Nina Bahati ya Kupendwa na Wanyama?

Nina Bahati ya Kupendwa na Wanyama?

Vien

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2020
Posts
8,370
Reaction score
14,844
Kuna jambo limekuwa likinitokea kwa muda sasa, na kila ninapolifikiria najiuliza kama ni jambo la kawaida au kuna watu wengine pia wamelipitia.

Ninaishi kwenye apartment ya kupanga. Jirani yangu anafuga mbwa, na cha kushangaza ni kwamba mbwa huyo ameonekana kunizoea sana. Karibu kila usiku ninaporudi kutoka kazini, nikikaribia geti huja mbio kunifuata, huanza kunirukia kwa furaha, na ninapofungua geti hujaribu kuingia ndani ya nyumba yangu. Hata hivyo, kila mara huwa namzuia.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba hili si tukio la mara moja. Limekuwa likitokea karibu kila siku.

Baada ya hapo kulitokea tukio lingine. Kulikuwa na paka aliyekuwa amehamia eneo letu. Badala ya kwenda kwenye nyumba nyingine, alianza kuja kulia mbele ya mlango wangu. Kila nilipofungua mlango alijaribu kuingia ndani. Hali hiyo iliendelea kwa takribani siku tatu mfululizo, lakini siku zote nilimzuia kuingia.

Kuna tukio lingine ambalo limenifanya nizidi kujiuliza. Kwenye kibaraza changu huwa naweka viatu. Mara kadhaa nimekuwa nikikuta chura amejificha ndani ya viatu hivyo. Si mara moja tu, limejirudia zaidi ya mara moja.

Sasa nikijumlisha haya yote –mbwa kunizoea sana, paka kutaka kuingia ndani kwangu, na hata vyura kujificha kwenye viatu vyangu–naanza kujiuliza kama haya ni matukio ya kawaida tu, au kuna watu ambao kwa namna fulani wanyama huwazoea zaidi kuliko wengine.

Matukio haya yamenifanya nijiulize kama kweli kuna watu ambao wanyama huwazoea kwa urahisi kuliko wengine, au haya ni matukio ya kawaida tu ambayo yanaweza kumtokea mtu yeyote.

Je, nyinyi mnalitafsiri vipi hili? Ni bahati ya kupendwa na wanyama, ni tabia ya kawaida ya wanyama, au kuna maelezo mengine?
 
Kuna tukio lingine ambalo limenifanya nizidi kujiuliza. Kwenye kibaraza changu huwa naweka viatu. Mara kadhaa nimekuwa nikikuta chura amejificha ndani ya viatu hivyo. Si mara moja tu, limejirudia zaidi ya mara moja.

Hii ya chura ni kwasababu Wanafuata harufu ya soksi zako 😊😊😊. (Natania)

Wanyama huwa wanatabia ya kuonyesha kumpenda mtu kwa mara ya kwanza.
Na ukiwaendekeza basi wanajua ww rafik yao, na watakuganda ganda.

Ila ukiwa unawafukuza. Wanakukariri (kwa harufu) na wanabalance shobo zao kwako..

Kwahiyo ni kawaida hiyo.
 
Hii ya chura ni kwasababu Wanafuata harufu ya soksi zako 😊😊😊. (Natania)

Wanyama huwa wanatabia ya kuonyesha kumpenda mtu kwa mara ya kwanza.
Na ukiwaendekeza basi wanajua ww rafik yao, na watakuganda ganda.

Ila ukiwa unawafukuza. Wanakukariri (kwa harufu) na wanabalance shobo zao kwako..

Kwahiyo ni kawaida hiyo.
Dah kweli Mungu fundi
 
Hii ya chura ni kwasababu Wanafuata harufu ya soksi zako 😊😊😊. (Natania)

Wanyama huwa wanatabia ya kuonyesha kumpenda mtu kwa mara ya kwanza.
Na ukiwaendekeza basi wanajua ww rafik yao, na watakuganda ganda.

Ila ukiwa unawafukuza. Wanakukariri (kwa harufu) na wanabalance shobo zao kwako..

Kwahiyo ni kawaida hiyo.
Hapa kuna nzi ananizonga sana,toka asubuhi kaninyanyasa sana, angekua anazurula tu poa.
Ila mda wote nikijaribu kulala anakuja sikioni kichwani 'nzee,nzee,nzeeh"
Nikijitingishika tu kapotea.
Na simuoni tena.
Nimemkosa mabanzi mara tano leo.
Kesho napiga dawa funga nyumba nione atakaaje humu shenzy kabisa.
 
Kuna jambo limekuwa likinitokea kwa muda sasa, na kila ninapolifikiria najiuliza kama ni jambo la kawaida au kuna watu wengine pia wamelipitia.

