TAKUKURU wanalipwa mishahara ya kazi gani kwa uozo na rushwa zilizoelezwa kwa Waziri Mkuu?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
876
4,101
Mkurugenzi wa TAKUKURU na wafanyakazi walio chini yake wanalipwa fedha nyingi kutoka kwenye kodi za wananchi.

Pamoja na malipo mazuri hakuna kazi yoyote ya msaada wanayotoa kwa serikali na jamii kwa ujumla. Kama wangekuwa active hizi taarifa za madhila ya wafanyabiashara wangekuwa wanazo na kuchukua hatua, lakini hakuna kesi yoyote walioripoti kuipokea kuhusu changamoto hizi. Je, kuna umuhimu wa kuendelea kuwa na hii taasisi?

Lakini pia wanaolalamikiwa ndio waliomlea boss wa sasa wa TAKUKURU; Je, ilikuwa sahihi kwa Mhe. Rais kuteua Mkuu wa TAKUKURU kutoka kwenye taasisi inayoongoza kwa rushwa (polisi)?

Hata kama angekuwa muadilifu kiasi gani, anaendaje kuwakamata watendaji wa bosi wake? IGP ni senior kwa Kamishna wa Polisi anayeongoza TAKUKURU, je, anawezaje kumkwepa IGP na kwenye kukamata vijana wake? Najiuliza maswali haya nikitambua kwamba mfumo wetu wa uteuzi unaweza kumtengua na kumrejesha polisi, atatazamana vipi na ndugu zake?

Muundo huu wa TAKUKURU utaendelea kuwatesa viongozi wakuu nakuwalazimisha wawe maafisa TAKUKURU huku wenye dhamana wakiwa wanalipwa salary bila tija.
 
Kwani nchi hii kuna taasisi au idara yoyote wanayolipwa mishahara kwa kufanya kazi wanazopaswa kufanya? Kama ipo naomba mtu anijuze nami niijue. Nchi hii ngazi zote watu wanalipana mishahara na marupurupu juu just for doing nothing. Watu wanagawana pesa tu!
 
Takukuru ni chombo kisichokuwa na meno. Kazi yake ni kudhibiti tu rushwa ndogo ndogo za uchaguzi wa kata, matrafiki, na uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivi kuanzia kimeanzishwa, ni nani aliyewahi kufungwa kwa rushwa hata tu ya milioni 50?
Nakataa. Traffic wanakula rush rushwa bila woga kutoka chombo chochote
 
HIlo litasisi nadhani lipo kama mtego wa kunasa mikopo ya kimataifa na kujaribu kuficha watoto wetu huko ilimradi tu wasizurule mtaani.
 
Mkurugenzi wa TAKUKURU na wafanyakazi walio chini yake wanalipwa fedha nyingi kutoka kwenye kodi za wananchi.

Pamoja na malipo mazuri hakuna kazi yoyote ya msaada wanayotoa kwa serikali na jamii kwa ujumla. Kama wangekuwa active hizi taarifa za madhila ya wafanyabiashara wangekuwa wanazo na kuchukua hatua, lakini hakuna kesi yoyote walioripoti kuipokea kuhusu changamoto hizi. Je, kuna umuhimu wa kuendelea kuwa na hii taasisi?

Lakini pia wanaolalamikiwa ndio waliomlea boss wa sasa wa TAKUKURU; Je, ilikuwa sahihi kwa Mhe. Rais kuteua Mkuu wa TAKUKURU kutoka kwenye taasisi inayoongoza kwa rushwa (polisi)?

Hata kama angekuwa muadilifu kiasi gani, anaendaje kuwakamata watendaji wa bosi wake? IGP ni senior kwa Kamishna wa Polisi anayeongoza TAKUKURU, je, anawezaje kumkwepa IGP na kwenye kukamata vijana wake? Najiuliza maswali haya nikitambua kwamba mfumo wetu wa uteuzi unaweza kumtengua na kumrejesha polisi, atatazamana vipi na ndugu zake?

Muundo huu wa TAKUKURU utaendelea kuwatesa viongozi wakuu nakuwalazimisha wawe maafisa TAKUKURU huku wenye dhamana wakiwa wanalipwa salary bila tija.
Watu kule takukuru wananenepeana tu.
 
Lakini pia wanaolalamikiwa ndio waliomlea boss wa sasa wa TAKUKURU; Je, ilikuwa sahihi kwa Mhe. Rais kuteua Mkuu wa TAKUKURU kutoka kwenye taasisi inayoongoza kwa rushwa (polisi)?
Mtu unaonekana unayo akili nzuri tu ya kufikiri na kuelewa mambo; sasa sijui tatizo lako ni nini hasa?

Hapa kidogo ulikaribia kujijibu swali lako mwenyewe kuhusu hiyo TAKUKURU, lakini kwa kujitoa ufahamu, tena kwa maksudi kabisa unajifanya kujisahaulisha mwenyewe, kwamba hujui tatizo ni nini hasa?

TAKUKURU ya wapi itashindwa kufanya kazi zake vizuri, kama hao unaojisahaulisha kuwa wapo wangetaka taasisi hiyo ifanye kazi zake kwa ufanisi.

Sasa, hapa nahofia kwamba utaendelea kujifanya huelewi kinachoelezwa!

Hii ni tabia mbovu sana inayopatikana Tanzania pekee; tabia ya kutafuta visababu na kulaumu sehemu ambayo ubovu wake unasababishwa na ubovu ulioko juu kabisa. Huu ni unafiki.
 
Kwani nchi hii kuna taasisi au idara yoyote wanayolipwa mishahara kwa kufanya kazi wanazopaswa kufanya? Kama ipo naomba mtu anijuze nami niijue.
Nchi hii ngazi zote watu wanalipana mishahara na marupurupu juu just for doing nothing. Watu wanagawana pesa tu!
Nitamwomba huyo aliyeweka mada yake hapa akusome, huenda andiko lako likawa msaada kwake, kama kweli alikuwa hajui alipoiweka hii mada hapa.

Siku hizi mada zinabandikwa tu hapa JF, mradi tu mtu anajisikia kuanzisha mada.

Hakuna fikra zozote zinazotumika kujaribu kudadisi uzito wa mada yenyewe.
 
Takukuru ni chombo kisichokuwa na meno. Kazi yake ni kudhibiti tu rushwa ndogo ndogo za uchaguzi wa kata, matrafiki, na uchaguzi wa serikali za mitaa.

Hivi kuanzia kimeanzishwa, ni nani aliyewahi kufungwa kwa rushwa hata tu ya milioni 50?
Takukuru cha kuwekea mapingamizi wagombea tu
 
Back
Top Bottom