DOKEZO TAKUKURU na Serikali ya Mkoa Songwe ielezeni jamii kilichotokea kuhusu tuhuma za Kaimu Meneja wa TANROADS

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Kuna jambo limetokea linahusu rushwa, sijajua kwa sababu zipi halitangaziwi au halitajwi hadharani, inawezekana kuna bado mamlaka zipo kazini au inawezekana pia kuna vitu havipo sawa.

Hapa kwetu Mkoani Songwe kuna jambo limetokea likimhusisha Kaimu Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Songwe ambaye anajulikana kwa Eng. Suleiman Bishanga.

Inasemekana wiki moja au mbili zilizopita maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) walizikamata gari ambazo zilikwepa kupita kwenye Mzani (Mzani wa Mpemba) kwa ruhusa ya Eng. Bishanga.
1692130693063.jpg

1692130657326.jpg

Baada ya TAKUKURU kuingilia ‘Mchongo’ huo, wamezikamata gari nne, mbili nyeupe na mbili za njano ambazo mpaka leo tarehe 16 mwezi wa nane, 2023 zimepaki kwenye yard yao.

Inadaiwa kampuni inayomiliki magari hayo (mali ya Mchina) ilikuwa inatoa fungu (zaidi ya shilingi milioni 4) kwa Meneja ili aruhusu malori yake yapite bila kupimwa kila wanapopitisha magari hayo ambayo huwa yanabeba lami.

Hata hivyo, TAKUKURU walivyokamata magari, yakapimwa na kukutwa na uzito mkubwa sana kiasi kwamba kwa gari zote nne jumla ya faini iliyotozwa ni zaidi ya Shilingi milioni 90.

Hoja yangu ni kuwa mbona kuna ukimya kuhusu hiki kilichotokea, si TAKUKURU wala Serikali ya Mkoa ambayo imejitokeza kueleza micheo michafu iliyokuwa inaendelea.
 
Wakati mwingine wafanya kazi wa vyombo vetu huwa hawatumii weledi kikazi. Kuna tatizo gani kupima uzito, kurekodi uzito kama ushahidi, halafu kuachia vifaa vya kazi kuendelea na ujenzi wa Taifa?
 
Wakati mwingine wafanya kazi wa vyombo vetu huwa hawatumii weledi kikazi.
Kuna tatizo gani kupima uzito, kurekodi uzito kama ushahidi, halafu kuachia vifaa vya kazi kuendelea na ujenzi wa Taifa?
Mkuu kuachia hayo magari ni unaita kuendelea na ujenzi wa taifa au ubomoaji wa taifa.

Hivi wanavyo zidisha uzito hivyo ndio wanajenga taifa kweli?

Hivi unahisi Hao wachina wangeweza kufanya hivyo kwao?
 
Mkuu kuachia hayo magari ni unaita kuendelea na ujenzi wa taifa au ubomoaji wa taifa.

Hivi wanavyo zidisha uzito hivyo ndio wanajenga taifa kweli?

Hivi unahisi Hao wachina wangeweza kufanya hivyo kwao?
Ulivyoeleza ndivyo zilivyo akili za mtu wa kawaida katika vyombo vyetu. Akili ya ziada itakuambia huyu mchina ana mkataba. Ambao unaendelea. Kukamata vifaa vyenye nyenzo ya ujenzi, lami, ni kuhujumu mradi.

Hivyo rekodi kosa, piga fine, wahusika wote wawajibishwe. Kuzuia vifaa ni ushamba.
 
Ulivyoeleza ndivyo zilivyo akili za mtu wa kawaida katika vyombo vyetu.
Akili ya ziada itakuambia huyu mchina ana mkataba. Ambao unaendelea. Kukamata vifaa vyenye nyenzo ya ujenzi, lami, ni kuhujumu mradi.
Hivyo rekodi kosa, piga fine, wahusika wote wawajibishwe.
Kuzuia vifaa ni ushamba.
Ofcoz mimi ni mtu wa kawaida.

Wewe sio mtu wa kawaida?
 
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.

ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

My take.
Muda si mrefu tutasikia Tanzania yashindwa kesi na DP world yatakiwa kulipa trillioni 15.

Njia mpya iliyobuniwa na wajibu ndani ya serikali kuchota kodi za walala hoi, unasaini mkataba wa kijinga ambao ni kichaa tu anayeweza kuuvumilia alafu ukiulizwa unasema tumeshindwa kesi tulipeni tu.
 
Eng suleiman ahmad malinzi bishanga sio kaimu meneja bali ndo meneja wa mkoa, haya mambo huwa yanapigwa sometimes na Eng anayesimamia mzani ukute hata Regional Manager hajui, sometimes kama wanafanya kazi ya ujenzi na mzigo unatoka karibu huwa wanaomba kubypass maana huwa kweli wamezidi, kama imetokea ivo kuna mtu wa chini ametaka tu kumwaribia uyu jamaa angu bishanga.
 
Wakati mwingine wafanya kazi wa vyombo vetu huwa hawatumii weledi kikazi.
Kuna tatizo gani kupima uzito, kurekodi uzito kama ushahidi, halafu kuachia vifaa vya kazi kuendelea na ujenzi wa Taifa?
Kama gari imeoverlaod inamaana ukikeep record unakeep na ile fine anayotakiwa kulipa, cha muhimu huwa wanafanya kuwaruhusu wakiomba kubypass kama hawatoki umbali mrefu na wanapofanyia kazi. Labda tu kuna mtu anamfuatilia mwana (eng bishanga) kutaka kumwaribia.
 
Wakati mwingine wafanya kazi wa vyombo vetu huwa hawatumii weledi kikazi.
Kuna tatizo gani kupima uzito, kurekodi uzito kama ushahidi, halafu kuachia vifaa vya kazi kuendelea na ujenzi wa Taifa?
Kweli kabisa maana shughuli zinasimama.Ukiwa na ushahidi unatosha tatizo polisi wanatumia nguvu kuliko akili
 
Back
Top Bottom