Ninaishi kwenye apartment ya kupanga. Jirani yangu anafuga mbwa, na cha kushangaza ni kwamba mbwa huyo ameonekana kunizoea sana. Karibu kila usiku ninaporudi kutoka kazini, nikikaribia geti huja mbio kunifuata, huanza kunirukia kwa furaha, na ninapofungua geti hujaribu kuingia ndani ya nyumba yangu. Hata hivyo, kila mara huwa namzuia.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba hili si tukio la mara moja. Limekuwa likitokea karibu kila siku.

Baada ya hapo kulitokea tukio lingine. Kulikuwa na paka aliyekuwa amehamia eneo letu. Badala ya kwenda kwenye nyumba nyingine, alianza kuja kulia mbele ya mlango wangu. Kila nilipofungua mlango alijaribu kuingia ndani. Hali hiyo iliendelea kwa takribani siku tatu mfululizo, lakini siku zote nilimzuia kuingia.

Kuna tukio lingine ambalo limenifanya nizidi kujiuliza. Kwenye kibaraza changu huwa naweka viatu. Mara kadhaa nimekuwa nikikuta chura amejificha ndani ya viatu hivyo. Si mara moja tu, limejirudia zaidi ya mara moja.

Sasa nikijumlisha haya yote –mbwa kunizoea sana, paka kutaka kuingia ndani kwangu, na hata vyura kujificha kwenye viatu vyangu–naanza kujiuliza kama haya ni matukio ya kawaida tu, au kuna watu ambao kwa namna fulani wanyama huwazoea zaidi kuliko wengine.

Matukio haya yamenifanya nijiulize kama kweli kuna watu ambao wanyama huwazoea kwa urahisi kuliko wengine, au haya ni matukio ya kawaida tu ambayo yanaweza kumtokea mtu yeyote.

Je, nyinyi mnalitafsiri vipi hili? Ni bahati ya kupendwa na wanyama, ni tabia ya kawaida ya wanyama, au kuna maelezo mengine?
Una miaka mingapi?
 
Kuna jambo limekuwa likinitokea kwa muda sasa, na kila ninapolifikiria najiuliza kama ni jambo la kawaida au kuna watu wengine pia wamelipitia.

Ninaishi kwenye apartment ya kupanga. Jirani yangu anafuga mbwa, na cha kushangaza ni kwamba mbwa huyo ameonekana kunizoea sana. Karibu kila usiku ninaporudi kutoka kazini, nikikaribia geti huja mbio kunifuata, huanza kunirukia kwa furaha, na ninapofungua geti hujaribu kuingia ndani ya nyumba yangu. Hata hivyo, kila mara huwa namzuia.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba hili si tukio la mara moja. Limekuwa likitokea karibu kila siku.

Baada ya hapo kulitokea tukio lingine. Kulikuwa na paka aliyekuwa amehamia eneo letu. Badala ya kwenda kwenye nyumba nyingine, alianza kuja kulia mbele ya mlango wangu. Kila nilipofungua mlango alijaribu kuingia ndani. Hali hiyo iliendelea kwa takribani siku tatu mfululizo, lakini siku zote nilimzuia kuingia.

Kuna tukio lingine ambalo limenifanya nizidi kujiuliza. Kwenye kibaraza changu huwa naweka viatu. Mara kadhaa nimekuwa nikikuta chura amejificha ndani ya viatu hivyo. Si mara moja tu, limejirudia zaidi ya mara moja.

Sasa nikijumlisha haya yote –mbwa kunizoea sana, paka kutaka kuingia ndani kwangu, na hata vyura kujificha kwenye viatu vyangu–naanza kujiuliza kama haya ni matukio ya kawaida tu, au kuna watu ambao kwa namna fulani wanyama huwazoea zaidi kuliko wengine.

Matukio haya yamenifanya nijiulize kama kweli kuna watu ambao wanyama huwazoea kwa urahisi kuliko wengine, au haya ni matukio ya kawaida tu ambayo yanaweza kumtokea mtu yeyote.

Je, nyinyi mnalitafsiri vipi hili? Ni bahati ya kupendwa na wanyama, ni tabia ya kawaida ya wanyama, au kuna maelezo mengine?
Una uhakika wanakuwa hawana njaa?
 
Hapa kuna nzi ananizonga sana,toka asubuhi kaninyanyasa sana, angekua anazurula tu poa.
Ila mda wote nikijaribu kulala anakuja sikioni kichwani 'nzee,nzee,nzeeh"
Nikijitingishika tu kapotea.
Na simuoni tena.
Nimemkosa mabanzi mara tano leo.
Kesho napiga dawa funga nyumba nione atakaaje humu shenzy kabisa.
Kaoge kwanza
 
Back
Top Bottom