Ni usiku mnene. Naamua kuandika DOKEZO hili.
Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.
Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.
Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.
Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala TAKUKURU hawafanyi kazi yao iliyotukuka.
1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.
Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.
Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi fulani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.
Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha. Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.
Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.
Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.
Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??
Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!
Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?
2. Mradi wa mwendokasi Mbagala
Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.
Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.
Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!
Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.
Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.
Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?
3. UHABA wa Petroli sasa hivi nchini.
Hapa siandiki sana.
Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!
Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...
Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.
Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!
Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.
4. Nauli za mabasi za LATRA.
Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!
USHAHIDI upo.
Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!
Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.
Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.
Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.
Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!
Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.
Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.
Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.
Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.
Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.
Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.
Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala TAKUKURU hawafanyi kazi yao iliyotukuka.
1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.
Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.
Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi fulani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.
Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha. Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.
Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.
Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.
Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??
Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!
Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?
2. Mradi wa mwendokasi Mbagala
Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.
Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.
Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!
Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.
Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.
Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?
3. UHABA wa Petroli sasa hivi nchini.
Hapa siandiki sana.
Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!
Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...
Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.
Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!
Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.
4. Nauli za mabasi za LATRA.
Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!
USHAHIDI upo.
Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!
Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.
Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.
Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.
Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!
Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.
Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.
Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.
Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.