Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 876
- 4,101
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa imekabidhiwa mikononi mwa wanajeshi na Askari. Kazi hii aliifanya Magufuli kwa lengo la kumwezesha kutoa amri ya kutimiza malengo yake .
Baada ya JPM bado aliteuliwa Afisa wa Polisi kuongoza taasisi hii. Madhara ya uteuzi ule ni kwamba taasisi imeacha misingi yake na sasa inasikiliza amri kutekeleza majukumu yao. Ni taasisi inayosubiri mwanasiasa aseme kamata na siyo taasisi yakujieneza kwa jamii kubaini wizi na kuchukua hatua.
TAKUKURU inapaswa kuwa na mifumo mizuri ya kubaini viashiria vya rushwa kwenye taasisi na kisha kukutana na mkuu wa taasisi husika kumwelekeza visharia na risks zilizopo anazopaswa kuzifanyia kazi.
TAKUKURU haipaswi kukamata inapaswa kuita mtuhumiwa kwa mahojiano. Haipaswi taasisi yakisubiri wizi utokee bali iwe taasisi yakuona wizi kabla hakutendeka na kudhibiti isitokee.
Kwa ufupi TAKUKURU ilipaswa kuangaika na mapapa siyo dagaa.....dagaa walipaswa kudhibitiwa kwa kuwabaini kabla ya kuiba ili wasifanikiwe kuiba.
Nashauri mamlaka za uteuzi ziondoe TAKUKURU polisi na kuirudisha kwa RAIA wenye integrity. Haiwezekani watumishi wa TAKUKURU wafanye kazi ndani kwao wanapofikia nafasi ya ukurugenzi mkuu waletewe mtu kutoka nje ya taasisi na anayeletwa akapata uungwaji mkono. Tukubali kwamba hizi taasisi wapo watu wamesota miaka na miaka wakifanya kazi wafikie nafasi ya juu, tuwape nafasi badala ya kuwaletea watu kutoka nje.
Rushwa imekithiri kwa sababu wanaopambana na rushwa leo walikulia kwenye rushwa. Kila wakitaka kuchukua hatua wanakumbuka maovu yao.
Baada ya JPM bado aliteuliwa Afisa wa Polisi kuongoza taasisi hii. Madhara ya uteuzi ule ni kwamba taasisi imeacha misingi yake na sasa inasikiliza amri kutekeleza majukumu yao. Ni taasisi inayosubiri mwanasiasa aseme kamata na siyo taasisi yakujieneza kwa jamii kubaini wizi na kuchukua hatua.
TAKUKURU inapaswa kuwa na mifumo mizuri ya kubaini viashiria vya rushwa kwenye taasisi na kisha kukutana na mkuu wa taasisi husika kumwelekeza visharia na risks zilizopo anazopaswa kuzifanyia kazi.
TAKUKURU haipaswi kukamata inapaswa kuita mtuhumiwa kwa mahojiano. Haipaswi taasisi yakisubiri wizi utokee bali iwe taasisi yakuona wizi kabla hakutendeka na kudhibiti isitokee.
Kwa ufupi TAKUKURU ilipaswa kuangaika na mapapa siyo dagaa.....dagaa walipaswa kudhibitiwa kwa kuwabaini kabla ya kuiba ili wasifanikiwe kuiba.
Nashauri mamlaka za uteuzi ziondoe TAKUKURU polisi na kuirudisha kwa RAIA wenye integrity. Haiwezekani watumishi wa TAKUKURU wafanye kazi ndani kwao wanapofikia nafasi ya ukurugenzi mkuu waletewe mtu kutoka nje ya taasisi na anayeletwa akapata uungwaji mkono. Tukubali kwamba hizi taasisi wapo watu wamesota miaka na miaka wakifanya kazi wafikie nafasi ya juu, tuwape nafasi badala ya kuwaletea watu kutoka nje.
Rushwa imekithiri kwa sababu wanaopambana na rushwa leo walikulia kwenye rushwa. Kila wakitaka kuchukua hatua wanakumbuka maovu yao.