi? Nani hamjui uhuni wake?

Tatizo la Tanesco haliko ndani ya Tanesco, liko Ikulu na Bungeni, fanyeni mabadiliko huko. Tanesco idumu milele kuwa shirika la umma 100% kwa usalama wa taifa lako.
 
Hilo la security, ni mawazo ya kizamani sana.

Hivi likiwa au lisiwe chini ya Serikali, security inahusu nini hapo? Watendaji wote si binaadam? tena nje ya Serikali kunaweza kuwa ni secure zaidi kuliko ndani ya Serikali.

Security inayoongelewa siyo hiyo unayotaka kurahisisha! Kwa ufupi tu wiki inatosha kuyumbisha utawala au hata kuondoa watawala kwa kutumia tanesco. Mwenye tanesco akiamua anaweza kuleta ya Misri ndani ya muda mdogo sana!
 
Back
Top Bottom