Nakumbuka mwaka jana mwezi kama wa 8 hivi....kuna mdada mmoja.. tulikuwa marafiki miaka 5 iliyopita...ananipigia wiki nzima mfulululizo, kunimomba nimtumie pesa...tupo mikoa tofauti...nimemzungusha kwa wiki yote..pesa nilikuwa nayo ila nilikuwa mzito. Siku ya mwisho kanipigia sim, akawa anaongea kwa huruma sana, mpaka nikajishtukia...nikamwambia nitakutumia muda sio mrefu.
Nakumbuka ilikuwa kama saa moja na ushee usiku, umeme umekatika. Nikajisogeza duka la Mpesa kumtumia...kufika pale wakasema kiwango kilichopo hakitoshi...wakaniambia nenda duka la karibu na stendi, pale hukosi. Hilo duka lipo barabara kuu ya Singida-Arusha. Nikaanza kwenda kwenye hilo duka....Nilipoanza kuliona hilo duka kwa mbali, maana ni lazima uvuke hiyo barabara kuuu ndio ufike. Sijui ni nini kilinipata, sikupata ishara yoyote, wala sikuhisi chochote...nikakuta naghairi tu...pesa sikutuma tena.
Hata robo saa haikupita, jamaa yangu akanipigia simuu... ananiuliza nilipo....akaja muda huo....akaanza kusimulia.."Lile duka la Mpesa pale barabarani(Singida-Arusha) limevamiwa na Majambazi, yule jamaa anayeuza ameuawa, mwili wake upo mpaka sasa...polisi hawajaja bado". Nikajiuliza je ningeenda pale, ningekutana nao...kingetokea nini?....Mpaka leo huwa najiuliza sana.